Mkataba wa Lugumi wapelekwa kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama!

Mkataba wa Lugumi wapelekwa kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama!

Hivi ni kwanini huyo mtoto wa rais mstaafu anahusishwa na mambo mengi ya kashfa kuliko kusifiwa kwa kutenda mambo mema?hivi marehemu jk nyerere mbona alikuwa na watoto lkn hadi leo hii hatujasikia mambo ya maovu kama ya huyu?
Mkuu huyo katoka ukoo wa mchwa.
 
Kitendo cha mkataba kupelekwa kwa mwingine na sio aliyeomba yaani kamati ya PAC hapo mjue tumeishapigwa changa la macho , mwenye akili na afahamu.
 
Huyu Balozi Adadi Rajabu alikuwa DCI wa Jeshi la Polisi,hizi mashine za Finger Print zina uhusiano mkubwa sana na ofisi ya DCI sababu ya aina ya makosa ya jinai ambayo vielelezo vyake hutokana na mashine hizo.Haiwezi kuwa ajabu kuwa ununuaji wa mashine hii uliishirikisha pia ofisi ya huyo bwana,hivyo ni mgao wa 10% basi ulipita kote
Mimi nigeshauri kamati ya PAC igome kuendelea na ukaguzi kwani hakuna sababu ya wao kuingiliwa.
Huu mkataba una mengi sana huu,huu ni mtihani kwa JPM na harakati zake.Hakuna ubishi kuwa kwa kupelekwa kwenye kamati ya Adadi "kashfa" hii inaenda kufa kifo cha mende[/QUOT
 
Kitendo cha mkataba kupelekwa kwa mwingine na sio aliyeomba yaani kamati ya PAC hapo mjue tumeishapigwa changa la macho , mwenye akili na afahamu.
Nitashangaa sana kama JPM atakubali hizi zifanyike naye akae kimya na wananchi walio mwamini kauli zake waanze kumtilia shaka bila yeye kujali.
Hata miezi sits bado tayari anaingia kwenye kundi la kusema uongo? Hapana, kama kuna watu wanapitia hapa na wako karibu naye na wanampenda wamwambie kuwa unachafua dhamira yako na hata hayo maombi unayoomba wakuombee hawatafanya maana hustahili
 
Enzi zetu sekondary kitu kinachoitwa "tata" kilikuwa hakina namna ya kuweze kikielezea
au kuuliza swali.

Kwa ufahamu wangu ndogo,hivi inakuwaje taasisi nyeti/dola/interegensia ya jeshi la polisi inakubali kuingizwa mtegoni ilihali ndio ambayo inategemewa na watu maskini katika haki,ulinzi na usalama wa mali zao?

Kama kuna watu wameingia mkataba wa finger print/alama za vidole si na waanze hiyo kazi mara moja kama kuna tuhuma za udanganyifu katika mkataba huo nini kifanyike mara moja hasa ukizingatia kuwa Jeshi letu la Polisi la sasa si kama la zamani.

Hii tabia ya kuingiza watu/mtu au kikundi cha watu kwenye masuala muhimu ya kitaifa eti tu kutokana na statas zao.vyeo,ukaribu na mtu/watu fulani bila ya kuwa na ushahidi wowote si sawa.

Lakini pia ikitokea mtu/watu/kikundi cha watu kikfanya kinyume na utaratibu wa watu waliojiwekea/sheria haijalishi kafanya nani,yupi ni lazima sheria ichukue mkondo wake.

Kamwe tusiwalee mabepari wachache wanaotumia fursa za vyeo,ukaribu na mtu/watu fulani maarufu kujifanza wanyonyaji na wahujumu uchumi,hakika hatutofika salama kwenye Tanzania ya viwanda.
 
Nitashangaa sana kama JPM atakubali hizi zifanyike naye akae kimya na wananchi walio mwamini kauli zake waanze kumtilia shaka bila yeye kujali.
Hata miezi sits bado tayari anaingia kwenye kundi la kusema uongo? Hapana, kama kuna watu wanapitia hapa na wako karibu naye na wanampenda wamwambie kuwa unachafua dhamira yako na hata hayo maombi unayoomba wakuombee hawatafanya maana hustahili
mkuu upo sahihi, sina uhakika record ya JPM inaweza kuvulugwa na jambo dogo hivi, kwanza itakuwa dharau,

nashangaa sana kamati iliyoagiza kupewa taarifa nyingine na iliyopewa taarifa nyingine, sasa cjui kama wizara hawajui kusoma au wanatufanya watz woooteeee hatujui,

ki ukweli kama ni kwelk hyo taarifa imewasilishwa kamati ya mambo ya nje, basi hapo ni kulindana, kwa kuwa haina kazi huko maana walioihitaji si wao, sasa watatoa taarifa vp?

nitakuwa wa mwisho kuamin hili kutokea, na hapo ndipo kipimo cha magu kinapokuja sasa...
 
