#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

Clip ya tano (na ya mwisho kabisa) siku ya TATU

Your browser is not able to play this audio.


Maelezo ya nyongeza kwenye baadhi ya clips hizi yatafuata baadaye
 
UPDATE WEDNESDAY 04TH AUGUST 2022

KUHUSIANA NA MKUU WA KITENGO (MKTE) CHA MAFUNDI WANAOSHUGHULIKA NA MIUNDOMBINU YA MABOMBA YANAYOPITISHA MAJI TAKA

MAELEZO YA UTANGULIZI:


J4 ya wiki hii tarehe 02/08/2022, mhusika alifika tena idara ya miliki za nyumba kwa ajili ya kujaza fomu ya maombi ya huduma ya mafundi kwa ajili ya bomba lililokuwa kwa mara nyingine, limeziba tena jikoni

  • Muda ulikuwa kati ya “baada ya saa 4 asubuhi na kabla ya saa sita mchana”
  • Bomba hili lilikuwa limeziba kwa mara ya tatu sasa ndani ya muda usiozidi wiki tatu
WALICHOONGEA MHUSIKA NA MKTE BAADA YA MHUSIKA KUWASILI ZILIPO OFISI ZA MILIKI YA NYUMBA NA HATIMAYE KUJAZA FOMU YA MAOMBI

MKTE na mhusika walibadilishana namba za simu na kukubaliana kwa kauli moja kuwa MKTE atamjulisha kabla mhusika siku na muda wa ujio wa fundi atakayemtuma kwenda kushughulikia tatizo la nyumbani kwake (mhusika)

Leo Alhamis tarehe 04/08/2022 MKTE amemtuma fundi nyumbani kwa mhusika ila kwa bahati mbaya akawa amesahau kumjulisha mhusika juu ya ujio wa fundi huyo

  • Hata hivyo, mhusika akiwa yupo ofisini, alipokea simu kutoka kwa mgeni aliyepo nyumbani kwake kuwa fundi alikuwa amefika nyumbani
  • Baada ya mhusika kuongea na mgeni wake, mhusika alimweleza mgeni kuwa amweleze fundi kuwa ndani ya dakika 5 atakuwa tayari ameshafika hapo nyumbani
  • Baada ya hapo, mhusika aliwasha gari na aliwasili nyumbani ndani ya muda huo lakini kwa bahati mbaya hakumkuta fundi
Ndani ya muda huo mfupi wa dakika 5 fundi alikuwa tayari ameshamaliza kazi na kuondoka

Kwa hali hiyo mhusika hakubahatika kumuona fundi aliyetumwa na MKTE kwenda kufanya kazi nyumbani kwake, na wala hakubahatika kufahamu kama alikuwa ni mfanyakazi wa taasisi ama la!

……………………inaendelea
 
MENGINE YA MUHIMU YALIYOJIRI SIKU HIYO BAADA YA MHUSIKA KUWA AMEWASILI KWENYE MAZINGIRA ZILIPO OFISI ZA MILIKI YA NYUMBA

Akiwa yupo umbali kidogo anakaribia kwenye geti la kuu la kuingilia ndani zilimo ofisi hizo mbele yake aliwaona watu watatu wakiwa wanatembea

  • Mmoja alikuwa upande wa kushoto mwa bararbara akiwa anatembea kuelekea getini.
  • Huyu allikuwa ni Ofisa wa Nyumba, jirani yake na mhusika
  • Wengine wawili walikuwa mbele nao vile vile walikuwa wanatembea kuelekea kwenye geti la kuingilia ndani
  • Hawa walikuwa kijana mmoja wa makamo na binti mmoja mwenye umri wa miaka kati ya 28-32
  • Wawili hawa wote walikuwa wamevaa kiraia, ila baada ya kuwakaribia mhusika alimuona binti akiwa ameshika radio-call mkononi
  • Kitendo cha kumuona binti akiwa ameshika radio call, kilimpa mhusika hisia kuwa pengine alikuwa ni Askari wa zamu aliyekuwa amevaa kiraia
  • Hadi mhusika anafika getini, wawili hawa nao walikuwa tayari wameshafika pale
Baada ya mhusika kusimama getini ili asubiri ruhusa ya kuingia ndani kutoka kwa askari yule ambaye huwa anakuwa yupo getini muda wote

  • Huku gari la mhusika likiwa bado lianendelea kuunguruma, binti huyu alimsogelea mhusika na kumuuliza kuwa analekea wapi
  • Mhusika alimjibu binti na binti huyu alimruhusu mhusika kuingia ndani
Mpaka hapa uhakika uliopo kwa sasa ni kuwa maongezi haya yaliyofanyika nje ya geti kati ya mhusika na binti huyu hayakusikika kwa kijana yule aliyekuwa amembatana na binti kwa sababu gari la mhusika lilikuwa bado linaunguruma

  • Hata hivyo kabla mhusika hajaondoa gari ili aingine ndani, alijitokeza tena askari mwingine safari hii kutokea ndani ya geti.
  • Huyu wa pili yeye alikuwa amevaa sare za jeshi
  • Askari huyu naye pia alimuuliza mhusika kuwa alikuwa anaelekea wapi
  • Mhusika alimjibu na baada ya hapo, askari huyu naye alimruhusu mhusika kuingia ndani
Kitendo cha askari huyu naye kumruhusu tena mhusika, kilianza kumppa hisia mhusika kuwa binti aliyekuwa na radio call na askari mwinine huyu aliyekuwa ndani getini, hawakuwa na maasiliano na kama walikuwa nayo, basi hayakuwa yako coordinated



