Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Najua kwamba kutoa ni moyo na sio utajiri ......... na Waa Tanzania kuchangiana ni jambo la kawaida katika shughuli mbalimbali za kijamii ...... sio siri upande fulani inaumiza lakini kukwepa pia inakuwa vigumu .......Jamani kumbe hii michango mbalimbali tunayotoa ukiijumlisha kumbe ni balaa hebu angalia yaliyonisibu tangu januari hadi sasa na bado
  1. Michango kwa ndugu zangu 300,000
  2. Michango kwa marafiki 200,000
  3. Michango kwa ninaofanyanao kazi 150,000
  4. Michango kwa ninaosali nao 200,000
  5. Michango ya ndugu wa mke wangu 200,000 ,,,,,,,,,, hapa imevuka 1m
 
Wewe wakati unafanya wedding ulichangiwa kiasi gani ???Na vipi baa ulishapiga hesabu uliacha kiasi gani kwa mwaka huu
 

Pole sana nilikuwa nalitafakuli hili last week. Sikuweza kutunza records zote, ila so far yangu ni kama zaidi yako. Mmoja kataja mbuzi sijui wangekuwa wangapi hapo.
 
Mimi nilichanga zaidi ya 1m kabla sijaoa. Nilivyokuja kuoa nilichangiwa 2m. Sasa sitaki michango.
 
Natakunguliza samahani kama hoja hii imeshawahi kujadiliwa humu jamvini.

Suala la michango ya harusi linazidi kuwa tanzi kwa jamii ya Tanzania. Unakuta ndani ya mwezi mmoja una kadi tano za kuchangia na usipochanga watu wanakununia. Ombi linageuka kuwa haki.

Ninachoomba tujadili ni je ni lazima kutoa michango ya harusi, kwa wenye uzoefu wa nchi zingine wenzetu wanafanyaje linapokuja suala la gharama za harusi? Je ni lazima kufanya tafrija kubwa baada ya ndoa?

Naomba kuwasilisha
 
Ngoja na mimi nikishaolewa tu ndo ulete hii mada hapa, nimechanga sana sana mpaka nachanganyikiwa na hapa nina kadi 5 ndani kwa mezi huu na 4 tu. sasa subiri na mimi waje wanichangie zen ndo tujadili ilihata kama wataacha au kupunguza na mimi niwe nimeshafaidi
 
sioni sababu ya kusumbua watu! unaeoa/ kuolewa ni wewe. mimi naona ni ujasiliamali mpya. hata ikekuwa vyema kama wangekuwa wanadumu kwenye ndoa zao. mchipuko kibao! huwa nasikia vibaya kuona mtu niliye mchangia anachipuka.
 
Michango ya sikuhizi inataja kiwango na kutoa deadline.....kama michango yenyewe ni hiari hilo sijui. Ninachojua ni kwamba sherehe ni watu na watu lazima wale, wanywe n.k ambavyo ni gharama.

Changia rafiki wa karibu, ndugu au jirani ili mujumuike kufarahi pamoja. La kama unataka kuchangia kila mtu hapo tatizo ni la kwako.
 

Unachanga elfu 50 halafu siku ya sherehe unaenda kukutana na juisi ya Azam ya kopo
 
Aiseeee,

Utafiti usio rasmi unasema kwamba ndoa nyingi huvunjika kirahisi rahisi (maamuzi mepesi ya kuachana wanandoa) kwa kuwa moja ya sababu ni kuwa wanandoa wanasahau kwamba walichangiwa ( hawana uchugu na hela zilizotekea kufanya harusi yao). Hii tabia ya kuchangishana mpaka makazini maofisi harusi ya jirani yako inakera sana. Mtu anakuletea kadi ya mchango ofisin eti mtoto wa mjomba/shamgazi yake anaoa/olewa. Mfyuuuuuuuuuuuu

Binafsi michango ya harusi nilishaachaga kuchanga tokea 2012. Kwahiyo sitegemei nichangiwe kwa chochote kile ! Msiba mchange 10,000 halafu eti harusi unaongeza sifuri moja(100,000). Kama una tabia hiyo wewe ni mujinga na uchomwe moto.
 

wazo zuri
 
Da hii thread imedumu.2010 watu wana share hadi 2015.hakika ilikuwa nyeti.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…