#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

UPDATE: FRIDAY, 07 AUGUST 2020



Inaendelea………………………..



UJANJA WA KUTUMIA SECRET CODE YENYE UHUSIANO NA MAANDIKO MATAKATIFU ANAYOSOMA MLENGWA/ MSHAMBULIWA

“SECRET CODE BY INTERCEPTION OF THE HOLY SCRIPTURES”



NAMNA BOOKMARKS ZA MHUSIKA ZILIVYOWEZA KUJULIKANA NA VIONGOZI WA KANISA A




Ukiondoa mafungu yanayotoka kwenye sura za Zaburi 119 na Wakolosai 3:1-17 ambayo watu wengi Kanisani na /au ofisini walikuwa wanamuona mhusika akiyasoma, mafungu ya kwenye bookmraks yenyewe haikuwa rahisi sana kwa mtu mwingine yeyote kuweza kuyajua kuwa yalikuwa yanatoka kwenye vitabu vipi. Hii ni kwa sababu yallikuwa ni mengi mno; yakiwa yamechukuliwa pasipo mpangilio wowote ule, japo yalipangana kwa kufuata vitabu husika, na pia namna ambavyo mpangilio wa vitabu hivyo ulivyo kwenye Biblia.

Hata hivyo mhusika anapenda aziongelee kidogo sura hizo mbili alizozitaja hapo juu, kabla hajaenda ndani kuelezea nini kilitokea hadi ikafikia bookmarks zake zikajulikana na mahasimu wake

Kuhusu sura hizi mbili Zaburi 119 na Wakolosai 3:1-17

  • Mhusika ameshabaini mpaka sasa kuwa, anapoanza kusoma sura nzima ya Zaburi 119 ambayo ina mafungu 176, huwa inamchukua takribani dakika 18 kuimaliza
  • Kutokana na ukweli huo hapo juu, si vigumu kwa mtu yeyote yule aliyekuwa na hamu ya kutaka kujua namna mhusika ambavyo huwa anaisoma sura hiyo, yaani kama huwa anaisoma yote au anaisoma kwa kuiikata sehemu
  • Kuhusiana na Wakolosai 3:1-17, sura hii amekuwa akiisoma hivyo tangu akiwa uhamishoni Kanisa B, na kuna siku alishawahi kuisoma mbele ya waumini wote wakati wa Ibada ya jioni, kwa kuikata katika mafungu huyo machache kama yalivyoonyeshwa hapa
  • Hivyo ilikuwa inajulikana bayana kabisa kuwa mhusika alikuwa anasoma sura hizi mbili kwa mtindo huo, siku nyingi huko nyuma tangu akiwa bado yuko uhamishoni Kanisa B
Kutokana na ukweli huu hapa juu, haikuwa kazi ngumu kwa Kiongozi Mkuu (KM) kuweza kushughulika na sura hizo mbili kwa sababu kulikuwa na njia nyingi tu za kumuwezesha kujua kuwa mhusika alikuwa anazisoma, na kwa jinsi gani. Hivyo baada ya mhusika kurudi tena Kanisa A, KM alianza mara moja kushughulia na sura hizo mbili kwa kuanza kufundisha somo lenye kichwa SISI NI WATU WA NENO, na wakati anafanya hivyo, huku akiwa katika mkakati mwingine wa kutaka kujua sasa ni mafungu gani mhusika alikuwa anasoma kwenye bookmraks zake. Baada ya muda wa mwaka na ushee hivi kupita, by August/ September 2018, KM akawa tayari sasa amekamilisha kazi hiyo na kuanza kufundisha somo jigine tena la pili, UPENDO KATIKA UTUMISHI WETU



TUKIRUDI SASA KWENYE NAMNA BOOKMARKS HIZO ZILIVYOJULIKANA NA TIMU YA KIONGOZI MKUU (KM)

Ni kwamba, baada ya mhusika kurudi kutoka uhamishoni Kanisa B, alikuwa na tabia ya kukaa kwenye viti vya pembeni kabisa upande wa kulia wa Kanisa, akiwa anaielekea madhahabu; na mara zote alikuwa anakaa kiti cha mwisho kabisa kwenye mstari husika na ambacho mara zote kilikuwa kinakuwa pembeni, kikiwa kimepakana na korido ambayo watu wengi walikuwa wanapita mara kwa mara.

Mara nyingi, mhusika alikuwa na tabia ya kukaa kwa mtindo huu, wakati wa kusubiria kuanza kwa ibada ya kwanza, mara baada ya kumalizika Ibada ya kipindi maarufu cha asubuhi kinachojulikana kama morning glory

Kwa hiyo bookmarks za mhusika zilijulikana kwa njia ya:

  • Kusomwa na watu waliokuwa wanapita pembeni mwa korido hiyo kwa kipindi chote kuanzia mara tu aliporiudi kutoka uhamishoni Kanisa B (April 2017) mpaka August 2018, KM alipoanza kufundisha somo la UPENDO KATIKA UTUMISHI WETU. Baada ya kuwa zimesomwa kikamilifu, ndipo KM alianza tena kufundisha somo jingine la UPENDO KATIKA UTUMISHI WETU
  • Ukiondoa waumini wengine waliokuwa wakipita mara kwa mara kwenye korido hiyo, miongoni mwa hao kati yao walikuwa Kiongozi X, Kiongozi W, Kiongozi mhubiri wa uzinzi, na kiongozi mwingine tena ambaye mhusika bado hajamwongelea kwenye taarifa hizi.
  • KM yeye hakuwahi kabisa hata siku moja, kupita kwenye korido hiyo kwa kipindi chote mbacho mhusika alikuwa akikaa kwenye sehemu hiyo ya pembezoni mwa nyumba hiyo ya Ibada, akisubiria kuanza kwa Ibada inayofuata
  • Kwa hiyo jumla ya viongozi waliokuwa wanapita mara kwa mara kwenye korido hiyo ni wanne, ukiondoa KM mwenyewe pamoja na Kiongozi mwingine ambaye bado yuko masomoni Dodoma
  • Hapa tunawaondoa tena na viongozi wengine vijana ambao wameanza kufanya huduma ya kuchunga hivi karibuni
  • Ikumbukwe pia kuwa, viongozi hawa walikuwa na haki zote za kupita kwenye korido hiyo tu kwa sababu ndiyo njia pekee iliyopo ambayo wanaweza kuitumia, wanapokuwa wanaelekea mbele madhabahuni
  • Kwa hiyo katika hili, kwa upande mwingine, mhusika yeye ndiye alikuwa amewafuata kwenye njia yao, japo nao pia vilevile hawakuwa na haki ya kumdukua, pamoja na kwamba alikuwa amewafuata kwenye njia yao
  • Mhusika anawakumbuka viongozi hao wanne kwa sababu mara zote alikuwa ananyanyuka kwenye kiti kusimama kwa ajili ya kuwasalimia, kila walipokuwa wakipita kwenye korido hiyo. Hii ni kwa sababu mhusika yeye mpaka leo bado anamini kuwa katika hali ya kawaida, si sahihi kumsalimia SENIOR ukiwa umekaa kwenye kiti, yeye akiwa amesimama
  • Hicho ndicho kitu pekee kinachomfanya awakumbuke vizuri viongozi hao wanne aliokuwa akisimama mara kwa mara kwa ajili ya kusalimiana nao
  • Kwa hiyo udukuzi kwenye bookmarks za mhusika, ulikuwa unafanywa na viongozi hao pindi walipokuwa wanapita wakitokea nyuma kuelekea mbele madhabahuni, mhusika akiwa anasoma mafungu hayo, huku mwenyewe akiwa amewaelekezea kisogo
  • Kilichokuwa kinafanyika ni kwamba wakiwa bado wapo nyuma ya mhusika huku wakitembea kuelekea mbele, viongozi hao walikuwa wanaweza kusoma headings za mafungu aliyokuwa akisoma, ukizingatia kuwa headings hizo ziko kwenye font ya rangi ya blue, ambayo pia ni rangi tofauti na ile ya mafungu; yenyewe yako kwenye font rangi nyeusi
  • Kwa hiyo walikuwa wanasoma headings tu na kuzirekodi, na ilikuwa ni rahisi sana kuzisoma kwa sababu ya kuwa ziko fupi na zikiwa kwenye rangi tofauti na maandishi mengine. Zilikuwa zinasomeka kwa urahsi zaidi hata kwa umbali mrefu
  • Mkakati huo ulifanyika kwa kipindi cha angalau mwaka mzima. Hii ni kwa sababu bookmarks hizo ni nyingi sana. Tuseme mhusika akiamua kuzisoma zote kwa mkupuo mmoja, huwa zinamchukua angalau zaidi ya saa nzima kuanzia kitabu cha Mwanzo mpaka kile cha mwisho, yaani Ufunuo
  • Baada ya kuwa wamepata continuation ya bookmarks hizo kuanzia MWANZO mpaka UFUNUO, ndiyo sasa KM akaingia kazini kuanza kushughulika nazo kwa ku-embed secret codes zake, kati ya mafungu hayo ya mhusika, akifundisha somo la UPENDO KATIKA UTUMISHI WETU
Hivi ndivyo bookmarks za mhusika, zilivyoweza kujulikana na viongozi hao



HITIMISHO:

Inaonyesha kuwa, baada ya bookmarks za mhusika kujulikana na viongozi hao:

  • Walizikabidhi kwa KM
  • Wao nao walibaki nazo pia, japo details za ushahidi kuhusu hili si za lazima sana kwenye mada hii
Baada ya hapo, hatimaye tena ndiyo akakaribishwa Kiongozi / mhubiri mgeni ambaye mhusika alipata nafasi ya kumkaribisha nyumbani kwake.