Kwa hiyo mpaka muda huo, mhusika akawa ameruhusiwa kuingia ndani na askari wawili isipokuwa akawa hana uhakika kama huyu askari wa pili aliyekuwa amevaa sare, aliweza kufahamu kama wakati yeye (askari wa getini) anamruhusu mhusika kuingia ndani, alikuwa tayari amesharuhusiwa na binti aliyekuwa ameshika radio-call (yaani kuna set-up zingine hadi wakati mwingine mhusika huwa analazimika kucheka akiwa yuko peke yake)

OFISA WA NYUMBA ALISHUHUDIA KUMUONA MHUSIKA AKIWA ANAONGEA NA BINTI ALYEKUWA AMESHIKA RADIO CALL


Wakati haya yote yakiwa yanaendelea (na ambayo yalichukua muda mfupi sana), Ofisa wa Nyumba naye sasa ndiyo alikuwa ameshafika kwenye maeneo hayo ya lango la geti hilo na hivyo aliwapita mhusika na binti wakiwa wanafanya maongezi hayo na hivyo aliwaona walipokuwa wanaongea

…………………..inaendelea
 
BAADA YA MHUSIKA KUFIKA KWENYE OFISI INAYOHUSIKA NA UJAZAJI FOMU ZA MAOMBI

Safari hii alimkuta mtu anayehusika na ofisi hiyo; binti

Mhusika alijaza fomu na binti aliiweka kwenye rekodi na baada ya hapo, mhusika alielekea ofisini kwa MKTE kwa ajili ya kumpa taarifa isiyo rasmi tu kuwa ameshajaza fomu. Hiki kitu huwa siyo lazima kifanyike ila wakati mwingine huwa kinasaidia kusababisha huduma kutolewa kwa haraka pindi panapokuwa pana nafasi ya kufanya hivyo

BAADA YA KUWASILI MAENEO OFISINI KWA MKTE; MHUSIKA AGONGANA TENA NA VIJANA WAWILI; BINTI MWENYE RADIO CALL PAMOJA NA KIJANA MWANAUME

Baada ya kufika ofisini kwa MKTE, mhusika aliwakuta huko vijana wawili aliogongana no getini, wakiwa wamekaa nje ya ofisi kwenye viti

  • Mhusika alimjulisha MKTE kuwa ameshajaza maombi tena kwa sababu sink lilikuwa limeziba tena
  • Zaidi mhusika alimsisitiza MKTE kwa ombi kuwa atakapokuwa ame-assign fundi kwa ajili ya kazi hiyo, basi itapendeza zaidi kama atamjulisha mhusika
MKTE alikubaliana na ombi hilo na walibadilishana mawasiliano kwa mara nyingine tena na mhusika akaaga ili aondoke

Hapo hapo tena mara MKTE, hata kabla hajaipokea au kuiona fomu ya maombi ya mhusika, akapata wazo la kumpatia mhusika fundi muda huo huo ili aondoke naye kwenda nyumbani kwake

MKTE alimwita fundi kijana aliyekuwepo nje maeneo yale na kutaka kumkabidhi kwa mhusika ili aondoke naye, lakini mhusika alitoa udhuru kuwa kwa wakati huo alikuwa haelekei tena nyumbani kwake bali alikuwa anarudi ofisini. Hii ilileta logic pia kwa sababu wakati mhusika anaelekea kwenye ofisi hizo, alikuwa ametokea ofisini vilevile

Kijana huyo alibaki pale na MKTE na mhusika aliwasha gari na kurudi ofisini

Kijana wa kike mwenye radio-call na yule mwenzake wa kiume nao pia aliwaacha wakiwa bado wapo maeneo hayo ya ofisini kwa MKTE.

Zaidi ni kuwa kijana wa kike alikuwa na ujauzito ambao mhusika ana wasiwasi kama wiki hii ataimaliza kabla hajachukua likizo ya uzazi

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: FRIDAY 05 AUGUST 2022

SINK LA MAJI MACHAFU JIKONI TAYARI LIMESHAZIBA TENA!!!!

KUMBE ISSUE YA SINK HILO NI KUBWA ZAIDI KULIKO MHUSIKA ALIVYOKUWA ANAIDHANIA.

…more is to come, stay tuned................

…………………….itaendelea
 
Kwa kifupi tu ni kwamba leo tena kulikuwa na "PLAN B" ambayo mhusika alitakiwa aende tena ofisi za miliki ya nyumba kwenda kujaza tena fomu ya maombi ya kurekebishiwa sink kwa mara nyingine tena; kwa mara ya tatu sasa.

Kama siyo kujaza fomu, basi alitakiwa angalau afike tu kwenye ofisi hizo; angalau kuwasilisha malalamiko yake halafu kuanzia pale sasa, ingechukuliwa kuwa alikuwa ameghafirika.

Kile ambacho kingefuata baada ya kuchukuliwa kuwa ameghafirika, wasomaji wa siku zote wa uzi huu wanakielewa, mhusika hahitaji kukiongelea

Malelezo zaidi yatafuta wiki ijayo
 
UPDATE: TUESDAY 09 AUGUST 2022

KWA WAUMINI WA KANISA A: KUHUSIANA NA NABII NA UNABII


Kwenye clip ya pili siku ya kwanza #1,093; kwenye dakika kuanzia ya sita; mwalimu anasisitiza mambo kadhaa yafuatayo:

Kwa kila mshiriki wa kawaida au muumini wa kawaida; mwalimu anasema (kwa kutumia Maandiko Matakatifu) kwamba kila muumini ana sehemu ya kila huduma

  • Kuna sehemu ya utume kwake, lakini sehemu hiyo haimfanyi muumini huyo kuwa mtume
  • Kuna sehemu ya unabii kwake, lakini sehemu hiyo haimfanyi muumini huyo kuwa unabii
  • Kuna sehemu ya uinjilisti kwake, lakini sehemu hiyo haimfanyi muumini huyo kuwa muinjilisti
HITIMISHO

Zaidi mwalimu anamalizia kwa kusema hivi (kuanzia dakika ya nane (8) na kuendelea)………………….KUNENA KWA LUGHA SI KWA AJLI YA KILA MUUMINI!

