Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Katika dini ya kiislam ww unaingia kwenye kundi la wanafiki. Wanafiki wana sifa kuu tatu, mojawapo ni Akiahidi Hatimizi ahadi. Jiepushe na ahadi. Wambie watu kuwa nikipata fursa nitachangia kuliko kutoa ahadi.
Hayo majibu nimetoa sana lakini watu bado wanang'ang'ania basi naishia kuwambia sawa.
 
Hayo majibu nimetoa sana lakini watu bado wanang'ang'ania basi naishia kuwambia sawa.
Ni kweli wakati mwingine watu hawa wanakera maana wanatuma sms kama vile anakudai. Anakufuata hadi ofisini kwako kukumbushia. Mimi sasa hivi nimeamua mtu akija akinipa kadi naweza nikapokea nikaitia kwenye droo au nikiamua namwambia tu kuwa huwa sichangii harusi na sherehe nyingine. Kama ana mgonjwa akikwama anifuate nitakuwa tayari kumsapoti.
 
Hili ni jipu kubwa sana kwa sasa. Ningefurahi kama serikali ingepiga marufuku. Na ndio maana ndoa nyingi zinavunjika. Jitu linachangiwa kuoa, unakuta limekopa na gari then linakopa na kujenga... Baada ya hapo maisha yanaanza kuwa magumu. Mwanamke anadhani zile pilika pilika za harusi ni kila siku maisha yanakuwa mazuri.

Unakuta vitu vya ndani mnapewa na kamati kutokana na michango ya watu. Mkiingia ndani mnaona hii siyo.....

wengine waliochanga huwa wanapenda kurudisha gharama zao hivo wanaanza kumuwinda bibi harusi.

Fanya kitu unachoweza. Kilicho ndani ya uwezo wako, sio kutaka kufanyia honey money huko serengeti SERENA. HOTEL ambayo huwezi kwenda kwa mfuko wako.
 
Inabidi tubadilike, mwenye awe harusi yake awe na zaidi ya 50% ya budget ya sherehe yake ndiyo aje kuomba mchango, ni jambo la kipuuzi kabisa unakuta eti mtu ana chini ya 5% ya budget ya sherehe, iliyobakia eti anategemea achangiwe. Hivi ukifanya sherehe ya watu 50 tu (na wewe na bi harusi inclusive) hiyo haitakua ndoa?kuna haja gani ya kupanga kufanya sherehe ya watu 300 wakati hata sherehe ya watu 100 inakushinda? Tutaendelea kupenda ufahari hadi lini?
 
Habari ya leo wadau,

Hivi hii issue ya kuchangishana hela ili watu wafanye sherehe kuuuuuubwa ya harusi itaisha lini? Jamani zama zimebadilika hivyo yatupasa hata na sisi tubadilike pia, hali sasa hivi ni ngumu jamani si utani, mbaya zaidi unapangiwa kabisa kuwa kima cha chini ni kiasi flani cha fedha, tunatafutana ubaya ujue, ifike mahali furaha yako isiwaumize wengine.

............

Hapa sasahivi tayari nina kadi za mchango 8 mpaka wengine hata siwafahamu, sasa najiuliza nitamchangia yupi nitamuacha yupi.

Nawasilisha.

Agreed agreed
 
Habari ya leo wadau,

Hivi hii issue ya kuchangishana hela ili watu wafanye sherehe kuuuuuubwa ya harusi itaisha lini? Jamani zama zimebadilika hivyo yatupasa hata na sisi tubadilike pia, hali sasa hivi ni ngumu jamani si utani, mbaya zaidi unapangiwa kabisa kuwa kima cha chini ni kiasi flani cha fedha, tunatafutana ubaya ujue, ifike mahali furaha yako isiwaumize wengine.

