#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

UNAFIKI WA VIONGOZI KANISA A

Tuseme tu ule ukweli. Hakuna MA-viongozi manafiki kama MA-viongozi ya KANISA A. Kila siku yako bize kurusha mapepo Kanisani halafu eti leo hayo ndiyo yanahamasisha waumini kuombea mtu?

Tumefika hapa tulipo kwa sababu kuna watu kwenye nyumba za Ibada, hawajasimama sawasawa kwenye nafasi zao, wakiwemo hawa wapumbavu wanaotusumbua kila siku kwenye nyumba za Ibada. Wasubiri tu atoke huko alikojichimbia halafu baadaye huko mbele ya safari watakuja kuuona huo moto utakaokuja kuwawakia, kama watakuwa bado wanaendekeza na huo upumbavu wao.

Naona hata Waziri Mkuu wakati anaongea hawajamsikia, hawana macho wala masikio, yote ya kimwili na ya kiroho
 
UPDATE: MONDAY 15 MARCH 2021

MAELEZO MUHIMU YA NYONGEZA KUHUSIANA NA KUSANYIKO KUBWA LA KWANZA LILOFANYIKA MWAKA 2016 NDANI YA MAZINGIRA YA TAASISI ANAYOFANYIA KAZI MHUSIKA


Kama alivyoelezea hapo awali, ni kwamba kwenye kusanyiko hili, kuna kitu pia alikiona mhusika na ambacho kilipelekea kumuweka kwenye tahadhari kubwa siku hiyo, kipindi kusanyiko hilo likiwa mazingira hayo ya ofisini
  • Kikubwa cha msingi kwenye tukio hili ni kwamba MR Y alikuwa anahusika, pamoja na wenzake wawili
  • Kusanyiko lilifanyikia uwanjani ambako hapakuwa na sehemu ya watu kwa ajili ya kujisetiri, na hivyo kulikuwa kumewekwa vyoo vya muda vile vya kuhamishika
  • Kama kumbukumbu zake zinamwonyesha vizuri, usanyiko hili lilifanyika katika kipindi ambacho wanafunzi walikuwepo mazingira ya ofisini
JARIBIO JINGINE LA NDANI YA JENGO AMBALO MR Y ALIWAHI KUHUSIKA
  • Tukio hili ilikuwa litokee siku ya UKUTA, ambayo ilikuwa ni siku ya Alhamis tarehe 01 Septemba 2016.
  • UKUTA “was something to do with” KUPINGA UDIKTETA TANZANIA
  • MR Y alipanga hili kwa kushirikiana na mwanafunzi wake mmoja
  • Mwanafunzi huyo aidha ni ndugu yake au ni jamaa yake wa karibu kwa sababu ni mtu ambaye wanaongea ligha moja na wametoka sehemu moja
  • Ni mwanafunzi wa elimu ya ngazi ya juu, tofauti na wanafunzi wa kawaida
KWA BAHATI NZURI, kabla ya siku hiyo kuwadia, UKUTA ulitangazwa kuwa umeahirishwa, na mara baada ya kuwa imetokea hivyo
  • Mhusika ndiyo akawa ameongeza zaidi kiwango cha tahadhari aliyokuwa nayo hapo awali
  • Badala ya kufika ofisini na kuchukua tahadhari akiwa yupo ofisini huku akifanya kazi kama alivyokuwa amepanga hapo awali, mhusika alibadilisha uamuzi na kuchukua hatua ya kutokwenda kabisa ofisini siku hiyo; hivyo alifanya kazi akiwa katika mazingira ya nyumbani
Baada ya siku hiyo ya UKUTA kupita, Ijumaa kesho yake mhusika alipofika ofisini, Ofisi ya Mkuu wa Idara ikawa iko ina shauku kidogo ya kutaka kujua kwa nini jana yake hakuwa amefika ofisini. Hivyo ilimuomba mhusika kuwapa maelezo yoyote ya mdomo kwa ajili ya kutofika kwake siku hiyo, kama alikuwa nayo

Huyu aliyehitaji maelezo haya alikuwa ni KMH wa MWI, na alikuwa anayahitaji ili yaweze kumsaidia kujaza ripoti zake za kila siku za mahudhurio ya kila siku ya wafanyakazi wa idara yake

Kwa wakati huo, mhusika akiwa hana ushahidi mwingine wa nyongeza ambao ulikuwa una-pinn na kile alichokuwa amekiona kuwa kingetokea na hiyvo kumpelekea asiweze kufika kazini siku hiyo
  • Mhusika alimjulisha KMH wa MWI kuwa alishindwa kufika kazini siku hiyo kutokana na mafundi waliokuwa wamepakaa rangi chumba jirani na ofisi yake jana yake na hivyo kuepelekea uwepo wa harufu kali ya rangi mpya hadi ndani ya ofisi yake
  • Na kweli kipindi hicho walikuwepo pia mafundi waliokuwa wakifanya kazi ndani ya jengo na walikuwa wamepakaa rangi chumba jirani na ofisi ya mhusika
Hata hivyo, ukweli ni kuwa si rangi iliyopelekea mhusika asifike ofisini siku hiyo, bali ulikuwa ni UKUTA, especially baada ya kuwa umetangazwa kuwa haupo, umeahirishwa. Kuahirishwa kwa UKUTA ndiyo kulikopelekea asifike ofisini siku hiyo, na si rangi iliyokuwa imepakaliwa chumba jirani na ogfisi ya mhusika

HITIMISHO


Mpaka hapa, msomaji inabidi akumbuke pia kuwa
  • Baada ya wiki hii ya UKUTA kupita, Jumamosi ya wiki iliyofuata ndipo lilitokea tetemeko la Kagera
  • Tetemeko hilo lilipelekea aliyekuwa kaimu MWI kusafiri kwenda Kagera, ndani ya wiki nyingine iliyofuata baada ya tetemeko hilo kutokea
  • Baada ya kaimu kusafiri, aliingia kaimu mwingine ambaye alikuwa ni MR Y
Baada ya kuwa MR Y ameikaimu nafasi ya MWI, ndani ya wiki hiyo ndiyo yakatokea sasa mengine yale ambayo mhusika tayari ameshayaelezea hapo awali
  • Watu karibia wote hawakuwepo ofisini, walibaki watu takribani wanne ndani ya jengo zima
  • Mhusika alihama ofisini kwake na kuhamia ofisini kwa MWI
  • Ijumaa ya tarehe 16/09/2016 ilipofika, mhusika akawa amebaki peke yake tena ofisini kwa MWI, baada ya KMH kupata udhuru wa kwenda kuonana na “SPECIALIST” na hivyo kupelekea mhusika abkai peke yake ndani ya ofisi ya MWI
Mhusika akiwa amebaki peke yake, hapo hapo ndiyo akaja sasa yule mtu ambaye alijitambulisha kuwa ni dereva wa SENIOR MSTAAFU WA KIUME (SMME), akiwa na gari ya Seikali na ambayo ilikuwa imekuja kumchuka SMME kumpeleka uwanja wa ndege, kwa safari yake ya kwenda China, ambayo SMME mwenyewe alikuwa akiifanyia maandalizi kwa muda wote ndani ya wiki hiyo

Reporting time uwanja wa ndege ilikuwa saa 8.00 kamili mchana, lakini hadi inafika saa 8 kasorobo, dereva huyu aliondoka peke yake bila SMME kuonekana, tofauti na makubaliano yao walivyokuwa wamekubaliana kwamba dereva aje amchukue SMME mazingira ya ofisini na kumplekea airport



MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
NEXT:

“KANISA B”, “KANISA B”, “KANISA B”, “KANISA B”, “KANISA B”

MZEE KIONGOZI WA KANISA B (MZK-B)

MATUKIO MUHIMU SANA AMBAYO MZK-B AMEWAHI KUYAFANYA KIPINDI MHUSIKA ALIPOKUWA KANISA B
 
“KANISA B”, “KANISA B”, “KANISA B”, “KANISA B”, “KANISA B”

MZEE KIONGOZI WA KANISA B (MZK-B)

MATUKIO MUHIMU SANA AMBAYO MZK-B AMEWAHI KUYAFANYA KIPINDI MHUSIKA ALIPOKUWA KANISA B



TUKIO MUHIMU –I
: MAELEZO YA UTANGULIZI YA TUKIO LENYEWE

Ikumbukwe kuwa mhusika alihamia Kanisa B tarehe 14 April 2017, kwa hiyo hadi kufikia tarehe 7 Julai 2017, mhusika alikuwa hajakamilisha hata miezi mitatu akiwa yupo Kanisa A. Na kwa hali hiyo basi, hadi kufikia kipindi hicho, Kiongozi Mkuu wa Kanisa B (KM-B) alikuwa bado hajamfahamu vizuri mhusika, pamoja na watu wengiine baadhi, ukiondoa kikundi lmaalumu chini ya MZK-B ambacho chenyewe kumbe klilikuwa tayari kimeshafnaya “phishing’ ya taarifa zake kutoka kwa wale wanamfahamu,yaani kule alikokuwa ametokea, Kanisa A

MWANZONI MWA JULAI 2017: MHUSIKA APATA WAZO LA KIBIASHARA AKIWA YUPO OFISINI KWAKE ANAFANYA KAZI

Siku moja akiwa yuko ofisini, Julai 2017, mhusIka alijiwa na wazo fulani la kibiashara na kuamua kulifanyia kazi.