Mhusika aliwahi kukaa Kanisa B kwa takribani miaka mitatu na hakuwahi kumsikia muumini hata mmoja akinena kwa lugha katika kipindi chote hicho

Mbali na hapo, kwenye clip ya tatu siku ya kwanza; #1,094 (kuanzia dakika ya tano (5) na kuendelea); mwalimu anazidi kusisitiza kuwa kila mtu aliyeokoka, anaye Roho wa Mungu. Mwalimu anazidi kusisitiza pia kuwa huwezi kuwa umeokoka halafu ukawa huna Roho wa Bwana

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Kwenye clip hiyo hiyo #1,094 kuanzia dakika ya 13, mwalimu anaendelea kusisitiza kuwa kuna degree mbili za Roho Mtakatifu kuwa ndani ya mwamini

  • Kwanza ni siku pale anapozaliwa upya au anapookoka; yaani mafuta ya awali kwa ajili ya mwamini (first level anointing)
  • Kazi ya upako huu ni kumuongoza muumini kwenye kweli (mtoto wa Munhgu hakuachwa gizani)
Muumini huwa anazaliwa mara ya pili kwa Roho na kwa NENO

Pili ni siku ya kujazwa Roho Mtakatifu na KUNENA KWA LUGHA; hii ni level nyingine ya pili ya anointing. Kujazwa RM ni dimension nyingine na ina kazi yake

NAWATAKIENI USIKILIZAJI MWEMA NA MAKINI
 
UPDATE: WENESDAY 10 AUGUST 2022

KWA MARA NYINGINE TENA: AJALI NYINGINE MBAYA YA BARARABANI IMEGONGANA NA WIKI YA MAOMBI YA KANISA:

OMBI LA MHUSIKA KWA VIONGOZI WA KANISA A


Mhusika anawaomba sana viongozi wa KANISA A walifanyie kazi swala hili; kwamba kila wanapotangaza maombi wiki inayofuata zinafungulia ajali mbaya za barabarani

Imefikia hatua hadi KIONGOZI MKUU WA KANISA-A (KM-A), ameanza kukwepa kutangaza tangazo la maombi

  • Kawaida mara zote huwa anatoa tangazo la aaombi yeye mwenyewe, na kama siyo basi tangazo hilo hutolewa na kiongozi mwingine aliye chini yake, halafu yeye naye hufuata tena baadaye kuja kuweka msisitizo kwenye ombi hilo
  • J2 iliyopita kwa mara ya kwanza (ndani ya kipindi kirefu sana) maombi hayo yalitangazwa na kiongozi mwingine na KM-A wala hakufuatia tena kuja kuweka msisitizo kama ilivyo siku zote
AJALI NYINGINE MBAYA YA BARABANI IMEGONGANA NA WIKI YA MAOMBI YA KANISA A

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
NYONGEZA MUHIMU


Kwa kutumia jicho jingine la pili, hii ni ajali ya pili yenye kuhusisha vyombo vya moto zaidi ya viwili kuwahi kutokea baada ya maombi ya Kanisa A kuwa yametangazwa

Na kwa jicho jingine la tatu, hakuna ajali nyingine yeyote ambayo imeshatokea na kuhusisha vyombo vya moto zaidi ya viwili, tofauti na hizi mbili

Hii ni mojawapo ya COMPOUND ACCIDENTS zinazoweza kuwa zinasababishwa na failure ya BRAKING MECHANISM vyombo vya mot
 
KWA WALE WALIOKUWEPO KANISA A JUMAPILI ILIYOPITA: WANAWEZA KUKUBALINA NA MHUSIKA KUWA BADO TAA ZA NYUMA ZA GARI LA MHUSIKA ALIZOWAHI KUWEKA BAADA YA KUWA AMEVUNJA ZA AWALI KWA AJLAI YA GARI, BADO ZINATUMIKA KUFANYA MASHAMBULIZI YA KIROHO
...............inaendelea
 
KWA WALE WALIOKUWEPO KANISA A JUMAPILI ILIYOPITA: WANAWEZA KUKUBALINA NA MHUSIKA KUWA TAA ZA NYUMA ZA GARI LA MHUSIKA ALIZOWAHI KUWEKA BAADA YA KUWA AMEVUNJA ZA AWALI KWA AJALI YA GARI, NDIYO ZILE AMBAZO BADO ZINATUMIKA KUFANYA MASHAMBULIZI YA KIROHO

KILE KILICHOTOKEA J2 ILIYOPITA BAADA YA MHUSIKA KUWASILI KANISANI NA HADI KUINGIZA GARI NDANI YA UZIO WA KANISA


Mhusika aliwasili Kanisa A na kukuta Ibada ya kwanza ikiwa tayari imeshamalizika, waumini wakiwa wanatoka nje na magari yao. Kutokana na hali hiyo, mhusika alilazimika kupaki nje kwa muda, akisubiria magari ya waumini wa Ibada ya kwanza yatoke kwanza

