Mkataba wa Bandari: Mbunge Aida Khenani akiri kupelekwa Dubai, lakini mpaka wanarudi hakujua walikwenda kufanya nini

Mkataba wa Bandari: Mbunge Aida Khenani akiri kupelekwa Dubai, lakini mpaka wanarudi hakujua walikwenda kufanya nini

Ila mheshimiwa Angekuwa amefanya vizuri kama angetusanua kabla ya kwenda Dubai.
Huyo Muheshimiwa aaminiki tangu kelele za bandari zilipoanza ndio anaongea leo je hizi kelele zisingekuwepo angeongea hayo aliyoongea? Au anatuletea mambo ya siasa ya kupima upepo na kutaka umaarufu?

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Ile mzazi ushakula kishika uchumba na mahari ya watu halafu bint yako hataki kuolewa
 
WABUNGE 30 walipelekwa kwa ndege binafis na kupokelewa as VVIP, wamefanya shopping kwa ajili yao na familia zao pamoja na posho ndefu kwa gharama za DP WORLD , wamerudi na kushawishi wenzao ila bado WASOMI wa kitanzania na wasio soma wakaona MANGONGO CONTRACT IS LAANA, wakagoma:

Wakatafutwa influencer, wa kwanza alikuwa DIAMOND PLATINUMZ na ZUCHU pamoja na OMMY DIMPOZ na SHEKHRAN wakagoma maana wangegawa mashabiki zao, madalali wakaona isiwe shida wakawanunua MAULIVI wa -KIKANGA na ZE-MBWELEE, wameshadalalia na shopping washafanya sasa wanarudi na kioo nyumbani baada ya kuacha almasi kwa mkoloni.
 
Rudi kwenye hoja yako ya awali niliyoikwoti Kisha linganisha na jibu lako hili☝️☝️

Anyway, acha ni - recall. Nilikuuliza hivi

"Kama ni ishu ya kwenda kuona na kujifunza ili waje washauri serikali kabla ya kuingia makubaliano/mkataba, hiyo mantiki ya lengo la safari hiyo ya wabunge iko wapi maana MoU na mkataba wenyewe ulishasainiwa tayari na Rais na watu wake tangu mwaka 2022 na mkataba umeingia bungeni juzi ukiwa signed already?

Umenielewa?

Kama umenielewa, sasa maswali yangu kwako wewe na kwa kadiri ya akili na ufahamu wako, ni haya;

1. Hiyo wewe unaipa tafsiri gani?

2. Bado unadhani tu kuwa hiyo ilikuwa ni safari ya kawaida tu kwa wabunge kwa kuwa ni kawaida yao kusafiri mara kwa mara kwa shughuli za kibunge siyo?

3. Bado huoni tu kuwa ni safari ya kirushwa rushwa waliyopewa ili waje kutumika ku - rubber stamp maamuzi haya ya hovyo na mabaya ya Rais Samia Suluhu Hassan na wenzake dhidi ya Tanganyika na rasrimali zake ambazo ni urithi wao halali walizopewa na Mungu kupitia hiki kinachoitwa mkataba??

4. Je, unajua kuwa hata wabunge wasio wa kamati husika akiwemo huyu Aida Khenani nao walipelekwa? Unadhani ni kwanini?

MWISHO;

Kama bado huelewi tu, basi utabaki hivyo hivyo na maneno yako ya "si ni kawaida tu kwa wabunge kusafiri nje" bila kutumia kichwa na akili yako sawasawa kufikiria nje ya box..

To cut it short, mimi nakuambia safari zingine za wabunge nje ya nchi na hata za ndani ya nchi huwa si za kawaida bali huwa kama rushwa ya ushawishi kuwalainisha wapitishe jambo fulani la serikali ikiwemo hii tunayojadili. Narudia tena wakati mwingine tuwe tunatumia akili vyema kufikiri nje ya boksi kudadisi mambo..!!...
Hii sio hoja ila.ni miongoni mwa vioja , hivyo kutoa wanajumuia kwenue hoja kuu
 
Hii sio hoja ila.ni miongoni mwa vioja , hivyo kutoa wanajumuia kwenue hoja kuu
Kwa ufahamu wako, "hoja kuu" uijuayo wewe ni ipi kwani?

Nimekusoma, nimeona kuwa, umeandika kana kwamba umekurupushwa toka usingizini na bila kujua kinachojadiliwa, ukafyatua chochote kilicho kuja kwenye ufahamu wako!