Baada ya wazo hilo kuwa limemjia

  • Aliamua kuingia kwenye website ya Kampuni ambayo ilikuwa inahusiana na wazo lake hilo na akafanikiwa kupata mawasiliano ya simu ya Kampuni hiyo
  • Alivyowapigia akitaka kujua zaidi juu ya details za bidhaa zao, kampuni hiyo walifurahi sana na wakaenda mbali kwa kumuuliza yeye anaishi maeneo gani hapa Dar es Salaam
  • Alipowatajia sehemu anayoishi, ikaonekana kuna wakala wao mwingine ambaye anaishi maeneo jirani na eneo analoishi mhusika, na wakamwahidi kuwa wakala wao huyo anaweza akapata nafasi ya kumpitishia mhusika brochure zao katika moja ya safari zake atakapokuwa anarejea nyumbani jioni akitokea ofisini
Maongezi hayo hatimaye kweli yalipelekea siku moja ndani ya wiki hiyo, wakala wa kampuni hiyo kufika nyumbani kwa mhusika akiwa na brochure za kampuni yao kwa ajili ya kumkabidhi mhusika. Baada ya hapo wakala huyu aliaga kuelekea nyumbani kwao, na kwa sababu hakuwa na gari, mhusika aliamua kumepeleka angalu kituo cha mwisho cha karibu na anapoishi

  • Wakala huyu alikuwa ni binti umri kati ya miaka 24-26
  • Wakati wa maongezi yao na mhusika, binti huyu alimjulisha mhusika kuwa weekend hiyo wangekuwepo pia Mlimani City kwa ajili ya matangazo zaidi ya bidhaaha zao, ikiwa ni pamoja na kugawa brochure kwa watu mbalimbali ambao huwa wanafika hapo
  • Binti huyu alimkaribisha mhusika aweze kufika pia Mlimani City Jumamosi ya wiki hiyo, na mhusika alikubali
Ilipofika Jumamosi, kweli mhusika alifika mlimani city na akawa amefanikiwa kufika kwenye banda la Kampuni hiyo, na huyu binti akiwa ni mmoja wa waliokuwepo kwenye banda hilo siku hiyo.

Kumbe huku nyuma kulikuwa na watu wanafuatilia mienendo hiyo na hadi kufikia hatua hii, wakawa wame-conclude kwamba mhusika na binti huyu wameshakuwa na mahusiano.

  • Baada ya hapo taarifa hizi zikapelekwa kwa Kiongozi Mkuu wa Kanisa B (KM-B)
  • Zaidi ya kupelekewa taarifa hizi, KM-B, akashauriwa pia kuwa kesho yake (yaani Jumapili) wakati wa Ibada, aitishe wazinzi wapite mbele madhabahuni
Kesho yake mhusika akiwa yupo kanisani, alistukia mara KM-B anasimama na kuanza kuita watu wazinzi wapite mbele. KM-B aliita mpaka akachoka, pande kuu nne za Kanisa, hakuna mtu aliyejitokeza. Kwa kifupi ni kwamba siku hiyo KM-B hakupata mtu yeyote ambaye aliitikia wito wa tuhuma hizo, hapakuwa na mtu hata mmoja. Mzee wa watu alionekana wazi kabisa kuaibika baada ya kukosa mtu hata mmoja, wakati kwa kumwamngalia tu wakati anasimama na kuanza kuita watu, alikuwa na uhakika kabisa kuwa lazima kulikuwa na mtu mmoja. Hakuwa amepewa maono na Roho Mtakatifu bali alikuwa maeelezwa na chanzo ambacho alikiamini kuwa ni cha uhakika na ambacho hakiwezi kumdanganya

Hapa vijana wa kisasa huwa wanasema “aliingizwa uchaka” mithili ya siku ile ya tangazo la MABOMU YA MAREKANI. Siku hii nayo pia alikuwa ameshauriwa kuwatambulisha baadhi ya watu mbele ya kundi la watu wengi wageni kanisani hapo, mhusika akiwa mmoja wao, kitu ambacho hapo awali, mhusika na KM-B walikuwa wamekubaliana kuwa wasiwe wanakifanya, unless kama kuna ulazima wa sana wa kufanya hivyo.



……………..inaendelea

NEXT:

MARA YA KWANZA MHUSIKA AGUNDUA WALAKINI KWENYE TANGAZO LA UZINZI LA KM-B NA KUANZA KUONA KUWA KUNA UWEZEKANO LILIKUWA LIMEPIKWA


  • Ni baada ya kupata taarifa kutoka kwa MKE WA “KIONGOZ-XB”
  • “KIONGOZ-XB” ni yuke ambaye aliwahi kuwa mwenyeji wa Kiongozi Mkuu wa Kanisa A, siku kiongozi huyo (KM-A) alipozuru Kanisa B,
  • Vile vile, huyu “KIONGOZ-XB” ndiye aliyewahi kumtuhumu mhusika mbele ya KM-A kuwa alihama Kanisa A na hakumuaga KM-A kwa kusema “kumbe huyu mtu aliondoka na hakukuaga!”
Kwa wasomaji wa tangu mwanzo wa taarifa hizi, hawawezi kupata shida kumjua “KIONGOZ-XB” japo huko nyuma mwandishi anaweza akawa amemtaja kwa jina tofauti

  • Kwa hiyo hints hizi ambazo alianza kuzipata mhusika, zilikuwa zinatoka kwa MKE WAKE na “KIONGOZ-XB” na si kwake yeye “KIONGOZ-XB”
  • Baada ya kupata taarifa za walakini wa tangzao hilo lililowahi kutolewa na KM-B, mhusika kwa mara ya kwanza aliona walakini kutoka kwa kiongozi wake huyo
Hata hivyo kwa sasa anaelewa vizuri kilichotokea, ni MZK-B alikuwa kazini na yote yaliyokuwa yametokea yalikuwa ni mapishi kutoka kwa MZK-B
 
MARA YA KWANZA MHUSIKA AGUNDUA WALAKINI KWENYE TANGAZO LA UZINZI LA KM-B NA KUANZA KUONA KUWA KUNA UWEZEKANO LILIKUWA LIMEPIKWA

……………..inaendelea


Kwa hiyo, mhusika alikuja kugundua walakini kwenye tangazo la KM-B, baada ya kuwa amefanya maongezi na MKE WA KIONGOZI XB

  • Haukuwa umepita muda mrefu sana tangu kupita kwa tangazo la KM-B na kufanyika kwa maongezi ya mhusika na MKE WA KIONGOZI XB
  • Yalikuwa ni maongezi yao kwa mara ya kwanza
  • Vile vile, haukuwa umepita muda mrefu sana tangu mhusika wafahamiane na huyu mama na kufikia hatua ya angalau kufanya maongezi
Vile vile hadi kufikia muda huo, mhusika alikuwa hajamujua kwa undani mtu yeyote yule kanisani hapo kuanzia waumini hadi viongozi wa waumini

SIKU AMBAYO MAONGEZI YA MHUSIKA NA MKE WA KIONGOZI XB YALIFANYIKA

Ilikuwa ni siku ya J2 jioni na ambayo ilikuwa ni J2 ya pekee kwa sababu ilikuwa ni siku ya Ibada ya Harusi pia

  • Maongezi yalifanyika baada ya Ibada ya harusi kuisha
  • Mhusika wa harusi hiyo alikuwa ni kijana ambaye naye ni mtumishi Kanisani hapo, akiwa anatumika chini ya uangalizi pamojan na ridhaa ya KM-B
  • Kwa hiyo ilikuwa ni harusi ya kijana ambaye yuko karibu sana na KM-B
Kwenye matukio ya aina hii kanisani, kawaida siku zote mhusika huwa anatoa michango ya harusi ila kwenye sherehe ile ya jioni huwa hahudhurii. Alikuwa anaweza kuwepo kwenye Ibada tu, halafu baada ya Ibada kuisha, huondoka na kurudi nyumbani kimoja.