  • Baada ya takribani nusu saa kupita, magari yote ya waumini wa Ibada ya kwanza yalikuwa tayari yameshatoka nje
  • Baada ya hapo, mhusika aliamua kutoka nje kwenda kuchukua gari lake ili aje alipaki ndani ya uzio wa Kanisa
Hadi kufikia muda huo mhusika anatoka nje kwenda kuleta gari lake ndani ya uzio wa Kanisa, hakuna muumini wa Ibada ya kwanza hata mmoja aliyekuwa hajatoka

Magari yote ya waliokuwa wanatoka nje yalikuwa yameisha na yaliyokuwa bado yapo ndani yalikuwa yametulia kwenye parking zake kuonyesha kuwa yalikuwa hayatoki nje

Mhusika alienda akawasha gari lake na baada ya kufika usawa wa geti la kuingia Kanisani, kabla hajakata kona ili aingie ndani

  • Mbele yake aliona gari aina ya VANGUARD nyeusi iliyokuwa tayari imeshaingia kidogo ndani ya geti
  • Gari hii ilikuwa ni ya muumini wa Ibada ya pili aliyekuwa anajaribu kuingia ndani
Wakati gari ikiwa ipo bado usawa wa geti la kuingilia ndani, ghafla gari nyingine nyeupe aina ya V8 yenye vioo tinted, ilianza pilika pilika za kutoka nje muda huo

  • Kutokana na pilika pilika za V8 hiyo, VANGUARD ililazimika kurudi nje kwa muda kwa sababu V8 ni gari kubwa na wawili hawa wasingeweza kupishana kwa ubavu wakiwa ndani ya uzio wa Kanisa
  • Kwa muda wote huu, mhusika alikuwa amesimama barabarani karibu na geti akishuhudia kilichokuwa kinaendelea ndani ya GETI LA NYUMBA HIYO YA IIBADA
Kwa configuration ya magari haya matatu namna yalivyokuwa yamekaa, yaani lile la mhusika pamoja na yale mengine mawili; mhusika sasa alitakiwa ARUDI NYUMA KWA REVERSE GEAR, ili kuiruhusu VANGUARD iweze kurudi nyuma na hatimaye iweze kuacha nafasi kwa V8 kuweza kutoka nje

MHUSIKA ASTUKA KURUDI NYUMA KWA REVERSE GEAR.

ALICHOFANYA MHUSIKA NA GARI LAKE BAADA YA KUONA UPUMBAVU HUO UKIENDELEA HAPO GETINI


Badala ya kurudi nyuma kwa REVERSE GEAR kama ambavyo huwa anafanya siku zote, mhusika aliamua kuendelea mbele akilipita geti,uelekeo wa Barabara kuu ya Morogoro. Hii yote ilikuwa ni kukwepa kurudi nyuma kwa REVERSE GEAR kwa sababu anayajua madhara ambayo ameshayaona huko nyuma

Kabla hajaifikia Barabra hio, alipinda na kugeuza akaanza kurudi kule alikokuwa ametokea pasipo kutumia REVERSE GEAR

  • Baada ya kufika tena usawa wa getini alipokuwa awali, ndipo aliweza kupishana sasa na V8 iliyokuwa na vioo tinted na hivyo kushindwa kumfahamu muumini aliyekuwa ndani ya gari hiyo
  • Na kwa bahati mbaya vile vile alisahau kusoma namba ya gari hilo
Wakati huo VANGUARD ilikuwa tayari imeshaingia ndani. VANGUARD hiyo nayo pia ni ngeni Kanisani hapo ila inamilikiwa na mtu ambaye ni mwenyeji sana Kanisani hapo na ambaye hapo kabla alikuwa hatumi gari hiyo. J2 iliyopita ilikuwa ni mara ya pili kwa mhusika kumuona muunini huyo akiwa anatumia gari hiyo

Baada ya kuingia ndani, mhusika alikuta configuration ambayo ilikuwa haimruhusu kupaki gari akiwa amegeukia uelekeo wa kutokea

Kulikuwa na gari nyingi kiasi J2 hiyo na possibly kuna na baadhi ya magari ya watu wa Ibada ya kwanza ambao hawakuwa wameondoa magari getini

Mhusika alienda akapaki gari katika namna ambayo wakati wa kutoka ILIBIDI AENDESHE GARI KWA REVERSE GEAR HADI KUTOKA NJE YA GATE LA KANISA.

J2 hiyo, humo ndani getini, hapakuwa na nafasi yoyote ya kumruhusu mhusika ageuze na kuendesha katika namna ambayo angeweza kutoka nje ya geti pasipo kutumia REVERSE GEAR

Zaidi ni kuwa, KIONGOZI ALIYETOA TANGAZO LA MAOMBI na ambalo halikuambatana na msisitizo wa KM-A kama ilivyo siku zote, NI YULE AMBAYE ALIWAHI KUMSABABISHIA MHUSIKA AJALI YA KUTOBOA TAA ZA GARI LAKE NA HIVYO KULAZIMIKA KUNUNUA ZINGINE AMBAZO NDIYO ZILIZOPO KWENYE GARI LAKE MUDA HUU NA NDIZO ZINAZOPELEKEA AENDELEE KUTEGESHEWA KUENDESHA GARI KWA KUTUMIA REVERSE GEAR

Inaonyesha safari hii KM-A aliamua kuepuka malalamiko ya tangazo la maombi lenye kuambatana na ajali za gari; possibly ni kwa sababu alikuwa anajua ni nini kitatokea