Hata hivyo, nawe asante kwa kutia mguu kwenye mjadala kwa staili hii..!
 
Anyway, acha ni - recall. Nilikuuliza hivi

"Kama ni ishu ya kwenda kuona na kujifunza ili waje washauri serikali kabla ya kuingia makubaliano/mkataba, hiyo mantiki ya lengo la safari hiyo ya wabunge iko wapi maana MoU na mkataba wenyewe ulishasainiwa tayari na Rais na watu wake tangu mwaka 2022 na mkataba umeingia bungeni juzi ukiwa signed already?

Umenielewa?
huo mkataba umesainiwa lini? au unazungumzia makubaliano?
 
Kama hayo anayoyasema ni kweli na sikutaka umaarufu kwa nini akuyasemea bungeni na nafasi ya kuyasema aliipata?

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
Na kwani kuyasema huku nje kuna ubaya gani? Au amevunja sheria gani kiasi cha wewe kuhoji na kupaniki?

By the way, huku nje kwa umma ndo kwenyewe maana hili ndilo bunge kuu la wananchi na halina figisu figisu za ki - CCM na za akina Tulia Ackson na hakuna cha kupewa dakika 5 au 10 za kuchangia...

Huku kwenye bunge la wananchi unamwaga Kila kitu hadharani na Kwa muda utakao wewe..

Kwa hiyo isikupe shida. Aida Khenani yuko sahihi. Jamii imemwelewa vyema na ujumbe umeeleweka kwa usahihi kwa umma wote isipokuwa labda wewe wa ukae..
 
huo mkataba umesainiwa lini? au unazungumzia makubaliano?
Kumbe unajadili kitu usichokielewa bitimkongwe?

Na kwa kadiri ya ufahamu wako wewe, unadhani ni ipi tofauti ya "mkataba" na "makubaliano?"..

Ukijibu vyema swali hili, uje tuendeele na majadiliano...
 
Kuwa na genge ndani ya Serikali linalofanya uhaini sio jambo la kushabikia, hata mwalimu Nyerere kuna watu walikua wanamfanyia uhaini mpaka ikafikia muda akawaweka detention .
Kama ndiyo iko hivi kwa suala hili, Rais Samia Suluhu Hassan anasubiri nini kuwa - detain hao wenzake?

Na unadhani Rais Samia aweza kuji - detain mwenyewe? Yeye si ndiye mwanzo na mwisho wa ishu hii yote? Nani alisaini MoU? Nani alisaini IGA? Hakusoma kabla ya kusaini?

How come huu upuuzi uwe ni fault ya vyama vilivyo nje ya serikali a.k.a vyama vya upinzani?

Mimi nasema, HAPANA. Vyama vya upinzani viendelee kupiga kelele sana Kwa hili. Vitumie udhaifu huu wa Serikali na chama kinachoongoza Serikali kuwaambia hawafai kubeba dhamana hii.

Yaani lazima isemwe kuwa serikali yote kuanzia Rais Samia na chama chake ni wahaini..!!

Nani atam - detain mwenzake???
Pili, kuwa mpinzani sio kushabikia serikali iporomoke, bora ushabikie chama kiporomoke kwa maana ya CCM kama wewe ni CHADEMA,
Chama kinachoongoza serikali kikiporomoka na serikali yake huporomoka vivyo hivyo na siku zote hii huwa ni fursa na furaha kwa vyama vilivyo nje ya serikali. Na ndiyo siasa yenyewe..!!
lakini Serikali ikiporomoka ama isipoelewana kwa sababu ya uchu wa madaraka wa watu flani , wanaoumia ni ndugu zetu wanaotegemea kutibiwa kwa mkono wa serikali, kusoma kwa mkono wa serikali.
Obviously ndivyo ilivyo, nakubaliana na wewe kwenye hili. Lakini, kumbuka tena kuwa, kuanguka kwa chama kilicho madarakani tena kilicho kizee (kilichokaa muda mrefu madarakani) kama CCM, basi itakuwa ni kwa neema ya Mungu pekee iwapo kitang'oka au kung'olewa madarakani bila kuacha madhara ya aina fulani kwa nchi...
Vyama vya upinzani hasa CHADEMA kitendo cha kuwa tayari cheza ngoma yeyote ile ilimradi inadhoofisha nchi sio uzalendo.
Aisee likely wewe huijui siasa!!

