Mjadala: Je, ni kweli Magari aina ya Nissan Xtrail ni mabovu?


Mkuu! Kama una hela chukua tu hiyo gari. Achana na maneno ya vijiweni. Spea chungu nzima.
 
Hiyo oil inapatikana wapi mkuu?

There is a special oil for nissan xtrail....sikumbuki jina lake but mafundi wa nissan xtrail wanazijua....

Nilikuwa namiliki Defender Td5 engine, bei ya engine oil yake ilikuwa Sh. 30,000/- kwa lita, na ilikuwa inatumia control box na ikiharibika lazima iletwe diagnosis machine ili itambue tatizo liko wapi; ilikuwa gharama kubwa ikipata tatizo maana nimeshawahi kuvutwa kutoka Kondoa hadi Arusha wakati gari linaunguruma vizuri tu, gia inaingia lkn gari halisogei!

Kwa kuwa wakati nanunua mileage yake ilikuwa 150,000+ niliendelea kutumia oil ya kawaida tu hadi ilipokufa na nikaamua kuweka engine ya kibongobongo Tdi 300; sasa naenjoy driving bila hofu yoyote.

Vv
 
Wakuu nissan xtrail ni maumivu matupu kwa beginners zaidi ya mngurumo na bodi kubwa mengine ni kupeana umaskini ungali kijana
 
Hivi NISSAN tumeanza kuzijua leo jamani,au ndio haya majina yake ya Ziada ndio yanatuahadaa.
Nissan kama una pesa ya mawazo ni gari shida sana,labda utumie mwaka na umtafute wa kumuuzia nusu bei.Na ndio maana wanabadisha miundo kibao.

Na kampuni hii inachofanya ni kuingia mikataba na Serikali za nchi Mbalimbali ili kuuzia Magari hayo katika idara zake mbali mbali,ndio maana watu tunayaona mengi na wengine wananunua kwa kuangali housing.

Hembu kumbukeni wale mliofanya kazi Bima miaka ya 90s,HYUNDAI walikuja na mikopo nafuu sana kukopesha magari hayo kwenye Taasis ya NIC na nyinginezo,kuna walioingia mkenge na wajanja walioulizwa hawakuchukua Mkopo huo.
 
Hivi NISSAN tumeanza kuzijua leo jamani,au ndio haya majina yake ya Ziada ndio yanatuahadaa.
Nissan kama una pesa ya mawazo ni gari shida sana,labda utumie mwaka na umtafute wa kumuuzia nusu bei.Na ndio maana wanabadisha miundo kibao.

Na kampuni hii inachofanya ni kuingia mikataba na Serikali za nchi Mbalimbali ili kuuzia Magari hayo katika idara zake mbali mbali,ndio maana watu tunayaona mengi na wengine wananunua kwa kuangali housing.

Hembu kumbukeni wale mliofanya kazi Bima miaka ya 90s,HYUNDAI walikuja na mikopo nafuu sana kukopesha magari hayo kwenye Taasis ya NIC na nyinginezo,kuna walioingia mkenge na wajanja walioulizwa hawakuchukua Mkopo huo.
 
SECRETE we ndo umetoa mpya ya huyo kaka yako. Kanunua xtrail bodi tu hapo. Maana kama kafunga engine ya rav4 si bora angenunua rav4 kimoja?
 
Mmmmmmmmmmmmm! mbona mimi ninayo hainisumbui? Tena yangu ni Manual Transmission ila ni yaa Mjerumani iko poa sana kwa kweli. Labda hizo za Mjapani ndo zinasumbua.
 
Gari za kiume ni vw golf hapo utakua na gari mjapan anaboronga sana
 
kinachopelekea nissan kusiwepo na spea feki nini wakati toyota kampuni kubwa pia spea feki kibao?
 
katika gari vimeo basi toyota, nissani patrol mie ninayo nilinunua tabora mwaka 2000 lakini mpaka leo hii inadunda tu na ukiiona ni kama mpya....tatizo watu wengi mnalialia coz nissani haitaki spea feki, sijui unaambiwa filter 40,000 wewe unasema unataka ya 7,000 hapo nissani lazima ikushinde tu.........kwa mjapani gari ya maana ni nissani, toyota landcruiser, honda basiii, zaidi ya hapo nenda tu kwa mjerumani, muingereza na mmarekani ndio wanaojua kutengeneza gari......hila hizi zilizojaa bongo ni basi tu umasikini eti mtu anamiliki vitz, ist, platz, alaf anakalazimisha december aende nako mwanza kutoka dar alaf kakimfia analalama
 
Swali: unaitambuaje spea feki? Mimi zaidi ya kukanyaga mafuta kwenye vitz yangu sina ninalojua zaidi
 

Kinachozungumzwa hapa ni gharama ya kuhudumia x trail kwa mfano unaishi maeneo ya kigonsera ,kakonko,chemba,tandahimba,nanyumbu hiyo oil ya x trail utaipata wapi alafu bush lake laki mbili ki ukweli x trail inagharama mno hilo gari haliihitaji hela ya mawazo hata fuel consumption yake iko juu ni zaidi ya gx 100 six cylinder
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…