Mke wangu hataki niendeshe gari alilonunua. Nakereka sana

Mke wangu hataki niendeshe gari alilonunua. Nakereka sana

Mimi ni mwanaume wa kawaida, nimejaaliwa kipato cha wastani tu kinachotokana na juhudi za kujihusisha na hiki na kile kwa kupitia kujiajiri.

Mke wangu pia ni mchakarikaji na anaitumikia biashara ya vyombo vya ndani na mapambo ya ndani ambayo kwa pamoja tuliifungua na inafanya vzr sana.

Tumejaaliwa kuwa na gari moja Suzuki modeli mpya ambayo kiukweli aliinunua yeye mwaka Jana January. Kwasasa mimi ni fundi wa mashine za aina mbalimbali ikiwemo majenereta, magreda, kreni n.k. Na kwa kuwa mishe zangu za kiufundi hazihusishi sana matumizi ya gari ya kutembelea kwahyo huwa naitumia mara chache sana.

Baada ya kumfundisha mkewangu kuendesha akawa nayo kuanzia hapo. Mie Nina pikipiki ambayo hunipeleka huku na kule na kunifanikishia mishughukiko yangu yote bila tashwishi . Ninapohitaji gari kwa ajili ya matumizi ya hapa na pale au ninapoonyesha dalili ya kwamba nitatumia gari siku hiyo, papo hapo mke wangu huanza kujiskia karaha na ataanza kuongea maneno ambayo yanatoa ishara kwamba hataki ntumie gari.

Ukweli sipendezwi na hali hiyo maana inaudhi sana. Kwakuwa nimeshamjulia huwa nampuuza afu nachukua gari naenda kwenye kusudi nililolenga lkn furaha yake hutoweka kwa siku hiyo na hukereka kiukweli. Ingawa mie ndo niliyemfundisha kuendesha lkn pia haniamini napoendesha gari na hapendi nimuendeshe na kila wakati anasikika akinikosoa ninapoendesha, yani huwa dereva namba moja wakati aliyeshika usukani ni mimi.

Na kwa vile ameshajua pia nampuuza katika hilo, mara nyingi mke wangu huamua kukaa siti ya nyuma kwa vile haamini udereva wangu na huona kama nitamsababishia ajali akikaa mbele.

Kwa ufupi hapendezwi ninvyoendesha gari na hili jambo linanikera sana.

NAOMBENI USHAURI WENU WA KUNIJENGA KTK HILI.

Sent using Jamii Forums mobile app


Huyo Mke wako:
1) Ni mchoyo sana Chake chake , chako chetu.
2) Ni Malaya inawezekana hataki mabwana zake wamwone na wewe ndo maana anakaa nyuma, Mke wako lazima akae mbele kwa furaha kama hana makondakonda kama ya mke wako
3) Huyo mama hakupendi ndo maana hataki watu wengine watabuwe kwamba yeye ni mke wako.
4) Inawezekana wewe siyo handsome wa kula naye bata ndo maana anaona choo kuendeshwa na wewe mzee wa spana za mashine muda wote unanuka greese na oil chafu.
5) Huyo mke wako akishapata pesa za kutosha ataomba taraka kwa vile atakuwa na pesa za kumusukuma mwaka mmoja.
 
Ha ha umenikumbusha kipindi hicho kuna demu akaniganda tubadilishane simu [emoji3][emoji3]..
Nimpe Note 4 yeye anipe kitecno chake, niliwaza sana akili ya hawa watu!

Kama unamwelewa unamwachia, au unamtafutia yake nzuri.

Wameumbwa hivyo, hakuna namna.
 
Huyo ni mke au takataka? Kwanza ana umri gani?

Infact, wewe pia una umri gani? I must be honest, kuna utoto na irresponsibility mahali fulani!

Kuwa nae makini sana huyo mkeo ana tabia ya uchoyo na ubinafsi! Jiandae baada ya muda kugawana mali pasu kwa pasu baada ya talaka! Na talaka haiko mbali!

