Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

nilishaacha siku nyingiiiiiiiii kuchanga, tena wasivyo na adabu wameweka na viwango!! ndio kabisaaaaaaaa, yangu yakinikuta nitajua mbeleni! ila kwa sasa hell no! imekuwa ni business, unajikuta u spend a lot kwenye hii makitu!
saa hizi tuko busy na kuchangia huduma za afya na elimu kwa wasio na uwezo.
Karibuni wana JF kwenye movement yetu
 
Sijawahi kuwa na utaratibu wa kuchangia harusi, ukiwa na shida nyingine your mostly welcome, wabongo wanapenda sana sifa za kijinga, unajua huna uwezo fanya kile chenye uwezo wako, usipomchangia ndo ujue umeshakuwa adui yake na kukununia juu.

mkuu naomba nichangie ada ya mtoto ya shule hata laki2
 
mkuu naomba nichangie ada ya mtoto ya shule hata laki2

Wa kike?? Nna kidume changu nianze kukiwekezea akimaliza la saba tunachukua mwali wetu

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Hoja yako nimeependa
sana.

Kweli kuna watu wanatoa taarifa ndani ya muda mfupi. Mfano Mwezi mmoja
au miwili. Hapo usipomchangia anakuja leta lawama kibao.

Pia kuna wengine wanapanga kufunga ndoa miezi ya Dec, Jan, na february.
Kwa kweli miezi hii haijakaaa vizuri kwa michango ya harusi.

Mwezi Dec. ni maandalizi ya sikukuu ya X-mass pamoja na ada za watoto
shuleni.

Mwezi January pale bado tunachakalika na ada.

February tunalipa madeni tulikokopa ili kulipa ada za watoto.

Hivyo mimi binafsi miezi hii mtu akiniletea adi au kunialika kikao cha
harusi itakayofanyika miezi hii, najua huyu ananitafuta ubaya tu.



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!

Umenikumbusha. Jirani yangu pua na mdomo jana kaleta card ya mchango kawaachia watoto,harusi 18 jan. Nahisi ananitafuta undani tu na kutangaziana ubaya.
 
liwalo na liwe wakisema nimejitenga shauri zao. watoto zangu wakija kuoa au kuolewa nitajipinda na mume wangu kitu gani bwana kwanza siku hizi tunasimplfy sio misherehe kidinner tu cha kiushkaji cha kusema nendeni kwa amani ikiwezekana vinywaji tu na kugonga chiazzzzzzzzzzzzzzzzz halafu wanaenda zao katika fungate watakalokuwa wamejiandalia wenyewe kama hawajaandaa basi wataenda zao kwao kulala.
 
kati ya wale niliowachangangia mimi ni asilimia 5 tu ndio waliokuja kunichangia. hivyo basi wanaochanga eti kwa sababu na wao watakuja kuwachangia itakapofika siku yao nawapa pole sana. sio wote watafanya hivyo. bora usave visent vyako kwa mambo ya msingi zaidi.
 
kati ya wale niliowachangangia mimi ni asilimia 5 tu ndio waliokuja kunichangia. hivyo basi wanaochanga eti kwa sababu na wao watakuja kuwachangia itakapofika siku yao nawapa pole sana. sio wote watafanya hivyo. bora usave visent vyako kwa mambo ya msingi zaidi.
Ni kweli, mwenyewe nilibaki kinywa wazi maana wote niliowachangia hasa classmates ukiachilia mbali ndugu wa karibu hakuna hata mmoja aliyenichangia. Mtu anakuahidi lakini mwishowe anapotea. Bila kuwa na hela yangu mwenyewe ningetia aibu.
 
Kwanza kabisa, wakuu hongereni kwa sherehe za miaka 49 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar! Pili, nitangulize samahani iwapo nita-sound vibaya kwa baadhi yetu kwani binadamu tumeumbwa tukiwa na mitazamo tofauti ktk masuala mbalimbali.
Leo nazungumzia juu ya MICHANGO YA HARUSI, hasa za siku hizi, nalisema hili bila kumung'unya maneno, utakuta mtu yuko Lindi, na wewe uko Mwanza, anadai kakuweka kwenye kamati kuu ya harusi yake na hivyo kadirio la chini utapaswa kuchangia Tsh. 100,000 na itakubidi uhudhurie sherehe hizo Lindi ukitokea Mwanza! Piga picha, utakuta mtu mwenyewe ulikutana nae Advanced Level miaka minane iliyopita na wala haujakutana nae tena zaidi ya kuongea naye kwa simu kwa interval ya mara moja kwa mwaka huku mkikumbushiana yalopita!
Harusi imekaribia utapokea sms mara tano kwa kutwa unakumbushiwa juu ya mchango wako! Usipotoa atanuuuuuna, atakuseeeeema.....! Hii imekaaje wakuu?
Naomba kuwasilisha.
 
Ni tatizo kubwa. Unajikuta una kadi 5- 10 eti mchango wa harusi na send off. kazi kweli kweli
 
vitu vingine kuingizana umaskini tu,yuko Lindi anakudai mchango halafu hata sio rafiki kihivyo,amua mwenyewe ukimpa sawa ukimnyima sawa. Halafu kashakupangia kabisa kima cha chini laki moja we ulishawahi kuomba mchango kwake?
 
Mee too inanikera xana nina kadi 4 za workmates wanasema najiwekea hazina ya wachangiaji kwenye harusi yangu while marriage is not on my life plan list
 
Amua tu mkuu, weka msimamo, na isikusumbue watu wengine watakuonaje.Nikupe mfano, mimi hiyo biashara ya kuchangia harusi nilishaona haifai ..... nimeiacha siku nyingi sana .....sichangii, saaaana nikiamua kukupa mchango ni shilingi za kiTanzania elfu ishirini tu. Sababu ni kuwa siamini ktk dhana hiyo.Nachangia mambo mengine ya muhimu na maendeleo zaidi.Ila kama na wewe unaamini na unategemea kuwa utawahitaji waje kukuchangia harusi yako siku zijazo ............
 
vitu vingine kuingizana umaskini tu,yuko Lindi anakudai mchango halafu hata sio rafiki kihivyo,amua mwenyewe ukimpa sawa ukimnyima sawa. Halafu kashakupangia kabisa kima cha chini laki moja we ulishawahi kuomba mchango kwake?
Wala mie sikuwahi kuchangisha mtu! Mimi na mke wangu tulikubaliana tusisumbue watu, tukamaliza kwa gharama zetu!
 
Mee too inanikera xana nina kadi 4 za workmates wanasema najiwekea hazina ya wachangiaji kwenye harusi yangu while marriage is not on my life plan list

Hazina? Kwani wewe huwezi kujiwekea hazina? Ama ndo utapeli huu?
 
Wala mie sikuwahi kuchangisha mtu! Mimi na mke wangu tulikubaliana tusisumbue watu, tukamaliza kwa gharama zetu!

mpotezee avimbe mpaka aburst,tuone kama bila hiyo laki moja ndoa haifungwi.
 
Halafu kuna watu ukiwauliza 'kwa nini msifanye harusi ndogo tu ambayo haihitaji mamilioni ya pesa' wanakushangaa.[/QUOTE
Ok, wanakushangaa! Wakati hata hizo ndoa zao za mamilioni zikidumu sana, mwaka! Hii laana?
 
Mbaya zaidi wanaweka masharti, mfano utaambiwa double sh. 50000/=
Single 30000/= inakera mnoooo,
 
Back
Top Bottom