MJADALA: Kwanini pale alipo mtu mweusi hali ya uchumi huwa ni tete? Nini chanzo cha umasikini?

Hapo nakupinga Afrika ni kubwa na maendeleo yanatofautiana, kuna nchi za Afrika ambazo ni middle income, mfano Botswana inazidi nchi nyingi tu Asia hata Namibia wanajitahidi pia, hivyo labda uongelee Tanzania yetu ingawaje ni kweli nchi za Afrika ni masikini lkn Kidunia ni nchi chache sana tajiri.
 
Ukisoma historia ya kale sana tunaambia watu weusi tulikuwa watawala wa hii dunia (kemet) watanisahihisha wanaojua zaidi, uingereza, Australia, japan na china waligundua mtu wale zaidi kuwepo kwao alikuwa mweusi ( cheddaman kwa uingereza ).. Yote hayo naona kama yanafikirisha maana kama ndivyo tungewatawa sisi hao watu weupe..

Mimi naamini tuna tatizo namna ya kufiki hili halina ubisha coz kujihisi uko timan haijustify kuwa uko timan kama wengine, UBINAFSI ndio unazaa rushwa na kila kitu( MSD juzi tuu hapa ), pia tuna roho mbaya kwa sisi wenyewe, self hatred nalo tatizo na mwisho ni kucopy kila kitu cha nje kuanzia administration mpaka religions
 
Kaka hata mbio za viwete kuna kiongozi, ata hapa bongo kuna kanda nyingine wana afadhali nyingine hoi so hatufanani 100% ila in general wote ni masikini tuu
 
Hapo kweli changamoto sasa tufanye nini maana hao West walitupatia uhuru. Magu kapambana sana na wara rushwa hadi utamaduni ukaanza kuwa ukiwa mchapakazi una kuwa rewarded. Mama kaja na uendeshaji mwingine kupunguza uonevu maana TRA/DPP nao walikuwa wanakandamiza watu.
 
Kaka hata mbio za viwete kuna kiongozi, ata hapa bongo kuna kanda nyingine wana afadhali nyingine hoi so hatufanani 100% ila in general wote ni masikini tuu

Yeah lkn sehemu tajiri Duniani ni ndogo sana ukilinganisha na masikini, Asia yote ukiondoa visiwa Japan, Korea, Singapore au Taiwan ni masikini pia, South Amerika yote ni masikini pia, Eastern Europe kabla ya fedha za EU walikuwa masikini pia, hivyo don’t be so hard on your self!
 
Nafikiri una maanisha institutions. Tufanye nini mkuu?
Lazima tuwe na mifumo imara,dira na taasisi nzuri zenye usimamiaji wa dhati..

Swala la kuachia uzalendo wa mtu ndo uongoze tutapotea!,watu wanatafuna pesa na wanachekewa tu!. Ifike hatua hata tukiweka jiwe kwenye uongozi serikali iweze kujiongoza maana miongozo mizuri ipo,nidhamu na uwajibikaji.. itoke mentality ya ukipata nafasi basi ukaonyeshe uwezo wako wa kutatua changamoto na sio akili za upigaji.
 
 
Umasikini ni nadharia tu ya wenye malengo yao, kwa uhalisia hakuna umasikini.

Neno tajiri/masikini lipo kama namba sita kutegemea upande uliopo.

Binadamu anaposhindwa kuyatambua na kumudu mazingira yake yanayomzunguka ndipo hapo tatizo linapoanzia.

Jamii ikielewa na kufahamu kutumia rasilimali zilizopo kwa usahihi kutatua changamoto zake hapo ndio ustaarabu unakuwepo.
 
Hapa ndipo inabidi tuwaze kwa kina maana ulichosema hapo ni ukweli 100%
Ukiangalia Haiti issue kwelikweli, Africa si zote lakini asilimia nyingi sana ni shida, yaani mfano Tanzania ni nchi ya wakulima na wafanyakazi lakini hata sisi wenyewe hatujitoshelezi. Ukraini vita njaa Somalia.
 
Hapo sawa kabisa Japan hawana raw material wamewekeza kwenye brain.
 
Uwezo wetu wa kiakili ktk kutatua changamoto zinazotukabili ni mdogo sana.

huo ndio ukweli mchungu.
Hapo ndio tuna feli. Nini shida elimu? au nini? exposure?
 
Umasikini ni kutokujikimu basic needs kwa mazingira yetu Chakula, maji salama, maradhi safi na free of diseases.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…