O kawaida yake, siku hiyo pia, mhusika alikuwa katika harakati za kujiandaa arudi nyumbani mara baada ya Ibada ya Harusi kuisha. Ilikuwa ni mida baada ya saa 10 jioni na ndiyo pale MKE WA KIONGOZI XB alipomfuata mhusika na kumuomba waongee kidogo. Maongezi yao siku hiyo yalianzia nje Kanisani hapo kwenye umati wa watu waiokuwepo kwenye Ibada hiyo ya jioni lakini hatimaye walihamia kwenye kibanda cha wachoma chips kilichokuwepo karibu kwa wakati huo maeneo hayo. Hii ilitokana na sababu moja kubwa kwamba MKE WA KIONGOZI XB alikuwa anahitaji kula chakula, alikuwa hajala siku nzima

MUDA MFUPI KABLA HAWAJAHAMIA KWENYE KIBANDA CHA CHIPS: TUKIO LA KIPEKEELAJITOKEZA KIPINDI MHUSIKA AKIWA HAPO NJE ANAENDELEA KUONGEA NA MKE WA KIONGOZI XB

Wakiwa bado wako nje kabla hawajahamia ndani kwenye kibanda cha chips, walikuja vijana wawili na kumnong’oneza maneno mhusika, maneno ambayo huyu MKE WA KIONGOZI XB hakuweza kuyasikia

  • Vijana hao walihitaji kuazima kwa muda gari la mhusika ili wakalitumie kwa ajili ya sherehe ya siku hiyo
  • Mmojawapo wa vijana hao wawwili, kipindi kifupi baadaye mbele alikuja kuwa mkwe wa MZK-B
  • Kijana huyu alikja baadaye kumuoa binti wa MZK-B
  • Ni vijana ambao kwa wakati huo, mhusika hakuwa na mazoea nao wala hakuwa anafahamiana kivile kiasi cha kufikia kuaminiana katika kiwango cha kuazimana vyombo vya moto
  • Ni kwa sababu mhusika alikuwa bdo mgeni kabisa kanisani hapo
Mhusika alitoa udhuru kwa ombi la vijana haokuwa ana ratiba ya kurudi nyumbani mapema, ukizingatia kuwa kawaida magari yote ambayo huwa yanatumika kwenye sherehe kama hizi huwa yameandaliwa kabla na kamati ya maandalizi. Lakini alishangaa vile vile kwa nini vijana hao walifikia hatua kubwa kama ile kwa mtu ambaye hawafahamiani kwa ukaribu huo.

Baada ya kukosa gari, hatimaye vijana hao waliondoka, huku MKE WA KIONGOZI XB akiwa hajasikia ni nini waliongea na mhusika, na wala mama huyu hakumuuliza mhusika waliongea naye nini baada ya kuwa wameondoka

Hii ilikuwa ni kabla mhusika na mama huyu, hawajahamia ndani kwenye kibanda cha chips

Hata hivyo vijana hao kumbe walikuwa wame-syncronize operations zao na huyu mama. Yeye wakati huo akiwa anatumika kama kuwa-cover na umati wa watu uliokuwepo pale kanisani, lakini pia akiwa yuko tayari kutumika kama shahidi kwa iwapo lolote lile lisilokuwa la kawaida, lingeweza kutokea siku hiyo au mbele ya safari baada ya siku hiyo

MHUISKA NA MKE WA KIONGOZI XB WAHAMISHIA MAONGEZI YAO NDANI YA KIBANDA CHA CHIPS
  • Ilikuwa ni baada ya MKE WA KIONGOZI XB kudai kuwa hajala chakula
  • Walihamia ndani ya kibanda cha chips muda mfupi tu baada ya vijana waliokuwa wanataka kuazima gari kuondoka
  • Baada ya kuhamia, ndani ndiyo pale sasa MKE WA KIONGOZI XB alipopata nafasi ya kumuuuliza mhusika kuwa vijana hao walikuwa wanahitaji nini
  • Mhusika alimweleza mama huyu shida yao na mama huyo hatimaye kumuonya mhusika kuwa asije akajaribu kuwapatia gari lake hata siku moja
Hata hivyo kadri siku zilivyoenda, baadaye mhusika alikuja kugundua kuwa MKE WA KIONGOZI XB na aliyekuja kuwa MKWE WA MZK-B, ambaye alikuwa ni mmojawapo wa vijana wawaili waliokuja kuazima gari la mhuskka, ni watu maswahiba wa karibu sana, na wa kipindi kirefu sana

NEXT:

MAONGEZI YA MHUSIKA NA MKE WA KIONGOZI XB NA TANGAZO LA UZINZI LA KM-B
 
……………inaendelea

NDANI YA KIBANDA CHA CHIPS: MAONGEZI YA MHUSIKA NA MKE WA KIONGOZI XB KUHUSIANA NA TANGAZO LA UZINZI LA KM-B


Wakiwa ndani ya kibanda cha chips huku MKE WA KIONGOZI XB anakula chakula, mama huyu alianza kumponda KM-B kuwa anatumia mapepo, na ndiyo maana alitoa tangazo la wazinzi kupita mbele ya madhabahu lakini hakujitokeza hata mtu mmoja. Mara baada tu ya mama huyu kusema haya:

  • Mhusika akagundua kuwa alitoa mchango wa harusi ya siku hiyo lakini hakuwa amepewa kadi ya mwaliko, wakati mwenye harusi alikuwa ni mtu wa karibu sana na KM-B
  • Kuna watu asiowafahamu vizuri wametaka kuaziima gari lake, nia yao ikiwa possibly kumfanya aonekane kuwa hayupo maeneo ya Kanisani, na pengine hata kufanya hujuma kwenye gari lake
Baada ya kuwa ameyaona haya yote, mhusika aliamua muda huo huo kuondoka maeneo yale na kurudi nyumbani. Hapo ilikuwa sasa ni mida ya saa moja jioni usiku, na hafla ya usiku ilikuwa inafanyikia maeneo hayo ayo ya Kanisani

Mpaka hapa, mhusika akawa anaanza kupata picha isiyoridhisha kutoka kwa KM-B, na hadi siku anaondoka Kanisa B na kurudi tena Kanisa A bado alikuwa na picha ambayo haikuwa sahihi kuhusiana na KM-B

HITIMISHO

Hata hivyo, akiwa yuko Kanisa A, hatimaye alikuja kugundua mambo makubwa manne kwenye tukio hili kama ifuatavyp

Tangazo la uzinzi alipelekewa na watu anaowaamini na akaambiwe alitangaze mbele ya kanisa zima

Hii ni kutokana na ukweli kuwa, kabla ya hapo, KM-B hakuwa amewahi kutoa tangazo la aina hiyo, na baada ya hapo hakuwahi tena kutoa tangazo la aina hiyo au linalofana na hilo, hadi siku mhusika anaondoka kanisani hapo kurudi tena Kanisa A

Swala la mhusika kutoa mchango wa harusi kwa kijana ambaye yuko karibu sana na KM-B na mhusika kutopewa kadi ya ukaribisho, yalikuwa ni maelekezo ya makusudi na yenye nia njema sana kwa mhusika, kutoka kwa Mk-B

Ikumbukwe kuwa mhusika wakati huo alikuwa amebadilisha mazingira, na angeweza kupewa kadi ya mwaliko halafu akaamua kwa mara ya kwanza, kuwepo kwenye hafla ya harusi jioni baada ya saa moja, kitu ambacho hapo awali alikuwa hafanyi. Chochote kingeweza kumtokea akiwa kwenye hafla hiyo halafu ambaye angetakiwa kujibu ni yeye KM-B

Pamoja na jitihada za MK-B kuchukua hatua za kumkwepesha mhusika ili asiwepo kabisa kwenye hafla hiyo ya usiku, bado kuna mtu alijitokeza na kufikia hadi hatua ya ku-organize watu wa kuazima gari la mhuiska.

