TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini



Huo[emoji115] ni mwonekano wa ndani wa stand mpya ya mabasi itakayojengwa eneo la Kyakailabwa.



[emoji115] Mwonekano wa nje wa stand mpya ya mabasi ya kyakailabwa


Huo[emoji115] ni mwonekano wa ndani wa stand mpya ya mabasi itakayojengwa eneo la Kyakailabwa.



[emoji115] Mwonekano wa nje wa stand mpya ya mabasi ya kyakailabwa

Happiness Essau. Nakupongeza kwa kazi nzuri unayoifanya ya kutuhabarisha lakini pia kutukumbusha juu ya kile macho na masikio ya wanakagera wapenda maendeleo wangependa kukiona au kukisikia leo hii.

Kwa masikitiko makubwa inanilazimu niandike hapa asubuhi ya leo hii juu ya miradi tajwa katika mji wetu wa bukoba zikiwa zimebaki siku tano kutimia mwaka tangu wanabukoba walipoamua kufifisha sumu chuki na unafiki vilivyokuwa vimeanza jenga matabaka kutokana na sababu zisizo za msingi hasa ninazoweza ziita uchu wa madaraka.

wana bukoba waliamua kumpa kura Mh. Lwakatare kuwa na madiwani hasa wale waliowaamini kuwa wataweza kaa meza moja kujadili na kulisukuma gurudumu la maendeleo liende mbele hasa baada kuziona siasa zilizokwamisha mawazo na maono ya kuufanya mji wa bukoba ung'are.

Kinachonisikitisha ni ukimya wa wawakilishi wetu katika miradi ambayo kwa sasa imekuwa ndo inasubiriwa kwa hamu ianze kwakuwa inategemewa kuleta sura mpya ya mji wa bukoba. Mh. Mbunge hatoi mrejesho wa nini kinaendelea juu ya maandalizi na utekelezaji wa miradi hiyo.

Mbali na Mbunge tunaye Meya na naibu Meya tena mbao kwa bahati nzuri wote ni viongozi wanaotoka chama kimoja hivyo imani ya wana bukoba ni kubwa kwao kwakuwa hatutarajii msuguano wa kimasilahi katika kutekeleza miradi hiyo.

Swali langu hapa je wanabukoba waendelee kukibeba kimya hiki kwa kutaraji ule usemi wa kimya kingi kina mshindo? Je, kuna namna yoyote ya kuzuiliwa utekelezaji wa miradi hiyo na ndio sababu ya kuwa na kigugumizi kiasi hiki? Madiwani wetu mnaweza kutueleza lipi katika hili?


Mh. Mbunge na baraza zima la madiwani wa manispaa kwanza niseme nyinyi ni watu mna bahati sana na mshukuru sana kwakuwa mgogoro baina ya Mbunge na Meya waliopita umewanufaisha sana kwakuwa hata hiyo miradi tunayolilia kuona ikianza si mawazo bali mmekuta tayari watu walishaibuni na master za miradi hiyo zipo kazi yenu ilikuwa ni kuweka mambo kwenye msitari na kuanza utekelezaji wake.

Inasikitisha sana ukimya huu ambao hatuuelewi ni mgomo wa ndani kwa ndani au ndo yale yale kuwa mlipochaguliwa na kuaminiwa kazi yenu imekwisha?

Bukoba uchuguzi wa mwaka 2015 ndo ulifungua fursa maana wananchi walipata walichostahili lakini binafsi naona kama tumeingia chaka tena chaka baya watoto wa mjini kama wasemavyo watoto wa mjini.
 
Mkuu hatuitaji ushauri wako wa kinafiki, suala hilo nadhani limekuwa addressed kwa wazaliwa wa Mkoa wa Kagera - sasa wewe unajitumbukiza na kuleta hoja zenye kashfa ukiwa na lengo gani?
Wanajikaribisha sijuhi ili iweje na kibaya zaidi ni fitina tu na mambo kama hayo

Wakafie mbele
 
Umekasirika? Wazawa hamna jeuri hio-mna maneno mengi sana na vitendo zero, yaani mpo design yako.
Umekaribishwa mkuu ...good/bad, who invites you?
 
Ukiona unaongea sana na husikilizwi ama unaowaambia hawana mda na wewe njia nzuri ni kufunga mdomo vinginevyo utaonekana zuzu

No one is interested, come on boy.
 
CHANGAMOTO YA UPATIKANAJI WA TAARIFA NA USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI KATIKA MIRADI YA MAENDELEO KAMA INAVYOONEKANA KATIKA VIDEO ZIFUATAZO;




 
Ukiona unaongea sana na husikilizwi ama unaowaambia hawana mda na wewe njia nzuri ni kufunga mdomo vinginevyo utaonekana zuzu

No one is interested, come on boy.
Nadhani ili ni jukwaa huru linalompa nafasi mtu kuwasilisha kilio chake hivyo ni dhairi kuwa sijakosea kuleta hoja yangu kama unahisi ina namna inakukera pita kimya mkuu
 

You can choose wherever as long as Tz is your country, don't complicate things
 

You can choose wherever as long as Tz is your country, don't complicate things
 
CHANGAMOTO YA UPATIKANAJI WA TAARIFA NA USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI KATIKA MIRADI YA MAENDELEO KAMA INAVYOONEKANA KATIKA VIDEO ZIFUATAZO;
Pongezi nyingi sana kwako dada yetu kwa kazi nzuri sana, kwa jinsi unavyostruggle si sawa kuanza kuwabeza wengine lakini kwa hakika unaonesha uwezo mkubwa kwa kile unachokifanya. Kwanzia unavyokusanya habari, kufatilia na hata kuonesha njia. Natamani hata wale wanaohusika na baadhi ya mambo kama utarii hapo mkoani basi wangeungana nawe ama wakajifunza kwako jinsi na unuhimu wa kutumia njia kama hizi za mawasiliano

Hizi picha na kila kitu unachokiweka hapa kinabeba ujumbe mkubwa sana, unastahiri pongezi kubwa saaaana.

