Mkakati wa mama mwenye nyumba kushinda uchaguzi mkuu wa 2025 kwa 95% huu hapa umeshawiva tayari

Wewe hata kuandika hujui lakini umejilazimisha kuandika ili na wewe uonekane kuwa ni mmoja wa waliopo humu kumtetea Mbowe na genge lake. Hivi ushawahi kujiuliza ni kwanini watanzania ambao walikuwa tayari kupigwa mabomu, kukamatwa, kuumizwa na hata kuuwawa wakati wa Dr Slaa leo hii hawako tayari kukutwa na kadhia hiyo baada ya Dr Slaa kuondoka CDM?
Unajua kati ya 2010 hadi 2015 ni watu wangapi walifungwa, walipigwa, waliteswa na wengine waliuwawa kwa sababu tu ya kuandamana na bado watu hawakuchoka wala kuogopa kuandamana? Je ni kwanini baada ya uchaguzi wa 2015 hadi leo watu ndo wamegoma kuandamana?

Ukweli ni kwamba kuanzia mwaka 2010 hadi 2015, watanzania wengi waliamini kwamba wapinzani haswa CDM ikiongozwa na mwana mapambano hodari katibu mkuu wa enzi hizo mh dr Slaa wapo kwa ajili ya kupigania demokrasia, kupambana dhidi ya ufisadi uliokuwa unafanywa na baadhi ya viongozi wa serikali akiwemo mzee Lowasa. Sasa ilipofika mwaka 2015 huyu mlamba asali ninaemzungumzia hapa ndo akaingiza nuksi ndani ya chama baada ya kupewa chake mfukoni ili agawane na genge lake kisha wawapitishe wale waliowaita mafisadi wagombee uraisi kupitia chama chake. Hapo ndo watanzania walipoanza kuona usaliti, uongo na unafiki walio nao wapinzani katika siasa za Tanzania.

Sasa watanzania hao wakaona hamna tena sababu y wao kuwaamini tena viongozi wa upinzani iwe kwa njia ya maandamano, maneno matupu nk.
 
Waambie hao
Hebu fikiria eti mpaka leo bado kuna mtu mwenye akili zake timamu, anaamini kwamba huyu mwamba atawapeleka katika nchi ile ya asali na maziwa 🤣🤣🤣 ama kweli akili ni nywele kila mtu ana zake.

Jamaa atakuwa ana mganga mkali sana ambae kampa huyu mwamba uwezo wa kumiliki akili zaidi ya milioni 2 za wanachama wake katika mfuko wake. Ndo maana kila analosema chamani ndio hilo hilo 🤣🤣🤣
 

Attachments

  • images (39).jpeg
    24 KB · Views: 1
Acha Kuandika huku ukiwa kirabuni,Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani haihitaji kumshawishi kiongozi wa upinzani asusie uchaguzi ili yeye ashinde, kwa kuwa Rais wetu anakubalika na kupendwa Sana na watanzania,Anaungwa mkono na makundi yote kutokana na kazi kubwa aliyoifanya ndani ya muda mfupi,Hii ndio sababu ya wenye kuutamani Urais kupata kigugumizi Cha kuchukua fomu kushindana naye,Maana kila mtu anatambua kuwa hakuna mwenye ubavu wa kushindana na Rais Samia iwe jukwaani au kwenye boksi la kura
 
Vyovyote iwavyo, kususa sioni kama ni suluhu kwa nchi kama hii.
 
mpinzani yupi anayejielewa atapigania wapumbavu wanaoambiwa kupigania haki zao zilizoporwa yamekaa tu kama mazezeta.
Hao unaowaita wapumbavu ndio waliouwawa Unguja na Pemba mwaka 2001, lakini bado hawakuchoka wala kuogopa kuandamana, hao unaowaita wapumbavu ndio waliouwawa kwenye bomu la Soweto Arusha, ndio waliopigwa, walioadhibiwa na kufungwa na polisi katika maandamano mbali mbali ya kudai haki kuanzia mwaka 2010 hadi 2015 bila kuogopa kufa, kuteswa wala kuujeruhiwa.

Iweje baada ya mwenyekiti wa chama fulani kumkaribisha yule waliomwita fisadi papa agombee ndani ya chama chao ndio kibao kilipoanza kugeuka kuanzia maandamano ya ukuta na mengineyo?

Kuna jambo limejificha na baadhi ya wanaharakati wanalijua lakini ni nani wa kuthubutu kuongea ukweli kuhusu hilo. Kila mtu anakataa kuongea ukweli ili asije kuonekana ni msaliti wa mwenyekiti wa chama na chama kwa ujumla. Kinachofanyika sasa hivi ni hii style ya kuwatupia wananchi jumba bovu kwa kuwapa lawama mbali mbali kama hizi ulizoandika hapo juu ili kumnusuru mwenyekiti na kashfa ile ya mwaka 2015 ambayo imebadili kabisa mwelekeo wa mioyo ya watanzania kuhusu upinzani, maandamano nk. Ni mtanzania gani mwenye akili timamu ambae atakuwa tayari kudanganywa kizembe hivi na mtu ambae alikuwa anamuamini kwa asilimia zote?
 

Attachments

  • images (1).jpeg
    27.8 KB · Views: 1
  • download.jpeg
    10.7 KB · Views: 1

Wangeshughulika kwanza kulipa mdeni na mishahara 2025 bado mbali. Maana watofautishe kuwawin CHADEMA na kuwatumikia wananchi.
 
Moja ya mbinu zao ni hiyo ya kuwatumia wachumia tumbo wakubwa wa vyama vya upinzani.
Kama unafikiria kuwa kuna mpinzani au mwanasiasa ambae atakukomboa ujue unajidanganya sana.

Maneno mengi kumbe lengo lako ni kuusema upinzani. Unaona aibu kuisema ccm iliyokamata vyombo vyote vya maamuzi, inatoza tozo, inatoza kodi, inakopa njee lakini unausema upinzani kana kwamba ndio imeunda serikali. Jifanye kipofu ipo siku utaona.
 
Ikiwa wale viongozi waliotegemewa kuleta mageuzi kupitia vyama vyao ndio hao wanaolamba asali na kupigania matumbo yao.

Ni njia gani nyingine unadhani inaweza kutumika kuleta mageuzi ya kweli nchini kupitia sanduku la kura?

Upinzani sio Viongozi, upinzani ni spirit ndani ya wafuasi wa upinzani. Hata Viongozi wakinunuliwa na serikali , upinzani utaendelea. Wameondoka wangapi upinzani bado upo?
 

CCM walishajimilikisha serikali. CCM kushinda uchaguzi sio hadithi, wao washughulike na uchumi wa mwananchi na taifa. Mwezi januari watu hawana mishahara.
 
watz mnapenda story za umbea umbea tu ambazo mtu huwezi hata kuzithibitisha
 
Hayo uliyoandika hayana msingi wowote, ushindi kwa CCM upo wazi na njia ni nyeupe kabisa, pia kumbuka haiwezi kutokea upinzani ukaja kushinda uchaguzi sahau hilo, na kama kudhibitiana hayo yatakuwa ni ndani ya CCM wenyewe kwa wenyewe.
#SSH2025-30.

CCM Mara ya mwisho kushinda uchaguzi ilikuwa 2005 kkipindi Cha kikwete. Baada ya hapo wanatumua dola kubaki madarakani. Akili za kuongoza hawana ndio maana serikali inategemea mikopo kulipa madeni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…