Mke wangu amenyoa nywele na zilikuwa zinanivutia sana

Mke wangu amenyoa nywele na zilikuwa zinanivutia sana

Mtoa mada upo sahihi kabisa.
Alipaswa akushirikishe hasa kama huwa unamweleza namna unavyozipenda nywele zake. Mbali na kunyoa hata kama alitaka kuweka dawa ilipaswa akushirikishe. Sisi wengine tunawashirikisha wapenzi wetu hadi mitindo tunayotegemea kwenda kusuka ili watuchagulie mmoja au watushauri.

Wanaume wengi wanapenda sana nywele, na kitu mwanaume anachokipenda kwa mwanamke sio cha kukipuuzia eti kwa madai "kama ulinipendea nywele" anatakiwa ajue yeye ni pambo /ua kwa mumewe anatakiwa awe kwenye namna ambayo mume wake anapenda cha msingi mume awe anatoa huduma.
Huyo mwanamke kamu disapont mumewe bana, wanaume wengi hupenda nywele ndefu[emoji23][emoji23] wangu nilimtania na nyoa alini mind kweli
 
Sio mda wote mtu ana furaha tujaribu kulielewa hilo kwanza.
Sasa wanaume wengi hawajuagi kua hata wanawake nao ni binadamu, akiwa na stress akajibiwa tofauti na matarajio yake ndo kama mjomba apa anasema dharau zimeanza.

Labda nywele zilikua zinamchosha kweli lakini alijua akikwambia utakataa na yeye kuendelea kupata kupata tabu.
Mpe muda atakua sawa tu.
 
Kama ulimkuta na hizo nywele uko sahihi kuhoji

Lakini kama alikua ananyoa wewe ndo ukamshawishi asuke,itakuwa kachoka vya kusuka kaamua kunyoa

Hajakuambia kwa sababu alihofia utamkatalia na yeye ndo kashachoka kabisa.

Wengine tunapenda nywele fupi,kusuka tunajioneaga usumbufu tu
 
Nywele zina uzuri wake jamani, tena kama sisi wenye sura za baba ukinyoa unaweza shangaa hata mwanaume hasimamishi tena[emoji23][emoji23][emoji23]
Nywele kweli hutusitiri wenye sura za baba kutotofautisha Sasa tukinyoa tunazidi ubovu wa sura waume zetu bana. Huyo mke wa mleta mada had mumewe kamwona hajapendeza itakuwa nywele zilikuwa zina msitiri
 
Habari wakuu, mimi sio mgeni jamiiforums mara nyingi hapenda tu kuangalia nyuzi za watu na kuchangia inapobidi.Leo nimeona niwashirikishe yaliyonisibu

Nipo kwenye ndoa zaidi ya mwaka sasa na kati ya vitu vilivyonivutia na vinavyonivutia sana kwa mke wangu kwakweli ni nywele zake zilivyo ndefu na natural na yeye pia analifahamu hili manake nimekua nikimuambia mara kwa mara.

Cha ajabu Jana wife kafika nyumban amenyoa nywele zote na wala hakunifahamisha kama atanyoa na wala sikuona dalili zozote kama hili litatokea.

Kwa kweli imeniuma sana na mpaka sasa bado inauma nahisi kama amenidharau kwa kutokunishirikisha kwenye jambo la muhimu kama hilo.

Sura imebadilika ata kutoka nae out nadhani itakua changamoto nilimuuliza sababu za kunyoa anasema kua amezichoka nywele ndefu na wala hazitaki tena.

Nimemuambia ninavyohisi anadai kama nlipenda nywele na sio yeye basi ananipa pole. ninaanza kupata wasiwasi kua anaanza kubadilika manake naanza kuona kama dharau zinakuja kwa mbali.

Wakuu embu nitoeni wasiwasi, ni mimi nawaza vibaya ama ndo tayari mwanamke anataka kunipanda kichwani?
Hii mbona simple tuu kung'amua..

Ni kuwa mkeo kapata mchepuko bab kubwa, ambao haupendi hizo nywele...