Tunaomba ofisi ya mbunge ituweke vizuri katika hili, kwamba miradi iliyotegemewa kuanza ujenzi, eti kupitia serikali imezuiwa isianze kutokana na njama kibao, kuna ukweli katika hili? na je kama si kweli ukweli ni upi na kwanini haianzi mpaka sasa. Hizi picha za michoro tumeshaziona mpaka tumezichoka, tunachokitaka sasa ni kitu harisi.

Narudia kukupongeza Happy, tunaomba uendelee kutuweka wima kila unapopata nafasi nasi tutajibu iwe kwa vitendo ama kwa kuchangia mawazo
 
Shukran sana ndugu Rweye.
Swali lako wahusika wameliona, bila shaka watatoa majibu.....

Inshaallah[emoji120]
 
Shuran ndugu Ntare II
Hoja zako bila shaka zimefika kwa wahusika, natumai watakuja kutoa maelezo na kukuondoa wasiwasi

Inshaallah[emoji120]
 
CHANGAMOTO YA UPATIKANAJI WA TAARIFA NA USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI KATIKA MIRADI YA MAENDELEO KAMA INAVYOONEKANA KATIKA VIDEO ZIFUATAZO;

Ndio maana nikasema nasikitishwa na Ukimya wa viongozi wetu katika miradi hii. kimya chao kinatujengea hisia kuwa haidha haipo au hawaoni umuhimu wa kutushirikisha. Wanatakiwa kufahamu kuwa hapa hatulalamiki kiitikadi bali tuko hapa kuhakikisha gurudumu linasonga mwisho wa siku wote tuushangilie ushindi. Kupaza sauti kwetu kutasaidia kuwaamsha na kukumbuka wajibu wao, ila endapo wataona kukaa kimya ndo suluhisho basi watambue 2020 sio mbali tutawahoji ahadi zao wamezitendea haki au ilikuwa ni "nipe kura nipate kula"
 
Naipenda Bk yangu mitaa niliyochezea komborela sasa haipo kila kitu kimebadilika nahisi nikija Hamgembe nitapata kichaa niacheni nipumzike hukuhuku Lindi[emoji27]
 
Naipenda Bk yangu mitaa niliyochezea komborela sasa haipo kila kitu kimrbadilika nahisi nikija Hamgembe nitapata kichaa niacheni nipumzike hukuhuku Lindi[emoji27]
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] nimecheka

Lindi mnatuzidi nini huko?
 
Wanatuzidi watoto wao kuchezwa ngoma, kuolewa wakiwa wadogo.

Happiness Essau unafanya kazi nzuri sana, tuombe Mungu labda miaka hii mitano Bukoba itapiga hatua kubwa nasi tujisifu huku kwa wanyamahanga.
Hahaaaa.......nacheka[emoji38] [emoji38] [emoji38]

Ila Lindi tusiwachukulie poa, wana korosho.....na umeona jitihada za serikali katika zao hilo, wana zao la nazi (hili si zao la mchezo mchezo[emoji23]), wana matunda kama embe. Na wana sekta nyingne likely to develop km uvuvi. Pia ni karibu na Daslama.......

Lakini pia wana sehemu kubwa za kitalii kama Husuni Kubwa, Songo Mnara, Kilwa Kivinje na Kilwa Kipatimo ambako vita ya Maji Maji ilianzia. Na Wizari ya Maliasili na Utalii inawekeza Kilwa kama kipaumbele chake (Southern Circuit)

Sisi Kagera tunahitaji jitihada kubwa sana kupata pa kusimamia kiuchumi[emoji24] [emoji24] [emoji24]

Ila bwana Lindi wanapenda sana ngoma na kuolewa aseeee[emoji87]
 

Sometimes utani Muhimu. japo kuoa au kuolewa nayo ni maendeleo.
Lindi bhana kwa sasa inaangaliwa kwa jicho la kipekee hasa kama ni mfatiliaji mzuri wa habari nadhani unaona PM anavyopajali nadhani tangu ameingia madarakani ameenda zaidi ya mara tatu hiyo ni ishara kuwa kilio chao kinasikika na istoshe serikali sasa inawekeza nguvu kubwa kwenye southern Circuit kwakuwa pana tija kwa taifa (GAS) na kama uliona jana Engineer wa maji katumbuliwa mbele ya adhara na hii imetokana na wananchi kupaza sauti hivyo Bukoba nasi tukipaza sauti zikasikika tutasonga. na katika kupaza sauti zetu tuanze kuwaamsha hawa tuliowapa ridhaa wakishamka na kusikiliza wakaanza kutenda ndo tupige hatua kwenda juu zaidi.
Pamoja tunaweza.
 
Pia wametoa waziri Mkuu, haipiti miezi miwili bila kufanya ziara ya zaidi ya sikuu saba, na mpaka sasa yuko Lindi kwa siku zisizopungua nne. Korosho zimepanda bei, bodi ya korosho imevunjwa na kuunda nyingine. Nadhani unaona faida walau mkoa/wilaya kutoa kiongozi mkuu wa nchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…