Nia ya mtu huyu ilikuwa ni kutengeneza mazingira yanayoonyesha kuwa mhusika hayupo maeneo yale ya Kanisani na hivyo kupelekea watu wajue kuwa alikuwa tayari amesharudi nyumnbani kwake kama ilibvyo kawaida yake, kumbe hapana

  • Huyu mtu alijua kuwa KM-B ameagiza mhusika asipewe kadi ya mwaliko, kukwepesha chochote kile ambacho kingeweza kujitokeza.
  • Hata hivyo hapo hapo akatokea tena MKE WA KIONGOZI XB akiwa na counter strategy ya kuhakikisha kuwa, kinatokea kile ambacho KM-B alikuwa amelenga kukikwepa
  • Vile vile, kitendo cha MKE WA KIONGOZI XB kuhamishia maongezi ndani ya kibanda cha chips, nacho pia kinaonyesha kama ilikuwa ni strategy nyingine ya kuhakikisha kuwa mhusika anaendelea kuwepo maeneo yale nje ya muda ambao yeye mwenyewe alikuwa amepanga kuwepo maeneo hayo
MKE WA KIONGOZI XB na vijana waliokuja kuazima gari ilikuwa ni syndicate moja. Tangazo alilotoa KM-B alipewa na akashauriwa alitoe, sawa na lile alilowahi kutoa akiwatambulisha watu kwa majina kanisani pasipo kuwa na ulazima wowote wa kufanya hivyo

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Vipi habari za Rais Magufuli? Hali yake iko vipi?

Rumors ati ametuacha 🙁
 
UPDATE: TUESDAY, 16 MARCH 2021

MZEE KIONGOZI WA KANISA B (MZK-B)

……………..inaendelea

MATUKIO MENGINE MUHIMU SANA YANAYOHUSIANA NA MZK-B NA KUNDI LAKE

A: MZK-B AAMURU MHUSIKA ANYIMWE AU ASIUZIWE DVD ZA MAHUBIRI YA MCHUNGAJI MGENI ALIYEKARIBISHWA KUJA KUHUHUBIRI KANISA B AKITOKEA MBEYA

  • Hii ilitokea baada ya mhusika kuwa ameonana na KM-B na kumuomba auziwe DVD za mahubiri hayo kwa sababu alikuwa anazihitaji
  • MZK-B alimchukua mhusika na kumpeleka hadi kwa kijana aliyekuwa anahusika na kutengeneza DVD za mahubiri hayo
  • MZK-B alimkabidhi mhusika kwa kijana huyo huku akimpa maelekezo (kijana) kuwa ahakikishe mhusika anapata kanda za mahubiri hayo
  • Kijana alikubali na mhusika alilipia kabisa hela kwa ajili ya matengenezo ya DVD hizo
Baada ya muda, kijana huyo aligoma kutengeneza DVD hizo na kuamua kumrudishia mhusika pesa aliyokuwa amelipia kwa ajili ya matengenezo ya DVD hizo.
  • Mhusika alikosa DVD hizo na hakuwahi kuzipata tena hadi leo
  • Baadaye alikuja kugundua kuwa ni MZK-B aliyetoa zuio la mhusika kutokuuziwa DVD hizo
Maelezo zaidi ya nyongeza kuhusiana na tukio hili yatafuata baadaye

B: MZK-B ASAMBARATISHA KIKUNDI CHA WANAUME KILICHOKUWA KINAFANYA MAZOEZI YA NYIMBO JIONI MOJA, MAZOEZI HAYO YALIYOKUWA MARA ZOTE YANAONGOZWA NA MHUSIKA
  • Yalikuwa ni mazoezi ya nyimbo kwa ajili ya sikukuu ya wanaume Kanisani hapo
  • Mhusika ndiyo alikuwa anaongoza mazoezi hayo akiwa kama mwalimu wa nyimbo
  • Ilikuwa ni siku ya Ijumaa jioni ambapo sikukuu tarajiwa ilikuwa siku ya J2 ya wiki hiyo
  • Ilikuwa ni mwezi Mei 2018
Maelezo zaidi ya nyongeza kuhusiana na tukio hili yatafuata baadaye

C: MZK-B AAGIZA KUTOLEWA KWA TANGAZO HEWA WAKATI WA IBADA YA IJUMAA JIONI, TANGAZO LILILOPELEKEA MHUSIKA KWENDA MPAKA KANISA LA TAG KINONDONI KESHO YAKE
  • Tangazo hili lilitolewa na Kiongozi wa Chama cha Wanaume kwa agizo la MZK-B
  • Lilitotelwa kwenye jioni ya siku ile ile ambayo MZK-B alisambaratisha mazoezi ya nyimbo ya kikundi cha wanaume; siku ya Ijumaa
  • Tangazo hilo lilihusiana na utoaji wa damu kesho yake Jumamosi kabla ya J2 ile ambayo ndiyo ilikuwa ni ya sikukuu ya wanaume
  • Tangazo liliwataka wanaume wote kesho, yaani Jumamosi, wafike TAG Kionondoni kwa ajili ya utoaji wa damu, kama mojawapo ya mambo yaliyotakiwa kuambatana na sherehe za sikukuu yao hiyo J2 iliyokuwa inafuata
  • Mhusika aliitikia wito huo na kweli kesho yake alifika TAG Kinondoni
Hata hviyo, hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa amefika hapo TAG Kinondoni kwa ajili ya zoezi hilo la utoaji wa damu, na wala Mchungaji aliyemkuta Kanisani hapo siku hiyo, hakuwa na taarifa zozote zilizohusiana na swala la utoaji damu mahali hapo
  • Mhusika alifika pale akajikuta yuko peke yake
  • Hata yule aliyekuwa ametumwa kutoa tangazo hilo, yaani kiongozi wa wanaume wa Kanisa B, naye hakuwa amefika na hakufika TAG Kinondoni siku hiyo
Baada ya mhusika kufika TAG Kinondoni, alimpigia kiongozi wa wanaume na kumjulisha kilichokuwa kimejiri, na kiongozi huyo alimjibu mhusika kuwa wao wapo Kanisani wanaendelea na mazoezi ya uimbaji kwa ajili ya sikuuu kesho yake, yaani J2

Maelezo zaidi ya nyongeza kuhusiana na tukio hili yatafuata baadaye

D: BAADA YA MZK-B KUWA AMESAMBARATISHA KIKUNDI CHA MAZOEZI SIKU YA IJUMAA, ALIAGIZA MAZOEZI HAYO YAFANYIKE KESHO YAKE JUMAMAOSI NA “DRUMS” ZIONGEZWE KWENYE MZIKI WA NYIMBO ZILIZOTAKIWA KUIMBWA KESHO YAKE, YAANI J2 KWENYE SIKUKUU HIYO YA WANAUME