Labda tu kwa kifupi sana kwa sasa, kiongozi huyu mgeni

  • hakuwa amepewa jukumu la kwenda kumpa mafungu hayo aliyompa mhusika, na ambayo yamepelekea mhusika kuandika haya yote aliyoandika kuhusiana na mafungu hayo ya Biblia
  • Jukumu halisi alilopewa lilikuwa jingine kabisa, mhusika ataliongelea kwenye sehemu itakayofuata
  • Ni kweli kwamba alitakiwa pia awe na mistari ambayo angemwachia mhusika baada ya kuwa wamefanya maongezi, lakini mgeni huyu alifanya KOSA LA KARNE kumwachia mafungu yale ambayo yalihusiana na taarifa za udukuzi kutoka kwenye bookmraks zake (mhusika)
  • Alitakiwa ampe mafunngu ambayo yangekuwa hayajatokana na udukuzi wa bookmarks zake (mhusika),
Kwa kufanya hivyo, mhusika asingeweza kujua chochote kuhusiana na udukuzi uliokuwa tayari umeshafanywa kwenye bookmarks hizo, na pia vilevile kuja na mada hii aliyonayo hapa muda huu. Ni kwa sababu hangeweza kujua kama bookmarks zake zilishadukuliwa na kuanza kutumika kutoa mafundisho madhabahuni yenye madhara kwake (mhusika)

Kwa kifupi tu ni kwamba udukuzi huu ulisababisha madhara makubwa sana kwa mhusika. Mashambulio ya kila mara ambayo yalimgharimu muda pamoja na fedha nyingi sana



………..itaendelea



Mathayo 19:14

Mathayo 23:23

Mathayo 23:24



Mathayo 19:14

Lakini Yesu akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu; wala msiwazuie; kwa maana walio mfano wa hao, ufalme wa mbinguni ni wao.



Mathayo 23:23

Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache.



Mathayo 23:24

Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia.



MUBARIKIWE TENA NA BWANA


Next: Nama mhusika alivyoweza kumkaribisha na kuktana na mhubiri/ kiongozi mgeni nyumbani kwake na yaliyojiri katika maongezi yao

MwiH
elly obedy
 
Ile ku scrow down tu nije nikujibu nimechoka. Hivi kuna mtu kweli amesoma vyote hivi ??!!
Hahaaa😹😹huu uzi niliuona toka enzi za corona kila nikitaka kuufungua roho inakataa...Leo kujaribu kufungua nimechoka kabisa.
Nyuzi kama hotuba ya bajeti,aisee ni shida.
 
Stay tuned for today's update. Anachofanya hapa mhusika ni kutoa summary, maana akitaka kueleza yote inaweza ikachukua miaka. Zaidi ni kuwa kinachoendelea Kanisani ni 5% na 95% ya mambo yote iko ofisini, ambako hadi barua za kutishiwa kufukuzwa kazi alishawahi kupewa, halafu baada ya miaka kadhaa tena, zikafutwa bila kuonyesha sababu yoyote kwa nini zimefutwa. Hawa wa Kanisani wanatumiwa tu kucheza ngoma ambayo mziki wake hasa upo ofisini, ngoma ya mziki huo huwa inapigwa ofisini siku zote na ni miaka mingi sasa. Sasa haya ya ofisini inabidi asiyaongele akae kimya kwa sababu akiyaongelea, anaweza akafukuzwa kazi!
 
UPDATE: MONDAY, 12 AUGUST 2020



Inaendelea………………………..



NAMA MHUSIKA ALIVYOWEZA KUKUTANA NA KUMKARIBISHA MHUBIRI/ KIONGOZI MGENI NYUMBANI KWAKE NA YALIYOJIRI KATIKA MAONGEZI YAO


Katika kuelezea kwa kifupi mazingira ambayo yalipelekea mhusika kukutana na Mtumishi Mgeni wa Mungu (MMM), mhusika anaomba awarudishe nyuma wasomaji hadi muda kipindi alipokuwa uhamishoni Kanisa B

Ni kwaba ilikuwa ilikuwa J2 moja mhusika akiwa bado uko huko uhamishoni Kanisa B, ndipo alipobahatika kutana na MMM.

  • IJ2 hiyo MMM alipewa nafasi ya kuhudumu Kanisani hapo
  • Baada ya huduma Ibada kuu J2 hiyo, MMM alifanya mambo mawili makubwa yafuatayo
  • MOJA: Alipitisha harambee kwa muda mfupi sana ambayo ilimuwezesha kukusanya kiasi cha fedha taslimu kisichopungua TZS 400,000/= (laki nne)
  • PILI: Aliwaita mbele ya madhababhu akina mama wajane, kwa ajili ya kuwatamkia baraka. Wakati wakiwa wanajiandaa kwa ajili ya kuitikia wito huo, akahisi kama wanataka kukwepa wito wake, kitu kilichopelekea awakaripie kwa kuwaambia “NIMESEMA AKINA MAMA WAJANE WAPITE MBELE, ……, KWA SABABU WEWE HATA UKIJIFICHA NI MJANE TU
Maneno hayo yaliyo kwenye bold, hayakumfurahisha sana mhusika kwa sababu hayakuwa yamekaa kiroho sana, na possibly ndiyo yalisababisha amkariri sura MMM tangu siku hiyo, ukizingatia kuwa aliokuwa anawaita kwa ajili ya mibaraka, lilikuwa ni kundi la watu ambao halitakiwi kuburuzwa kwa namna yoyote ile na mtu yeyote yule bila kujali mburuzaji ni mtumishi wa Mungu ama la

Zaidi ni kuwa siku hiyo MMM alijitambulisha pia kwa umri wake akisema kuwa ana miaka zaidi ya 80. Hapa sasa ilikuwa ni kabla ya April 2017



BAADA YA MHUSIKA KURUDI TENA KANISA A AKITOKEA UHAMISHONI KANISA B APRIL 2017:

Ilitokea kwa mara nyingine tena, MMM akaonekana na akapewa nafasi ya kutoa huduma kwenye Ibada kuu, safari hii sasa kwenye Kanisa jingine, yani Kanisa A

  • Hiyo sasa ilikuwa ni August /Septemba 2018
  • Ilikuwa ni zaidi ya mwaka tangu mhusika akutane kwa mara ya kwanza na MMM
  • Mhusika alimkumbuka MMM
  • Wakati wa huduma kanisani hapo, MMM aliuliza akitaka kujua ni waumini wangapi waliokuwa wanamfahamu
  • Baadhi ya waumini walinyosha mikono, mhusika akiwa ni mmoja wao
  • Baada ya huduma J2 hiyo, safari hii MMM hakufanya harambee kama alivyofanya kule Kanisa B, wala hakuombea wajane isipokuwa alitoa namba yake ya simu kwa Kanisa zima
  • Namba hii ilikuwa ni kwa wale watakaohitaji msaada kutoka kwake
  • Mhusika naye alichukua namba hiyo ya simu
  • Ndani ya wiki iliyofuata, mhusika aliwasiliana na MMM kutaka kujua kama alikuwa na nafasi; alikuwa anahitaji msaada kutoka kwa MMM kwenye mambo kadhaa yayokuwa yakimtatiza kwa kipindi hicho
  • MMM alikubali kuwa nafasi anayo, na mhusika aliwasha gari na kuanza safari ya kumfuata sehemu aliyokuwa amefikia, kwani yeye alikuwa ni mgeni hapa dare s Salaam
  • Kwa maelezo yake, MMM alisema kuwa anachunga Kanisa moja huko Kongwa, Dodoma
  • Alikuwa amefikia Moshi Hotel iliyopo Manzese Tip Top
Mhusika hakupata shida ya kumfuata kwa sababu yeye amekulia meneo hayo, na kuna rafiki yake ambaye ana ofisi maeneo, nyuma ya hiyo Moshi Hotel. Walikubaliana kukutana kwenye kituo cha mafuta kilichopo karibu, na mhusika alifika hapo kwa muda waliokubaliana na kumchukua MMM. Kitu cha pekee alichokiona kwa MMM siku hiyo ni kuwa alikuwa amevaa kofia. Na kwa sababu mara mbili zote alizowahi kukutana na MMM huyo ilikuwa ni katika mazingira ya Kanisani, mhusika hakuweza kujua kama MMM alivaa kofia kwa siku hiyo tu au huwa anavaa siku zote. Hili swala la kofia ni muhimu kulijua kwa sababu wakati mwingine limekuwa likitumiwa na watu kama comouflage ya wao kujificha ili wasijulikane kirahisi na watu wasiohusika, especially wanapokuwa wapo kwenye secret mission. Kwa mfano mstaafu ambaye mhusika amewahi kumwongelea huko nyuma, yule aliyewahi kukaribishwa katika mazingira ya ofisini kwa mhusika na kuendesha kikao ambacho kilithibitisha ulipwaji wa maslahi ambayo mhusika amekuwa akiyadai kwa miaka kadhaa pasipo mafanikio, naye pia alivaa kofia siku hiyo, ilhali katika kipindi chote ambacho mhusika alipata kumfahamu mtu huyu (kabla ya kustaafu kwake), hakuwahi hata siku moja kumuona akiwa amevaa kofia, kwa kipindi cha takribani zadi ya miaka 15. Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa mhusika siku hiyo kumuona mtu huyu naye akiwa amevaa kofia pia

Wakiwa ndani ya gari wakielekea nyumbani, mhusika ilibidi aweke wazi mambo kadhaa kwa MMM akimweleza kuwa yeye (mhuiska)

  • Anahitaji msaada wa kiroho lakini si mafundisho ya kwenye Biblia wala si maombezi
  • Anahitaji kuelekezwa tu namna ya kutatua baadhi ya mambo ya kiroho ambayo yamemtatiza
  • Alisisitiza kuwa HAHITAJI KULISHWA SAMAKI, ANAHITAJI KUFUNDISHWA NAMNA YA KUVUA SAMAKI. Kwa hiyo alisisitiza sana kuwa msaada aliuohitaji kutoka kwa MMM unatakiwa uwe kwenye mfumo wa namna hiyo
Baada ya MMM kuwa amesikia hitaji la mhusika, yeye alijibu kwa kifupi tu akisema NGOJA KWANZA TUFIKE NYUMBANI

Baada ya MMM kufika nyumbani, mhusika alieleza kwa kina kilichokuwa kinamsibu.

