Mjue Jini Mahaba: Fahamu mengi kuhusu jini mahaba

mche mungu tuu vya wanadamu wenye maarifa nao ni majini mahaba wengine au watafuta mali
 
Kaka ila mungu mwenyewe anasema kuwa Quran ni kitabu ambacho hakina shaka wala hakiitaji kukifanyia marekebisho ndio mana kwenye Quran wageni aliwaita kwa jina lao na jinn aliwaita kwa jina lao hvyo tusikosoe Quran au kutafsiri vibaya tutafute wana wa zuoni tuulize kupata majibu yaliyo sahihi
 


Pia Qur'ani sio kitabu cha majini--- Subiani, Makata, nk--- wala siyo kitabu cha kupungia majinni bali ni kitabu kilicho muongozo kwa watu.
 
wewe unapingana na kitabu hicho hicho ambacho kinasema miongoni mwetu kuna vitu wachache tu ndio wamepewa sasa kama wewe hujapewa kitu endelea kuwa looser

Rakims
 
Ndoto zangu nyingi huwa nipuliza pumzia naonaga wanao taka kunishambulia huwa wananguka na wengine hata kufa... au wanakimbia.. so sijui hata ila huwa ndio ndoto zake nyingi. Sasa ivi nimeacha haya mambo
Basi kuna swala huitwa swala ya ISTIKHARA kumtaka mwenyezi Mungu ushauri na maelekezo ukisali hiyo majibu mengine unayokosa utayapata hapo!

Rakims
 
Sahihi,
 
Too Shallow
 
Pia Qur'ani sio kitabu cha majini--- Subiani, Makata, nk--- wala siyo kitabu cha kupungia majinni bali ni kitabu kilicho muongozo kwa watu.
Wapi nimeandika Quran ni kitabu cha majini--- Subiani, Makata, nk? au cha kupungia majini? anaepunga majini hiyo ni yeye na nafsi yake na pia anaesema ni kitabu cha majini ni yeye na nafsi yake! ama kwa hapa umesema wewe basi ni wewe na nafsi yako!

Rakims
 
mche mungu tuu vya wanadamu wenye maarifa nao ni majini mahaba wengine au watafuta mali
Hii ni jamii Intelligence usisahau hilo unapoweka kitu weka kama kwamba kitaonyesha how intelligence you are!

Rakims
 
Kuhusu bazia ambalao hufanya watu wasuwaone majin. Pia yup kati ya bin adam na jin ana nguvu kuliko mwenzake endapo wote wakifikia maximun based in spirituality and quantum mind set
Fanya mark unikumbushe mkuu!
 
Kuhusu bazia ambalao hufanya watu wasuwaone majin. Pia yup kati ya bin adam na jin ana nguvu kuliko mwenzake endapo wote wakifikia maximun based in spirituality and quantum mind set
Ok kuhusu pazia lililowekwa kutokuonekana kwa macho ya mtu ya kawaida ni kwa sababu ya maumbile yao na kutokuwa na umbo moja thabiti ambalo wamepewa wengi hubadirika badirika hivyo kwa maumbile yao ya kutisha na kuogopesha ndio wakawa wamehifadhiwa wasionekane kwa macho tu ya dhahiri kwa maana dunia ingekuwa ni vurugu tu, lakini kwa wenye kutaka kuona ndio ikawepo elimu jinsi ya kuweza kuwaona, na kuhusu nguvu baina ya jini na binadamu ni sawa na kutaka kujua nguvu kuhusu binadamu na mnyama sasa hapo nguvu binadamu anazidiwa na jini isipokuwa yeye ndio mtawala wa ulimwengu huu na alijaliwa akili zaidi kuliko jini na kuna baadhi ya majini wanawazidi watu akili wasioweza kuzitumia!

Rakims
 
wewe unavijuaje, unaundugu navyo?
 
wewe unapingana na kitabu hicho hicho ambacho kinasema miongoni mwetu kuna vitu wachache tu ndio wamepewa sasa kama wewe hujapewa kitu endelea kuwa looser

Rakims


Niendelee kuwa looser wa kitu gani??, hivi mimi na wewe nani looser??.