Pole sana mkuu kama ntakuwa nimekukwaza
 
Habari wakuu, mimi sio mgeni jamiiforums mara nyingi hapenda tu kuangalia nyuzi za watu na kuchangia inapobidi.Leo nimeona niwashirikishe yaliyonisibu

Nipo kwenye ndoa zaidi ya mwaka sasa na kati ya vitu vilivyonivutia na vinavyonivutia sana kwa mke wangu kwakweli ni nywele zake zilivyo ndefu na natural na yeye pia analifahamu hili manake nimekua nikimuambia mara kwa mara.

Cha ajabu Jana wife kafika nyumban amenyoa nywele zote na wala hakunifahamisha kama atanyoa na wala sikuona dalili zozote kama hili litatokea.

Kwa kweli imeniuma sana na mpaka sasa bado inauma nahisi kama amenidharau kwa kutokunishirikisha kwenye jambo la muhimu kama hilo.

Sura imebadilika ata kutoka nae out nadhani itakua changamoto nilimuuliza sababu za kunyoa anasema kua amezichoka nywele ndefu na wala hazitaki tena.

Nimemuambia ninavyohisi anadai kama nlipenda nywele na sio yeye basi ananipa pole. ninaanza kupata wasiwasi kua anaanza kubadilika manake naanza kuona kama dharau zinakuja kwa mbali.

Wakuu embu nitoeni wasiwasi, ni mimi nawaza vibaya ama ndo tayari mwanamke anataka kunipanda kichwani?
Hebu kuwa specific mkuu, amenyoa nywele za sehemu gani? Isijekuwa kwenye papuchi
 
Nilikuwa na dreadlocks nilizotunza kwa miaka 9.
Nilizianza kwa mahaba, kwa kugharamiwa mno.
Nywele ilikuwa traaaam ileeee.
Nywele ilikuwa inapeeeendwaaa ileeeee.

Kuna kipindi I went through hell, vuruuuuugu, mapito ya kiwehu haifai.
Katika kitu nilijua nikikiondoa kitanipa mtazamo mpya juu ya maisha, mapenzi , mwonekano binafsi ni kuondoa zile nywele.

Nilitaka kudare kufanya kitu nilikwishaapa sitakuja kufanya. Hata iweeeeje.
Nilitaka kuvuka duara langu la uthubutu.
So it was a dare or die decision.

Dreadlocks zenye budget ya si chini ya 100K kwa mwezi, bidhaa za kuzitunza, uzuri wa ile nywele.
Halafu miaka 9, zilikuwa ndefu, Nene, rangi nyeusiiii, nzitooo, yani traaaam.

Siku nikatoka kazini, paaap!
Nikapita saloon.
Nikazikata ,nikaweka dawa, nikaweka rangi.

Wakati nazikata waliokuwepo saluni najumbuka mmoja alilia, alikuwa Radhi anilipe njsikate.
Ila kulikuwa hakuna kitu nilitamani kufanya for my inner peace kama kukata zile nywele.

So I cut them off.
Na nilizjkata kata kiasi hazikufaa kufanyiwa chochote.
I just wanted to end its era and everything.
Usingizi niliolala hiyo siku anajua Mungu.

Nazikumbuka sometimes, ila sijutii.
 
😂😂😂😂😂😂 Best we injinia soma hiyooooo! Kwani hujasikia ME wanaonuna kisa GF/Mke kanyoa vuzi lote!? 😜😜😜

Best 😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂🙌
 
Nywele zina uzuri wake jamani, tena kama sisi wenye sura za baba ukinyoa unaweza shangaa hata mwanaume hasimamishi tena[emoji23][emoji23][emoji23]
Mimi nimfanyeje mke wangu jamani anyoe nywele? Haiingii akilini nimeishi na mwanamke more than 7 years halafu sijui akinyoa anakuaje..! Mimi nataka anyoe nimuone anavyokua yeye anasema eti ana kichogo, mara sijui nini.. yaani kila nikileta hiyo mada ni ugomvi.
 
😂😂😂😂😂😂 Best we injinia soma hiyooooo! Kwani hujasikia ME wanaonuna kisa GF/Mke kanyoa vuzi lote!? 😜😜😜
Hahahhahhahahhaa umenikumbusha kesi zisizokuwa na akili ila zina akili!

Vile hiyo ni kesi kubwa sana.
 
  • Kicheko
Reactions: BAK
Back
Top Bottom