Wewe unataka CHADEMA wafanye nini? Waanze awamu nyingine ya "maridhiano" ili kiwapatanishe CCM wanaosalitiana wao kwa wao ndani ya chama na serikali yao?

Bro, mimi sio CHADEMA wala ACT Wala chama chochote kingine ikiwemo CCM. Lakini napenda tu ufahamu pia naichukia na siipendi CCM kama nisivyompenda shetani. Natamani hata leo kiondoke/kife na kutoweka kabisa..

Mr poisonous, kwangu mimi it doesn't matter CCM itakufa na kutowekaje ktk uso wa Tanganyika. What matters ni kuwa iondoke bila kujali itaondokaje iwe ni kwa kifo cha kawaida ghafla au kuvurushwa Kwa nguvu..

Kumbuka hili: Ili uvune mahindi mengi, basi lazima upande punje ya hindi moja, ioze chini ya ardhi/udongo, na kisha iote na kumea na kuzaa mahindi mengine mengi..

Huwezi kupata mazao usipokubali kufa kwanza ili baadae ufufuke kama mhindi, umee na kutoa mazao...!!

Tukubali tu CCM ife zake. Tunajua fika kuwa "Probably" wataondoka huku wakiacha makovu na maumivu kwa nchi na watu Kwa sababu ya mizizi waliyokwisha ichimbia. Lakini ni heri hiyo, maana nchi hii itazaliwa upya Kwa mara ya pili ikiwa safi bila CCM...!
 
Aida kasema neno muhimu sana ,kuwa taharuki hii inatokana na Hofu tuliyonayo kutokana na uzoefu wa mikataba kadhaa ambayo tumeingi huko nyuma ambayo Watanzania tumepigwa na imeonekana haina maslahi kwa Taifa.

Hoja hi ni ya msingi.sana.

Na m,zee mboe yeye katahadharisha kuwa hili suala ni la Kimuungano, kwa nini bandari za Zanzibar hazimo?
Ukweli ni kuwa Waziri alijibu kuwa Mkataba huu unaihusu bandari ya Dar es salaam tuu.

Ila ikonekana kuna ufanisi tunaweza kungia kwenye mikataba ya nyongeza huko mbeleni .

Ama hili la Kimuungano kuwa Bandari ni za Muungano kweli limo ndani a Katiba, ya 1977. lakini ukweli ni kuwa katiba hii haitumiki tena tanzania, Serikali ya CCM inatuma Akili na uzoefu tuu.
Tazama hapo chini:
_________
NYONGEZA YA KWANZA
_________
(Imetajwa katika ibara ya 4)
Mambo ya Muungano
1. Katiba ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
2. Mambo ya Nchi za Nje.
3. Ulinzi na Usalama.
4. Polisi.
5. Mamlaka juu ya mambo yanayohusika na hali ya hatari.
6. Uraia.
7. Uhamiaji.
8. Mikopo na baiashara ya Nchi za Nje.
9. Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
10.Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika,
ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa
nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha.

11.Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na
simu.

12.Mambo yote yanayohusika na sarafu na fedha kwa ajili ya
malipo yote halali (pamoja na noti); mabenki (pamoja
mabenki ya kuweka akiba) na shughuli zote za mabenki;
fedha za kigeni na usimamizi juu ya mambo yanayohusika
na fedha za kigeni.
13.Leseni ya viwanda na takwimu.
14.Elimu ya juu.
15.Maliasili ya mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa ya
motokaa na mafuata ya aina ya petroli na aina nyinginezo za
mafuta au bidhaa, na gesi asilia.

16.Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania na mambo yote
yanayohusika na kazi za Baraza hilo.

17.Usafiri na usafirishaji wa anga.
18.Utafiti.
19.Utafiti wa hali ya hewa.
20.Takwimu.
21.Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano.
22.Uandikishaji wa Vyama vya siasa na Mambo mengine
yanayohusiana navyo.

Article nilizo tia Rangi zina utata mkubwa , CCM wenyewe upande wa ZNZ na Tanganyika hawakubaliani ,
Zanzibar wan baraza lao la Mitiani,
Zanzibar wanakusanya kodi kwa idara yao inayoitwa ZRB(zamani) /(sasa ZRA)
zanzibar wana simamia Bandari yao wenyewe (ZPA) iko chini ya SMZ
Zanzibar inapata shida sana kukopa , ndo maana inataka itolewe kwenye Muungano suala la Mikopo.
Zanzibar imekwama kwa kushindwa kutowa leseni za Viwanda, Kila kiwanda kinapoanzishwa Zanzibar Tanganyika inadai Haki ya Kutoa leseni na Kupata Mrejesho wa Kodi, Kiwanda kinakufa au kufungwa.


