TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini

Kyakairabwa kunajengwa stendi mbili ya mabasi na hiace za wilayani hivyo watu wote wanaoingia mjini kwa magari watashukia kyakairabwa phase ya pili itakuwa ujenzi wa jengo la wasafiri kati kati ya stendi hizi .route za daladala za kutoka kyakairabwa kuelekea maeneo mengi ya mji ni muhimu sana hasa za kyakairabwa kuelekea mjini ,bandari, kahororo, airport, ihungo na kibeta vinginevyo watu watateseka sana na usafiri
 
Huyo mjamaa anataka kutuharibia Uzi ili ufungwe usionekane tena ni moja ya watu wachache wanaochukia maendeleo ya bk achana nae hivi kweli MTU una akili timamu unasema bandari ya kemondo inaizidi ya bukoba kwa watu na shughuli wakati kemondo hupita tu,halafu unasema magari yote huishia kemondo? Hivyo barabara zisipanuliwe kweli ni ujinga au sio wa bukoba anataka isipige hatua
 
Lazima muisome namba kwa kumpiga chini Kagasheki! Mtavuna mlichopanda! Ukiachilia mbali siasa Kagasheki was better than Rwakatare tena mara kumi ....
 
Lazima muisome namba kwa kumpiga chini Kagasheki! Mtavuna mlichopanda! Ukiachilia mbali siasa Kagasheki was better than Rwakatare tena mara kumi ....
Uzuri wake tunauona kwa lipi alilofanya kwenye kipindi chake????
 
Lazima muisome namba kwa kumpiga chini Kagasheki! Mtavuna mlichopanda! Ukiachilia mbali siasa Kagasheki was better than Rwakatare tena mara kumi ....
Umeanza siasa sasa hayo mambo yalishaisha na watu wa bukoba walishajuta .bil 18 zilipotea hivi hivi kwa sababu ya siasa .siasa hatuitaji huku tunajadili maendeleo na changamoto mbalimbali za mji wa bk after all maendeleo yameshapatikana ndo maana bk unakuwa kwa kasi siku hizi kulinganisha na nyuma na stand inajengwa ,huku soko taratibu za kuwahamisha watu zikiendelea siasa hatuzitaki tena bk
 
Haya endelea na kamanda wenu! Mwafa
Watu wengi wa bk mbona wanamkubali sana na bk maendeleo mbona yanaonekana siku hizi hebu nikitajie kidogo
1 stendi inajengwa
2 barabara ya stendi imejengwa upya
3 barabara za mafumbo,nhc kashai,hamugembe, nk
4 manispaa imekomboa bil 5 kati ya 18 zilizopotezwa na malumbano ya meya na mbunge
5 stendi ya bugabo imehamishiwa machinjioni
6 hayo ni machache tu yaliyotokea kwa miaka miwili tu mkuu acha siasa tujadili maendeleo
 
Mpige kazi asee... mkoa wenu ulisifika kwa elimu... 2017 mmejitahidi ktk hilo! Mjenge kwenu, anzisheni biashara kwenu nk.
Sema nasikia kuna wadada poa siku hizi na asilimia ya waliothirika ni kubwa kidogo/imeongezeka
 
Nini hasa lengo lako mpaka umendika hivi??

1)Kemondo ilijengwa specifically ku-handle wagon-ferries. Inamaanisha wagonferry inatumika kama ro-ro, which means unaweza ku-drive in and out trailer au semi-trailer. Uoni kama ukiweza ku-drive in malori kwenye wagon-ferry unafupisha safari za malori kati ya Bukoba na mikoa mingine?

2)Barabara ya Kemondo-Rwamishenye tayari ni designed ku-accommodate magari makubwa ya mizigo. Ukipenda unaweza kukarabati barabara ya Kemondo-Katoro-Kyaka ichukue magari makubwa (ni fupi kuliko Kemondo-Rwamishenye-Kyaka) hivyo ukawa umeondoa magari makubwa kupita halmashauri.

