Mjadala kwa wanaokubali kuoa (Ndoa)
Bila shaka mu wazima wa Afya, basi tumshukuru Mungu hata tukiwa si Wazima pia.

Lengo langu kuandika 'Uzi' huu ni kuwahasa na kuwasihi vijana wenzangu ambao bado hatujaoa, kuwa makini na maneno/mawazo/mashauri 'Mabaya' ya watu 'Waliotoswa' na ndoa.

Ndugu zangu; kwa kawaida maisha hayana furaha, uwe umeoa ama hujaoa, ukiwa peke yako shida, ukiwa na mwenza shida, ukiwa na watoto shida na usipokuwa nao pia.

Vile vile maisha ni furaha, ukiwa peke yako raha, ukiwa na mwenzio raha, ukiwa una watoto raha na usipokuwa nao raha; Namanisha kuwa, hakuna neno moja kuhusu jambo lolote. Hata bahati mbaya ina uzuri wake.

Hakuna dunia hii mahala pazuri kama 'Nyumbani' simaanishi lile jengo, namaanisha zile 'Hisia' ambazo kimsingi zinajengwa na Familia, haya wenye pesa na wenye nguvu Ulimwenguni wanafanya maamuzi mengi huku wakiwa wamevuta kamba zao upande wao yaani kwenye "Familia zao".

Usikatishwe tamaa na watu walioacha ama kuachika, na hata wewe ukifanya maamuzi ya kuacha ama kuachika juwa kwamba huyo ni wewe na Moyo wako, usiwakatishe tamaa na wengine. Wape Moyo, kuwa sehemu ya nguzo yao.

images%20(41).jpg


"Familia" ni Upendo, familia ni furaha familia ni baraka, Mungu hubariki Familia zaidi kuliko chochote, labda ndio mana Wayahudi, Wazungu na Waajemi wamebarikiwa zaidi kuliko sisi, kwa sababu, Shughuli zao nyingi wamezikabidhi kwa 'Mungu' kupitia Mikono ya Familia. Ila, taasisi inayosimamia Familia ni "Ndoa" Yes, ni Ndoa.

"Ndoa na Iheshimiwe na Watu wote" Kwa maana Mungu hubariki maamuzi ya taasisi hii, Kama Mungu ni Upendo, na Familia ni Upendo, Kwanini Mungu asikae kwenye "Familia"?

Oa, ikifika wakati unataka na unapaswa kuoa, Oa, usikatishwe tamaa na watu aidha kwa 'Kutumwa' au kwa kufanya kwa 'Kunuwia' wanapiga vita ndoa.

Kama ni Muumini, kumbuka Shetani alipiga vita Ndoa ya kwanza pale Edeni, ndio mana ilikuja kuwa chukizo kwa Mungu, lakini kwa Kuwa Mungu aliilinda "Ndoa" miaka mingi baadae, Shetani akashuhudia 'Familia' yenye nguvu zaidi Ulimwenguni, nayo ni Yusufu, Maria na Yesu, kupitia Herode Familia hii ilitafutwa lakini kwa Mapenzi ya Mungu, dunia ilikombolewa.

Ndoa ipo kwenye vita hata leo, simama, kuwa na busara, songa.
images%20(69).jpg
 
Hii mada ya kuoa na kutooa inatrend sana aseeee [emoji23][emoji23][emoji23] ikifuatiwa na mada za walimu humu ndani.
Turudi kwenye uhalisia anayeona Ndoa inamfaa aende akafurahie maisha !! Anayekataa pia ana sababu zake !
Zamani mara nyingi tulifanya vitu kwa ushawishi wa watu waliotutangulia (wakubwa) ndo maana kulikua na age fulani msichana au mvulana ukifikisha huna mtoto au hujaolewa ilikua inakutatiza sana !! Kwa hiyo wengi waliingia kwenye ndoa kwa mtego huo !! Kwa sasa vijana wengi wamejikita katika kutafuta pesa sana , na tamaa ya mali inakua kubwa kila kukicha sio kwa wanaume hata wanawake pia vigezo ni vingi ! Pia sherehe kubwa kubwa za kusimamisha mtaa.

Pia msiwalaumu kuna Childhood trauma mtoto aliyezaliwa kwenye familia yenye migogoro ya ndoa anaona mama anavyopigwa ,anasikia habari mtaani kwamba Mama alimuua Baba amiliki vitu , anaona dharau anazofanyiwa Baba na mama huyu mtu Ndoa kwake ni kipengele ni ngumu sana hizi trauma za utoto hawazisemi au hawazitambui ila zinawatafuna watachagua sababu nyingine za kutumia kuikataa ndoa ila ukweli unakua moyoni ,Binti amelelewa bila baba , kijana amelelewa na watu tofauti tofauti leo yuko kwa mjomba kesho kwa Babu keshokutwa yuko kwa jirani humwambii habari za ndoa. Mtoto aliyelelewa na mama wa kambo mkorofi anajua ndoa ni kifungo pia

Mwisho mimi nawasupport wanaokataa ndoa kwa hiyari yao , inasaidia pia walio tayari kupata wenzi sahihi kwa sababu walio wengi hawapendeki utajituma vya kutosha umwoneshe mahaba yote lakini yeye hajali kwa baadhi yao ! Wengi ni Sadist .
Inapunguza na vifo [emoji23][emoji23][emoji23] No string attached
Analysis nzuri kabisa. Hongera mkuu. Naona mwisho umeweka na disclaimer kwamba ' no strings attached'..[emoji2]
 
Inayovunja ndoa ni MIMAMA MKWE MIPUMBAVU....inawashika masikio mitoto yao ili itawale na iwe na sauti kwa waume zao.....**PUUUMBAAVUUU......SHEENZIII.[emoji34]
 
Leo kuna mzee aliniambia nakuhurumia sana kijana ukifika umri wa kuoa nakuonea huruma
Akasema wanamke walikuwa zamani sasa hivi kuna majikedume ambayo yanataka kujiongoza
 
Mnaendelea Kufanya uharibifu na kuwapa ujauzito watoto wa watu.

Humu mtu akileta Uzi analalamika kuhusu mapenzi na ndoa utaona comments,

"Kijana kataa ndoa."

"Kimbia ndoa."

"Hakuna kuoa."

"Kindly evacuate, do you copy."

"Mbususu zimejaa."

Mbona hamsemi kataa uzinzi.🤨

Mmekulia familia za single parents? Mbona wengine hapa mmelelewa na baba na mama?

Cha kushangaa Kila siku vijana ndo wanaoongoza kwa kuoa Tena wale wa under 30😂. Mimi naona hizi anonymous ID zinatufanya tudanganyane kumbe Kuna wengine wapo kwenye harakati za kuoa.

Kwa niaba ya wanawake wa JF tunakataa kubeba ujauzito kabla ya ndoa.


View attachment 2452960

NB:: Sijapewa ujauzito ❗
 

Attachments

  • F3FBC2FC-3B67-484C-AC7C-63C3D38398B2.jpeg
    F3FBC2FC-3B67-484C-AC7C-63C3D38398B2.jpeg
    50.3 KB · Views: 4
Back
Top Bottom