  • lilikuwa ni tatizo la bidhaa alizokuwa ananunua kurushiwa mapepo lakini kwa wakati huo, alikuwa hajui kama hata bidhaa nazo zinaweza zikarushiwa au zikawa na mapepo.
  • Alikuwa anaona madhara na kujua kuwa yanatokana na bidhaa hizo, lakini alikuwa hajui kama ni mapepo, na alikuwa hata hajui hata namna ya kulitatua tatizo hilo
  • Yeye kwa wakati huo, alikuwa anajua kuwa ni binadamu tu anayeweza akarushiwa pepo na si bidhaa au kiumbe kingine tofauti na binadamu
Mhusika atalielezea kwa kina swala hili atakapokuwa anatoa wasifu wake wa nyuma wa kiroho kwenye sehemu itakayofuata. Kwa sasa itoshe tu kueleza kuwa alikuwa ananunua bidhaa ambazo akishakuwa nazo ndani nyumbani kwake au akishaanza kuzitumia, zinaonyesha kuwa haziko kawaida, na kwamba alikuwa na uwezo wa kujua hilo tu lakini pasipo kuwa na ujuzi wa namna ya kulirekebisha

Kwa hiyo, kwa kifupi tu ni kwamba mhusika alimkaribisha MMM ili ampe msaada wa namna ya kutatua tatizo hilo na kama ikiwezekana, apate msaada wa mafungu kutoka kwenye Maandiko Matakatifu yanayoweza kumsaidia kuziwekea kinga ya kiroho, bidhaa hizo alizokuwa akinunua

Baada ya mhusika kuwa amemweleza MMM hayo yote wakiwa tayari wapo nyumbani kwa mhusika:

  • MMM akawa hatoi majibu yanayoeleweka, au majibu ya moja kwa moja
  • Akawa anauliza uliza maswali zaidi, halafu mhusika akiyajibu, MMM anarukia tena kwenye kitu kingine au anauliza swali jingine tofauti
Hatimaye wawili hawa walipoteza FOCUS yao ya kufundishana KUVUA SAMAKI, badala yake waliingia kwenye KULISHANA SAMAKI, na ilipofikia hatua hiyo, mhusika alistukia anamuona MMM anasimama na kuanza kufanya maombi ya kimya kimya huku akigusa:

  • Kila kitu kilichokuwa sebuleni kuanzia viti meza, meza ya TV, TV yenyewe, Radio n.k
  • Kuta za nyumba huku akiwa anatembea, mikono akiwa ameiweka juu ya kuta mithili ya mtu aliyewekwa ukutani akisechiwa na Polisi baada ya kuwa amekamatwa
MMM akiwa amebadilika na kuwa katika mood ya namna hiyo, angeweza hata kufungua mlango wa kuingia master bedroom, ili aendelee na maombi hayo ila aligundua kuwa mhuiska hakuwa tayari kwa hili

Kwa ufupi tu ni kwamba, mpaka hapa MMM:

  • Hakufanya kile alichokuwa amemwahidi mhuiska kuwa atafanya, maana wakiwa bado wako njiani mhusika baada ya kuwa ameeleza hitaji lake kwa MMM, mwenyewe alijibu kwa kusema NGOJA KWANZA TUFIKE NYUMBANI
  • Kufika nyumbani kwa mhusika kwake ilikuwa muhimu zaidi kuliko kufanya kile ambacho mhusika alikuwa amemwitia / ameomba asaidiwe. Target kubwa ya MMM ilikuwa kufika nyumbani kwa mhuiska
  • Alianza kufanya maombi ya kimya kimya nyumbani kwa mhusika, kitu ambacho mhusika hakuwa anahitaji
  • Hakuweza kumwonyesha mhusika tiba halisi ya tatizo alilokuwa nalo, bidhaa alizokuwa akinunua na hatimaye kupelekea matatizo anapozitunia
  • Hakufanya kile ambacho aliitiwa, alifanya kile alichotaka kufanya mwenye, na hakufanya hivyo kwa bahati mbaya au kwa kupitiwa
As a temporary measure, yeye (mhusika) chochote kile kilichokuwa kinamletea matatizo alikuwa anakitupa bila kujali gharama. Kuna kipindi aliwahi kuchana na kutupa kiatu kipya ambacho alikinunua kwa TZS 180,000/= . Pia ni bidhaa nyingi tu za thamani ambazo alikuwa akizitupa, mostly sabuni za kuogea na vitu kama kahawa au majani ya chai

Wakati MMM anakaribia kuondoka, ndiyo mhusika akaomba angalau amwachie pia mafungu ya kwenye Biblia, na ndipo MMM alipomtajia kutoka kichwani, mafungu ambayo tayari ameshayaongelea hapo juu, ambayo ndiyo yalipelekea sasa mhusika kuona pattern nyingine kwenye mafungu aliyokuwa natumia Kiongozi Mkuu wakati akifundisha mafundisho yenye kichwa SISI NI WATU WA NENO pamoja na LUPENDO KATIKA UTUMISHI WETU.

Vile vile, wakati mhusika anamchukua MMM kumrudisha Hotelini, mtu huyu alirudia kufanya kosa jingine tena. Aliuliza swali akisema HILI GARI NI LA KWAKO AU LA OFISINI?

Hili swali lilimpa indicator nyingine tena mhusika kwa sababu MMM

  • Alifika nyumbani kwa mhuiska na kukiri kuwa kuna majirani zake na mhusika anawafahanu, na kwamba alishawahi kufika nyumbani kwao
Hawa walikuwa ni wale ambao kwa sasa ni wastaafu na kwa muda huu walishahama. Kipindi hicho walikuwa bado wapo, ila walikuwa wameshabadilisha nyumba ya Ibada kutoka Kanisa A na kuhamia Changanyikeni

  • Alikuwa anajua kuwa nyumba hizo ni za watumishi wa umma
  • Si mtu ambaye uelewa wake uko katika kiwango (au hata kukarinbiana tu na kile) cha kutoweza kutofautisha kati ya namba za usajili za gari ambalo ni la umma na lile ambalo ni la mtu binafsi
  • Alikuwa ameziona namba za gari la mhusika kipindi mhusika anampokea MMM na kumchuka pale kituo cha mafuta Shekilango


….itaendelea

2Wakorintho 5:14

2Wakorintho 5:15

2Wakorintho 5:17



2Wakorintho 5:14

14
Maana, upendo wa Kristo watubidisha; maana tumehukumu hivi, ya kwamba mmoja alikufa kwa ajili ya wote, basi walikufa wote;

2Wakorintho 5:15

15 tena alikufa kwa ajili ya wote, ili walio hai wasiwe hai tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa akafufuka kwa ajili yao.



2Wakorintho 5:17

17 Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.



MUBARIKIWE TENA NA BWANA​



NEXT: 1 Yale ambayo mhusika alikuja kuyabainisha kuwa MMM alikuwa ametumwa kuja kuyafanya nyumbani kwake mhusika

2 Wasifu wa kiroho wa mhusika tangu aanze kuwa muumini wa kanisa A hadi siku wanakutana na MMM


MwiH
elly obedy
 
SAHIHISHO MUHIMU

Fungu lilolokuwa kwenye bookmarks za mhusika, juu ya 2Wakorintho 5:14 lilisahaulika.Ni 2Wakorintho 4:16. Kwa hiyo mpangilio wa mafungu haya unatakiwa uonekana kama ifuatavyo

2Wakorintho 5:14

2Wakorintho 4:16

2Wakorintho 5:15, 17





2Wakorintho 4:16

16 Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.



2Wakorintho 5:14

14
Maana, upendo wa Kristo watubidisha; maana tumehukumu hivi, ya kwamba mmoja alikufa kwa ajili ya wote, basi walikufa wote;

2Wakorintho 5:15

15 tena alikufa kwa ajili ya wote, ili walio hai wasiwe hai tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa akafufuka kwa ajili yao.



2Wakorintho 5:17

17 Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.
 