3)Jiulize ili kuiweka barabara ya Bukoba port/Rwamishenye ichukue magali makubwa ya mizigo itabidi ivunjwe mali ya kiasi gani i.e anza na Bukop, Cocacola depot, Fuel storage tanks, office za ELCT, daraja jipya, - - ni majengo mengi ya kuvunjwa kabla ya kufika daraja la Kanoni.

4)Kwa nini tuhangaike kugundua gurudumu wakati tunalo tayari?
 
I agree, but insist heavy cargo and heavy trucks be relocated to Kemondo.
 
Lakini hata sasa hakuna meli lakini barabara zina magari mengi kwa nini tusiangalie mbele mfano mzr ni rais wetu anatengeneza barabara kubwa na ya kisasa mjini bukoba ili kuhamisha kashozi road kupisha uwanja wa ndege. Halafu isitoshe vitu vingi na wafanyabiashara wakubwa wako bukoba na maduka mengi yapo bk ndo maana custum unakuwa busy muda wote kuliko kemondo .na bukoba ndo kuna idadi kubwa ya watu hivyo bandari ya bk ni muhimu sana na itabidi ifanyiwe upanuzi kemondo ni kipitio tu cha meli meli hutia nanga bukoba sio kemondo .
 
a)Mtu kutukana ni nyumba gani alilelewa.

b)Nikifichua uchinga wangu napata fursa ya kujifunza.

c)Kama uelewa wangu ni mdogo si wewe kama mwema ungenisaidia kuuinua?

d)Sijawahi kuwa mwanasiasa na sitegei maishani

e)Mbuzi wa kisasa wanachungwa kwenye vitalu.

Mwisho jaribu ku-adjust speed yako ya ku-type iendane na ya kutafakari.
 
I agree, but insist heavy cargo and heavy trucks be relocated to Kemondo.
Sisi tunaongelea abiria ndo maana tunaongelea daladala na upanuzi wa barabara kwa sababu ya wingi wa magari na standard ya barabara za mjini.barabara ya rwamishenye kuelekea mjini hadi bandari ni inabidi ipanuliwe maana meli na stendi huleta watu mjini na daladala zinahitajika sio bodaboda na wakazi wengi wa bk wameshaomba hilo
 
Haya endelea na kamanda wenu! Mwafa
Najua unajisikia vibaya sana kuona tunaongea lugha moja ila ndo ilivyo, hatuna la kufanya ili ufurahi. Endelea na hesabu zako nzuri za kutoa wakati sie tunajumlisha
 

Sikutaka kukujibu lakini nimeona nikujibu kwa mifano harisi ambayo iko positive na inayosapoti maono yetu. Unaelewa ni kwanini lile jengo la Tanesco Ubungo pamoja na kelele zote eti litaleta hasara bado raisi alisisitiza livunjwe (kiuchumi)?

Unashindwa kuona mantiki ya kupanua barabara mjini lakini unakubaliana nasi kwamba ni juzi tu raisi kaagiza u/ndege upanuliwe ili kuanza kupokea cargo flights, umejiuliza hiyo mizigo ikishuka ama wakati wa kupakiwa itapita barabara zipi?

Umeshajiuliza kwamba pale custom kuna mizigo kutoka viwandani itabidi kuelekea kwenye hizo cargo flights for export na ushajiuliza itapita barabara zipi ili ielekee huko?.

Nimeona nianze na hayo then tutaendelea, twende taratibu hatua kwa hatua na utupe majawabu na si majibu.
 
Huu mjadala mzuri sana sema unakosa mawazo ya wengi
Hata mi huwa nashangaa watu wanauona Uzi tena ni wa bukoba halafu wanapita tu sijui bukoba nani alituroga yaani watu tunasahau nyumbani kiasi hicho tunahitaji sala nyingi kweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…