Mke wangu ananikera anataka attention yangu kila saa

Mke wangu ananikera anataka attention yangu kila saa

Oa mke wa pili ndio utaijua thamani yake sasa....huyo yupo kama huyu hapa anakupigia simu kutwa mara 10...na hachoki kuongea na wewe....hadi unajiuliza kweli mimi sina shukrani mtu hakuchoki kila kukicha...kijana mpende mkeo huo ni upendo wa dhati kabisa kutoka moyoni ukibugi hapo ujue umepotea njia.
Hamna hayo mapezi ya design hiyo siapendi hayaniongezee chochote zaidi ya stress
 
Hamna hayo mapezi ya design hiyo siapendi hayaniongezee chochote zaidi ya stress
Ndio kawaida ya mwanaadamu...huomba jambo akilipata sasa anaona halina faida kwake analizioea na kulichukulia poa.
Hata utajiri,elimu,umaarufu, kabla haujavipata unavipa thamani kubwa ila ukishakuona navyo unaviona vya nini si lolote si chochote kwako.
 
Una bahati ya Mtende BADILIKA Mkuu. Mpe Mkeo attention aitakayo toka kwako kwani utapungukiwa kipi? Ole wako wahuni wamnase kwa URIMBO.

I can't leave her plz.....ni muzri kasoro ni hiyo tu.
 
Umepata mke mwema sana. Piga magoti hapo ulipo na umshukuru Mungu. Ukisikia wenzio mambo wanayopambana nayo huko kwenye ndoa nadhani ungewaomba mods tu waufute uzi huu.

[emoji3591][emoji3591][emoji3591] Kimsingi wanawake wote wanapenda attention sema tu wengi wamejikatia tamaa kwa sababu ya waume zao kutojali. Na wanawake wengi walio katika ndoa wanachapwa nje sana siyo kwa ajili ya pesa bali kwa kupewa attention tu, kusikilizwa, kujaliwa na kuheshimiwa.

Narudia tena: wewe umepata mke mwema na anayekujali na kukupenda. Mhakikishie tu kuwa unampenda sana na kwamba upo kwa ajili yake mpaka kifo. Vizawadi vidogo vidogo na ukipata mwanya huko kazini mpigie...hata kama ni kusema tu "Niko mkutanoni lakini nilitaka tu kukukumbusha kuwa nakupenda sana mke wangu" na kukata simu inatosha. Na siku hiyo kama una kahela mkononi mchukulie kakitafunwa kake akapendako...hata kama ni kipande cha nanasi au chips (ili azidi kuwa bonge zaidi [emoji16][emoji16][emoji16]). Ndoa zinahitaji kazi na una bahati huyo wa kwako angalau unajua anachohitaji ili kuwa na furaha. Wengine (hasa vimbaumbau) ni minuno tu na ghubu kwa kwenda mbele hata tatizo hulijui.

Akiona kuwa unamjali sana; na akawa na uhakika kuwa penzi lako kwake halijapungua; na kwamba huna wengine huko nje hata ukimwambia kuwa waifu leo naomba privacy kidogo nifanye hiki...na kibusu kidogo ukampa au ukamparaza kikofi chokonozi cha takoni - atakuelewa tu...na ukipata mwanya na wakati sahihi unaweza kuongea naye tu kwa ustaarabu kuhusu nawe kuwa na privacy yako sometimes. Atakuelewa...labda awe na matatizo mengine ya kisaikolojia.

Take care of that marriage my man. That's your duty na ukishindwa mabaharia watakusaidia...na wanajua kutoa attention na ku-care hao usiombe....Usiwape hiyo nafasi maadam unajua weakness ya mkeo!
[emoji1376][emoji1376][emoji1376]
 
Mkuu amini usiamini huyo ndiyo Mke bora kabisa! Anakupenda upeo,nikupe hongera kwa kupata mkeo wa aina hiyo.
 
Back
Top Bottom