BAADA YA KUWA AMEINGIA NDANI YA UZIO WA KANISA; KUELEKEA KWENYE NAFASI YA PARKING ALIFUATANA NA GARI NYINGINE HARRIER NYEUSI YA MAMA AMBAYE NI SHEMASI KANISANI HAPO

…………………….inaendelea
 
NAMNA GARI HII HARRIER ILIVYOKUWA IKITEMBEA NDANI YA UZIO WA KANISA

Mhusika akiwa yupo nyuma huku HARRIER ikiwa mbele yake, kabla ya kuifikia nafasi ya pekee ya parking iliyokuwa imebaki; HARRIER hii iliamua kusimama njiani kwanza na hivyo kumlazimisha mhusika aisimame na kuisubiria kwanza

Configration iliyokuwepo wakati huo ni kwamba pembeni mote kulia na kushoto kulikuwa na gari zikiwa zimepaki na hivyo mhusika pamoja na mwenye HARRIER, wote walikuwa wanalazimika kunyoosha moja kwa moja hadi mbele kabisa kwenda kuanza kupanga mstari mwingine wa tatu na wa katikati ambao ulikuwa tayari umeshatengenezwa na gari kadhaa zilizokuwa mbele ya HARRIER hiyo

Baada ya HARRIER hiyo kusimama mara ya kwanza, ilitembea tena kidogo halafu ikaenda ikasimama tena mahali kwa mara ya pili, huku kukiwa bado kuna nafasi kubwa ya kujaza kati ya HARRIER na gari iliyokuwa mbele ya HARRIER hiyo kwenye mstari huo wa parking

Hadi kufikia hapa (baada ya HARRIER kusimama mara ya pili), mhusika alikata tamaa na kuamua kushuka kwenye gari iili awahi kwenye Ibada kwa sababu tayari ilikuwa imeshaanza

Mama huyu kuona hivyo, aliamua sasa kusogea mbele hadi kwenye nafasi stahiki alipotakiwa kupaki, kitu kilichopelekea mhusika alazimike kurudi tena ndani ya gari ili kuisogeza katika nafasi sawa kutoka kwenye usawa wa HARRIER ya mama huyu

Baada ya hapo mhusika alishuka kwenye gari na kuelekea kwenye Ibada

HITIMISHO

Ikumbukwe kuwa kila wakati HARRIER ilipokuwa inasimama, mhusika alikuwa analazimika kukanyaga brake na kusimama
  • Ukikanyaga BRAKE, TAA ZA BRAKE HUWA ZINAWAKA
  • Ukiweka REVERSE GEAR, TAA ZA BRAKE HUWA ZINAWAKA VILE VILE
Baada ya Ibada kuisha J2 hiyo, na kutokana na uwingi wa magari tofauti na ilivyo kwenye J2 zingine ukiunganisha na configuration ya namna yalivyokuwa yamepaki,mhusika alitlazimika kuoka kwa kutumia REVERSE GEAR hadi nje ya uzio wa nyumba ya Ibada

Hili swala la taa za brake kutumika kama njia ya mashambulizi ya kiroho siyo geni na alishawahi kuliongelea kwa kina humu jukwaani hapo kabla

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
NYONGEZA MUHIMU

KILE KINACHOONEKANA KUWA ZILIKUWA NI “PLAN A” NA “PLAN B” J2 ILIYOPITA HAPO KANISA A


Kilicho dhahiri ni kwamba mhusika alitakiwa arudi reverse kabla hajaingia ndani ya uzio wa nyumba ya Ibada ili TAA ZA BRAKE za gari lake ziwake. Hiyo ilikuwa ni PLAN A

Baada ya mhusika kukwepa hilo akiwa bado yupo nje ya uzio wa Kanisa, PLAN B ikawa sasa ni ile gari HARRIER kumtangulia mbele halafu ikawa inasimama simama njiani kabla haijazifikia nafasi za parking zilizokuwepo ili mhusika akanyage brake na hivyo kusababisha TAA ZA BRAKE za gari lake ziwake

Hii ndiyo ilikuwa ni “PLAN B”

Pale mwisho wa Ibada ndiyo sasa akakoswa koswa kufutiwa data zote kwenye smartphone yake baada ya kuwa amekuwa PROMPTED ku-connect kenye WIFI ya mtandao wa Kanisa A.


Hili nalo ni jingine na linahitaji muda wake peke yake, kuna siku atakuja kuliongelea kivyake peke yake, ambapo yeye kwa mawazo yake finyu anadhani pengine kilichopelekea hatua hiyo kuchukuliwa ni mambo kadhaa aliyoyatoa kuanzia kwenye post hii hapa #1,091

 
Ndani ya wiki hii hadi kufikia leo Alhamis tayari kuna ajali mbili mbaya muno




Iwapo anayesoma taarifa hizi muda huu siyo msomaji wa siku zote wa uzi huu, basi anashauriwa asome kwanza taarifa zilizopo hapo juu kabla ya kuendelea na hizi zilizopo kwenye post hii
 
Clip ya pili siku ya TATU

View attachment 2312967

UPDATE: FRIDAY 12 AUGUST 2022

KUHUSIANA NA “BLUNDER” YA MAKUSUDI AMBAYO IMEKUWA IKIFANYWA NA KIONGOZI MKUU WA KANISA A (KM-A) AKISHIRIKIANA NA KIONGOZI MWINGINE MWANDAMIZI

KUHUSIANA NA SWALA LA YESU KUFANYIKA “LAANA”


Mwalimu anatoa ufafanuzi kwa kutumia mafungu ya 1Wakorintho 12:1-3 kwenye clip hii hapa #1,098 (clip ya pili ya siku ya tatu) hasa kuanzia dakika ya 10 na kuendelea

1Wakorintho 12:1-3

Karama za Roho


1 Basi, ndugu zangu, kuhusu karama za roho, sitaki mkose kufahamu.

2 Mwajua ya kuwa mlipokuwa watu wa Mataifa, mlichukuliwa kufuata sanamu zisizonena, kama mlivyoongozwa.

3 Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu.
 
UPDATE: MONDAY 15TH AUGUST 2022

KILICHOKUWA KIKIENDELEA KWENYE MADHABAHU YA KANISA A J2 ILIYOPITA KAMA ALIVYOKIONA MHUSIKA KWA JICHO LAKE YEYE


MHUSIKA ANAOMBA KAMA KUNA KITU VIONGOZI WENYE MAMLAKA NA KANISA HILI WATAKIONA KWENYE HAYA ALIYOAANDIKA HAPA CHINI, BASI KAMA KUNA UWEZEKANO, ANASHAURI WACHUKUE HATUA KWA KIONGOZI ALIYEHUSIKA KUTOA MATANGAZO J2 ILIYOPITA

AIDHA MHUSIKA ANAOMBA KIONGOZI HUYO ASHAURIWE KUHUDHURIA “MAFUNZO PROFESSIONAL” KAMA
AMBAVYO WALISHAWAHI KUFANYA VIONGOZI WENZAKE WENGINE WOTE KANISANI HAPO



MAELEZO YA UTANGULIZI:

KUHUSIANA NA “MAFUNZO PROFESSIONAL
KWA VIONGOZI WA KANISA A

Uhakika alionao mhusika mpaka muda huu ni kwamba kiongozi huyu ndiyo pekee aliyepo Kanisa A ambaye hajawahi kuhudhuria “mafunzo professional” kwa kazi anayoIfanya Kanisani hapo

Kazi anayoifanya kiongozi huyu, alipewa tu Kanisani hapo kutokana na uzoefu wake baada ya kuwa amekuwa Mzee wa Kanisa kwa kipindi kirefu sana

Vinginevyo kiongozi huyu hajawahi kuhudhuria mafunzo yoyote professional ya kazi hiyo

  • Kwa upande mwingine, viongozi wengine wote Kanisani hapo, katika muda tofauti tofauti, wamewahi kuhudhuria kila mmoja wao, mafunzo professional ya kazi wanayoifanya Kaniasni hapo
  • Hata hivyo, hapa mhusika anamu-exclude KIONGOZI MKUU WA KANISA A (KM-A) ambaye hakuwahi kumuona akihudhuria mafunzo hayo, isipokuwa ana imani kuwa KM-A alishawahi kufanya hivyo kipindi kirefu nyuma kabla mhusika hajawa muumini wa Kanisa A
KILE (KIKUBWA) KINACHOPELEKEA MHUSIKA ALETE MAELEZO HAYA KWA WAUMINI WA KANISA A

Ni baada ya Ibada ya J2 iliyopita kuhamishwa kutoka KANISA JIPYA, almaarufu kama “JENGO JIPYA”, na kupelekwa kenye JENGO JINGINE, AMBALO KWA MARA YA KWANZA LILIKUWA LIMEBATIZWA JINA JIPYA KUANZIA J2 HIYO.
Jina hilo jipya, lilikuja kujulikana tu na waumini wa KANISA A wakati ule wa matangazo ya kuhitimisha ibada

Kwa hiyo kilifanyika J2 iliyopita ni kwamba MADHABAHU YA BWANA ILIKUWA IMEHAMISWHA KIROHO kutoka kwenye NYUMBA YA BWANA AU KANISA JIPYA na kuhamishiwa kwenye UKUMBI ambao katika hali ya kwaida, UKUMBI siyo nyumba ya Ibada!

IBADA YA J2 ILIYOPITA ILIHAMISHIWA KWENYE KANISA LA ZAMANI ALMAAARUFU KAMA “JENGO LA ZAMANI”, HUKU KANISA HILO LIKIWA LIMEPEWA JINA “UKUMBI WA SULEMANI”


Ukumbi huo ambao ulisemekana J2 iliyopita kuwa jina lake ni “UKUMBI WA SULEMAN”, HAPO KABLA ULIJULIKANA KAMA KANISA LA ZAMANI AU “JENGO LA ZAMANI”

Kwa kumbukumbu zake mhusika, hadi kufikia J2 ya tarehe 07/08/2022, alimsikia mmojawapo wa wazee wa Kanisa kwenye mojawapo ya matangazo yake, akii-refer nyumba hiyo ya zamani ya Ibada kama “JENGO LA ZAMANI”

Kwa hali hiyo Kanisa la zamani ambalo kwa ghafla J2 iliyopita lilibadilika jina na kuwa UKUMBI WA SULEMAN, lilikuwa na madhabahu iliyokuwa imewekwa wakfu kwa Bwana. Kwa hiyo, kitendo cha kanisa hilo la zamani kubadilika jina na kuwa ukumbi wa Sulemani; automatically kuliondoa wakfu kwenye nyumba hiyo ya zamani ya Ibada kwa sababu WAKFU WA BWANA HAUWEZI KUKAA KWENYE MADHABAHU ILIYOKO KWENYE UKUMBI. UNLESS UKUMBI HUO UNABADILISHWA NA KUWA NYUMBA YA IBADA