  • Baada ya mazoezi ya uimbaji kusambatrtaishwa Ijumaa, MZK-B aliagiza mazoezi hayo yafanyike kesho yake Jumamosi, ila pasipo mhusika kuwa anajua hilo
  • Siku zote za nyuma kabla ya siku hiyo mazoezi hayo yyalikuwa yanafanyika pasipo kutumia drums
  • Ni kinanda tu kilichokuwa kinatumika
MZK-B alihitaji mhusika asiwepo kwenye mazoezi hayo ya mwisho Jumamosi hiyo kwa sababu vinginevyo mhusika nagezuia matumizi ya drums kwenye uimbaji huo kwani yeye ndiyo alikuwa amepewa mamlaka na KM-B pamona na Kiongozi wa wanaume, ya kuamua vyombo vya aina gani vitumike katika uimbaji na uimbaji huo ufanyike kwa namna gani
  • Ni kwa sababu yeye ndiye aliyekuwa ametunga nyimbo kwa ajili ya sikuku hiyo na ndiye aliyekuwa anafundisha nyimbo hizo
  • Kwa hiyo MZK-B alihitaji mwalimu wa nyimbo asiwepo siku hiyo ya Jumamosi iliyokuwa inafuatana na j2 ya sikukuu, ili aweze kufanya marekebisho aliyoyahitaji yeye
  • Hii ni kutokana na ukweli kuwa MZK-B amejipa mamlaka makubwa kuzidi watu wote hapo Kanisa B
Kwa hiyo alichofanya MZK-B kwenye mpango mkakati wake siku ya Ijumaa wakti anasambartisha zoezi la uimbaji, ni kumwagiza kiongozi wa wanaume atoe tangazo hewa la utoaji wa damu, ili mhusika asiwepo kwenye mazoezi siku iliyokuwa inafuata.
  • Na kama possibly mhusika angeamua kutokwenda TAG Kinondoni kesho yake kwa ajili ya zoezi hilo la utaji damu,basi kulikuwa na possibility kwamba angefika Kanisani na kuwakuta wenzake wote hawapo
  • Maelezo ya kutokuwepo kwao yalikuwa ni rahisi tu kwamba “wameenda TAG Kiondondoni kwa ajili ya zoezi la utoaji damu kama wanaume wote walivyotangaziwa jana kwenye ibada ya jioni”
  • “Vipi, wewe mbona hujaenda, hukulisikia tangazo jana jioni baada ya Ibada?”
Huyu ndiye MZK-B. Na mtu anapokuwa anamuongelea mtu huyu, ujue anamuongelea MZK-B pamoja na kundi la watu wake, baadhi yake wakiwa ni wafuatao
  • Mshiriki-1 (MSH-1)-huyu ni yule mshiriki ambaye waliwahi kushitakiana na mhusika ofisini kwa KM-B mara mbili
  • “KIONGOZI XB”
  • “MKE WAKE NA KIONGOZI XB”
Kwa hiyo mara zote, kwenye kikosi kazi cha MZK-B, hao wote walikuwa hawakosekani. Wanaweza kuwa walikuwepo na wengine lakini hizo namba lazima zilikuwa hazikosekani katika set-up zote zilizokuwa zinafanywa na MZK-B

Maelezo zaidi ya nyongeza kuhusiana na tukio hili yatafuata baadaye

HITIMISHO


Kwa hiyo katika maelezo yake yote, mhusika anapokuwa anaongelea chochote kuhusiana na MZK-B, ni kwa wakati huo huo pia ambapo anakuwa anawongelea wafuatao, japo pasipo kuwataja au kuawaelezea uhusika wao kwa kina kwenye tukio, isipokuwa uhakika kabisa ni kuwa details za uhusika wao katika kila tukio linalomhusu MZK-B; MZK-B mwenyewe anakuwa anazo. Watu hawa ni watatu nao ni:
  • Mshiriki-1 (MSH-1)
  • “KIONGOZI XB”
  • “MKE WAKE NA KIONGOZI XB”
……………….inaendelea


NEXT: MAELEZO YA NYONGEZA TIMILIFU KUHUSIANA NA:

A: MZK-B AAMURU MHUSIKA ANYIMWE AU ASIUZIWE DVD ZA MAHUBIRI YA MCHUNGAJI MGENI ALIYEKARIBISHWA KUJA KUHUHUBIRI KANISA B AKITOKEA MBEYA

B: MZK-B ASAMBARATISHA KIKUNDI CHA WANAUME KILICHOKUWA KINAFANYA MAZOEZI YA NYIMBO JIONI MOJA, MAZOEZI HAYO YALIYOKUWA MARA ZOTE YANAONGOZWA NA MHUSIKA

C: MZK-B AAGIZA KUTOLEWA KWA TANGAZO HEWA WAKATI WA IBADA YA IJUMAA JIONI, TANGAZO LILILOPELEKEA MHUSIKA KWENDA MPAKA KANISA LA TAG KINONDONI KESHO YAKE

D: BAADA YA MZK-B KUWA AMESAMBARATISHA KIKUNDI CHA MAZOEZI SIKU YA IJUMAA, ALIAGIZA MAZOEZI HAYO YAFANYIKE KESHO YAKE JUMAMOSI NA “DRUMS” ZIONGEZWE KWENYE MZIKI WA NYIMBO ZILIZOTAKIWA KUIMBWA KESHO YAKE, YAANI J2 KWENYE SIKUKUU HIYO YA WANAUME
 
MZEE KIONGOZI WA KANISA B (MZK-B)

……………..inaendelea

A: MZK-B AAMURU MHUSIKA ANYIMWE AU ASIUZIWE DVD ZA MAHUBIRI YA MCHUNGAJI MGENI ALIYEKARIBISHWA KUJA KUHUHUBIRI KANISA B AKITOKEA MBEYA


Tukio hili lilitokea baada ya Mchungaji mgeni kutoka Mbeya, kufika Kanisa B na kuendesha kongamano la ndani kwa muda wiki nzima
  • Mchungaji huyu alionekana si maarufu sana lakini alikuwa ana mafundisho mazuri sana na yenye ushuhuda unaogusa sana
  • Mchungaji huyu alikuwa pia ana shuhuda nyingi sana ambazo zinaweza kumjenga muumini wa ngazi yoyote ile, mchanga au hata mkomavu pia
  • Vile vile, Mchungaji huyu alionekana kuwa na aina za shuhuda ambazo zinaweza kuwepo na wachungaji wachache sana ndani na nje ya nchi yetu
Ni kawaida kwenye nyumba zote za Ibada kuwa ugeni mkubwa na wa muhimu kwa kiwango hiki unapokuwa umetokea, baadaye huwa zinatengenezwa DVD kwa ajili ya washiriki kununua na kuendelea kusikiliza mafundisho ya wachungaji wao wakiwa majumbani mwao
  • Kongamano lilipoisha, waumini wakatangaziwa kuwa DVD za mafundisho ya muda wote wa wiki nzima zitakuja kutolewa hapo baadaye
  • Kweli baada ya muda mfupi kuwa umepita, waumini wote walitangaziwa kuwa DVD hizo ziko tayari, na wakaelekezwa mtu wa kumona ili waweze kuzinunua
Mhusika naye alienda kununua DVD hizo ila akakuta kuna DVD moja ambayo kwa wakati huo ilikuwa tayari na ilikuwa ya siku moja tu kati ya siku zote nane (8) ambazo Mchungaji huyo mgeni aliweza kufanya huduma hapo Kanisa B
  • Baada ya hapo mhusika alipewa maelezo kuwa zingine ziko njiani zinatayarishwa, asubirie kidogo
  • Mhsuika alikaa anasubiria kwa takribani miezi mitatu lakini DVD hizo zilikuwa bado hazijawa tayari
  • Kongamano la kwanza la Mchungaji huyu lilifanyika Septemba 2017, na hatimaye alirudi tena kwenye kongamano jinge la pili mwezi Desemba 2017, DVD za kongamano la kwanza zikiwa bado haziko tayari
Baada ya kongamano la kwanza kuisha, mtumishi aliondoka huku waumini wakiwa wamependekeza kuwa inabidi arudi tena; na kweli baada ya miezi mitatu kuppita, ilipofika Desemba 2017, mchungaji huyu alikaribishwa tena kwa ajili ya huduma ya kongamano jingine la pili na aliitikia wito

KONGAMANO JINGINE LA PILI LAFANYIKA TENA MWEZI DESEMBA 2017, MTUMISHI AKIWA NI YULE YULE ALIYEWAHI KUHUDUMU KWENYE KONGAMANO LILE LA KWANZA

  • Mtumishi huyu alirudi tena kwa mara ya pili, huku akiendelea na mtindo wake wa mahubiri yenye ushuhuda kemkem, na safari hii alikuja na ujumbe uliokuwa na kichwa “ANZA MWAKA NA BWANA”
  • Mchungaji alifika siku ya J2 na kuanza kongamano (siku hiyo hiyo), ambalo lilikuwa linaendelea hadi J2 nyingine ya wiki iliyokuwa inafuata
Kwenye kongamano hili la pili, mhusika alifanikiwa kuhudhurai siku tano (5) kati ya nane (8) alizotarajia kuhudhuria