Tuwe na subira. Hapana chezea serikali ya Magufuli
Endelea kuweka kumbukumbu zako vizuri...

1. Meremeta- HOLA
2. Deep Green- HOLA
3. Kiwira - HOLA
4. Nyumba za Serikali-HOLA na ndio ishakuwa HOLA kabisaaaaaaa
5. Epa- HOLA
6. Richomond- HOLA
7. Mabehewa- HOLA
8. Escrow- HOLA
9. NSSF- HOLA
10. NIDA- HOLA
11. LUGUMI- ........

Hii ndio CCM bana. Kila mtu mwizi, baba jizi, mama jizi watoto wezi, wajukuu MAJAMBAZI, vitukuu Vibaka..
 
Kitendo cha mkataba kupelekwa kwa mwingine na sio aliyeomba yaani kamati ya PAC hapo mjue tumeishapigwa changa la macho , mwenye akili na afahamu.
Roho imeniuma sana! Halafu watanzania wanategemewa kuwa wazalendo. Sio kwa staili hii. Magufuli ingilia kati kama ulivyofanya Shinyanga. Tunataka kujua ukweli. Ukiwafilisi hawa tutajenga madarasa mengi.
 
Ndio maana vigumu sana kuziamini sarakasi za Magufuli kama ni mtumbua majipu kweli au ni visasi na usanii. Kwa sisi non believers tumeamua kujipa muda walau miaka miwili ili tuone huu utumbuaji majipu. Huenda ni mbinu tu inaitwa Quick winning halafu waanze kupiga dili kuliko Kikwete.

Nini kigugumizi kumkamata Saidi Lugumi? Kwa nini mkataba upelekwe kwenye kamati ambayo haijaomba, je wataujadili vipi wakati hawakuwa na ratiba nao? Kwa nini hiyo kamati isikabidhi kwa kamati iliyoomba? Spika haoni hapo kama kuna figisu? Raisi hasomi Magazeti? Au ameacha kuangalia kile kipindi alichosema anakipenda cha Mawingu 360? Jamani Magufuli hizi sanaa utazifanya hadi lini? Kwa nini usiachie rangi yako halisi ya CCM ni ile ile?
 
Hivi ni kwanini huyo mtoto wa rais mstaafu anahusishwa na mambo mengi ya kashfa kuliko kusifiwa kwa kutenda mambo mema?hivi marehemu jk nyerere mbona alikuwa na watoto lkn hadi leo hii hatujasikia mambo ya maovu kama ya huyu?
Riz,Freddy,Sioi ni vijana waliotumia nafasi za wazazi wao kupiga.
 
Hii ndio Tanzania.

Hii habari imeandikwa na gazeti la mtanzania la leo na Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Bunge, Balozi Adadi Rajabu amethibitisha mkataba huo kati ya Jeshi la Polisi na Kampuni ya Lugumi Enterprises kuwasilishwa mbele ya Kamati yake siku ya jana.

===============

Njama nzito kuficha mkataba wa Lugumi

MKATABA tata wa Kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd inayomilikiwa na mfanyabiashara Said Lugumi, umezidi kuchukua sura mpya baada ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), kushindwa kuendelea na sakata hilo kutokana na kuhamishiwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.

Hatua hiyo inatokana na utata uliogubika mkataba huo ambao unawahusisha vigogo kadhaa wa Jeshi la Polisi pamoja na baadhi ya watendaji wa Serikali ya Rais Dk. John Magufuli, huku ikidaiwa kuwa huenda ikawa njia ya ‘kulindwa’.

Wiki iliyopita PAC ilipokutana na jeshi hilo kupitia taarifa ya hesabu zao za mwaka 2013/14 zilizokaguliwa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ilibainika kuwa mwaka 2011 liliingia mkataba na kampuni hiyo kwa ajili ya kufunga mashine za kuchukua alama za vidole katika vituo vya polisi 108 nchi nzima kwa gharama ya Sh bilioni 37.

Lakini hadi sasa mashine hizo zimefungwa katika vituo 14 pekee na kampuni hiyo kulipwa Sh bilioni 34 ambazo ni sawa na asilimia 99 ya fedha za makubaliano ya mkataba.

Kutokana na hali hiyo, PAC ambayo ilibaini kuwapo viashiria vya ufisadi katika tenda hiyo, iliwaagiza watendaji wa jeshi hilo kuwasilisha taarifa za mkataba huo pamoja na vielelezo vyake ili wajumbe waweze kuupitia pamoja na kutoa maagizo.

Chanzo cha kuaminika kiliambia MTANZANIA kuwa katika sehemu ya mkataba huo kati ya Jeshi la Polisi na Lugumi, imebainika kampuni hiyo kufanya mafunzo kwa watu watano ambayo wametumia Sh bilioni 5, huku mshauri mwekelezi akilipwa Sh bilioni 46 nje ya fedha zilizopo kwenye mkataba.