NYONGEZA NYINGINE MUHIMU

Kuna mbinu nyingine tena Kiongozi Mkuu (KM) aliwahi kuitumia kipindi fulani, akiwa anafundisha maandiko matakatifu kwenye Ibada za jion za kila wiki J5. Kwa bahati mbaya mhusika hakuweza kuwa na mafungu yaliyotumika kwenye Ibada hizo kwa sababu ilibidi aikimbie, baada ya kuwa amegundua hilo. Alisikiliza kwenye J5 ya wiki ya kwanza, halafu J5 ya wiki iliyofuata, KM alipoanza tu kufundisha akiwa na uelekeo ule ule wa J5 ya wiki iliyopita, mhusika alitoka kwenye Ibada hiyo, akawasha gari na kurudi nyumbani

Ni kwamba ulikuwa unatumika utaalamu fulani wa kufundisha Maandiko Matakatifu kwa kutumia mistari ambayo alikuwa anaichezesha katika namna ambayo ilimuwezesha kuwa anamponda Yesu na kumsifu Shetani.

Utaalamu wa kutumia Maandiko Matakatifu kufanya Ibada za sanamu upo, na Kiongozi Mkuu anazijua mbinu hizo! Mhusika anatamani angekuwa na mamlaka juu ya kiongozi huyu, mbinu zote hizi ambazo huwa anatumia huyu KM lazima angeziweka wazi, zote kabisa!
 
NYONGEZA MBILI MUHIMU

1 KUHUSIANA NA PROGRAM YA UJENZI WA “JENGO JIPYA”


  • Mhusika alianza kuabudu Kanisa A mwaka 2011
  • Kipindi anaanza kuabudu hapo, kuna staffmate wa mhusika naye alikuwa na kawaida ya kuwa anaenda kuabudu mahali pale, japo kwa nadra sana
  • Staffmate huyu akawa anamwambia mhusika kuwa “UNAABUDU KWENYE KANISA LA KIONGOZI YULE AMBAYE HUWA ANAJENGA KANISA HALIISHI”?
  • Kwa sababu wakati huo ilikuwa ni mwaka 2011, na Kanisa inasemekana lilianza kujengwa mwaka 2005, mhusika akawa anapuuzia hoja za staffmate wake
  • IIlipofika mwaka 2017, mhusika akampigia staffmate (alikuwa tayari ameshastaafu) kumjulisha kuwa kumbe alikuwa yuko sahihi
  • Alimweleza kuwa Kanisa hilo bado halijaisha mpaka muda huo, na kuwa halina dalili zozote za kuisha
KITU AMBACHO NI CHA PEKEE SANA KUHUSIANA NA KANISA HILO JIPYA, YAANI “JENGO JIPYA”

  • Mhusika hana uhakika ila anahisi kama linaweza kuja kuwa miongoni mwa makanisa machache sana yaliyotumia gharama kubwa sana kujengwa, aidha Afrika Mashariki au hata kwa Afrika nzima
  • Kwa makanisa yaliyopo Tanzania mhusika ana imani kuwa possibly hili ndiyo litakuwa linaongoza kwa sasa kwa kuwa na gharama kubwa, pamoja na kwamba bado halijaisha
  • Kama hakosei, mpaka muda huu, limeshatumia zaidi ya Billion 2, na bado halijaisha, liko njiani likiwa linahitaji tena angalau Billion moja, kwa mujibu wa taarifa za mwisho zilizotolewa Kanisani wakati wanapitisha mchango wa ujenzi awamu ile ya mwisho
Fedha zote hizi ni zaka na sadaka zinazotolewa na wale waumini ambao muda wote wanakaa wanatuhumiwa kuwa ni wazinzi, wanawageuza wake zao nyuma, na wasiokuwa na Roho Mtakatifu. Bado hapo pia waumini hao hao ndiyo wanaotoa mamia ya mamillion mengine kwa ajili ya mikutano ya Injili kila mwaka unaokuja. Kwa mwaka wanatoa michango miwili mikubwa, mmoja wa ujenzi na mwingine wa Injili

Viongozi hawa hawana hata ile hekima ya kusema angalau mwaka huu tuahirishe mikutano ya Injili tujenge Kanisa liishe halafu mwakani ndiyo tutaendelea na mikutano ya injili, hilo halipo bora punda afe mzigo ufike. Hii ni kwa sababu mikutano ya Injili kwao ina priority zaidi kuliko huo ujenzi wa Kanisa. Yaani wana roho ya kwenda kujenga nyumba kwa wengine, wakati kwao wanalala nje na kunyeshewa mvua huku waumini wao wanaotoa hizo hela za mikutano ya injili, wakitiririkiwa maji yaliyochanganyikana na kinyesi, na kuvuta hewa chafu wakati wa Ibada

Juzi kwenye TV walionyesha Kanisa moja Dodoma limejengwa kwa miezi kadhaa ndani ya mwaka huu tu, na kwa gharama ya Million 90 tu na inaonekana ni nyumba nzuri mno ya Ibada, na ni kubwa sana. Million 90 tu



2 KUHUSIANA NA TANGAZO JINGINE JIPYA LA UZINZI KANISANI (LA HIVI KARIBUNI SANA)

Wiki chache tu zilizopita, Kiongozi Mkuu (KM) alisimama tena madhabahuni kutoa tangazo la kumsimamisha ushirika mtu ambaye ilisemekana kuwa ni mzinzi.

Kosa alilofanya (KM) wakati anatoa tangazo hilo ni kwamba:

  • Alidai kuwa mtu huyo wamemvumilia kwa takribani miaka 11
  • Kama umemvumila kwa miaka karibia 11, why now? Why not let’s say, 8 years ago? 5 years ago? Au juzi juzi kwenye kipindi ambacho mahubiri ya uzinzi yalikuwa yamepamba moto sana?
  • Kwa nini huyu mkongwe wa zamani, walimwacha kwenye kundi la hivi karibuni na wakawasimamisha wengine ambao ni wapya?
  • Unawezaje kuendelea kusimamisha wakosaji wapya wa sasa na kwa awamu nyingi tena tofauti tofauti, halafu katika awamu hizo zote, ukawa unamwacha wa zamani ambaye ni mkongwe? Mtumishi wa Mungu anaweza kupitiwa pitiwaje hadi akafikia kuwa anchukua hatua kwa mtindo huu?
Kwa sababu chances ni kwamba hata hawa wapya wanaweza kuwa walikuwa wanakuwa influenced na yule mkongwe wa siku zote, aidha kimwili (kwa kumuona kwa macho akitenda uovu huo) au kiroho; kwamba roho yake chafu ialiyonayo ilikuwa nasambaa AUTOMATICALLY na kuwapata watu wengine Kanisani na hivyo kupelekea na wao kuwa kama yeye.

Hivi kwa mfano, ukishajua pale lilipo shimo la nguchiro mharibifu wa mahindi shambani kwako, unaenda tena kumsubiria shambani ambako huwa anakuja kuharibu mazao badala ya kuziba shimo la makazi yake anapoishi na yeye akiwa yumo ndani shimoni?



Mbali na hayo, kama kiongozi umeshafikia hadi hatua ya kuwa unatangaza waumini waliobadilisha imani na kufunga ndoa kwenye madhehebu mengine, kuwa ni wazinzi, maana yake ni kwamba you are so strict kwamba huwezi ukawa na uvumilivu wa kipindi kirefu chote hicho. Angalau basi ingekuwa hata miaka mitatu, Kumi na moja? Haileti mantiki kichwani.

Kwa hiyo mhuiska yeye anadai hawa watu wamebadilisha tu sequence na technique za ku-invoke message zao wanapokuwa wamesimama madhabahuni. Na wakishaanza kufanya hivyo, ujue kuna plan mbele, muda siyo mrefu

Ukweli usiopingika ni kuwa mtu akishaanza kufanya mambo ya ajabu namna hii huwa siyo rahisi tena akamgeukia Mungu, ataendelea kutwanga hivyo hivyo tu mpaka siku lishetani litakapomkamata vizuri. Ni kwa sababu anakuwa anafanya mambo chini ya laana fulani hivi ambayo hawezi kuiondoa au kuikwepa tena

MUBARIKIWE TENA NA BWANA

MwiH
elly obedy
 
DOKEZO MUHIMU

1 SIFA PEKEE YA KANISA A LINALOONGOZWA NA KIONGOZI MKUU(KM)

  • Lina sifa moja tu ambayo ni UTOAJI
  • Possibly kwa sababu kuna kipindi fulani (nadhani ilikuwa mwaka 2011 au 20122) KM mwenyewe alifundisha kwa kipindi kirefu sana, somo juu ya UTOAJI
  • Huwa linasifiwa sana hasa na viongozi wageni wanaofika kuaubdu au kuhudumu kanisani hapo
  • Kwa utaoaji, inasemekana linaongoza kitaifa
2 UPOTOSHAJI MWINGINE WA MAKUSUDI WA MAANDIKO MATAKATIFU AMBAO UMEKUWA UKIFANYWA NA KM

Fungu la maandiko matakatifu kutoka Injili ya Mathayo 16:18 linasema hivi:

“Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.”

Kuna kipindi alikuwa anafundisha somo ambalo mojawapo ya mafungu makuu ilikuwa ni Mathayo 16:18

  • Aikuwa analitumia fungu hilo kama SECRET CODE pia
  • Alichokuwa akifanya ni kupotosha maana halisi ya fungu hilo
  • Akiwa madhabahuni, akishasoma fungu hilo, kwa haraka haraka alikuwa anatamka maneno akisema kuwa YESU ANAJITAJA MWENYEWE KWAMBA YEYE NDIYE MWAMBA, akimweleza Petro……………
  • Ukweli ni kuwa PETRO ANAAMBIWA NA YESU KUWA YEYE (PETRO) NDIYO MWAMBA, ambapo Yesu anasema atalijenga Kanisa lake
  • Ndiyo maana hata elimu ya miamba inaitwa PETROLOGY, hapa Petro ikimaanisha mwamba
  • KM alikuwa nafanya hivi kwa makusudi kwa sababu fungu hili lipo kwenye kipeperushi ndani ya gari la husika, tangu mwaka 2013
  • Kwa hiyo alikuwa anapotosha fungu hilo akilitumia kama SECRET CODE ya kuondoa ulinzi wa fungu hilo kwenye gari la mhusika
Mara ya mwisho alipofanya hivyo, ilibidi nhusika amshirikishe Mwalimu Shemasi. Alilalamika kwa mwalimu wake huyo na kumweleza wazi kabisa kuwa KM alikuwa anafanya hivyo si kwamba hajui maana ya fungu hilo, bali alikuwa anafanya kwa makusudi. Mwalimu Shemasi ni shahidi katika hili.

