Mke wa Profesa Jay afunguka, familia yaomba msaada wa matibabu

Mke wa Profesa Jay afunguka, familia yaomba msaada wa matibabu

“Jay ni mtu wa watu, sababu ya kuamua kuzungumza hadharani ni kwa kuwa ana mashabiki wengi, tukaona hatumtendei haki, tunaomba watu waungane nasi zaidi tumuingize lwenye maombi yetu ili apone, lakini suala la pesa nalo ni muhimu pia,” alisema Grace.
Mtu wa watu!

Wakati mnasema mnataka privacy hamkujua Jay ni mtu wa watu? Kuiga tamaduni za kizungu ambazo hatuzielewi wala hazituhusu....

Walitoa tamko kwa umma Jay na familia wanaomba tuwape faragha zao wakati wakiuguzana.... leo wanasema tuungane nao kwa mchongo wa pesa na maombi.... tushike lipi ?

Wenzenu Ulaya huko wakisema gwiji fulani jamani linaumwa linaomba privacy yake hawawezi kurudi baada ya siku tatu kupiga yowe tumsaidie....
 
Mtu wa watu my balls! Wakati mnasema mnataka privacy hamkukumbuka Jay ni mtu wa watu?

Kuiga tamaduni za kizungu ambazo hatuzielewi na hazituhusu....

Juzi walisema Jay na familia wanaomba tuwape faragha zao wakati wakiuguzana.... leo wanasema tuungane nao kwa mchongo wa pesa na maombi.... tushike lipi ?

Wenzenu Ulaya huko wakisema gwiji fulani jamani linaumwa linaomba privacy yake hawawezi kurudi baada ya siku tatu kupiga yowe tumsaidie....
Boss,hawajapiga yowe, kama hujapendezwa na kitendo walichofanya kaa tu kimya haina haja ya kusema. wapo watu watatuma pesa hata jero jero jamaa atapona
 
Familia ya msanii wa Bongo Fleva, Joseph Haule ‘Profesa Jay’ imejitokeza hadharani na kuelezea juu ya hali ya kiafya anayopitia staa huyo na kuomba msaada wa matibabu yake.

Jay ambaye pia alikuwa ni Mbunge wa Mikumi, alipoanza kuugua alipelekwa katika hospitali mitaa ya Tegeta, akahamishwa kupelekwa Lugalo na baadaye akahamishiwa Muhimbili ambapo ndipo alipo hadi sasa, lakini baadaye kukawa na ukimya wa taarifa.

Wakizungumza katika mahojiano ya Kituo cha Clouds FM, leo Jumatano, familia hiyo ikiongozwa na mke wa Jay, Grace Mgonjo pamoja na mdogo wa Jay, Black Rhino, wameelezea kuwa Profesa ni mgonjwa na wamekuwa wakitumia gharama kubwa katika matibabu yake bila kufafanua zaidi kuhusu ugonjwa unaomsumbua.

“Wakati tunaanza kuuguza hatukutarajia kama itakuwa serious, tulijua ni kitu cha muda mfupi kisha atapona.

“Jay ni mtu wa watu, sababu ya kuamua kuzungumza hadharani ni kwa kuwa ana mashabiki wengi, tukaona hatumtendei haki, tunaomba watu waungane nasi zaidi tumuingize lwenye maombi yetu ili apone, lakini suala la pesa nalo ni muhimu pia,” alisema Grace.

Baadhi ya wasanii na watu maarufu walipiga simu redioni hapo na kuchangia matibabu akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds FM, Joseph Kusaga ambaye alitoa mchango wa Sh milioni 2.

Walitaja namba na njia wanazoweza kutuma michango ya kusaidia matibabu ya msanii huyo kuwa ni:
MPESA: 0757919192 Joseph Haule,
TiGOPesa: 0715919192 Joseph Haule,
CRDB account no: 0112044845200 Joseph Leonard Haule
Kila wakati huwa nasema hawa wasanii wawe wanaangalia na kujifunza kutoka kwa wenzao,hawa wasanii nyota ni kama hawajui kuna kesho, hawa wasanii wakiwa kwenye good time hawajui kesho na hawajuia kama kuna watu wana shida na kuwa kuna siku nao watakuwa hawana kitu.

Mimi nikiugua au ndugu yangu akiuugua siji mitandaoni kuomba msaada,ni mzigo wangu. Ukienda pale Muhimbili kuna mwembe unaitwa Mwembe mawazo huwa wanakaa watu mbalimbali kila mtu anahangaika na mgonjwa wake,utasikia huyu anapiga simu uza shamba,au muambie baba mdogo achangie , na wala hutawasikia kusema tuweke namba zetu mtandaoni tuwaombe watu.

Pamoja na umasikini wao, mzigo wangu ni wa kwangu, kila mtu abebe furushi lake! hawa wasanii hakuna wanaowasaidia wakiwa kilingeni wao ni starehe na watu wao.
 
Mungu afanye miujiza tu .Ila itakuwa katika terminal. Unamkumbuka kocha Mziray(R.I.P)Na yeye ilipofikia terminal ndo ikawa basi tena.
Dah umenikumbusha kocha Mziray dah umenipa simanzi sana. Alikua akinipa moyo sana na mara kwa mara nikienda ofisini kwake pale OUT Kinondoni. Mzee wangu huyu alikua muungwana sana. Wallah Allah amsitiri kaburini mja wake.
 
Tatizo la wasanii wanaishi maisha ya kifahari sana na kuwaona raia wa kawaida kama kinyesi ila wakiumwa haraka sana wanatembeza bakuli tuwachangie.
Prof siyo mtu wa matambo, ila hii imenifanya niwaze jinsi Watanzania wengi tulivyo na shida.

Kama Prof mtu ambaye amekuwa msanii kwa muda mrefu, akawa mbunge kwa miaka mitano imekuwa hivi, je kwa karundage tulio wengi!

Serikali ifanye namna aisee kwenye suala la matibabu ya wananchi wake.

Tumchangie Prof hasa sisi ambao ni generation ya kipindi cha chemsha bongo
 
Back
Top Bottom