OBVIOUSLY; WAKFU WA BWANA UNAWEZA KUWEPO KWENYE MADHABAHU ILIYOKO KWENYE UKUMBI
IWAPO TU UKUMBI HUO NDIYO ULIOBADILISHWA NA KUWA NYUMBA YA IBADA; BUT THE VICE VERSA IS NOT TRUE

Kile kiilichofanyika J2 iliyopita ni THE VICE VERSA; yaani nyumba ya Bwana kubadilishwa kuwa ukumbi na hapo hapo tena madhabahu iliyokuwa kwenye ukumbi huo kutumika kama madhabahu ya Bwana, kitu ambacho siyo sahihi

  • Kwa hiyo kila kilichofanyika J2 iliyopita, kilifanyika huku MADHABAHU YA BWANA ikiwa imehamishiwa kwenye UKUMBI na hivyo MADHABAHU YA BWANA ilikuwa imechakachuliwa vya kutosha
  • Hapa mhusika anapata ujasiri wa kusema kuwa Ibada ya J2 iliyopita, haikufanyikia kwenye MADHABAHU YA BWANA
  • Kiroho, UKUMMBI huu ulikuwa ni mpya kabisa ndani ya uzio wa Kanisa A kwa sababu haukuwahi kuwepo hapo awali
  • Aidha hapo kabla, hapakuwahi kutolewa tangazo lolote Kanisani hapo kwa waumini kuwa NDANI YA UZIO WA KANISA A, kuna sehemu ambayo mamlaka za Kanisa A zime-deliberate kuiita kwa jina jipya la UKUMBI WA SULEIMAN
  • Still, hata kama pengine tangazo la aina hiii liliwahi kutolewa na kwa bahati mbaya mhusika hakulisika, MADHABAHU YENYE WAKFU WA BWANA HAIWEZI KUKAA KWENYE KANISA LILILOBADILIKA NA KUWA UKUMBI, ISIPOKUWA WAKFU HUO UNAWEZA KUKAA/ KUWEPO KWENYE UKUMBI ULIOBADILIKA NA KUWA KANISA
Jina la ukumbi huu liliibuka ghafla tu J2 iliyopita kutoka kwa kiongozi aliyekuwa anatoa matangazo siku hiyo

Kwa mujibu ya matangazo yaliyowahi kutolewa J2 nyingine iliyokuwa imepita nyuma (J2 ya tarehe 07/08/2022) kufuatia J2 husika

  • Hapakuwa na tangazo lolote J2 hiyo lililowajulisha waumini kuwa Ibada ya J2 inayofuata (yaani ile ya tarehe 14/07/2022), isingefanyika kwenye JENGO JIPYA bali kwenye UKUMBI WA SULEMANI
  • Aidha hapakuwa na tangazo lolote lile J2 hiyo lililowajulisha waumini wa Kanisa A, uwepo wa UKUMBI HUO WA SULEMAIN kama ulivyotajwa J2 hiyo
MARA YA MWISHO IBADA KUFANYIKIA NJE YA KANISA JIPYA

Mara ya mwisho Ibada kufanyikia nje ya “JENGO JIPYA”, ilikuwa ni miezi kadhaa iliyopita, na tangazo lake lilitolewa kabla kwenye J2 ya nyuma yake kufuatia ile ya Ibada iliyohamishiwa JENGO JIPYA. Hata hivyo, uhamisho wa Ibada hiyo nao pia uliambatana na maswali mengi yasiyjibika na ambayo mhusika aliwahi kuleta taarifa zake humu jukwaani

Vile vile Kiongozi aliyewahi kuhusika kuhamisha Ibada hiyo alikuwa ndiyo huyu huyu kiongozi wa sasa aliyekuwa anatoa matangazo J2 iliyopita

………………..inaendelea
 
KABLA YA KUENDELEA NA MADA ILIYOPO HEWANI: TUKIRUDI NYUMA KIDOGO HADI J2 YA TAREHE 07/08/2022

MOJAWAPO YA MATANGAZO YALIYOTOLEWA NA KM-A KWENYE MADHABAHU YA BWANA J2 YA TAREHE 07/08/2022


Mojawapo ya matangazo yaliyotolewa na KM J2 hiyo lilihusiana na muumini mmoja kufunguliwa baada ya kuwa amefungiwa, possibly sababu ilikuwa ni uzinzi.

KM-A alisimama madhabahuni J2 hiyo na kuwatangazia waumini wote kuwa kulikuwa na muumini aliyekuwa ametengwa na kuanzia siku hiyo alikuwa amefunguliwa tena. Sababu zilizopelekea muumini huyo kufungiwa hazikutajwa

MATANGAZO YALIYOTOLEWA NA KIONGOZI J2 ILIYOPITTA TAREHE 14/08/2022

Kwa mujibu wa matangazo ya J2 ya tarehe 07/08/2022, Kiongozi huyu hakupaswa kutoa matangazo hayo kwa sababu hapo kabla, kiongozi huyu hakuwa yule aliyekuwa ametangazwa kuwa angekuwa zamu wiki inayofuata

  • Aliyetangazwa kuwa angekuwa zamu ni Kiongozi yule aliyesimama kwa ajili ya kutoa chakula cha uzima siku hiyo
  • Possibly kutokana na jukumu hilo, Kiongozi wa zamu ilibidi awe replaced na kiongozi mwingine na hivyo kupelekea huyu aliyetoa matangazo J2 hiyo kushika nafasi ya Kiongozi mwenzake
MATANGAZO YALIYOTOLEWA SIKU HIYO: MOJAWAPO LILIKUWA LA ULAWITI NA UBAKAJI

Mojawapo ya matangazo yaliyotolewa J2 hiyo, kama kawaida lilihusiana na mambo ya ulawiti na ubakaji