By the way, gari la muhsika liliwekwa wakfu na watu watatu tu ambao ni KM, Kiongozi X na Kiongozi yule mhubiri waUzinzi. Ilitokea kwa namna gani stori yake ni ndefu itafuata baadaye. “Mama wa kiroho” ndiye alitengeneza setup hiyo ya uhakiaka na inaonyesha alikuwa amejiandaa kwa siku nyingi kuhakikisha kuwa watu hao pekee ndiyo wanashiriki kwenye kuweka wakfu gari hilo. Yapo mengi yatakuja katika hili

Kuna kipindi (mwaka 2013 au 2014) KM aliwahi kukaribisha kiongozi mgeni kuja kuhudumu pale Kanisani akitumia secret code ya fungu hilo la Mathayo 16:18. Ilikuwa ni kwenye semina ya siku za katikati ya wiki. Baada ya mhusika kusikiliza semina hiyo kwa muda wa siku tatu (J5 hadi IJumaa), alimgundua mtumishi huyo na hivyo J2 yake aliacha kuhudhuria Ibada Kanisani, ambapo siku hiyo ndiyo lilikuwa hitimisho la Semina ya mtumishi huyo mgeni. Huwa hana kawaida ya kukosa Ibada za J2 na ukimkosa Kanisani J2 ujue kuna sababu ya msingi, tena kubwa

Swala la naman gari lake lilivyowekwa wakfu atalileta kwenu kama swala linalojitegemea pamoja na mambo mengine ya ziada yanayohusiana na “mama wa kiroho”

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Mhusika anazidi kuwasisitiza wasomaji waulize maswali. Hii itasaidia kupima authenticity ya kile amabcho ameamua kukileta kwenu wasomaji. Tukio la kwanza kabisa lisiliokuwa la kawaida kwake, alilo na ushahidi nalo ni la miaka 20 iliyopita na alikuwa nje ya Afrika, nje ya nchi. Tafadhali mnaombwa muulize maswali
 
Alikuwa anaishi hapa: (angalia kuanzia dakika za 1:38 mpaka ya 1:48 na pia dakika za 2:24 mpaka ya 2:30 utaona kuna jengo la ghorofa la mduara). Hapo ndipo yalikuwa makazi yake kwa takrinbani wiki nane hivi). Najua baadhi yenu mtaweza kupafahamu vizuri. It was just a few meters away from the Railway Station you are ssing here!


 
Nyongeza muhimu:
Kuhusiana na sifa pekee za Kanisa A nilizozielezea hapo juu, ni kwamba ukiona waumini wa Kanisa A wamesifiwa na viongozi wao, iwe ni wa ndani ya Kanisa au hata nje, ya Kanisa, basi ni kwenye swala moja tu la UTOAJI. NI katika sifa hiyo tu ambayo mhusika amekuwa akisikia waumini wa Kanisa A wanasifiwa;, kwenye utoaji tu basi. Kwa hiyo mhusika yeye anadai kuwa hajawahi kusikia waumini hao wakisifiwa kwa sifa nyingine yeyote nzuri tofauti na hiyo ya UTOAJI
 
UPDATE: 19 AUGUST 2020

WASIFU WA MHUSIKA KWA KIFUPI SANA


Mada yetu ambayo bado iko hewani mpka muda huu ni ile inayomhusu Mtumishi wa Mungu Mgeni (MMM), lakini kabla hatujaendelea nayo, naomba kuwaletea wasifu wa mhusika kwa kifupi sana kama ifuatavyo:

AJIRA

  • Ni mwajiriwa wa umma kwa zaidi ya miaka 20 sasa
  • Kwa taasisi anayofanyia kazi sasa, yupo kazini tangu February 2000
  • Hana matatizo na ajira yake, isipokuwa mambo kadhaa madogo madogo ambayo yalianza kujitokeza kuanzia Julai 2006
  • Ni kwa upande wa maslahi yake na haki zake za msingi
  • Matatizo haya yote yanajulikana na wakuu wake wa kazi katika ngazi zote, ndani ya taasisi anayofanyia kazi
1 MATATIZO MADOGO MADOGO KWENYE AJIRA YA MHUSIKA: KUPANDISHWA NA KUSHUSHWA MADARAJA

  • Si tu kwamba mhusika amewahi kupanda madaraja, bali pia kushushwa
  • Amewahi kushushwa madaraja mara mbili
  • Mara ya kwanza kushushwa daraja ilikuwa Julai 2006 na mara ya pili, February 2014
  • Barua zilizotekeleza zoezi hilo anazo, na nakala zingine pia zipo kwenye faili lake
2 KUSHUSHWA MADARAJA JULAI 2006 NA FEBRUARY 2014: NAMNA ILIVYOTOKEA

  • JULAI MOSI 2006 ilikuwa ni tarehe yake nyingine tena ya kupandishwa daraja, kwa mara nyingine tena
  • Lakini pia Novemba 2005 alipata cheti kingine kipya (new/ highest qualifications) baada ya kuwa amehudhuria masomo kwa kipindi kisichopungua miaka miwili, 2003-2005
3 KUSHUSHWA CHEO/NGAZI/DARAJA KWA MARA YA KWANZA JULAI 2006

Tuseme sasa kabla ya JULAI MOSI 2006, mhusIka alikuwa kwenye cheo tukiite NGAZI A

Katika hali ya kawaida:

  • Kwa taratibu za kazi mahali anapofanyia kazi zilivyo na kulingana na barua aliyonayo inayohusiana na upandishwaji huo kwa kipindi hicho, alitakiwa kupanda kutokana na nyongeza ya elimu kutoka ngazi A kwenda Ngazi C, akirushwa ngazi B
  • Huku kulikuwa ni kupanda kutokana na NYONGEZA YA ELIMU, ambako kungefanyika kati ya Novemba 2005 na June 30, 2006 yaani wakati wowote kabla ya Julai mosi 2006
  • Baada ya hapo, alitakiwa pia kupanda cheo kutoka ngazi C kwenda ngazi D, mnano JULAI MOSI 2006
  • Hii ni kutokana na ukweli kuwa Julai mosi 2006 ndiyo tarehe ambayo alitakiwa kupanda cheo kwa mara nyingine tana, hata kama asingekuwa ameongeza elimu, yaani kupanda cheo kwa njia ya kawida bila nyongeza ya elimu
Hata hivyo, mchakato ulichelewa kidogo na hivyo ulifanyika kama ifuatavyo:

  • Taafira za kupanda cheo kutokana na nyongeza ya elimu zilimfikia mhusika Septemba 2006 badala ya kuwa zimemfikia kati ya Novemba 2005 na June 30, 2006
  • Wakati zinamfikia, tayari alikuwa ameshapanda cheo kwa njia ya kawaida kutoka ngazi A kwenda ngazi B, Julai mosi 2006
  • Hii ni kwa sababu kama ilivyoelezwa hapo juu, Julai mosi 2006 ndiyo ilikuwa tarehe yake nyingine tena ya kupanda cheo kwa njia bila nyongeza ya elimu
  • Kwsa hiyo mhusika alipanda kutoka ngazi A kwenda ngazi B, Julai mosi 2006 kwa sababu mpaka June 30, 2006, alikuwa bado yuko ngazi A
  • Ni kwa sababu marekebisho ambayo yalitakiwa yawe yameshafanyika kutokana na nyongeza yake ya elimu, hayakuwa yamefanyika
  • Baada ya hapo, Septemba 2006 ndiyo akapata tena barua iliyoelekeza kuwa alipanda cheo kutoka ngazi A kwenda ngazi C (akirushwa ngazi B) kuanzia June 23, 2006
  • Hii inamaanisha kuwa kama barua hii ya pili angeipata kwa wakati na kabla ya June 30, 2006, kufikia Julai mosi 2006, alitakiwa sasa apande kwa nija ile ya kawaida (si kwa nyongeza ya elimu) kutoka ngazi hii ya C kwenda ngazi D
  • Kwa hiyo, mambo yote haya mawili kwa ujumla wake yalikuwa yamempandisha mhuiska kutoka ngazi A na kumpeleka ngazi C, kitu ambacho hakikuwa sawa
  • IKupanda huku, kungekuwa ni shihi iwapo tu upandaji kutokana na nyongeza ya elimu usingekuwa una ile option ya KUMRUSHA MTUMISHI CHEO KIMOJA
Hivyo basi, kutokana na ukweli kuwa upandaji kutokana na nyongeza ya elimu ulikuwa na option ya kumrusha mtu kutoka A kwenda C, ni wazi kuwa mhusika alitakiwa kupanda cheo kwa hali ile hali ya kawaida pasipo nyongeza ya elimu, kutoka ngazi C kwenda ngazi D mnano JULAI MOSI 2006