Hatua ya mkataba huo kupelekwa mbele ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, inadaiwa kuwa njia ya kutaka kuwalinda baadhi ya vigogo ambao wanatajwa kuhusika na kashfa hiyo ambayo imelitia doa Jeshi la Polisi nchini.

“Hapa kuna kulindana tu, hakuna namna yoyote. Kama uchafu umebainika mbele ya Kamati ya PAC inakuwaje wengine wanadaka kitu ambacho hakikuanza kwao?

“Kuna kila dalili ya wingu na shaka, ila ukweli utajulikana tu, haiwezekani watu wanatumia fedha za walipakodi vibaya halafu inapokuja wanataka kushughulikiwa wanatafuta kivuli cha kujifichia,” kilisema chanzo chetu.

Mkataba huo uliibuliwa na PAC wiki iliyopita ambapo watendaji wa Jeshi la Polisi walishindwa kutoa maelezo ya kutosha ndipo ikawataka kuwasilisha taarifa juzi.

Pamoja na kutakiwa kufanya hivyo, hadi kufikia jana saa 10 jioni Makamu Mwenyekiti wa PAC, Aeshi Hilaly, alisema kuwa kamati yao haijapokea taarifa yoyote kuhusu Kampuni ya Lugumi hivyo wameliandika barua Jeshi la Polisi liwasilishe mkataba huo ndani ya siku tatu.

Alisema barua hiyo wamemuomba Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilillah, ili aweze kuwaandikia Polisi ili wawasilishe mkataba huo kwa mujibu wa utaratibu kama kamati ilivyoagiza.

“Hadi muda huu ninapozungumza nawe sijapata taarifa yoyote, kwa hali hiyo tumelazimika kumwandikia barua Katibu wa Bunge ili awaandikie barua polisi walete mkabata huo ndani ya siku tatu kutoka leo (jana) kama walivyotakiwa na kamati yetu,” alisema Hilaly.

BALOZI ADADI

Akizungumza na MTANZANIA jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu, alithibitisha mkataba huo kuwasilishwa mbele ya kamati yake.

“Mimi kama mwenyekiti wa kamati ninapenda kukiri kwamba tumepokea mkataba kati ya Jeshi la Polisi na Kampuni ya Lugumi na tutaufanyia kazi kwa kina.

“Tunahitaji kuona kama kuna wizara zilizohusika na mkataba huu na kama tutaukuta ni mbaya, tutatoa taarifa kwa umma. Kikubwa tunawaomba Watanzania wawe watulivu, hatuko kwa ajili ya kumlinda mtu wala kikundi cha watu, tunasimamia masilahi ya Watanzania wote,” alisema Balozi Adadi.

RIDHIWANI AKANA

Taarifa za mkataba huo zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii zikiwahusisha baadhi ya vigogo wa Serikali akiwamo Waziri wa Serikali ya Rais Magufuli pamoja na kumtaja Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete (CCM).

Hata hivyo, Ridhiwani alivunja ukimya na kukanusha taarifa hizo zilizodai yeye ni mmoja wa wamiliki wa Kampuni ya Lugumi pamoja na Said Lugumi na aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi, Said Mwema.

Akizungumza na gazeti moja la kila siku (Si MTANZANIA), Ridhiwani ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, alisema hahusiki na Lugumi ingawa wana urafiki wa kawaida na mmiliki wa kampuni hiyo.

“Kwanza kabisa mimi si mmoja wa wamiliki wa kampuni hiyo, hilo ni jambo la msingi kabisa watu waelewe, na sijawahi kufanya biashara yoyote na Lugumi. Said Lugumi ambaye ni mmiliki wa kampuni hiyo tunafahamiana naye na ni rafiki yangu,” alisema Ridhiwani.

Alisisitiza kuwa hana uhusiano wa kibiashara na mtu huyo na kwamba hafahamu ni kwanini amehusishwa na Kampuni ya Lugumi.

“Hapa ni watu tu wanaamua kuingiza tu maneno yao, haya maghorofa ninayotajwa kumiliki Dar es Salaam hata sijawahi kutembelea ujenzi wake, wameamua kuniingiza, Lugumi nafahamiana naye binafsi tu lakini wananiingiza,” alisema Ridhiwani.

Chanzo: Mtanzania
Mambo yote yanayohusu ulinzi na usalama hii ndio kamati yake,pia ina wabunge wa upinzani sio tabu.Tusubiri.
 
Maji mazito sana kwa Magu nadhani ataomba poo tena aende Chato akapumzike! Naona PM nae anapumzika! Huu mziki wa Mkwere hatari kila sehemu imeoza! Na wana mkono wao kwenye kuiba! Sasa utafanyaje? Jipu halitumbuki limekuwa ni ngozi ngumu ambayo haina maji ndani utatumbua nini? Inahitaji operation kukata hiyo nyama! Sio size yake JPM! Atayaacha!! Hawezi kumvaa Mwema na huyu wa sasa....Riz1 na Said Lugumi analindwa pande zote na kivuli cha mstaafu!!
 
Back
Top Bottom