Wewe ndiye looser kwa kuifanya Qur'an ionekane ni kitabu cha ngano za majini badala ya kuwa kitabu cha kuongoza mwanadamu kiroho na kimwili.

Leo watu wengine wanaogopa hata kuigusa Qur'an kwa khofu kwamba watapatwa na majini yenu mnayoyaamini katika mila zenu.

Leo waganga wa kienyeji wanaandika aya za Qur'an katika sahani kwa kutumia zafarani na kuuosha kwa maji na kuwanywesha watu (kombe)!!!, Quran imekuwa kitu cha mchezo kiasi hicho!!;;, inasikitisha sana..
 



Mimi nilifafanua juu ya aina za majini waliotajwa katika Qur'an, wewe unapinga, sasa ni juu yako na wewe utoe ufafanuzi kutetea jinsi unavyoelewa kuhusu hayo majini.

Toa maelezo ili mtu asiyejua hayo majini aelewe ni kitu gani, siyo kubisha tu ilimradi ionekane Rakim yupo.!!😝😝
 


Eti, sahihi !!, sahihi kitu gani??!!.

Wageni wanaozungumzwa katika Qur'an ni wale wageni wa Nabii Ibrahimu (as), na imeandikwa hivi;

------ ضيف إبراهيم المكرمين--- (dhwaifi Ibrahiim almukramiin), yaani; Wageni waheshimiwa wa Ibrahimu.

Neno lililotumika kwa maana ya wageni hapo ni "dhwaifi" (ضيف).

Neno lililotumika katika kamusi (Lane &Aqrab) kwa maana ya neno "jinn" (جن), ni neno "Stranger" ambalo kwa kiarabu ni "gharib" (غريب).

Neno "stranger" limetokana na neno la kilatini "strange" (adjective), na lina maana pana sana na maana zote hizo kimsingi zinaashiria hali/ sifa ya "ugeni" katika vitu na watu (unfamiliarity), hivyo neno "strange" likazaa "stranger" na maana yake hasa kwa kiingereza linapohusu mtu/watu ni ""FOREIGNER(S) ", hivyo niliposema wale majini waliotajwa kwenye Surah Jinn ni wageni nilikuwa na maana ya "strangers" au "Foreigners" kwa sababu maana za hayo maneno ni sawa japo katika kamusi limeandikwa hilo moja tu yaani "strangers".

Neno "Foreigners" kwa kiarabu ni (اجنبي) angalia hapo, kama wewe ni mjuzi wa Lugha ya kiarabu japo kidogo tu, utaona mzizi wa neno "janna" (جن) hapo ndani ukiwepo katika hilo neno licha ya hiyo "conjugation" iliyoongeza herufi ya ب na ي mwishoni na ا mwanzoni lakini hapo kati bado utaona huo mzizi wa ج na ن.

Hivyo sasa wale wageni wa Nabii Ibrahim (as) walikuwa "guests" wake na wale majini waliotajwa katika surah Jinn ni Foreigners (strangers).

Katika lugha ya kiswahili huwezi kutofautisha kati ya guests, foreigners / strangers. Wote tunawaita wageni.

Qur'an inasema yenyewe ni muongozo kwa watu, na ukisoma katika mwanzoni mwa hiyo sura jinn utaona hao majinn wakiisifia Quran wakisema hakika tumeisikia Quran ya ajabu inayoongoza kwenye uongofu" --- na baadaye wakaikubali, sasa Quran ni muongozo kwa watu na kwakuwa wale majinn waliipokea iwe kiongozi chao basi wale majinn lazima walikuwa ni watu (binadamu).

Kinyume na ufafanuzi huu aje ulamaa yeyote na alete hoja kupinga.

Quran ni kitabu cha watu wenye akili na fikra wala sio kitabu cha kupungia mapepo na majini mahaba, makata, na subiani na hayo yote ni uongo mkubwa hakuna vitu kama hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…