  • Na kama ingetokea hivyo ,kwa hiyo by Julai mosi 2006, mhusika alitakiwa kuwa ngazi D
  • Bahati mbaya haikutokea hivyo, isipokuwa mhusika alipanda cheo na kuwa ngazi C kwenye tarehe hiyo tajwa
4 KILICHOSABABISHA HALI HII

Kilichotokea hapa ni kwamba barua hizi mbili zilipishana; iliyotakiwa iwahii ilichelewa, na iliyowahi haikutakiwa kuwahi, kiasi kwamba zote zilimpandisha mhusika kutoka cheo kile kile, yaani ngazi A, kwenda ngazi zingine mbili tofauti; yaani:

  • Kupanda kutokana na nyongeza ya elimu kulimtoa ngazi A na kumpeleka ngazi C, kikamrusha ngazi B
  • Hiki ni kitenda kilichofanyika kabla ya Julai mosi 2006, ila barua yake aliipta Septemba 2006
Vilevile:

  • Kupanda kwa kawaida (bila nyongeza ya elimu) nako pia kulimtoa ngazi A na kumpeleka ngazi B,
  • Hiki ni kitenda kilichofanyika BAADA YA JULAI MOSI 2006, na barua yake aliipta mapema JULAI 2006, yaani ABLA YA SEPTEMBA 2006
Kwa hiyo hadi Septemba 2006, cheo cha mhusika kikawa ni ngazi C na siyo ngazi D kama alivyokuwa ametarajia

5. ALICHOFANYA MHUSIKA KATIKA JITIHADA ZA KUTAKA KUREKEBISHA HALI HII

Baada ya hapo mhusika aliijulisha mamlaka husika juu ya oversight hii kwa maandishi

  • Walikuwepo pia watumishi wenzake wengine ambao nao muunganiko unaofana sawa kabisa na huu uliwatokea
  • Nao pia walikuwa wamepanda ngazi kutokana na mambo mawili ambayo yalikuwa ni nyongeza ya elimu na ya kiwango sawia kabisa na ile ya kwake pamoja na pia muda wa utumishi kwenye ngazi huiska
  • Muunganiko wa mambo yote haya mawili, wenzake hawa wenyewe, yalikuwa yamewapandisha kawaida
  • Yaani tuseme waliokuwa ngazi A, vyeo vyao vililibadilika na kuwa ngazi D
  • Hawa ni wale hasa ambao mwaka 2006 walipanda kutokana na nyongeza ya elimu. wakatoka ngazi A na kupelekwa ngazi C, mwaka huo wa 2006
  • Ilipofika mwaka 2007, walipanda kwa kawaida kutoka ngazi C na kufika ngazi D
  • Yaani hawa ni wale ambao tarehe yao ya kupanda kwa njia ya kawaida (mwaka 2007 ilikuwa mbele ya tarehe (mwaka 2006) yao ya kupanda kwa njia ya nyongeza ya elimu
6 KILICHOTOKEA BAADA YA MHUSIKA KUWASILIANA NA MAMLAKA HUSIKA

Baada ya mhusika kuwa amewasiliana na mamlaka husika, alijulishwa kuwa kulikuwa na oversight kwenye swala lake

  • Mhusika sasa ikabidi aandikiwe barua zingine mbili
  • Ya kwanza ilikuwa inampandisha cheo kwa njia ya kawaida kutoka ngazi A kwenda ngazi B na nyingine
  • Ya pili ilikuwa inampandisha cheo kutokana na nyongeza ya elimu, kutoka ngazi B kwenda ngazi C
  • Kwa hiyo mhusika akawa amebaki ngazi C
  • Baada ya miaka mitatu, ndiyo akapanda tena kutoka ngazi C (Julai 2009) na kwenda ngazi D, ngazi ambayo alikaa nayo hadi Julai 2012 alipopanda ngazi kwa mara nyingine tena
Kabla hatujaendelea mbele tujikumbushe mambo kadhaa yafuatayo kwenye taarifa hizi kwamba:

  • Katika hali ya kawaida, ukizingatia barua ambazo mhusika alikuwa amezipata awali, mhusika alitakiwa kuwa ngazi D by Julai mosi 2006
  • Hakufanikiwa kuwa ngazi hiyo, bali alibaki ngazi C
7 KIPI ALIKOSA KUTOKANA NA KUBAKI NGAZI C BADALA YA KUWA NGAZI D

  • Alikosa mshahara mkubwa wa ngazi D, na kupata mshahara mdogo wa ngazi C
  • Ngazi D ilikuwa pia ndiyo ngazi ya kwanza ambayo mtumishi wa umma anastahili kupata posho ya nyumba kwenye taasisi hiyo ya mhusika. Kwa hiyo mhusika alikosa pia posho hiyo
  • Na kwa sababu alikuwa tayari anaishi kwenye nyumba ya Serikali, aliendelea kukatwa asilimia 10 kwenye mshahara wake kama malipo ya pango; makato ambayo yaliendelea kwa muda wa miaka mitatu mingine mbele
  • Makato hayo ya asilimia 10 yasingekuwepo tena kama angeweza kuwa katika ngazi inayolingana na maelezo ya barua alizozipata hapo awali
  • Malipo hayo ya pango yallikuja kukoma baadaye ilipofika Julai mosi 2009, alipofanikiwa sasa kupanda kwa mara nyingine tena kwenda ngazi D, ambayo ndiyo ilikuwa ngazi stahiki kwa mtumishi kupata posho ya nyumba, au kuishi kwenye nyumba ya serikali bila kulipia pango
Kwa hiyo mchakato wa kwanza wa kushushwa cheo ulichukua sura hiyo



KUSHUSHWA CHEO/ NGAZI KWA MARA YA PILI: FEBRUARY 2014



Inaendelea………………………….

MwiH
elly obedy
 
UPDATE-2: 19 AUGUST 2020

8 KUSHUSHWA CHEO/ NGAZI KWA MARA YA PILI: FEBRUARY 2014


Kwa hiyo, utaona kuwa mhusika alipanda na kufikia ngazi D, kuanzia Julai mosi 2009, ngazi ambayo aliendelea nayo kwa muda wa miaka mingine mitatu mpaka Juni 30, 2012

  • Ngazi hii ndiyo ile sasa ambayo ilimpa kwa mara ya kwanza, stahiki za kukaa kwenye nyumba ya Serkali bila kukatwa kodi ya pango ambalo lilikuwa ni asilimia 10
  • Kwa hiyo hadi kufikia Juni 30, 2012, alikuwa anatimiza muda wa miaka mitatu (3) akiwa anakaa kwenye nyumba ya Serikali bila kukatwa hela ya pango
  • Katika hali ya kawaida, kwenye tarehe hiyo tajwa, alitakiwa awe anafikisha miaka sita (6) akikaa kwenye nyumba bila kukatwa pango, badala ya mitatu
Baadaye tena, ilipofika Julai mosi 2012

  • Mhusika alipanda tena ngazi
  • Safari hii hakupanda kawaida, bali alirushwa ngazi mbili, yaani ile iliyokuwa inafuata, ngazi E pamoja na nyingine, ngazi F
  • Kwa hiyo alirushwa kutoka ngazi D kwenga ngazi G, akiziruka ngazi mbil za E na F
  • Ngazi hii ya G ndiyo ilikuwa ngazi ya mwisho ambapo juu yake hakuna ngazi nyingine tena, yaani hakuna ngazi H
  • Kwa hiyo baada ya kupanda ngazi 2012, alifika mwisho
  • Baada ya kuwa amepanda kutoka ngazi D kwenda ngazi G, na ambayo ni kubwa kuliko ngazi zote kwenye kada yake, mshahara mpya kutokana na ngazi hiyo mpya hakuanza kulipwa Julai 2012
  • Alianza kulipwa mshara wa ngazi hiyo mpya G mwezi Novemba 2012
  • Kwa hiyo akawa anatakiwa kudai malimbikizo ya mishahara kwa miezi minne kuanzia Julai 2012 mpaka Oktoba 2012
  • Malilmbikizo hayo yalikuwa yanazidi shilling million tatu (TZS 3,000,000/=) ukiunganisha na kodi ya Serikali
  • Mhusika alianza kudai malimbikizo hayo kwa njia isiyo rasmi, (hakuwahi kuandika barua), mara tu alipoanza kulipwa mshahara mpya
  • Alikuwa anayafuatilia malimbikizo hayo kwa kwenda kuwaona wahusika maofisini mwao
Hadi kufikia mwaka 2014 akiwa bado anaendelea na mchakato wa kudai malimbikizo hayo, ukizingatia kuwa huko nyuma nako pia kabla ya January 2013 kulikuwa na malimbikizo mengine ya takriban TZS 400,000/= ambayo nayo pia alikutwa bado anaendelea kuyadai

  • Ilitokea mwezi February 2014 akaletewa barua ya kushushwa cheo kutoka ngazi G na kurudishwa ngazi E (hapa alirushwa ngazi F kwa kurdi nyuma)
  • Barua hiyo iliambatana na barua nyingine ya pili iliyoeleza kuwa kuna makosa yalifanyika kumpandisha mhusika kutoka ngazi D kwenda G na hivyo hii ya sasa ilikuwa ndiyo ilikuwa inampandisha kiusahihi kutoka ngazi D kwenda ngazi inayofuata baada ya D ambayo ni E
  • Baruahiyo ilitoka ofisi ya Rasilimali watu
  • Ilikuwa inamshusha cheo mhusika kuanzia Julai mosi 2012
Kumbuka kuwa hapa sasa ilikuwa ni mwaka 2014; takribani miaka miwili (kasoro miezi kadhaa tu) tangu mhusika atumike akiwa katika ngazi ya cheo hiki kipya cha G

