Mkataba wa Lugumi wapelekwa kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama!

Mkataba wa Lugumi wapelekwa kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama!

UVCCM TOENI MSIMAMO WENU KUHUSU LUGUMI ISSUE HUWA SIWASIKII KWENYE MAMBO YA MSINGI YANAYOPELEKEA TAIFA KUPATA HASARA MFANO HILI JAMBO LENYE HARUFU YA KIFISADI.
MM MSIPOTOA MSIMAMO WENU KWENYE HILI MATAMKO YENU MENGINE NITAKUWA NAWAPUUZA. ESCROW NAYO MLIKUWA KIMYA KAMA HAMJASIKIA.
 
Alafu huyu Adadi Rajabu si ndie alikuwa DCI wa Jeshi la Polisi?
Sio hivyo tu itakuwaje kamati moja ianzishe jambo na kuagiza mkataba then hawa waupeleke ktk kamati nyingine ?
Huyu na Mwema si wote wameoa kumoja or something ?? Na anayetajwa tajwa aka tuhumiwa ni waziri wa wizara hiyo hiyo..?
Jana IGP na Katibu Mkuu walikuwa wanarushiana mpira nani anatakiwa atoe mkataba !! JPM ana kazi kubwa sana !
 
Kama ni kweli huo mkataba umepelekwa kamati nyingine tofauti na kamati iliyo uhitaji nimeamini nchi imeshindikana kwa madeal, Magu tutamwombea kama anavyoomba tumwombee lkn kwa style hii hayo maombi yataishia Ikulu mbinguni hayafiki.
 
Hakuna cha kujificha mbele ya Rais na serikali ya magufuli kwa ujumla tusubiri kila kitu kitakuwa ok.
 
Hapa ndio PA kuangalia uadilifu Wa viongozi Wa ccm mi nahamini ccm ni Ile Ile
 
Hii nchi imeibiwa asee! Keleuuuuwi....ivi tulikua vitani kwaivyo uongozi haukuwepo ama tulikuwa na likizo ndefu ya serikali!!! Hii ni zaidi ya ziada ya aibu kwa serikali iliyopita. Kwakweli imetosha tunataka jela rasmi yenye kazi nzito kwaajili ya mafisadi! Wamekuwa wengi sana,ishu za kufagia hatutaki kuskia tena
 
Nafurahishwa sana na maneno ya hawa wakuu wetu. Ati hatutamlinda mtu yeyote. Kusema, hakunyimwi mtu jamani ila, tangu lini mtoto akakate fimbo mwenyewe halafu alale chini ajichape mwenyewe?? Adadi ndiye alikuwa DCI wakati hilo zigo linaliwa. Haiwezekani kuwa hakuhusika kwa hili au lile kwenye huo mkataba. Sasa, ndiye tumemkabidhi uchunguzi kamili kwani yeye ndiye shushushu no 1.
Kama faili halitapotea, kuna kurasa kupotea
 
wale watoto wa nyerere walikuwa " WASHAMBA "
Hivi ushamba wao ni upi? walizaliwa shamba, au wamekulia shamba au wanaishi shamba au lipi? Mbona mimi nilisoma na mtoto wake wa kwanza pale H.H.Agah Khan secondary school Dsm kwani pale ni shamba?
 
Hivi ushamba wao ni upi? walizaliwa shamba, au wamekulia shamba au wanaishi shamba au lipi? Mbona mimi nilisoma na mtoto wake wa kwanza pale H.H.Agah Khan secondary school Dsm kwani pale ni shamba?
mkuu hebu soma vizuri ile washamba yangu iko kwenye mabano , unajua hata kwenye maofisi ya umma , kama huibi au hupigi michongo ya kupata hela unaitwa fala .
 
Back
Top Bottom