KWA WALE WALIOKUWEPO KANISA A JUMAPILI ILIYOPITA: WANAWEZA KUKUBALINA NA MHUSIKA KUWA TAA ZA NYUMA ZA GARI LA MHUSIKA ALIZOWAHI KUWEKA BAADA YA KUWA AMEVUNJA ZA AWALI KWA AJALI YA GARI, NDIYO ZILE AMBAZO BADO ZINATUMIKA KUFANYA MASHAMBULIZI YA KIROHO
KILE KILICHOTOKEA J2 ILIYOPITA BAADA YA MHUSIKA KUWASILI KANISANI NA HADI KUINGIZA GARI NDANI YA UZIO WA KANISA
Mhusika aliwasili Kanisa A na kukuta Ibada ya kwanza ikiwa tayari imeshamalizika, waumini wakiwa wanatoka nje na magari yao. Kutokana na hali hiyo, mhusika alilazimika kupaki nje kwa muda, akisubiria magari ya waumini wa Ibada ya kwanza yatoke kwanza
- Baada ya takribani nusu saa kupita, magari yote ya waumini wa Ibada ya kwanza yalikuwa tayari yameshatoka nje
- Baada ya hapo, mhusika aliamua kutoka nje kwenda kuchukua gari lake ili aje alipaki ndani ya uzio wa Kanisa
Hadi kufikia muda huo mhusika anatoka nje kwenda kuleta gari lake ndani ya uzio wa Kanisa, hakuna muumini wa Ibada ya kwanza hata mmoja aliyekuwa hajatoka
Magari yote ya waliokuwa wanatoka nje yalikuwa yameisha na yaliyokuwa bado yapo ndani yalikuwa yametulia kwenye parking zake kuonyesha kuwa yalikuwa hayatoki nje
Mhusika alienda akawasha gari lake na baada ya kufika usawa wa geti la kuingia Kanisani, kabla hajakata kona ili aingie ndani
- Mbele yake aliona gari aina ya VANGUARD nyeusi iliyokuwa tayari imeshaingia kidogo ndani ya geti
- Gari hii ilikuwa ni ya muumini wa Ibada ya pili aliyekuwa anajaribu kuingia ndani
Wakati gari ikiwa ipo bado usawa wa geti la kuingilia ndani,
ghafla gari nyingine nyeupe aina ya V8 yenye vioo tinted, ilianza pilika pilika za kutoka nje muda huo
- Kutokana na pilika pilika za V8 hiyo, VANGUARD ililazimika kurudi nje kwa muda kwa sababu V8 ni gari kubwa na wawili hawa wasingeweza kupishana kwa ubavu wakiwa ndani ya uzio wa Kanisa
- Kwa muda wote huu, mhusika alikuwa amesimama barabarani karibu na geti akishuhudia kilichokuwa kinaendelea ndani ya GETI LA NYUMBA HIYO YA IIBADA
Kwa configuration ya magari haya matatu namna yalivyokuwa yamekaa, yaani lile la mhusika pamoja na yale mengine mawili;
mhusika sasa alitakiwa ARUDI NYUMA KWA REVERSE GEAR, ili kuiruhusu VANGUARD iweze kurudi nyuma na hatimaye iweze kuacha nafasi kwa V8 kuweza kutoka nje
MHUSIKA ASTUKA KURUDI NYUMA KWA REVERSE GEAR.
ALICHOFANYA MHUSIKA NA GARI LAKE BAADA YA KUONA UPUMBAVU HUO UKIENDELEA HAPO GETINI
Badala ya kurudi nyuma kwa REVERSE GEAR kama ambavyo huwa anafanya siku zote, mhusika aliamua kuendelea mbele akilipita geti,uelekeo wa Barabara kuu ya Morogoro. Hii yote ilikuwa ni kukwepa kurudi nyuma kwa REVERSE GEAR kwa sababu anayajua madhara ambayo ameshayaona huko nyuma
Kabla hajaifikia Barabra hio, alipinda na kugeuza akaanza kurudi kule alikokuwa ametokea pasipo kutumia REVERSE GEAR
- Baada ya kufika tena usawa wa getini alipokuwa awali, ndipo aliweza kupishana sasa na V8 iliyokuwa na vioo tinted na hivyo kushindwa kumfahamu muumini aliyekuwa ndani ya gari hiyo
- Na kwa bahati mbaya vile vile alisahau kusoma namba ya gari hilo
Wakati huo VANGUARD ilikuwa tayari imeshaingia ndani. VANGUARD hiyo nayo pia ni ngeni Kanisani hapo ila inamilikiwa na mtu ambaye ni mwenyeji sana Kanisani hapo na ambaye hapo kabla alikuwa hatumi gari hiyo. J2 iliyopita ilikuwa ni mara ya pili kwa mhusika kumuona muunini huyo akiwa anatumia gari hiyo
Baada ya kuingia ndani, mhusika alikuta configuration ambayo ilikuwa haimruhusu kupaki gari akiwa amegeukia uelekeo wa kutokea
Kulikuwa na gari nyingi kiasi J2 hiyo na possibly kuna na baadhi ya magari ya watu wa Ibada ya kwanza ambao hawakuwa wameondoa magari getini
Mhusika alienda akapaki gari katika namna ambayo wakati wa kutoka
ILIBIDI AENDESHE GARI KWA REVERSE GEAR HADI KUTOKA NJE YA GATE LA KANISA.
J2 hiyo, humo ndani getini, hapakuwa na nafasi yoyote ya kumruhusu mhusika ageuze na kuendesha katika namna ambayo angeweza kutoka nje ya geti pasipo kutumia REVERSE GEAR
Zaidi ni kuwa, KIONGOZI ALIYETOA TANGAZO LA MAOMBI na ambalo halikuambatana na msisitizo wa KM-A kama ilivyo siku zote,
NI YULE AMBAYE ALIWAHI KUMSABABISHIA MHUSIKA AJALI YA KUTOBOA TAA ZA GARI LAKE NA HIVYO KULAZIMIKA KUNUNUA ZINGINE AMBAZO NDIYO ZILIZOPO KWENYE GARI LAKE MUDA HUU NA NDIZO ZINAZOPELEKEA AENDELEE KUTEGESHEWA KUENDESHA GARI KWA KUTUMIA REVERSE GEAR
Inaonyesha safari hii KM-A aliamua kuepuka malalamiko ya tangazo la maombi lenye kuambatana na ajali za gari; possibly ni kwa sababu alikuwa anajua ni nini kitatokea
BAADA YA KUWA AMEINGIA NDANI YA UZIO WA KANISA; KUELEKEA KWENYE NAFASI YA PARKING ALIFUATANA NA GARI NYINGINE HARRIER NYEUSI YA MAMA AMBAYE NI SHEMASI KANISANI HAPO
…………………….inaendelea