Mh.Mbowe hapa ndipo alipolenga na kuonesha Mgogoro tulionao kitaifa.


Ama Upande wa Jamuhuri ya Muungano imeshindwa hadi leo Kufungua Account Ya pamoja ya Muungano ambayo imo ndani ya Katiba.Imeshindwa kutekelezwa na kuisababaishia Zanzibar kukosa stahiki yake katika Mgao wa Muungano.
Hili likoUpande wa Tanganyika nalolimekwama.

Tanganyika lazima Irudi na Zanzibar ipewe mamlaka kamili.
Muungano wa ajabu sana huu
 
Hilo limama linakwendaje Dubai bila kujua limekwenda kufanya nini? Upuuzi mtupu.🤣🤣
 
Nami nikuulize aliyepeleka majina ya COVID-19 bungeni ni nani?

Mwanasheria mkuu wa Sirikali na Ofisi ya mwanasheria mkuu wa Sirikali ni vitu viwili tofauti.
Endapo kama hii ni kweli basi Mkataba huu ni BATILI (Null and Void ab initio) kwa sababu Sheria za nchi hii zinataka Mikataba yote ya Kimataifa ambayo Serikali inaingia, ni lazima ipitiwe kwanza ( yaani ifanyiwe Vetting) na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kabla ya kusainiwa.
Aidha, hata mikataba ya ndani ya nchi yenye thamani ya fedha kuanzia Tshs 1 bilioni na zaidi, lazima na yenyewe ipitie kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili ifanyiwe Vetting kabla ya kusainiwa.
Shehe, umewahi kupelekwa Dubayi weye.
Vipi, waonaje tufanye mpango upelekwe Dubayi? Usihofu gharama, yaani weye wapelekwa buure kabisa.
 
siwezi kujibu maana mimi siyo mwanasheria. Case closed
Afadhali umekuwa mkweli kwa nafsi yako mwenyewe...

Umekiri kuwa hujui kwa sababu wewe si mwanasheria..

Mimi na wewe, tumefunga mjadala. Endelea kuwasoma wengine na kujifunza toka kwao na mwisho utaelewa tu..

Case closed 🔒🔒🔒
 
Shehe, umewahi kupelekwa Dubayi weye.
Vipi, waonaje tufanye mpango upelekwe Dubayi? Usihofu gharama, yaani weye wapelekwa buure kabisa.
Yaani kupelekwa Dubai ndio sababu ya kuwasaliti Watanzania wenzako kwa kuwauza kwa Waarabu?? Huu ni UHAINI kabisa. Uzalendo kwa nchi yako ya kuzaliwa ni lazima iwe kipaumbele namba moja katika maisha ya binadamu yoyote yule hapa duniani.
 
Sipingi huja ya mbunge lkn Kuna shida nyingine naiona kwa sisi wa bongo.
Hivi mbunge atoke Tanzania hadi Dubai hajui alienda kufanya nn? Hatupo serious kiasi hiki kweli?

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app

Mkuu, inawezekana kabisa hata kama mnaambiwa sababu za kusafiri lakini hadidu za rejea na mwandishi wa ripoti ni mwenyekiti wa kamati. Mkifika kule mnafanya ziara kwenye bandari na kisha mnarejea.

Usichokumbuka ni kuwa sio ziara hii iliyokuwa chanzo za makubaliano. Makubaliano ya mkataba huu hakuna anayeweza kusema yalifanywa lini na kwa ushauri wa nani serikalini! Bunge lililetewa kuupa nguvu kisheria! Ulishakuwepo!!
 
Mkuu, inawezekana kabisa hata kama mnaambiwa sababu za kusafiri lakini hadidu za rejea na mwandishi wa ripoti ni mwenyekiti wa kamati. Mkifika kule mnafanya ziara kwenye bandari na kisha mnarejea.

Usichokumbuka ni kuwa sio ziara hii iliyokuwa chanzo za makubaliano. Makubaliano ya mkataba huu hakuna anayeweza kusema yalifanywa lini na kwa ushauri wa nani serikalini! Bunge lililetewa kuupa nguvu kisheria! Ulishakuwepo!!
Nakuelewa Sana shida ni kauli kuwa sikujua tunaenda kufanya nn

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom