Mkataba wa Lugumi wapelekwa kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama!

Mkataba wa Lugumi wapelekwa kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama!

UVCCM TOENI MSIMAMO WENU KUHUSU LUGUMI ISSUE HUWA SIWASIKII KWENYE MAMBO YA MSINGI YANAYOPELEKEA TAIFA KUPATA HASARA MFANO HILI JAMBO
Suala hilo limeshafikishwa mahali husika, hatutatoa tamko kwani mambo ya kijeshi huwa hayajadiliwi hadharani, ni hatari kwa usalama wa nchi. Tuna kazi kubwa ya kujenga nchi na mambo ni mengi ya kuhusu maendeleo, jambo moja tu lisisababishe tuache kazi kubwa ya kutumbua majipu. PAC tunawapongeza kwa kazi nzuri, ila kwa sasa waendelee na hesabu za mashirika mengine kwani hapo watahatarisha usalama wa nchi.
 
Hii ndio Tanzania.

Hii habari imeandikwa na gazeti la mtanzania la leo na Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Bunge, Balozi Adadi Rajabu amethibitisha mkataba huo kati ya Jeshi la Polisi na Kampuni ya Lugumi Enterprises kuwasilishwa mbele ya Kamati yake siku ya jana.

===============

Njama nzito kuficha mkataba wa Lugumi

MKATABA tata wa Kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd inayomilikiwa na mfanyabiashara Said Lugumi, umezidi kuchukua sura mpya baada ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), kushindwa kuendelea na sakata hilo kutokana na kuhamishiwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.

Hatua hiyo inatokana na utata uliogubika mkataba huo ambao unawahusisha vigogo kadhaa wa Jeshi la Polisi pamoja na baadhi ya watendaji wa Serikali ya Rais Dk. John Magufuli, huku ikidaiwa kuwa huenda ikawa njia ya ‘kulindwa’.

Wiki iliyopita PAC ilipokutana na jeshi hilo kupitia taarifa ya hesabu zao za mwaka 2013/14 zilizokaguliwa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ilibainika kuwa mwaka 2011 liliingia mkataba na kampuni hiyo kwa ajili ya kufunga mashine za kuchukua alama za vidole katika vituo vya polisi 108 nchi nzima kwa gharama ya Sh bilioni 37.

Lakini hadi sasa mashine hizo zimefungwa katika vituo 14 pekee na kampuni hiyo kulipwa Sh bilioni 34 ambazo ni sawa na asilimia 99 ya fedha za makubaliano ya mkataba.

Kutokana na hali hiyo, PAC ambayo ilibaini kuwapo viashiria vya ufisadi katika tenda hiyo, iliwaagiza watendaji wa jeshi hilo kuwasilisha taarifa za mkataba huo pamoja na vielelezo vyake ili wajumbe waweze kuupitia pamoja na kutoa maagizo.

Chanzo cha kuaminika kiliambia MTANZANIA kuwa katika sehemu ya mkataba huo kati ya Jeshi la Polisi na Lugumi, imebainika kampuni hiyo kufanya mafunzo kwa watu watano ambayo wametumia Sh bilioni 5, huku mshauri mwekelezi akilipwa Sh bilioni 46 nje ya fedha zilizopo kwenye mkataba.

Hatua ya mkataba huo kupelekwa mbele ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, inadaiwa kuwa njia ya kutaka kuwalinda baadhi ya vigogo ambao wanatajwa kuhusika na kashfa hiyo ambayo imelitia doa Jeshi la Polisi nchini.

“Hapa kuna kulindana tu, hakuna namna yoyote. Kama uchafu umebainika mbele ya Kamati ya PAC inakuwaje wengine wanadaka kitu ambacho hakikuanza kwao?

“Kuna kila dalili ya wingu na shaka, ila ukweli utajulikana tu, haiwezekani watu wanatumia fedha za walipakodi vibaya halafu inapokuja wanataka kushughulikiwa wanatafuta kivuli cha kujifichia,” kilisema chanzo chetu.

Mkataba huo uliibuliwa na PAC wiki iliyopita ambapo watendaji wa Jeshi la Polisi walishindwa kutoa maelezo ya kutosha ndipo ikawataka kuwasilisha taarifa juzi.

Pamoja na kutakiwa kufanya hivyo, hadi kufikia jana saa 10 jioni Makamu Mwenyekiti wa PAC, Aeshi Hilaly, alisema kuwa kamati yao haijapokea taarifa yoyote kuhusu Kampuni ya Lugumi hivyo wameliandika barua Jeshi la Polisi liwasilishe mkataba huo ndani ya siku tatu.

Alisema barua hiyo wamemuomba Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilillah, ili aweze kuwaandikia Polisi ili wawasilishe mkataba huo kwa mujibu wa utaratibu kama kamati ilivyoagiza.

“Hadi muda huu ninapozungumza nawe sijapata taarifa yoyote, kwa hali hiyo tumelazimika kumwandikia barua Katibu wa Bunge ili awaandikie barua polisi walete mkabata huo ndani ya siku tatu kutoka leo (jana) kama walivyotakiwa na kamati yetu,” alisema Hilaly.

BALOZI ADADI

Akizungumza na MTANZANIA jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu, alithibitisha mkataba huo kuwasilishwa mbele ya kamati yake.

“Mimi kama mwenyekiti wa kamati ninapenda kukiri kwamba tumepokea mkataba kati ya Jeshi la Polisi na Kampuni ya Lugumi na tutaufanyia kazi kwa kina.

“Tunahitaji kuona kama kuna wizara zilizohusika na mkataba huu na kama tutaukuta ni mbaya, tutatoa taarifa kwa umma. Kikubwa tunawaomba Watanzania wawe watulivu, hatuko kwa ajili ya kumlinda mtu wala kikundi cha watu, tunasimamia masilahi ya Watanzania wote,” alisema Balozi Adadi.

RIDHIWANI AKANA

Taarifa za mkataba huo zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii zikiwahusisha baadhi ya vigogo wa Serikali akiwamo Waziri wa Serikali ya Rais Magufuli pamoja na kumtaja Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete (CCM).

Hata hivyo, Ridhiwani alivunja ukimya na kukanusha taarifa hizo zilizodai yeye ni mmoja wa wamiliki wa Kampuni ya Lugumi pamoja na Said Lugumi na aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi, Said Mwema.

Akizungumza na gazeti moja la kila siku (Si MTANZANIA), Ridhiwani ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, alisema hahusiki na Lugumi ingawa wana urafiki wa kawaida na mmiliki wa kampuni hiyo.

“Kwanza kabisa mimi si mmoja wa wamiliki wa kampuni hiyo, hilo ni jambo la msingi kabisa watu waelewe, na sijawahi kufanya biashara yoyote na Lugumi. Said Lugumi ambaye ni mmiliki wa kampuni hiyo tunafahamiana naye na ni rafiki yangu,” alisema Ridhiwani.

Alisisitiza kuwa hana uhusiano wa kibiashara na mtu huyo na kwamba hafahamu ni kwanini amehusishwa na Kampuni ya Lugumi.

“Hapa ni watu tu wanaamua kuingiza tu maneno yao, haya maghorofa ninayotajwa kumiliki Dar es Salaam hata sijawahi kutembelea ujenzi wake, wameamua kuniingiza, Lugumi nafahamiana naye binafsi tu lakini wananiingiza,” alisema Ridhiwani.

Chanzo: Mtanzania
hayaaaa kumekucha... hapa sasa ndo nataka nione FUNDI WA MAJIPU AKITUMBUA HILI JIPU UCHUNGU... maana yaonyesha uchungu wa hili jipu wakati linapasuliwa naona hata mpasuaji nae atakuwa anaskia uchungu zaidi lkn afanyeje inabidi tu lipasuliwe litumbuliwe ili maumivu yaishe.
akishindwa kulipasua sasa itabidi dharula itumike atumbuliwe yeye mtumbuaji.
 
unajua mimi kinachonikera sana kwenye serikali ya magufuli ni usanii.Kama kweli magufuli ni mwanaume,akamate madili yote ya kikwete na wengine waliosabisha hii nchi hasara kubwa.
Mimi naamini magufuli anafanya uonevu kwa watu wadogo wadogo,na badala ya kujenga kujituma,uadilifu na patriotism.Lakni tumbua tumbua hii,inawahusu watu wadogo sana,tena wale kutoka mikoa ya kaskazni zaidi na sio sehemu nyingine zozote.
Magufuli,hii vita unayotaka kuanzisha hutaiweza.Ukileta ubaguzi wa ukabila na ukanda hutaifikisha nchi popote.Be a leader and not a commander.Be a change but not a pervert.
tukiacha unafiki mkubwa alionao magufuli,mimi nasupport kwa kiasi kikubwa uwajibikaji na maadili katika sekta za umma,lazima tuwe na uwajibikaji la sivyo hatutafika.
 
....""IPO HAJA YA KUIPITIA MIKATABA YOTE YA JESHI HILO""
.....Inashangaza sana pale chombo cha Bunge kinapodharauliwa!....
 
unajua mimi kinachonikera sana kwenye serikali ya magufuli ni usanii.Kama kweli magufuli ni mwanaume,akamate madili yote ya kikwete na wengine waliosabisha hii nchi hasara kubwa.
Mimi naamini magufuli anafanya uonevu kwa watu wadogo wadogo,na badala ya kujenga kujituma,uadilifu na patriotism.Lakni tumbua tumbua hii,inawahusu watu wadogo sana,tena wale kutoka mikoa ya kaskazni zaidi na sio sehemu nyingine zozote.
Magufuli,hii vita unayotaka kuanzisha hutaiweza.Ukileta ubaguzi wa ukabila na ukanda hutaifikisha nchi popote.Be a leader and not a commander.Be a change but not a pervert.

tukiacha unafiki mkubwa alionao magufuli,mimi nasupport kwa kiasi kikubwa uwajibikaji na maadili katika sekta za umma,lazima tuwe na uwajibikaji la sivyo hatutafika.
***
Are you sure on that?
 
unajua mimi kinachonikera sana kwenye serikali ya magufuli ni usanii.Kama kweli magufuli ni mwanaume,akamate madili yote ya kikwete na wengine waliosabisha hii nchi hasara kubwa.
Mimi naamini magufuli anafanya uonevu kwa watu wadogo wadogo,na badala ya kujenga kujituma,uadilifu na patriotism.Lakni tumbua tumbua hii,inawahusu watu wadogo sana,tena wale kutoka mikoa ya kaskazni zaidi na sio sehemu nyingine zozote.
Magufuli,hii vita unayotaka kuanzisha hutaiweza.Ukileta ubaguzi wa ukabila na ukanda hutaifikisha nchi popote.Be a leader and not a commander.Be a change but not a pervert.

tukiacha unafiki mkubwa alionao magufuli,mimi nasupport kwa kiasi kikubwa uwajibikaji na maadili katika sekta za umma,lazima tuwe na uwajibikaji la sivyo hatutafika.
***
Are you sure on that?
 
Hoja yako ipo wapi sasa? Kwani ni makosa kwa DCI kuwa mbunge?
Hapana siyo makosa kuwa mbunge ila ni kosa kubwa la kiufundi kushughulikia ufisadi unaomhusu yeye bila kutangaza maslahi. Ajitanzaze kwanza ufisadi unaoletwa mezani kwake unamhusu hata yeye kwa namna moja au nyingine,kwamba wakati yakitokea hayo yeye alikua ofisini kama DCI.
 
Hakuna cha kujificha mbele ya Rais na serikali ya magufuli kwa ujumla tusubiri kila kitu kitakuwa ok.
Serikali zimejengeka kwenye msingi wa unyonyaji, uonevu, upendeleo na hata mauaji kwa kutumia kivuli cha usalama wa taifa.
Jambo hili lilikuwepo,lipo na litaendelea kuwepo.
Mabadiko hufanyika tu pale baadhi ya watawaliwa wanapochukua nafasi za watawala kwa kupitia sanduku la kura au mapinduzi ya nguvu.
Hata hivyo, hali hii haiondoi tabia ya asili ya serikali.
Itakuwa ni kujidanganya kufikiria kuwa serikali ya Magufuli ni ya kipekee itakayoweka kila kitu wazi.
 
Anayo hoja, nwaka huo 2011 mkataba ukiwa unaandikwa jee Adadi alikuwa kesha staafu u DCI?
Watu wanaandika mambo wasiyoyajua ili mradi tu tuwaone humu JF. Adadi Rajabu aliacha kuwa DCI miaka imepita 10 iliyopita na kuwa Balozi nchini Zimbabwe kuanzia mwaka 2008. Baada ya Adadi kustaafu msaidizi wake akachukua nafasi naye anaitwa Robert Manumba ambaye alikua mkurugenzi mpaka mwaka 2013 alipostaafu baaada ya kutimiza miaka 60. Sasa sielewi kitu gani kinamhusisha balozi Adadi na Lugumi wakati yeye alikua balozi huko Zimbabwe mpaka mwaka jana July. Watu wanatakiwa kufanya research kabla ya kuandika utumbo vinginevyo mtaishia kupelekwa katika kanisa la Mtakatifu Kisutu halafu mseme mmeonewa.
 
Hivi ukawa wako wapi.. John mnyika kimya katibu mkuu wa chadema kimya
 
mkuu hebu soma vizuri ile washamba yangu iko kwenye mabano , unajua hata kwenye maofisi ya umma , kama huibi au hupigi michongo ya kupata hela unaitwa fala .
Ujue hapa ni wachache sana wenye kuelewa haya mambo, vitu kama nukta, kiulizo, alama za funga na fungua semi, alama ya mshangao na nyinginezo wengi hawajui zina matumizi gani.
Lile neno "washamba" kwa namna ulivyoliandika watu hawakupaswa kukutolea povu hata kidogo. Nadhani ubadirishe namna ya kucomment kwa kuzingatia uelewa wa watu.
 
Watu wanaandika mambo wasiyoyajua ili mradi tu tuwaone humu JF. Adadi Rajabu aliacha kuwa DCI miaka imepita 10 iliyopita na kuwa Balozi nchini Zimbabwe kuanzia mwaka 2008. Baada ya Adadi kustaafu msaidizi wake akachukua nafasi naye anaitwa Robert Manumba ambaye alikua mkurugenzi mpaka mwaka 2013 alipostaafu baaada ya kutimiza miaka 60. Sasa sielewi kitu gani kinamhusisha balozi Adadi na Lugumi wakati yeye alikua balozi huko Zimbabwe mpaka mwaka jana July. Watu wanatakiwa kufanya research kabla ya kuandika utumbo vinginevyo mtaishia kupelekwa katika kanisa la Mtakatifu Kisutu halafu mseme mmeonewa.
huyu jamaa anayeitwa chakaza ameuliza kama adadi alikwisha staafu huo mwaka 2011 , kwa hiyo badala ya kumtisha na mambo ya kisutu ulipaswa tu kujibu kama alivyouliza .
 
Adadi Rajabu ndiye mwenyekiti? Hapo tumeliwa
Huyu Adadi Rajabu akiwa DCI ndio waliokamata ule Mtambo wa kutengeneza Madawa ya Kulevya kwenye Nyumba moja, lakini mpaka leo hakuna ajuaye hatma ya ule mtambo na wahusika wake.
 
Hii ndio Tanzania.

Hii habari imeandikwa na gazeti la mtanzania la leo na Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Bunge, Balozi Adadi Rajabu amethibitisha mkataba huo kati ya Jeshi la Polisi na Kampuni ya Lugumi Enterprises kuwasilishwa mbele ya Kamati yake siku ya jana.

===============

Njama nzito kuficha mkataba wa Lugumi

MKATABA tata wa Kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd inayomilikiwa na mfanyabiashara Said Lugumi, umezidi kuchukua sura mpya baada ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), kushindwa kuendelea na sakata hilo kutokana na kuhamishiwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.

Hatua hiyo inatokana na utata uliogubika mkataba huo ambao unawahusisha vigogo kadhaa wa Jeshi la Polisi pamoja na baadhi ya watendaji wa Serikali ya Rais Dk. John Magufuli, huku ikidaiwa kuwa huenda ikawa njia ya ‘kulindwa’.

Wiki iliyopita PAC ilipokutana na jeshi hilo kupitia taarifa ya hesabu zao za mwaka 2013/14 zilizokaguliwa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ilibainika kuwa mwaka 2011 liliingia mkataba na kampuni hiyo kwa ajili ya kufunga mashine za kuchukua alama za vidole katika vituo vya polisi 108 nchi nzima kwa gharama ya Sh bilioni 37.

Lakini hadi sasa mashine hizo zimefungwa katika vituo 14 pekee na kampuni hiyo kulipwa Sh bilioni 34 ambazo ni sawa na asilimia 99 ya fedha za makubaliano ya mkataba.

Kutokana na hali hiyo, PAC ambayo ilibaini kuwapo viashiria vya ufisadi katika tenda hiyo, iliwaagiza watendaji wa jeshi hilo kuwasilisha taarifa za mkataba huo pamoja na vielelezo vyake ili wajumbe waweze kuupitia pamoja na kutoa maagizo.

Chanzo cha kuaminika kiliambia MTANZANIA kuwa katika sehemu ya mkataba huo kati ya Jeshi la Polisi na Lugumi, imebainika kampuni hiyo kufanya mafunzo kwa watu watano ambayo wametumia Sh bilioni 5, huku mshauri mwekelezi akilipwa Sh bilioni 46 nje ya fedha zilizopo kwenye mkataba.

Hatua ya mkataba huo kupelekwa mbele ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, inadaiwa kuwa njia ya kutaka kuwalinda baadhi ya vigogo ambao wanatajwa kuhusika na kashfa hiyo ambayo imelitia doa Jeshi la Polisi nchini.

“Hapa kuna kulindana tu, hakuna namna yoyote. Kama uchafu umebainika mbele ya Kamati ya PAC inakuwaje wengine wanadaka kitu ambacho hakikuanza kwao?

“Kuna kila dalili ya wingu na shaka, ila ukweli utajulikana tu, haiwezekani watu wanatumia fedha za walipakodi vibaya halafu inapokuja wanataka kushughulikiwa wanatafuta kivuli cha kujifichia,” kilisema chanzo chetu.

Mkataba huo uliibuliwa na PAC wiki iliyopita ambapo watendaji wa Jeshi la Polisi walishindwa kutoa maelezo ya kutosha ndipo ikawataka kuwasilisha taarifa juzi.

Pamoja na kutakiwa kufanya hivyo, hadi kufikia jana saa 10 jioni Makamu Mwenyekiti wa PAC, Aeshi Hilaly, alisema kuwa kamati yao haijapokea taarifa yoyote kuhusu Kampuni ya Lugumi hivyo wameliandika barua Jeshi la Polisi liwasilishe mkataba huo ndani ya siku tatu.

Alisema barua hiyo wamemuomba Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilillah, ili aweze kuwaandikia Polisi ili wawasilishe mkataba huo kwa mujibu wa utaratibu kama kamati ilivyoagiza.

“Hadi muda huu ninapozungumza nawe sijapata taarifa yoyote, kwa hali hiyo tumelazimika kumwandikia barua Katibu wa Bunge ili awaandikie barua polisi walete mkabata huo ndani ya siku tatu kutoka leo (jana) kama walivyotakiwa na kamati yetu,” alisema Hilaly.

BALOZI ADADI

Akizungumza na MTANZANIA jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu, alithibitisha mkataba huo kuwasilishwa mbele ya kamati yake.

“Mimi kama mwenyekiti wa kamati ninapenda kukiri kwamba tumepokea mkataba kati ya Jeshi la Polisi na Kampuni ya Lugumi na tutaufanyia kazi kwa kina.

“Tunahitaji kuona kama kuna wizara zilizohusika na mkataba huu na kama tutaukuta ni mbaya, tutatoa taarifa kwa umma. Kikubwa tunawaomba Watanzania wawe watulivu, hatuko kwa ajili ya kumlinda mtu wala kikundi cha watu, tunasimamia masilahi ya Watanzania wote,” alisema Balozi Adadi.

RIDHIWANI AKANA

Taarifa za mkataba huo zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii zikiwahusisha baadhi ya vigogo wa Serikali akiwamo Waziri wa Serikali ya Rais Magufuli pamoja na kumtaja Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete (CCM).

Hata hivyo, Ridhiwani alivunja ukimya na kukanusha taarifa hizo zilizodai yeye ni mmoja wa wamiliki wa Kampuni ya Lugumi pamoja na Said Lugumi na aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi, Said Mwema.

Akizungumza na gazeti moja la kila siku (Si MTANZANIA), Ridhiwani ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, alisema hahusiki na Lugumi ingawa wana urafiki wa kawaida na mmiliki wa kampuni hiyo.

“Kwanza kabisa mimi si mmoja wa wamiliki wa kampuni hiyo, hilo ni jambo la msingi kabisa watu waelewe, na sijawahi kufanya biashara yoyote na Lugumi. Said Lugumi ambaye ni mmiliki wa kampuni hiyo tunafahamiana naye na ni rafiki yangu,” alisema Ridhiwani.

Alisisitiza kuwa hana uhusiano wa kibiashara na mtu huyo na kwamba hafahamu ni kwanini amehusishwa na Kampuni ya Lugumi.

“Hapa ni watu tu wanaamua kuingiza tu maneno yao, haya maghorofa ninayotajwa kumiliki Dar es Salaam hata sijawahi kutembelea ujenzi wake, wameamua kuniingiza, Lugumi nafahamiana naye binafsi tu lakini wananiingiza,” alisema Ridhiwani.

Chanzo: Mtanzania



NIMEANZA KUIELEWA ILE MICHORO YA JANUARY MAKAMBA MALA MTU KAZUNGUSHIWA MINYORORO MALA NYANI ANARUKIA KILA TAWI RAIA WANAMCHORA TU LILE FUMBO TAMU SANA WA TZ TUMELIWA HAWA NI WALE WALE.
 
Back
Top Bottom