Mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA aliyebuni project ya " CHADEMA ni Msingi" ahamia CCM na kupaponda Ufipa!

Mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA aliyebuni project ya " CHADEMA ni Msingi" ahamia CCM na kupaponda Ufipa!

Mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA ambaye ndiye msomi pekee mbobezi aliyebuni miradi mbalimbali ndani ya chama ukiwemo ule wa CHADEMA ni msingi amehamia CCM na kupokelewa na mwenezi wa chama ndugu Polepole.

Chanzo: Channel ten!

Maendeleo hayana
Sio mbaya ni nyoya moja limedondoka kwenye mwili wa kuku
 
Kuna nini Chadema mbona wanapakimbia? Au ndio siku ya kufa nyani miti yote huteleza?
Inaonekana cdm imejaa madini. Kila siku ccm hawaishi kuchimba, halafu wanaulaumu mgodi kwamba madini yanaukimbia, wakati wao ndio wanachimba. Yajayo yatazidi kushangaza
 
Huu ni uwongo. CHADEMA ni Msingi tuliibuni Mwaka 2004 (tukianza kuita CHADEMA ni Tawi). Huyo mtu unayemsema ametoka wapi? Ni mwongo huyo


Ahsante sana Mheshimiwa Zitto ni vyema na haki umekuja kumjibu huyu kiherehere,itakuwa wamemwokota mtu huko Tandale kawadangaya ni mwanzilishi wa CDM ni msingi kavuta mpunga wake mrefu.
 
CCM kumesheheni PhD bwashee!
Kweli kabisa. Nakumbuka zile tatu zilizokwenda bondeni kwa Madiba kumsambaratisha mlowezi.Ziliporudi hatukulala. Naibu Waziri wa mambo ya nje alitumwagia maji baridi tusilale tumsikilize yeye. Lakini mlowezi alipoibukia Canada, nw kanyeshewa mvua za mawe na kupotea. Acha tuchape usingizi. Ndege yenyewe waliipokea kule Mwanza. Kijana wao kanunua ndege mpya. Nderemo, shangwe na vifijo(soma vifujo). Wengi ni madr Pasipo hadi Digrii. Chezea CCM wewe!
 
Ahsante sana Mheshimiwa Zitto ni vyema na haki umekuja kumjibu huyu kiherehere,itakuwa wamemwokota mtu huko Tandale kawadangaya ni mwanzilishi wa CDM ni msingi kavuta mpunga wake mrefu.
Hahahaaaa..... Subiri aje Pohamba!
 
Huu ni uwongo. CHADEMA ni Msingi tuliibuni Mwaka 2004 (tukianza kuita CHADEMA ni Tawi). Huyo mtu unayemsema ametoka wapi? Ni mwongo huyo
Huyu kasema alibuni chadema ni msingi, wewe unasema mlibuni chadema ni tawi. Sasa huoni tofauti Kati ya tawi na msingi?
 
Mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA ambaye ndiye msomi pekee mbobezi aliyebuni miradi mbalimbali ndani ya chama ukiwemo ule wa CHADEMA ni msingi amehamia CCM na kupokelewa na mwenezi wa chama ndugu Polepole.

Chanzo: Channel ten!

Maendeleo hayana
Naomba kuuliza, hivi ccm ni kaburi au mortuary? Maana huwa mnatuambia kuwa CHADEMA imekufa halafu mnakuja kutuambia kuwa mmepokea wanachama toka CHADEMA, iweje mnapokea wafu?
 
Huu ni uwongo. CHADEMA ni Msingi tuliibuni Mwaka 2004 (tukianza kuita CHADEMA ni Tawi). Huyo mtu unayemsema ametoka wapi? Ni mwongo huyo
Unashangaa hilo, hukumsikia mbunge wa siha akisema kuwa mwaka 2013 alisaidia kutibu majeruhi waliojeruhiwa na polisi Arusha akiwa mwanachama wa chadema, wakati usahihi ni kuwa alijiunga chadema mwaka 2015 baada ya kukatwa kugombea kwa tiketi ya ccm
 
Back
Top Bottom