Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

ha ha ha hata hizo sambusa alikopa. angekuwa kwetu wa kwetu angechezea vitasa hapo hapo
 
Hicho kipande cha maneno ya muoaji kimenichekesha sana.....Tuwe na utamaduni wa kutoa bila kutaraji kitu, chukulia kama umewasaidia maharusi au uliyempa.
 
mi nshagakataa kutoa michango inayozidi elfu kumi na tano. Nampa mtu kama sadaka hata nsipoenda harusin siumii sana. Ujinga sana mtu anakuchangisha elf hamsin na kuendelea alafu huduma zero. Watu wanachangsha hela za harus wanaenda kufungua biashara, kusoma masters etc.
 

Ha! Ha! Ha! Nyambaf mmezoea mkichanga mnataka mje kula hadi kusaza halafu baada ya shughuli maharusi wanalala na njaa. Big Up sana bwana Harusi hiyo michango kaanzie maisha.

Tatizo wabongo mkiambiwa mchangie mambo mengine mnakuwa wazito lakini harusi aah fasta mkono mfukoni hiyo ndio dawa yenu.
 
kwani michango huko ulipo ni lazima? mi huwa sichangi hata nikipewa kadi labda awe ndugu wa karibu sana.
 
Tuliwahi kuchangishwa ofisini hivyo hivyo kwa mkwara mzito, halafu ofisi nzima kadi ya mwaliko akapewa mtu mmoja eti atuwakilishe wote, kisa ilikuwa imepangwa bwana harusi apewe zawadi ya gari!
 
hongera tumejua una kabati languo na koti la suti sjui na suluali yake unayo au? mi nampa hongera hiyo hela akaanzie maisha
 
tatizo lako huna subira.
mpago mzima upo siku ya kuvunja kamati wee subiri mualiko tu utapenda.
 
usiombe mtoto wa boss ofisini ndio awe anaoa utajuta maana kuna watu kwa kujipendekeza kwa boss hutoa hata laki 5 ya mchango...
 
Hahahahahahahahaaaa!!!!!!! michango hii itatuua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…