  • Si kwamba alikosa nafasi ya kuhudhuria hizo siku zingine tatu, hapana
  • Kuna kitu kilitokea hapo katikati na hicho ndicho kilichopelekea mhusika asihudhurie zile siku tatu zingine kuanzia Alhamis hadi Jumamosi
  • Kitu hicho kilichoingilia kati kwenye kwenye huduma ta mtunishi huyu hakikuwa kizuri na kilikuwa engineered na MZK-B na kundi lake
Mtumishi huyu alibadilisha kichwa cha “ANZA MWAKA NA BWANA” na kuanza kufundisha mafundisho feki ya laana, huku akiwaombea waumini ili kuwaondolea laana hizo
  • Zilisemekana kuwa ni laana zinazotokana na maagano ya mababu na mababu zao waumini
  • Kitu hiki si sahihi kulingana na Doctine of Salvation and is almost a blasphemy ukilinganisha na kile ambacho Doctine of Salvation huwa inaki-advocate kuhusu laana
Huyu mtumishi aliamua kufundisha mafundisho haya si kwamba alikuwa haelewi kuwa yana matatizo hapana isipokuwa
  • Alikuwa ameshinikizwa na MZK-B na kundi lake
  • Lengo la shinikizo hilo mhusika atakuja kuliongelea zaidi baadaye atakapokuwa anaongelea huduma ambayo iliwahi kufanywa na mtumishi David Belela
  • Kwa hiyo mtumishi huyu aliombwa afundishe mafundisho hayo, na kwa kujua kuwa waumini wengi hawaekewi mambo mengi na hivyo wengi wao wangeitikia bila shaka yoyote
  • Lengo la yeye kushinikizwa kufundisha hivyo hakulijua, ila wale waliokuwa wamechukua hatua hiyo walikuwa wanalijua
  • Kwa hiyo waliamua kumtumiapasipo yeye mwenyewe kujua kuwa anatumika
Ukweli ni kuwa kwa mtu yeyote ambaye ameokoka, kumwambia unamuondolea laana ni sawa na kumweleza kuwa yupo kaburini amekufa ni maiti, wakati unamuona yuko hai mbele yako na unaongea naye; na wahubiri wote wanaodai wameokoka huku bado wanahubiri laana kwa waumini makanisani mwao, hao ni wale ambao ni wezi wa sadaka. Ni wale majambazi waliojificha kanisani wakidai kuwa ni watumishi wa Mungu

KONGAMANO LA PILI NALO LAFIKIA MWISHO

Baada ya kongamano hili la pili kuwa limepita, mhusika alienda tena kwa wahusika wa DVD, kuona kama angeweza kupata baadhi ya zile za kongamano la mwanzo, ikiwa ni pamoja na baadhi ya za hili jingine la pili.
  • Mhusika alifanikiwa kupata tena DVD nyingine ya siku moja tu iliyotokana kongamano hili la pili
  • Zadi mhusika aliambiwa asubirie tena DVD zingine za kongamano hili la sasa, ikiwa ni pamoja na zile za kongamano lile lililokuwa limepita mwanzo
Mhusika aliendelea kusubiria na ulipokuwa umepita muda mrefu sana, tuseme zaidi ya nusu mwaka tangu kongamano la pili liishe, ndipo alipoamua kwenda kumuona KM-B na kumweleza shida yake.

Ndiyo hapo sasa KM-B alipochukua hatua ya kumpeleka mhusika kwa kijana aliyekuwa anahusika na kutengeneza DVD hizo na kilichofuata baada ya hapo ni kama ambavyo mwandishi tayari ameshaelezea hapo awali.

Mhusika hakufanikiwa tena kupata DVD zingine zaidi ya zile mbili alizozitaja, na aliyefanya kazi ya kuzuia DVD hizo ni MZK-B

NEXT:

B: MZK-B ASAMBARATISHA KIKUNDI CHA WANAUME KILICHOKUWA KINAFANYA MAZOEZI YA NYIMBO JIONI MOJA, MAZOEZI HAYO YALIYOKUWA MARA ZOTE YANAONGOZWA NA MHUSIKA
 
NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA “UKUTA”WA ALHAMIS TAREHE 01 SEPTEMBA 2016

Kwa hiyo kutokana na maelezo yaliyotolewa awali hapo juu, msomaji anaweza kuona ni kitu gani kingine cha ziada kilichokuwa nyuma ya UKUTA, japo UKUTA ulikuja kuahirishwa na hatimaye kutokuwepo kabisa


  • Ndiyo maana mwaka jana ilipofika muda karibia na uchaguzi, mwandishi wa taarifa hizi alisitisha uzi huu kukwepesha mgongano wa maslahi ya kisiasa
  • Ni kwa sababu jambo kamaUKUTA lilikuwa la kisiasa na asingeweza kuliongelea kipindi hicho, lingeweza hata kusababisha mtafaruku
Na by the way, kwa wenye kumbukumbu nzuri, nani aliyetangaza kuwa kungekuwa na UKUTA, kabla haujafutwa? Kuna anayemkumbuka mtu aliyewahi kuutangaza UKUTA? Kama kuna mtu anamkumbuka, sasa hivi yuko wapi? Anafanya nini?
 
MASAHIHISHO/ NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA BAADHI YA TAARIFA ZILIZOPO HAPO JUU
  • Mchungaji mgeni kutoka Mbeya alikuja kuhudumu Kanisa A kwa mara kwanza, Septemba 2014 na alirudi tena kwa mara ya pili mwezi Desemba 2014
  • Mhusika alihamia Kanisa B mwanzoni mwa mwezi Juni 2014
  • Sikuku ya wanaume ambayo moja ya mazoezi yake ya uimbaji yaliwahi kusambartishwa na MZK-B, ilifanyika mwezi Mei 2015, yaani mwaka uliofuata baada ya mhusika kuwa amehamia Kanisa B
 
UPDATE: WEDNESDAY, 17 MARCH 2021



B: MZK-B ASAMBARATISHA KIKUNDI CHA WANAUME KILICHOKUWA KINAFANYA MAZOEZI YA NYIMBO JIONI MOJA, MAZOEZI HAYO YALIYOKUWA MARA ZOTE YANAONGOZWA NA MHUSIKA


MAELEZO YA UTANGULIZI

Mazoezi haya ya nyimbo yalikuwa ni kwa ajili ya sikuku ya wanaume iliyowahi kufanyika mwezi Mei 2015. Ikumbukwe kuwa mhusika alihamia Kanisa B mwezi Juni 2014. Kwa hiyo hadi kufikia muda huo alikuwa anaelekea kutimiza mwaka mzima akiwa yuPo Kanisa B

MAELEZO YA UTANGULIZI

Ni kwamba mazingira ya Kanisa B yalimvutia zaidi mhusika kushiriki kwenye huduma, ukilinganisha na kule alikokuwa ametoka. Kwa hiyo hadi kufikia wakati huo, alikuwa tayari amehshaanza kuwa anashiriki kwenye huduma mbalimbali.

Tofauti na kule alikokuwa ametokea yaani Kanisa A, huko kwenyewe hakuwahi kushiriki huduma yoyote na kilichokuwa kinapelekea asifanye hivyo ni sababu moja kubwa kwamba huko Kanisa A kulikuwa kunaonekana wazi kabisa kuwa ili mtu aweze kushiriki kwenye huduma, alihitaji kuwa na UPAKO wa hali ya juu sana. Hii ni kutokana na ukweli kuwa viongozi wa huko Kanisa A akiwemo Kiongozi Mkuu mwenyewe (KM-A), wanaonekana kuwa na UPAKO wa hali ya juu muno na wa kipekee sana, na hivyo haikuwa rahisi kwa muumini mchanga kama yeye kushiriki huduma yoyote ile pindi alipokuwa yuko huko

Kwa hiyo mhusika aliondoka Kanisa A akiwa hajawahi kushiriki kwenye huduma yoyote ya kipekee, hadi alipohamia Kanisa B.

