Mkataba wa Lugumi wapelekwa kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama!

Mkataba wa Lugumi wapelekwa kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama!

Kama ni kweli huo mkataba umepelekwa kamati nyingine tofauti na kamati iliyo uhitaji nimeamini nchi imeshindikana kwa madeal, Magu tutamwombea kama anavyoomba tumwombee lkn kwa style hii hayo maombi yataishia Ikulu mbinguni hayafiki.
au kamati ya mashirika ya umma imeingilia kazi siyo yake?,maana polisi sio shirika la umma.
 
Hivi ni kwanini huyo mtoto wa rais mstaafu anahusishwa na mambo mengi ya kashfa kuliko kusifiwa kwa kutenda mambo mema?hivi marehemu jk nyerere mbona alikuwa na watoto lkn hadi leo hii hatujasikia mambo ya maovu kama ya huyu?
Huo ndio mchezo wa ufipa,wamemchafua lowasa kumbe walikua wanajichafulia wenyewe!
 
Uncle siyo issue, mawe 3 mwepesi mno, jaribu la magu ni yule mtoto wa mfalme wa msoga ni kisiki, magu hapawezi pale.
Kama nikweli hawa watu wanaorukaruka humu kama maharage yanayochemka..kuwa Magufuli kiboko ya majipu....!!! Tangu lini shetani akamtoa shetani ..mwenzie
 
baada ya wiki moja utasikia , " mambo ya kijeshi hayatakiwi kujadiliwa hadharani , yatahatarisha usalama wa nchi " poor Tanzania !
Kwa wale ambao wamejiunga na JF majuzi, napenda kuwafahamisha kuwa mambo ya Meremeta yalizimwa kwa staili hii hii...kwamba kampuni hiyo iliyoanzishwa kifisadi, kwa kuwa ulidaiwa ni mradi uliolihusisha JWTZ, mjadala ukafungwa.

Kwa ufahamisho zaidi ni kwamba kulikuwepo na wakati hata mambo ya CCM yalikuwa marufuku kujadiliwa na Bunge kwa sababu eti Chama ndicho kilishika hatamu na hata Bunge, pamoja na kuwakilisha wananchi wote, lilikuwa chombo cha CCM!

Kwa ufahamisho zaidi ni kwamba mali zote zilizokuwa mikononi mwa wananchi pamoja na mali zote zilizokuwa mikononi mwa serikali kwa niaba ya wananchi pamoja na vyombo vyote vya dola, mmiliki mkuu kilikuwa ni Chama cha Mapinduzi!

Adui mkubwa wa taifa hili ni CCM...!
 
Hii kali aliyeomba mkataba amenyimwa asiyeomba huo mkataba amepelekewa. Kwa muda wa wiki nzima Bwana Hilary Aeshy alikuwa anahangaika walau autie machoni huo mkataba lakini wapi!
Je unafahamu mke mdogo wa IGP mstaafu ana mahusiano yepi na mwenyekiti wa kamati ya bunge ya ulinzi na usalama? Hii ndio tanzania
 
Kwa wale ambao wamejiunga na JF majuzi, napenda kuwafahamisha kuwa mambo ya Meremeta yalizimwa kwa staili hii hii...kwamba kampuni hiyo iliyoanzishwa kifisadi, kwa kuwa ulidaiwa ni mradi uliolihusisha JWTZ, mjadala ukafungwa.

Kwa ufahamisho zaidi ni kwamba kulikuwepo na wakati hata mambo ya CCM yalikuwa marufuku kujadiliwa na Bunge kwa sababu eti Chama ndicho kilishika hatamu na hata Bunge, pamoja na kuwakilisha wananchi wote, lilikuwa chombo cha CCM!

Kwa ufahamisho zaidi ni kwamba mali zote zilizokuwa mikononi mwa wananchi pamoja na mali zote zilizokuwa mikononi mwa serikali kwa niaba ya wananchi pamoja na vyombo vyote vya dola, mmiliki mkuu kilikuwa ni Chama cha Mapinduzi!

Adui mkubwa wa taifa hili ni CCM...!
Mungu akulinde sana mkuu .
 
Ni kweli kabisa alikuwa DCI ila ukiuliza kwanini kamati husika imepigwa chenga uta ambiwa ni bunge lile lile,ila mh! sijui naona kama iko namna,tusubiri hapa tuta yasikia.
Namna iliyopo balozi na igp mstaafu ni mtu na shemejie
 
Back
Top Bottom