Mjadala: Je, ni kweli Magari aina ya Nissan Xtrail ni mabovu?

Mjadala: Je, ni kweli Magari aina ya Nissan Xtrail ni mabovu?

Kwenye oil napenda tufahamishane ni oil zipi,sio kila oil unatakiwa uweke ya bp au castrol,wengine tunatumia total
 
Kwanza oil nyingi za engine za brand ya bp,castrol na total zinachakachuliwa, tahadhari penda kununua kwa recomended dealers
 
Nissan-X-Trail.jpg
Ni hii hapa kwa wanaopenda kuijua....
 
Subaru nying ni full time 4wd,issue ya kijiji huna hofu,mafuta 10km/L city kwa highway 12km hapa nazungumzia cc2000, kwa vipuli Shock up,bush,body,pump,plugg vyote bei ya kaiwada,

Jaribu forrester 2005 xt au cross sport ukishindwa hata impreza siyo mbaya maana engine za subaru structure ni moja.Zina tofautiana vitu vidogo kama cc,turbo, drive type

Forester X20, 2002-2004 Mimi ninayo KM 5 kwa lita, taa kubwa ya mbele 600,000 shock up si chini ya laki 550,000
 
Sio kweli.

CHA KWANZA KABISA UMJUE FUNDI ANAEJUA KUTENGENEZA NISSAN XTRAIL NA SIO TAPELI. FUNDI MWENYE UJUZI NA MUELEWA NA SIO MWENYE TAMAA!

Mimi fundi wangu miaka yote ni fundi mmoja anaitwa Deo yuko pale Mwenge alifundishwa na Nissan Wenyewe, yuko karibu na Maryland Bar opposite ITV.

Gari la kwangu nilinunua 2013 na mpaka leo ninalo na nimetembea nalo mikoa mingi sana nchi hii. Tayari tangu nimenunua nimetembea Kilometre 134,000 (nilizotumia mimi) Hili hapa:

View attachment 260838

Nimetumia magari mengi tangu ninunue gari la kwanza 1998. Nissan X-Trail haijawahi kuni-disapoint hata siku moja! Ni gari durable na comfortable hata ukiwa off road na stable barabarani sana. Nissan X-Trail spare zake ni ghali kidogo na sio kiasi kikubwa kama watu wanavyosema, ila bush, na stabiliser links ambazo ndio unabadilisha zaidi kama ni mtu wa pori kama mimi ukifunga ni mwaka. Spare zake karibu zote ni original. Vitu vikubwa vinavyokufaga na ni mara moja kwa mwaka ni sensors ambazo magari mengi ya siku hizi yanazo, usipoibadili ukaipuuzia basi unaweza kuharibu gari, gari ikaheat au tatizo lingine. Sensor moja inaweza kuwa laki mbili, ila sensor kama ya air filter mara nyingine huhitaji kusafishwa tu na spray maalum.

Muhimu usipitilize service milage, hakikisha unaweka collant na sio maji yako ya Dawasco, engene yake ni high efficient na moderm na ukiona tatizo lolote lile, peleka kwenye computer wa diagnose full stop. Iwe ni miss au engene ina mngurumo wa ajabu. Taa yoyote isiyo ya kawaida ikiwaka kwenye dashboard ni Computer tu ndio itakwambia.

Ujinga wa sisi Waafrika wengi tunataka gari ambalo hata usipofanya servie litakwenda tu na fundi yoyote ukimpa atategeneza. Ukimsikia fundi anakwambia hizi gari mbaya sana kama wanavyosema siku hizi gari za VVTI au D4 ujue huyo mbulula hana shule na hajui kulitengeneza. na ukimwachia atakuharibia gari.

Nissan X-trail haikuwahi kukwama katika tope, sio chini ya mara moja nimeziacha Rav 4, Suzuki Escudor na Hiluz Double cabin porini mimi nikapasua katika tope, vumbi na vichaka na sikupata shida yoyote. Pia clearance yake chini ni nzuri na sio rahisi kugonga.

Zingatia service yake, na ukifunga spare ni mkataba mwaka sio kama Toyota spare bei rahisi lakini utabibadili tu mara kwa mara na hutakumbuka mwisho wa mwaka umeingia gharama kiasi gani.

Kwa ealuation zaidi soma hapa: https://www.youtube.com/watch?v=GR7kHC6yiQI

Thanks
 
Ongea kitu kwa evidence dont just talk Nissan yoyote ile spea zake ni ghali na ni kwasababu ukishafunga unasahau thats one two hivi kuna gari ambayo haitasumbua? U will never get one kwani as it goes old itazingua tu, cha msingi ni utunzaji,binafsi ninatumia hiyo extra ila na iko sawa sana ni mwaka wa Pili sasa,by the time nanunua kuna jamaa alikua na yake kwa wakati huo ilikua na miaka mitatu na hana plan ya kuliuza wala kununua gari nyengine,kwahiyo msitoe shuhuda za uongo hapa,wacha mtu afate anachotaka,
 
wadau nataka kununua Pajero ios, naomba wenye uzoefu na hii gari wanipe mazuri na mapungufu yake kwani mimi kwanye tasinia hii ya magari ni mtupu kabisa
 
wadau nataka kununua Pajero ios, naomba wenye uzoefu na hii gari wanipe mazuri na mapungufu yake kwani mimi kwanye tasinia hii ya magari ni mtupu kabisa

Pajero sio gari ya kununua ni full kimeo, labda ung'oe injini uweke ya toyota
 
Forester X20, 2002-2004 Mimi ninayo KM 5 kwa lita, taa kubwa ya mbele 600,000 shock up si chini ya laki 550,000

Sasa kweli ulitaka bei ya spear za subaru zinanane na its au noah?

5km kwa lita hiyo kimeo badilisha plug na oxygen sensor,epuka mafundi wa vijiweni,Spear acha kutuma nenda mwenyewe ili wasikudalalie

Arusha shock up laki 2-3,taa laki 2-3,ukishindwa agiza Nairobi
 
Nime fatilia mada kuhusu u bovu wa nissan xtrail, ukweli ni kwangu nissan xtrail syo mbovu.
Nissan extrail ni service kufanya inayotakiwa ya extrail..na nissan ni vitu vitatu kuzingatia engen oil, hydronic gear box oil zote hizo uweke za nissan, na kuna mafuta ambayo yanapaswa kuweka kutokana na aina ya engen ya gari yako mfano labda mafuta ya kawa aina triple j au l etc.
Inategemea wewe uko katika kundi gani la mafuta yanayotakiwa kuweka.
Oil ya nissan extrail ya hydronic ni 250,000/ mpaka 200,000/
Engen oil nayo sh 70000/
Hiyo garama tu sasa sisi watz wengi tushazoea virahisi rahisi alafu badaye tunaanza lalamika...tunataka miliki vitu alafu kuviendesha hatuwezi.
 
Kingine cha kuzingatia Ktk nissan extrail
Ni lazima Rejeta iwe na maji nissan extrail engen haitakiwi kabisa ku over heat.
Asubuhi kabla hajaingia ndani ya gari check maji
 
Yapi ni magari bora? unanunua used car do you think it gonna be as good as new ones?
do you have really nissani secialist in your local area?
which school did he/she attended?
mie nakumbuka miaka ya 90 kuna mzee wa benzi alikuwa kariakoo na tata alikuwa kwa sokota
 
Back
Top Bottom