  • Mhusika alianza kushiriki kwenye huduma mbali mbali baada ya kuhamia Kanisa B
  • Mhusika hakuwahi kushiriki huduma yoyote alipokuwa bado yuko Kanisa A
Vile vile, baada ya kuhama tena kutoka Kanisa B (April 2017) na kurudi tena Kanisa A ambako ndiko aliko mpaka muda huu, mhusika hajawahi kushiriki tena huduma yoyote ile ya kipekee mithili ya zile alizowahi kushiriki pindi alipokuwa yupo kanisa B

Kuna sababu kuu mbili zilizopelekea mhusika asiweze kushiriki huduma za aina hii pindi aliporudi tena Kanisa A, nazo ni:

  • Kama alivyotangulia kusema hapo juu hivi punde, Viongozi wa Kanisa A, akiwemo KM-A wana upako wa hali ya juu muno, UPAKO unaopelekea waumini walio wengi wasiweze kuwa na qualifications za kutoa huduma Kanisani hapo, mhusika akiwa mmoja wao
  • Muda mfupi tu baada ya mhusika kurudi Kanisa A, lilijitokeza kundi la watu wa hatari kwa maisha yake, na ambalo lipo mpaka muda huu
Kundi hilo la hatari kwa maisha ya mhusika huwa linaongozwa na KM-A



…………………….inaendelea
 
…………….inaendelea

B: MZK-B ATUMIA MBINU KUSAMBARATISHA KIKUNDI CHA WANAUME KILICHOKUWA KINAFANYA MAZOEZI YA NYIMBO…………………


Kwa hiyo, ilipofika mwezi Mei 2015 muda ambao huwa kila mwaka kuna sikuku ya wanaume
  • Mhusika aliwasiliana na uongozi wa wanaume na kuuomba kama anaweza kuruhusiwa kutunga nyimbo kwa ajili ya kuimba siku hiyo
  • Hapo kabla, chama hiki cha wanaume Kanisani hapo hakikuwa na utamaduni huu wa kuwa na kwaya ya kuimba siku hiyo ya sikukuu ya wanaume
  • Kwa hiyo kwa safari hii, mhusika aliomba kitu hicho kifanyike na alipata ridhaa kutoka kwa viiongozi hao
Taarifa za mkakati huo wa uwepo wa kwaya siku ya sikukuu ya wanaume hatimaye zilikmfikia pia KM-B, ambaye naye pia aliridhia.

Mbali na KM-B kuridhia ombi hili la mhusika
  • KM-B alienda mbali zaidi kwa yeye naye pia kushiriki kwenye mazoezi ya uimbaji huo, siku zile mbili za mwanzo (Huyu KM-B yeye yuko tofauti kabisa na KM-A; ambaye yeye KM-A kwa mfano, huwa anafikia hadi hatua ya kuwapanga waumini namna ya ukaaji kwenye somo la uanafunzi na maandiko, halafu baada ya hapo hashiriki kwenye somo hilo isipokuwa huondoka na kwenda kunywa chai)
  • KM-B alishiriki siku ya kwanza kabisa pamoja na nyingine ya pili iliyofuata, halafu baada ya hapo akawaacha wanaume wakaendelea na mazoezi yao wenyewe
Katika siku zote hizo za mazoezi ya awali, MZK-B, hakuwahi kuhudhhuria hata siku moj;, na kwa kawaida yeye ilikuwa ni nadra sana kumuona kwenye Ibada za jioni.

Mazoezi haya ya uimbaji yalikuwa yanafanyika kila jioni mara baada ya Ibada za jioni kuisha.

Mhusika hakumbuki vizuri lakini katika kipindi chote cha takribani miaka mitatu aliyowahi kukaa Kanisa B, nadhani ni siku mbili au tatu tu, ambazo aliwahi kuwa pamoja na MZK kwenye Ibada za jioni, mojawapo ikiwa ni jioni ile aliyokuja kutawanyisha mazoezi ya uimbaji. Kwa taarifa zilizokuwa zinamfikia mhusika ni kuwa MZK yeye huwa ni mhudhuriaji mzuri wa Ibada za mikesha ambazo huwa zinafanyika kila wiki siku ya Ijumaa kuanzia saa tatu usiku; Ibada ambazo mhusika naye alikuwa hawezi kuhudhuria.

Kwa hiyo ukiondoa Ibada za kawaida za siku za kila Jumapili, haikuwa rahisi sana kwa MZK-B na mhusika kuwakuta wapo wote pamoja kwenye Ibada sababu zile ambazo mhusika alikuwa anahudhuia, MZK-B alikuwa almost hahuhdhurii, na zile ambazo MZK-B alikuwa anahudhuria (za mikesha), mhusika naye alikuwa hahudhurii kabisa Ibada hizo

MZK-B AHUDHURIA IBADA YA IIJUMAA JIONI NA AMBAYO ILIKUWA IWE SIKU YA MWISHO WA MAZOEZI YA UIMBAJI

Ni kwamba ilikuja ikatokea bahati kwamba kwenye siku ile ya mwisho kaibsa ya mazoezi ya uimbaji ambayo ilikuwa ni siku ya Ijumaa, na J2 yake ndiyo ilikuwa kilele cha sikukuu ya wanaume, mhusika na MZK-B walijikuta wako pamoja kwenye Ibada ya jioni, ambapo ilitarajiwa kuwa baada ya Ibada hiyo, mazoezi ya mwisho kwa ajili ya uimbaji siku ya J2 yangefanyika
  • Ilikuwa ni siku ya mwisho kabisa ya mazoezi ya uimbaji kwa ajili ya J2 ya sikukuu ya wanaume
  • Ilikuwa ni siku ya kwanza kwa MZK-B kuonekana kwenye Ibada za jioni tangu siku mazoezi hayo ya uimbaji yalipoanza
Ikumbukwe pia kuwa mhusika anapokuwa anamwongelea MZK-B, automatically anakuwa anawaongelea wafuatao pia
  • Mshiriki-1 (MSH-1)
  • “KIONGOZI XB”
  • “MKE WAKE NA KIONGOZI XB
…………….inaendelea
 
…………….inaendelea

B: MZK-B ATUMIA MBINU KUSAMBARATISHA KIKUNDI CHA WANAUME KILICHOKUWA KINAFANYA MAZOEZI YA NYIMBO


Kwa hiyo siku MZK-B alipoonekana kwenye Ibada ya jioni, na kwa mara ya kwanza tangu zoezi la uimbaji lianze
  • Baada ya Ibada lilitolewa tangazo na kiongozi wa wanaume likisema kuwa wanaume wote inabidi wabaki kuendelea na zoezi la uimbaji kwa ajlil ya siku ya sikukuu yao
  • Vile vile kiongozi huyo huyo alitoa tangazo kuwa kesho yake Jumamosi, wanaume wote wanaombwa kufika TAG Kinondoni kuanzia saa 3.00 asubuhi na kuendelea, kwa ajili ya zoezi la kuchangia damu, na watu wa BLOOD BANK watakuwepo mahali pale kwaajili ya shughuli hiyo
Baada ya matangazo kuisha na Ibada kuwa imeahirishwa, kikawa kinafuatia sasa kipindi cha zoezi la uimbaji

  • Safari hii badala ya mwenyekiti wa chama cha wanaume kuwakumbusha tena wanaume waendelee kuwepo Kanisani kwa ajili ya mazoezi hayo ya uimbaji, mwenyekiti alimfuata mhusika na kumpa kipaza sauti
  • Baada ya hapo, mwenyekiti alimwelekeza mhusika aanze kutoa tangazo wanaume wakusanyike sehemu ambayo walikuwa wakifanyia mazoezi siku zote ili zoezi la uimbaji liweze kuanza
  • Mhusika alitoa tangazo hilo kwa kulirudia rudia na baada ya muda, aligundua kuwa wanaume wote walikuwa wameshaondoka ikiwa ni pamoja na mwenyekiti aliyekabidhi kipaza sauti kwa mhusika
  • MZK-B naye pia alikuwa hayupo ameondoka
Baada ya hapo, mhusika alirudisha kipaza sauti hicho sehemu stahiki, akatoka nje na kuwasha gari lake akarejea nyumbani kwake

JUMAMOSIILIYOSEMEKANA NI YA UCHANGIAJI DAMU YAWADIA, MAHALI IKIWA NI TAG KINONDONI

Kesho yake mhusika alifika tena Kanisani asubuhi kuona kama kulikuwa na watu waliokuwa wanaelekea TAG Kinondoni kwa ajili ya zoezi hilo la uchangiaji damu, kama ambavyo walikuwa wametangaziwa jana yake, lakini kwa muda huo hapakuwa na mtu yeyote yule kwa ajili ya safari hiyo. Kuchangia damu huko kulikuwa kunaambatana na sikukuu hiyo ya wanaume, kama mchango wao kwenye sikukuu yao hiyo.

Baada ya hapo, mhusika aliamua kuondoka peke yake akielekea TAG Kinondoni, akijua kuwa pengine kuna baadhi walikuwa wameelekea huko moja kwa moja wakitokea majumbani kwao.