  • Hapa mhusika alitarajia kusikia pia tangazo la ajali za barabani ambazo ndizo zimepamba moto wiki hii, hadi jana J2 zimeendelea kutokea; lakini kwa bahati mbaya hapakuwepo na tangazo la aina hiyo
  • Mbaya zaidi katika kusisitiza kuhusiana na tangazo hilo la ulawiti na ubakaji; kiongozi huyu alifanya kitendo cha aibu akidhihirsha kukosa kabisa hekima ile ya anayotakiwa kuwa nayo “kiongozi wa kiroho”
Kiongozi huyu alisema kuwa kuna wakati fulani aliwahi kushuhudia binti akiletwa chumbani na kufanyiwa mambo ya ajabu na room-mate wake huku na yeye akiwepo chumbani; kipindi kiongozi huyu alipokuwa anasoma chuoni

Wakati huo huo pasipo mtoa matangazo huyu kujua; akiwa anaongea haya yote kumbe ndani ya kundi la waumini wa Ibada hiyo, walikuwepo pia VIONGOZI WENGINE WAGENI, WAKUBWA KUTOKA MAKANISA MENGINE NA MMOJAWAPIO ALIKUWA NI KIONGOZI WA KIMATAIFA; ANAFANYA KAZI HADI NJE YA NCHI; yaani ni aibu tupu.

Uzuri tu ni kwamba viongozi hawa wageni, hawawezi kujua kuwa Ibada hiyo ilikuwa imehamia kwenye nyumba nyingine na kama watajua, basi hawataweza kujua sababu za kwa nini ilikuwa imehamia huko

HITIMISHO:

KM-A NAYE ATOA TANGAZO LAKE KUHUSIANA NA VYOMBO VIPYA VYA MUZIKI VILIVYOKUWA TAYARI VIMEWEKWA WAKFU KWENYE MADHABAHU HIYO YA UKUMBI WA SULEMANI WAKATI WA IBADA YA KWANZA


Baada ya KM-A kupanda juu madhabahuni; alitoa tangazo la VYOMBO VIPYA VYA MUZIKI VILIVYONUNULIWA HIVI KARIBUNI, vitakavyokuwa vinatumika kwa ajili ya mikutano ya injili inayoendelea kufanyika sehemu mbali mbali hapa nchini

KM-A alisema kuwa vyombo hivyo vilikuwa tayari vimewekwa wakfu kwenye Ibada ya kwanza na hivyo alivitoa tu ili waumini wa Ibada ya pili wavione

  • Possibly kulikuwa na uharaka wa aina fulani wa vyombo hivyo vya muziki KUWEKWA WAKFU HUKU MADHABAHU YA BWANA IKIWA IMEHAMIA KWENYE UKUMBI WA SULEMANI
  • Vinginevyo vyombo hivyo vingeweza kusubiria hadi J2 ijayo ya tarehe 21/08/2022 na vikawekwa wakfu kwenye Ibada ya J2 hiyo
Zaidi ni kuwa waumini hawa wakiwa wanatangaziwa kuwekwa wakfu vyombo hivyo vya Muziki kwa ajili ya injili J2 hiyo;, kuna LORI KUBWA JIPYA LILISHANUNULIWA AMBALO MIEZI KADHAA NYUMA LILIWAHI KUTANGAZWA TU KUWA LIMENUNULIWA, LAKINI HAIKUTANGAZWA KAMA LORI HILO LILIWAHI KUWEKWA WAKFU. Wakati huo huo ajali za malori zinaendelea kufululiza nchini

Mhusika hana uhakika kama Lori hilo liliwahi pengine kuwekwa wakfu kwenye mojawapo ya Ibada za kwanza, hana uhakika!

Kwa ujumla tu tangu ahamie tena Kanisa A (April 2017), ameshaona vyombo vipya vya moto vikinunuliwa Kanisani hapo lakini hajawahi kuviona vinawekwa wakfu waumini wakiwa wanashuhudia, achilia mbali hata kule kusikia tu tangazo la kwamba vyombo hivyo vya moto viliwahi kuwekwa wakfu.

Lori limenunuliwa na kuwasili Kanisani hapo ndani ya mwaka huu ambao Ibada karibia zotte zimekuwa zikiruka LIVE lakini mhusika hajawahi kusikia tangazo la chombo hicho cha moto kuwekwa wakfu

KIONGOZI MTOA MATANGAZO J2 YA TAREHE 14/07/2022:

KUHUSIANA NA TANGAZO LA ULAWITI NA UBAKAJI


Tangazo la ulawiti na ubakaji liliambatana na maombi ya siku tatu kuazia J5 hadi Ijumaa

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Your browser is not able to play this audio.



UPDATE: MONDAY 16TH AUGUST 2022

KWA WAUMINI WA KANISA A


MADINI MENGINE MUHIMU KUTOKA KWENYE SEMINA YA CA’S MWAKA 2013 HAYO HAPO
 
NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA KIONGOZI MTOA MATANGAZO J2 YA TAREHE 14/08/2022
Kwa usahahidi alionao mhusika ambao sehemu yake nyingine hawezi kuitoa humu jukwaani; ni kwamba kwa kipindi kirefu sana KIONGOZI huyu amekuwa akitafuta upenyo wa kuelekea kwenye vyombo vya sheria ila tatizo linalotokea ni kwamba kila anapotaka kufanya hivyo, mazingira yanakwenda kinyume na alivyotarajia. Tangu mwishoni mwa mwaka jana, kiongozi huyu amekuwa na mkakati huo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…