Kama issue ni kufunga ndoa wewe nenda kwa Mchungaji/Paroko mueleza azma yako ya kufunga ndoa hivyo andaa fungu lako kodisha mapaparazi/wapiga picha tafuta sehemu tulivu ambayo mtaenjoy na baadhi ya mashuhuda, maliza mchongo bila kuwapa watu stress, kwa kufanya hivyo utakuwa umeepusha ndoa yako na manung'uniko ya watu, maana kama mjuavyo binaadam hawariziki utasikia mara oooh! pamoja na kuchangishwa fedha nyingi sherehe yenyewe ilikuwa na mapungufu kibao.

Hapa sasahivi tayari nina kadi za mchango 8 mpaka wengine hata siwafahamu, sasa najiuliza nitamchangia yupi nitamuacha yupi.

Nawasilisha.

Mkuu ulichoo leta jukwaan ni suala ambalo kwa kweli inabidi tubadilike. Inabidi watu kuandaa budget wanayoiweza na kufanya sherehe Yao Hii biashara ya kusumbuana Mara double elf 70 single 50 sio nzur kwa kweli: ndo maana mm nishasema sku ya harusi ni kadi ya mwaliko tu na hakuna ya mchango wala nn: utakuta watu wanacgangisha ml. 10 kwa mfano kwa ajili ya sherehe na wanatumia zote afu wanaenda kuanza maisha hawana kitu no bora hizo Pesa wangeweza hata kununua kiwanja au wakapata mtaji
 
Hao jamaa hata usipokuwa nchini, watatafuta namna tu wakutoe kiasi. Hawana aibu wala pride hata kidogo linapofika suala la kuzidai hizo. Mi ikifika zamu yangu, nta-demand from my old folks tu, wengine njooni na zawadi. Please return the favor.
Mpendwa fanya fanya uoe aisee.. haiwezekani mtunza sadaka huja"wowa"
 
Kweli kwa hali ya sasaivi kila kukicha mahitaji yanaongezeka na mishahara ipo pale pale,mimi nililetewa card ya harusi mchango laki5 au kuna list ya vitu uchague ukanunue ulete,fridge,cooker,kuweka mapazia,Sofa tena wamekwambia
ukisha chagua watakuelekeza wapi ukanunue,na hao watu hata wenyewe hawapikii gas wanapika na mkaa
nikasema wanatukomoa kila aliepewa card ya mchango wa hiyo harusi walisema mie ntakua nje ya nchi,wengine
sijui watakua makazini,nikasema ivi mtu unampa kiwango cha mchango atoe kwani ni harusi yake?
Hahahaah hao wametisha aisee....
 
Tuweke vyama vya kusaidiana kwenye harusi kama tunavyofanya kwenye vyama vya kusaidiana kwenye msiba, kuwe michango fixed kila mwezi na kiwango ambacho ni flat rate atakachopewa atakakapokua na sherehe.
 
Acheni ubahili hebu changieni...

Hamjui mnachangia hata mapato ya serikali kwenye kodi

Mnachangia ajira za mc, caterers, waiters, magari, mapambo, keki, ndafu, maduka kwa zawadi???


(Ila mimi msinichangishe nilishaacha kuchangia)
 
Mbaya zaidi hata wanaoishi na wanawake na wana watoto nao wanaitisha vikao wanapotaka kupasha viporo vyao !!
 
Habari ya leo wadau,

Hivi hii issue ya kuchangishana hela ili watu wafanye sherehe kuuuuuubwa ya harusi itaisha lini? Jamani zama zimebadilika hivyo yatupasa hata na sisi tubadilike pia, hali sasa hivi ni ngumu jamani si utani, mbaya zaidi unapangiwa kabisa kuwa kima cha chini ni kiasi flani cha fedha, tunatafutana ubaya ujue, ifike mahali furaha yako isiwaumize wengine.

.
Teh!
 
Chuki yako ni kwa pombe sio michango, hizo pombe ndo zinalipa kodi, ndio mcjango mkubwa kwa bajeti, na hayo masoda mnayokunywa kama maji ya sumu kiasi gani?

Pole sana mlevi
 
Back
Top Bottom