Baada ya mhusika kuwasili mahali husika
  • Alikuta hayupo hata mtu mmoja aliyekuwa ametoka Kanisa B, na hadi anaondoka hakuwahi kufika mtu yeyote mwingine zaidi yake
  • Vile vile hapakuwa na taarifa zozote za utoaji damu, na wala watu wa BLOOD BANK hawakuwepo mahali pale
Mhusika alibahatika kuonana na Mchungaji mmoja Kanisani pale ambaye naye pia alishangaa kusikia taarifa hizo zilizohusina na zoezi hilo la uchangiaji damu

Baada ya hapo, mhusika aliondoka na kurudi nyumbani kwake na baadaye tena kuelekea nyumbani kwa “KIONGOZI XB” ambako alikuwa amekaribishwa jioni ya siku hiyo

Ikumbukwe pia kuwa mhusika anapokuwa anamwongelea MZK-B, automatically anakuwa anawaongelea wafuatao pia
  • Mshiriki-1 (MSH-1)
  • “KIONGOZI XB”
  • “MKE WAKE NA KIONGOZI XB

…………………..inaendelea
 
…………….inaendelea

B: MZK-B ATUMIA MBINU KUSAMBARATISHA KIKUNDI CHA WANAUME KILICHOKUWA KINAFANYA MAZOEZI YA NYIMBO

HITIMISHO


Akiwa bado yuko huko alikokuwa ameenda kwa ajili ya zoezi la utoaji damu, mhusika alimpigia simu kiongozi wa wanaume aliyewahi kutoa tangazo hilo jana yake. Mhusika hakumbuki kiongozi huyo alijibu nini, ila mojawapo ya mambo ambayo kiongozi huyo alisema ni kwamba wanaume karibia wote walikuwepo Kanisani muda huo wakifanya mazoezi ya mwisho kabisa kwa ajili ya kesho yake, yaani J2 ya sikukuu. Na kwa sababu mhusika tayari alikuwa na ratiba nyingine ya ugeni nyumbani kwa KIONGOZI XB” jioni ya siku hiyo, hapakuwa na namna yoyote ile ambayo angeweza tena kuonekana kanisani kwa siku hiyo

Siku yenyewe ilipowadia, yaani Jumapili ya sikukuu, wakati walipokuwa wakiimba ndiyo pale mhusika alipobaini mabadiliko kadhaa yafuatayo, kwamba, zoezi la uimbaji lililofanyika siku ya mwisho kabisa na ambayo yeye hakuweza kuhudhuria

  • Liliingiza washiriki wapya kabisa kwa mara ya kwanza kwenye uimbaji huo, na ambao hapo awali, hawakuwa wameshiriki hata siku moja kwenye mazoezi ya uimbaji huo
  • Washiriki hawa ililkuwa ni muhimu waingizwe siku hiyo na katika muda ambao mwalimu wa nyimbo alitakiwa awe hayupo
  • Ni kwa sababu ilikuwa inajulikana wazi kuwa kama mwalimu wa nyimbo angekuwepo siku hiyo ya mwisho wa mazoezi,ni wazi kuwa asingeweza kuridhia marekebisho hayo kufanyika
Marekebisho yaliyofanyika siku hiyo yalikuwa ni ya kuongeza vyombo zaidi vya muziki kwa ajili ya uimbaji huo. Awali uimbaji huo ulikuwa unatumia kinanda tu, hali iliyopelekea nyimbo mbili alizokuwa ametunga mhusika kuwa zinatoa melody kiasi cha kuwafanya watu waliokuwa wanapita karibu, kusimama na kuanza kusikiliza waimbaji waliokuwa wakiimba ndani ya kanisa hilo, wakiwa wamevutiwa na uimbaji huo

Kwa hiyomhusika akiwa hayupo siku hiyo, ulifanyika utaratibu sasa wa kuongeza vyombo vya ziada vya muziki ili kuchuja melody nzuri za nyimbo hizo na hivyo ZILIONGEZWA DRUMS AMBAZO ZILIKUWA ZIKIPIGWA, MSIKILIZAJI WA WIMBO HAWEZI HATA KUSIKIA SAUTI ZA WALE WANAOIMBA.

Kwa hiyo ZILIONGEZWA DRUMS ili kuongeza kelele kwenye wimbo unaoimbwa, na si kuongeza uzuri wa wimbo masikioni mwa watu, hapana

Kwa hiyo wakati wa uimbaji huo, wala sauti ya kinanda ilikuwa haiwezi kusikika tena.

Washiriki wapya wa uimbaji walioongezeka Jumamosi ambayo mhusika hakuweza kuhudhuria mazoezi ya uimbaji, ndiyo wale waliokuwa wakihusika na kupiga vyombo hivi vya nyongeza vya mziki vilivyopelekea kinanda na sauti za waimbaji kutosikika kabisa

Ikumbukwe pia kuwa mhusika anapokuwa anamwongelea MZK-B, automatically anakuwa anawaongelea wafuatao pia

  • Mshiriki-1 (MSH-1)
  • “KIONGOZI XB”
  • “MKE WAKE NA KIONGOZI XB
MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Kwenye machapisho hayo hapo juu, mwandishi ameunganisha mada zote zifuatazo, kama alivyokuwa amezitaja hapo awali:

B: MZK-B ASAMBARATISHA KIKUNDI CHA WANAUME KILICHOKUWA KINAFANYA MAZOEZI YA NYIMBO JIONI MOJA, MAZOEZI HAYO YALIYOKUWA MARA ZOTE YANAONGOZWA NA MHUSIKA

C: MZK-B AAGIZA KUTOLEWA KWA TANGAZO HEWA WAKATI WA IBADA YA IJUMAA JIONI, TANGAZO LILILOPELEKEA MHUSIKA KWENDA MPAKA KANISA LA TAG KINONDONI KESHO YAKE

D: BAADA YA MZK-B KUWA AMESAMBARATISHA KIKUNDI CHA MAZOEZI SIKU YA IJUMAA, ALIAGIZA MAZOEZI HAYO YAFANYIKE KESHO YAKE JUMAMOSI NA “DRUMS” ZIONGEZWE KWENYE MZIKI WA NYIMBO ZILIZOTAKIWA KUIMBWA KESHO YAKE, YAANI J2 KWENYE SIKUKUU HIYO YA WANAUME

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UP NEXT:

KILICHOTOKEA WAKATI MTUMISHI MGENI KUTOKA MBEYA ALIVYORUDI KUJA KUHUDUMU KANISANI B KWA MARA YA PILI, NA KINAVYOHUSIANA NA KILE KILICHOTOKEA KIPINDI MTUMISHI DAVID BELELA (DB) ALIPOKUJA KUHUDUMU KANISA B


Tofauti iliyopo kati ya watumishi hawa wawili ni kwamba

  • Mtumishi kutoka Mbeya ALIKARIBISHWA kwa mara ya pili baada ya kuwa amehitajika na waumini, baada ya waumini wao wenyewe kupendekeza arudi tena kwa mara nyingine, isipokuwa baadaye alikuja akakumbana na vigingi katikati ya huduma yake, vilivyosababishwa na baadhi ya wenyeji wa Kanisa B
  • Waweka vigingi hawa walikuwa MZK-B na kundi lake
Ikumbukwe pia kuwa mhusika anapokuwa anamwongelea MZK-B, automatically anakuwa anawaongelea wafuatao pia

  • Mshiriki-1 (MSH-1)
  • “KIONGOZI XB”
  • “MKE WAKE NA KIONGOZI XB


Zaidi ni kuwa waumini wa Kanisa B walipendekeza mtumishi huyu kutoka Mbeya, awe anakuja kuhudumu kila mwaka kuanzia mwaka huo na kuendelea

Tofauti na huyu mtumishi wa Mbeya, David Belela (DB) yeye HAKUKARIBISHWA BALI ALILETWA

  • Baada ya kuwa AMELETWA, ndiyo baadaye ukaribisho wake ULIFUATA
  • Nia ya DB haikuwa kuja kutoa huduma ya kiroho bali ilikuwa kuhujumu huduma ya kiroho
Kwa haraka haraka ni kuwa, katika namna ya kuhujumu huduma za kiroho, DB anaweza kuwa anafanana sana na viongozi wa Kanisa-A, na pengine hata kuwazidi. Yaani anaweza kuwa katika kiwango ambacho hata hao wako chini, yeye yuko juu zaidi

Supplementary notice: (Post #37 )

 
Ila mhusika huwa ni mtiifu sana linapokuja swala la kanisani,
Kila wito ukitolewa ye huwa anautii

Kidogo kazini huwa ni mbishi...
 
Back
Top Bottom