Kawaida barua za namna hii huwa zina option ya kuyakubali au kuyakataa yaliyoandikwa humo kwa kuweka sahihi

  • Mhusika hakukubalina na kile kilichokuwa kimeandkwa kwenye barua hiyo, maelezo hayo aliyakataa na hakuisaini hiyo barua
  • Aliirudisha bila kuisaini kuonyesha kuwa hakuwa amekubaliana na kushushwa cheo kulikokuwa kumeelezwa kwenye barua hiyo
Ilipofika mwezi June 2014, kukaanza kufanyika maandalizi ya mfumo mpya wa tathmini kwa watumishi wa umma. Mfumo huu wa tathtmini ulibadilika na kuwa wa wazi badala ya ule uliokuwapo mwanzo, ambao ulikuwa ni wa siri

  • Hapa ndipo sasa mhusika alilazimika kukubalina na kushushwa ngazi kutoka G kurudi E kwa sababu bila kufanya hivyo, ilikuwa haiwezekani kuzijaza fomu hizo za tathmini, na wala Mkuu wa Idara asingeweza kuzipitisha
  • Kwa hiyo hapa sasa ndiyo ikabidi mhsika ajaze kwenye fomu ya tathmini kuwa cheo chake ni ngazi E na wala siyo G
  • Na baada ya kufanya hivyo, mwishoni mwa mwezi June 2014, mshahara wake ukakatwa sasa jumla ya pesa taslimu laki saba (TZS 700,000/=), ili uweze kuendana na ngazi mpya ya E
Kwa hiyo utaona kuwa pamoja na kuwa barua ya kushushwa cheo ilikuja February 2014, bado mhusika aliendelea kupata mshahara wa ngazi G tokea hapo hadi May 2014, na June 2014 ndiyo akaanza kupata tena mshara mpya wa ngazi mpya iliyoshushwa. Mshahara mpya alianza kuupta baada ya kuwa ameajza fomu za OPRAS June 2014

Hivi ndivyo mchakato wa kushushwa ngazi kwa mara pili ulivyofanyika, na hadi leo hii August 2020, mhusika bado anaendelea kupata mshahara huo ambao ulitokana na kushushwa cheo kulikofanyika mwaka 2014



9 KWA KIFUPI SANA: YALIYOFUATA BAADA YA KUSHUSHWA NGAZI MARA YA PILI

Terehe 07 Desemba 2017, mhusika alipata barua iliyokuwa inampandisha cheo kutoka ngazi E kwenda ngazi F. Kumbuka kuwa mnamo Julai 2012, mhusika alikuwa tayari ameshapanda mpaka ngazi G, ambayo ni kubwa kuliko hata hiyo ngazi F ailiyokuwa imetajwa kwenye barua hiyo ya Novemba 2017. Barua hiyo ilikuwa inaeleza kuwa kupanda huko kwa mhusika na kuwa kwenye ngazi hiyo mpya ya F kulikuwa kunaanza Novemba mosi, 2017

  • Safari hii mhuiska aliikubali barua hiyo na hatimaye kuisaini na kuirudisha ofisi husika
  • Matarajio ya mhusika sasa mpaka muda huu yakawa ni kuwa atapata mshahara mpya wa ngazi E mwishoni mwa mwezi Desemba 2017, na malimbikizo ya mwezi uliokuwa umepita nyuma yake, yaani Novemba 2017
  • Hata hivyo ilipofika Desemba 2017, mhusika hakupata mshara mpya
  • Alipofuatilia alielezwa kuwa inawezekana taarifa mpya za mshahara wake zilichelewa kuepelekwa hazina
  • Ilipofika January 2018 napo tena mshahara ukawa ule ule wa zamani, yaani wa ngazi D
  • Alipofuatilia tena akaambiwakuwa inabidi akamuone Ofisa Rasili mali watu ofisini kwake
Mhusika hakuweza kwenda kumuona Ofisa huyo kwa sababu moja kubwa: MTUMISHI WA UMMA UKISHAANDIKIWA BARUA YA KUPANDISHWA CHEO, HUHITAJI TENA KWENDA KUMUONA MTU YEYOTE YULE HALAFU NDIYO MALIPO YA MSHAHARA MPYA UNAOOENDANA NA CHEO HICHO, YAANZE KUFANYIKA. Huo utaratibu haupo

  • Kwa hiyo baada ya mhusika kukosa mshahara mpya January 2018, aliamua kukaa kimya bila kufanya ufuatiliaji wa aina yoyote ile
  • Ilipofika tena February 2018, mshahara wa mhusika ambao umeshindwa kuongezeka kwa miaka kadhaa, ukakatwa tena takribani shillingi laki tatu (TZS, 300,000/=)
  • Alipojaribu kufuatilia tena ofisi ya mishahara, akaambiwa kuwa ni kwa ajili ya pango la nyumba
  • Namna ya kulitatua tatizo hilo akaambiwa inabdi awaone Ofisa wa Nyumba pamoja na Ofisa Rasili mali watu
  • Kumbuka kuwa hapa pango la nyumba mara ya mwisho alikatwa June 30, 2009 na kuanzia Julai 1, 2009, mpaka muda huo wa February 2018, hakuwa anastahili tena kukatwa pango la nyumba, kulingana na waraka wa Serikali
  • Aliamua kwenda kumuona Ofisa wa Nyumba kutaka kujua kama pengine labda makato hayo yametokana na agizo jipya la waraka wa Serikali
  • Ilikuwa ni katika kutaka kujua iwapo kuna waraka mpya wa Serikali umetoka unaoagiza hivyo
  • Baada ya kuonana na Ofisa wa Nyumba, yeye alieleza kuwa ni kutokana na maagizo tu mapya ndani ya taasisi
  • Hakuwa na waraka wowote mpya wa Serikali uliokuwa ukiagiza makato hayo ya nyumba
Baada ya hapo mhusika aliandika barua ngazi za juu zinazohusika, kuomba apewe ufafanuzi wa sababu za makato hayo mapya kwenye mshahara wake, na ilipofika August 2018, (miezi sita baadaye) alipokea barua ikimdai pesa (mhusika) takribani million tatu (TZS 3,000,000/=) kama pango la nyumba na pia ikimjulisha kuwa

  • Makato hayo ni makato halali kutokana na uamuzi wa taasisi, na ni kwa ajili ya pango la nyumba
  • Zaidi barua ilieleza kuwa makato hayo yamepitishwa na taasisi, na yanaanzia Julai 2017 na si mwezi ambao mhusika alianza kukatwa makato hayo, yaani February 2018
  • Na kwa sababu mhusika alianza kukatwa February 2018, kuna miezi mingine saba (7) nyuma ambayo alikuwa anadaiwa fedha kwa ajili ya pango hilo, ambayo ni Julai 2017 mpka January 2018
  • Kwa hiyo kiasi kilichokuwa kimetajwa kwenye barua hiyo ndiyo kilichokuwa kinaendana na pango la miezi hiyo
Barua ilikuwa imemwagiza mhusika aende akailipe hela hiyo kwenye mojawapo ya akaunti za benki za tasisi, na atoe taarifa kwa mamlaka husika kwa kuwasilisha pay-in slip ya benki

Hata hivyo mhusika hakufanikwa kufanya hivyo kwa sababu

  • Pango la nyumba za Serikali huwa linafuata kanuni za Serikali zinazotolewa kwenye waraka wa Serikali na si maamuzi ya taasisi zilizopewa dhamana ya kumiliki nyumba hizo
  • Makato halali ya fedha kwenye mshahara wa mtumishi ni yale tu ambayo mtumishi anakuwa ameridhia na ku-authorize
  • Pamoja na kwamba taasisi inayo mamlaka fulani juu ya mishahara ya watumishi wake, lakini bado msahahara ni mali ya mtumishi mwenyewe ni si mali ya taasisi ambayo mtumishi ameajiriwa
  • Mhusika hakuwa amehusishwa katika kushiriki kwenye maamuzi ya makato hayo na hivyo yalikuwa ni batili
  • Makato hayo bado yapo na yanendelea mpaka leo hii August 2020
Baada ya mhusika kushindwa kufanya malipo hayo, August 2018, ilipofika mnamo August 2019 (mwaka mmoja baadaye tangu apate barua ya kumtaka afanye malipo hayo benki kwa ajili ya pango la nyumba), mhusika alipokea barua nyingine tena (ya pili) ambayo:

  • Ilimhitaji afanye malipo ya pesa za pango analodaiwa (zile alizoziongelea hapo juu) ndani ya siku 30, vinginevyo atafukuzwa (to be evicted) kutoka kwenye nyumba anayoishi
  • Barua ilitoka kipindi yeye akiwa likizo nyumbani
  • Wakati anaikuta barua hiyo ofisini na kuisoma, zilikuwa zimebaki siku kama 14 tu (au pungufu ya hizo) kati ya zile 30 ambazo alikuwa amepewa ili aweze kufanya malipo hayo
  • Kushindwa ku-meet deadline ya malipo hayo kulimaanisha afukuzwe ndani ya nyumba hiyo
Septemba 2019, mhusika alichukua hatua ya kuijibu barua hiyo na kueleza kuwa

  • Kama kuna waraka wa Serikali unaohusiana na pango hilo, hana tatizo atalilipa, na kuomba kujua kama pengine ulikuwepo
  • Vinginevyo aliomba apewe neema (favor) ya maelezo ya ziada ni kwa namna gani ayeye nastakiwa kulipia pango la nyumba kwa mara nyingine tena na kwa wakati huu, pasipokuwa na maagizo yoyote yanayotokana na waraka wa Serikali
  • Kumbuka kuwa hapo kabla, mara ya mwisho mhusika alilipia pango la nyumba June 2009, karibia miaka kumi iliyopita
Zaidi ni kuwa mhusika alieleza kuwa, yeye ndiye anayedai malimibikizo ya mshahara kwa sababu mpaka muda huo (na pia hadi mpaka sasa) alikuwa analipwa mshahara wa zamani wa ngazi D, baada ya kushushwa kutoka ngazi G mnamo February 2004.

