Mke wangu akiwa nami 'full kununa' ila tukiwa na rafiki zangu anatabasamu na kucheka sana

Ndoa ni ngumu jamani. Acheni tu!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sio zote mkuu. Zipo nzuri tu. Sema waja wa sasa viwango vya maadili na ufahamu halisi wa mahusiano na ndoa umeporomoka sana ndo maana unaona viroja vingi. Mkikutana mna uelewa na mtazamo chanya with good values ndoa ni tamu na baraka kwenye maisha.
 
Mkuu ukifika nyumban kama unapenda kukaa kimya ,jaribu kuwa unamuongelesha ,tafuta vichekesho uwe unabonga nae ,usiwe serious muda wote huenda mkeo anakosa hio kitu...

Ukiwa nyumban ,msumbue sumbue ,muagize ,mara mshike mkono ,mara mpige kofi la uchokozi ,akifua nguo mzingue kidogo hazijatakata ,yaani akuzoeee kwa namna yeyote ile ...

Sio mnakaa kama mtu na boss wake ndan
 
Inakuwa point of no return kama ni mke ndio dah! Inakuwa balaa
Mimi siwezi kuwa mfungwa wa hiari, ikiwa nimeharibu ntajishusha na kubadilika kabisa, nikiomba msamaha muda mrefu, nikampa muda wa kutosha apone lkn ikashindikana, ninamwachia nyumba nasepa nikaanze moja, mtakuja kuuana bure au yeye nanpa uhuru akatafute aliyesahihi kwake
 
Yes ukilea watoto katika mazingira hayo watakuwa na sumu mbaya
 
Yeah kukimbia hilo ni swala ambalo lipo akilini mwangu haswaa! Siwezi vumilia vituko vya mke ambaye hana habari na mimi
 
We unafikiri kwanini siku hizi ndoa hazidumu? Wanawake waliweza kuvumilia zamani maana hawakuwa na pa kwenda wala financial freedom. Hivyo ilibidi tu wavumilie walee watoto, ila msifikirie baada ya usaliti hali inarudi tu kuwa sawa. Fainali uzeeni unaona tu mama yuko busy na wanae wewe hawana muda na wewe na wakati huo ndio wewe unamuhitaji zaidi.
 
Dah kweli, zamani ilikuwa mzee ndio bread winner mama anatulia tu kuvumilia vimbwanga vya mzee
 
Sema kwa wanawake wazinzi kwao haiwaumizi so sio kwa wanawake wote! Mengine yanayokazwa ovyo huwa hayawazi
Labda kama hakupendi, ila kama anakupenda hata kama nae ni mzinzi maumivu yako pale pale. Unless awe aliolewa na wewe tu ilimradi nae aolewe.
 
Labda kama hakupendi, ila kama anakupenda hata kama nae ni mzinzi maumivu yako pale pale. Unless awe aliolewa na wewe tu ilimradi nae aolewe.
Eeh nazungumzia hawa wahivi ambao wengi still wanagongwa na ma EX zao
 
Una hoja Espy
Jambo muhimu kwetu wanaume ni kuheshimu, fanya ufanyavyo lakini usinaswe.
Mwanamke akijua umemsaliti hakika ni kitu kibaya sana sana.
 
Akichunguza simu ya mkewe ghafla atapata jibu kamili


Ataanzaje kwa mfano?!

Mara nyingi wanaume kwenye ndoa ndio huwa wanaanzaga kuweka misimamo ya kutoshika simu ya mwenza wake.

Tena wanaume wengi hupenda kusema kila mtu na simu yake tu asishike ya mwenzie [emoji108][emoji108][emoji108]

Sasa ataanzaje kuchunguza ya mkewe?

Halafu wanaume laiti wangejua?!

Unapoweka misimamo ya hivyo mwanamke mwerevu anajua okeiiiii sawa nimekuelewa baba lakini na mimi nitajua cha kufanya!

Ndio unakuta mwili mmoja lakini simu zina passcodes [emoji108][emoji108]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…