Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

JPM anadaiwa viwanda. Hayo mengine ni kutaka kumfanya aonekane anafanya kazi kumbe hakuna lolote. Kwani michango ya harusi ilikuwapo kwenye ilani ya uchaguzi ya sisiem? Viwanda na flyovers ndio level yake, haya ya harusi hata serikali za mitaa zina nguvu ya kuzuia.

Hata hivyo, wanaochanga na kuandaa sherehe hawavunji kipengele chochote cha katiba, na sijui kuna tofauti gani kati ya anayechangia sh. 100,000/= za sherehe kila mwezi na anayekula kitimoto au nyama choma ya sh. 5, 000 kila siku kwenye baa.

Tuachieni tujumuike maukumbini, ninyi endeleeni kujenga viwanda na flyovers kwenye majiji
 
Kuna tofauti gani kati ya anayechangia sh. 100,000/= za sherehe kila mwezi na anayekula kitimoto au nyama choma ya sh. 5, 000 kila siku kwenye baa? Mbona wewe unahonga zaidi ya iyo michango ya sherehe?

Sherehe inaonyesha umoja na mshikamano, kama umeamua kuwa kivyako sio lazima uchangie
 
Kuna tofauti gani kati ya anayechangia sh. 100,000/= za sherehe kila mwezi na anayekula kitimoto au nyama choma ya sh. 5, 000 kila siku kwenye baa? Mbona wewe unahonga zaidi ya iyo michango ya sherehe?

Sherehe inaonyesha umoja na mshikamano, kama umeamua kuwa kivyako sio lazima uchangie
Ulitakiwa umuulize anayepinga sherehe. Mi ndo kwanza namalizia kikao cha harusi hapa Kilimanjaro Pub
 
JPM hajalipa mishahara mwezi huu.Yaani aache kufikiria wapi akope hela za salaries aanze kupiga marufuku michango ya harusi?
 
Pia muda wa kula unachelewa sana. Tunakula saa 6.

Pia bia ziuzwe humo humo ukumbini.
 
Naunga mkono hoja.Futa michango.Sherehe ziwe ndogo.Kuhusu muda iwe mpaka asubuhi.
 
Nakubaliana sana na mtoa mada ila sio kwenye kufutwa. Nafikiri serikali kupitia wakuu wa wilaya ipate idadi rasmi na hadhi ya kumbi zote ambazo zinatoa fursa ya hizo harusi. Kisha iratibu zoezi zima la utoaji wa vibali vya sherehe.

Hapa serikali inatoza kodi kwenye kila kibali kitakachotolewa kwa ajili ya sherehe husika. Mathalani inaweza kuwa ni 15% ya gharama za sherehe zote zinazoanzia 5 to 15 milion then 25% kwa zote zaidi ya 15 milioni.

Watajuaje gharama za harusi? Hapa itakuwa ngumu kidogo lakini wakijitahidi wanaweza licha ya kuwa mapungufu ya hapa na pale yatakuwepo. Aina za kumbi za sherehe, sehemu vikao vinapoendeshwa, ni vigezo muhimu. Katika kila harusi ni muhimu afisa ustawi wa jamii ashiriki(hii pia ina changamoto zake, haswa rushwa) ili kujua uhalisia wa gharama.

Kwa mazingira hayo harusi zitakuo ghali, serikali itapata mapato na usumbufu utaongezeka vitu ambavyo kwa pamoja vitatufanya kufikiri mara nyingi zaidi kabla ya kukimbizana na hizi sherehe zisizo na tija.
 
Harusi huwa ni jumamosi unaamkia kazini na uchovu jumapili???

Cha muhimu hapo ni hiyo michango kwa watu masikini iangaliwe namna ya kupunguzwa kbs.

Harusi sio lazima iwe jumamosi mkuu, inaweza siku yoyote mnayopanga ninyi
 
Kwa wanaokumbuka, miaka ile ya themanini, halusi na sherehe zingine zilikuwepo, lakini ziliendeshwa tofauti na sasa hivi. Familia ya wahusika iliandaa sherehe, watu walialikwa bila kutoa michango,mwalikwa ulichotakiwa kufanya ni kuandaa zawadi.Kwa sababu hiyo, mahalusi walipata zawadi za kutosha na mtu hakutakiwa kutoa pesa kabisa.

Kamati za maandalizi ya sherehe zimekuwa dili,kuna watu kila anapoamka asubuhi anajiandaa kuongoza vikao vya halusi,mtu anaongoza vikao zaidi ya vitatu kwa siku.Asilimia kubwa ya michango ya halusi huwanufaisha wasiokusudiwa.Badala ya kuwaweka watu pamoja,sherehe zimeongeza mipasuko,matumizi mabaya ya michango huwa chanzo cha migogoro.

Nimeshuhudia vituko vingi baada ya sherehe,kuna sherehe ambazo wahasibu hukimbia na michango,kuna zile ambazo kamati hutoa tenda kwa watu dhaifu na hulipwa pesa nyingi mno,kuna sherehe ambazo mtu anachangia 100,000/-lakini anapata soda moja na bits basi wakati zawadi ya kamati ni 500,000/-huku baadhi ya viongozi wakivimba mashavu.

Sherehe nyingi, hasa halusi hufungwa usiku sana, hivyo mgeni mwalikwa analazimika kuandaa bajeti ya usafiri.Ili kurejesha dhima ya sherehe kuwa ni furaha na amani, upo umuhimu wa kurudia utaratibu wa miaka ya nyuma.Hakuna kamati ya maandalizi,sherehe inaandaliwa na familia,waalikwa mnatoa zawadi tu, na sherehe zote zinaisha kabla ya saa kumi na mbili jioni.

Nisisitize hapa,tunajadili sherehe,sio misiba,msiba ni tukio la dharula wakati sherehe huandaliwa. Ni muhimu na ni lazima kushiriki misiba kwa hali na mali lakini sio sherehe za harusi na nyinginezo. Naomba tena waziri atakayekuwa anasimamia ustawi wa jamii aingilie kati, atafute namna ya kukomesha tabia hii inayoanza kuwa kero katika jamii.
 
wengine wanachangisha waoane tu kuondoa gundu huku wanajua ndoa yao haitadumu mwaka, kadi walokupa haijapauka washa kuwa mabachela
 
Msituingilie uhuru binafsi maana naona sasa tutapangiwa hata idadi ya bia kwa wiki, tutaambiwa usinywe Cinzano au amarula ni kuharibu pesa, mara usinunue hiki na kile ni anasa na vimaudhi kibao.

Hakuna aliyelazimishwa kuchanga.... ni makubaliano na ukiamua kuacha unaacha kivyako vyako.... pesa yangu binafsi nina uhuru wa kuitumia nitakavyoo!
 
mimi labda kuwe nasheria wa wale wanaotulazimisha kuchangia ...yani kama deni vile hatupumui kabisa
 
Tatizo lako kwanza unashindwa kutofautisha kati ya ndoa na harusi, jambo la muhimu zaid ni ndoa ambalo hutanguliwa na kulipa mahari na kutangaza uchumba then kutamka kiapo cha ndoa kanisani, kwa sheik au kwa mkuu wa wilaya, harusu ni sherehe baada ya ndoa ambae mwamuzi ni wewe na mwenzi wako, kwa hiyo sio lazima ufanye kitu kikubwa sana, inataegemea wewe umejipanga vp.
 
Back
Top Bottom