Hat hivyo mhusika anashukuru kwamba hakufukuzwa ndani ya nyumba hiyo ila pia bado hajapata majibu ya barua yake aliyoiandika kipindi hicho, yaani August 2019, na anhofia isije ikatoka tena kipindi akiwa yuko likizo



10 MHUSIKA ASHUSHWA CHEO TENA KWA MARA YA TATU, AUGUST 2019

Mwandishi wa habari hii anapenda kuwaomba radhi kidogo wasomaji wa taarifa hizi kwamba kushushwa cheo kwa mhusika hakujafanyika mara mbili, kama alivyotangulia kusema hapo awali, bali mara tatu

  • Mhusika alishushwa cheo mara ya kwanza mwaka 2006, ya pili mwaka 2014 na ya tatu nay a mwisho mwaka 2019; yaani mwaka jana
  • Mnamo mwezi Novemba 2017, alipandishwa cheo kutoka ngazi D kwenda ngazi F, lakini mshahara ukaendelea kubaki ule ule wa ngazi D hadi leo
  • Lakini pia, kwa mara nyingine tena manmo mwezi August 2019, alipata barua ya kumshusha cheo kutoka ngazi F kwenda ngazi C (kumrusha nyuuma ngazi D)wakati mshahara anaopata mpaka muda huu ni ule wa ngazi D
Barua zote za michakato yote hii anazo, na anamini pia zipo kwenye faili lake

Kwa hiyo mpaka muda huu, mhusika ameshashushwa cheo tena kiasi kwamba pamoja na yote aliyoyaeleza hapo juu, bado mshahara anaoupata kwa sasa, yaani ule wa ngazi D, ni mkubwa kuliko ule anaostahili kuupata. Kwa sasa anapata mshahara wa ngazi D wakati barua ya mwsiho aliyoletewa mwaka 2019, inamtambua kuwa yuko ngazi C (ngazi aliyong’ang’anizwa mwaka 2006 kwa msomaji aliye na kumbukumbu sahihi



Itaendelea…………………….


MwiH
elly obedy
 
MASAHIHISHO MUHIMU!
MOJA:

Ngazi alizoziengelea mwandishi kwenye habari hiyo hapo juu, siyo ngazi za mishahara bali za vyeo

MBILI
:
Deni la pango la nyumba linalosemekana kuwa mhusika anadaiwa na uongozi wa juu wa taasisi anayofanyia kazi siyo Million tatu bali ni Million mbili (TZS 2,000,000/=) na kidogo.
Ni kwa sababu kwa wastani inasemekana kuwa anadaiwa karibia kama laki tatu hivi kwa kila mwezi kwa kipindi cha miezi saba (7), ambayo ni kuanzia Julai 2007 mpaka January 2018
 
Pole! hama hilo kanisa. Nimesoma nimesikitika acha ninyamaze nisihukumu maana kilicho nyuma ya pazia sikielewi.
Mungu huwa hampi mtu mzigo ambao hawezi kuubeba. Still, hata katika hali ya kawaida, binadamu huwa hawezi kubeba mzigo ambao uzito wake hawezi kuubeba. Hata gari pia vilevile. Huwezi ukakuta gari yenye uwezo waa kubeba mzigo wa tani 1 imebeba mzigo wa tani 2
 
UPDATE: 20 AUGUST 2020

WASIFU WA MHUSIKA KWA KIFUPI SANA

Inaendelea……………….


Kwa hiyo mpaka muda huu:

  • Cheo chake halali kinachotambulika na ofisi ya rasilimali watu ni kile cha ngazi C
  • Hiki ndiyo kile cheo ambacho kwa mara ya kwanza alikipta Julai 2006, baada ya kuwa amepunjwa ngazi moja iliyotakiwa impeleke kwenye cheo cha ngazi D kama alivyoeleza hapo awali
  • Msahara anaopata kwa sasa ni ule wa cheo cha ngazi D, ngazi ambayo kwa mara ya kwanza aliipata mnamo Julai 2009


HITIMISHO:

Ikumbukwe kuwa hadi kufikia Julai mosi 2012, mhusika alikuwa amepanda cheo hadi kufikia ngazi G; ngazi ambayo ni ya mwisho kabisa kwenye kada aliyopo, ila baada ya mabadiliko kutokea, mpaka muda huu (August 2020) yupo kwenye cheo cha ngazi C huku akipokea mshahara wa ngazii D

Barua zote zinazoonyesha matukio haya anazo, na pia anaamini kuwa zipo kwenye file lake pia

Zaidi ni kuwa mshahara huu wa ngazi D una makato yafuatayo ambayo yeye mwenyewe hakuwahi kuyaidhinisha ama kuyaridhia.

Ni makato yanayofanyika kwa lazima ambayo ni:

  • Makato yaliyoanza tangu Febrauary 2018 kwa ajili ya pango la nyumba----asilimia saba (7%)
  • Makato ya Bima ya Afya ambayo yeye si mwanachama, yaliyoanza tangu Desemba 2014---asilimia tatu (3%)
  • Makato kwa ajli ya maji nyumbani anapoishi, ambayo yalianza tangu mwaka 2011----elfu 25 kila mwezi
Kuhusiana na swala hili la maji, maji haya kwa sasa yalishakatwa tangu Novemba 2018, ila huwa anachota maji chini nje kwenye bomba na kuyapandisha juu ghororfa ya kwanza, au wakati mwingine anasomba kwa mikono kutoka ghorofa jirani. Wakati mwingine pia huwa anapandisha maji kwa kutumia mpira pale inapotokea kuwa kuna pressure kubwa kwenye bomba la maji liliko nje. By Oktoba 2020 (mwaka huu) atatimiza miaka miwli kamili pasipokuwa na huduma ya maji nyumbani kwake



11 MATUKIO MENGINE YASIYOKUWA YA KAWAIDA


Amenusurika mara mbili kukumbana na matukio yaliyoonyesha viashiria vya kutaka aonekane kama (yeye) alitaka kufanya fujo kwenye ofisi za wakubwa, pindi alipokuwa akitafuta msaada wa matatizo yaliyokuwa yakimkabili

  • Mara ya kwanza ilikuwa ni kipindi alipokuwa amekatiwa maji kwa mara ya kwanza kabisa
  • Kukatwa kwa maji anakokuoengelea kwa sasa, ni kwa mara ya pili
  • Yalipokatwa kwa mara ya kwanza, baada ya takribani mwezi kuwa umepita, alilazimika kwenda kutafuta msaada ngazi za juu, na ndipo tukio ambalo siyo la kawaida sana lilimtokea. Details za tukio hilo anazihifadhi kwa sasa
  • Mara ya pili ilikuwa ni mwaka jana April 2019
  • Alifika mojawapo ya ofisi za ngazi za juu akitafuta appointment ya kuonana na mkuu wake wa kazi, wa ofisi hiyo
  • Alikuwa anajribu kufuatilia majibu ya barua yake kuhusiana na maslahi yake (haya ambayo amejaribu kuyaongelea hapa kwa kifupi) ikiwa ni pamoja na pesa ambazo zimekuwa zikikatwa kwenye mshahara wake hususani zile zilizoanza kukatwa mwezi Novemba 2014
  • Kwa hiyo alihitaji appointment ya kumuona mkuu wake wa kazi kwa sababu barua aliyokuwa ameiandika tangu mwaka uliokuwa umepita nyuma yake, yaani 2018, ilikuwa haijapata majibu kutoka kwa mkuu huyo
  • Wakiwa katika maongezi ya kawaida, kwa ghafla tu Katibu Muhtasi aliyekuwa akiongea naye, alionyesha dalili za kukasirika na kutaka kulia huku akimpigia simu mkuu mwenye ofisi
  • Alichofanya mhusika ni kufungua mlango na kutoka mbio ofisini hapo
  • Kuanzia pale akaamua kuacha mara moja kufuatilia tena swala la maslahi hayo, kwa njia hiyo ya kupita pita maofisini kwa watu
  • Ataendelea kuyafuatailia kwa kutumia njia ya barua tu, ila si kwa kuingia maofisini kwa watu
Matukio haya mawiili ndiyo yalikuwa sasa yawe linked na tukio lile la Kanisani la Tarehe 26/04/2020 lililokuwa limepangwa kufanyika kwenye mkutano wa wanaume

Kama mhusika angefunua kinywa chake kuongea neno siku hiyo, kuna watu walikuwa wamejipanga kufanya fujo ili ionekane kuwa ni yeye amesabbisha fujo. Baada ya hapo ndiyo wange-link tukio hilo na haya mawili ya ofisini

Matukio haya matatu ukiunganisha na lile la Sanitizer yangetosha kabisa kuwahakikishia watu kuwa ni yeye ambaye huwa anaanzisha fujo



MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Back
Top Bottom