No wonder ni mroho wa chakula pia?

Kwanza huwa mnakula mezani nyie? Au mnajificha ficha tu na mabakuli ya mchuzi uvunguni?

Sent using Jamii Forums mobile app
Haaahaaa[emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole Sana..jitahidi ununue lako ili kuepuka hinda za shoga angu
 
Mimi ni mwanaume wa kawaida, nimejaaliwa kipato cha wastani tu kinachotokana na juhudi za kujihusisha na hiki na kile kwa kupitia kujiajiri.

Mke wangu pia ni mchakarikaji na anaitumikia biashara ya vyombo vya ndani na mapambo ya ndani ambayo kwa pamoja tuliifungua na inafanya vzr sana.

Tumejaaliwa kuwa na gari moja Suzuki modeli mpya ambayo kiukweli aliinunua yeye mwaka Jana January. Kwasasa mimi ni fundi wa mashine za aina mbalimbali ikiwemo majenereta, magreda, kreni n.k. Na kwa kuwa mishe zangu za kiufundi hazihusishi sana matumizi ya gari ya kutembelea kwahyo huwa naitumia mara chache sana.

Baada ya kumfundisha mkewangu kuendesha akawa nayo kuanzia hapo. Mie Nina pikipiki ambayo hunipeleka huku na kule na kunifanikishia mishughukiko yangu yote bila tashwishi . Ninapohitaji gari kwa ajili ya matumizi ya hapa na pale au ninapoonyesha dalili ya kwamba nitatumia gari siku hiyo, papo hapo mke wangu huanza kujiskia karaha na ataanza kuongea maneno ambayo yanatoa ishara kwamba hataki ntumie gari.

Ukweli sipendezwi na hali hiyo maana inaudhi sana. Kwakuwa nimeshamjulia huwa nampuuza afu nachukua gari naenda kwenye kusudi nililolenga lkn furaha yake hutoweka kwa siku hiyo na hukereka kiukweli. Ingawa mie ndo niliyemfundisha kuendesha lkn pia haniamini napoendesha gari na hapendi nimuendeshe na kila wakati anasikika akinikosoa ninapoendesha, yani huwa dereva namba moja wakati aliyeshika usukani ni mimi.

Na kwa vile ameshajua pia nampuuza katika hilo, mara nyingi mke wangu huamua kukaa siti ya nyuma kwa vile haamini udereva wangu na huona kama nitamsababishia ajali akikaa mbele.

Kwa ufupi hapendezwi ninvyoendesha gari na hili jambo linanikera sana.

NAOMBENI USHAURI WENU WA KUNIJENGA KTK HILI.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio lako nunua lako
 
Pole mkuu..hilo gari sio lake..yeye ni kivuli tu cha alionalo,atakua kuna mtu aliweka fungu lake kubwa ili amfanikishie anunue hilo gari ndo maana anaona jau ukiwa unataka kuliendesha usijepishana na mwenye nalo..yeye kukaa nyuma anahifia mkionwa pamoja..maana ukionwa wewe pekeako anaweza sema wewe ni mfanyakazi wao alikutuma..

Kama si hivyo nnavyofikiria tofauti na hapo huyo mwanamke ana roho ya uchoyo sana..


Sent using Jamii Forums mobile app
Kwel ..mkuu umegundua kitu...Ur genius.
 
Ila ukweli nime-date na wanawake nchi nyingi sijawahi ona wanawake vimeo kama wa Tanzania, sisemi wote wako hivyo ila wengi wana roho za ajabu ajabu, hivi maana ya kua in a relationship ni nini? Kama mmefika hatua hadi ya kuoana alafu gari tu kushare inakua kero basi ulikosea kuoa.

Rule ya relationship iko hivi, kuna giver and taker,
giver + giver = very good relationship (hii inadumu muda mrefu sana)
taker + giver = mwanzoni nzuri inafiika muda moja anakereka ni downhill from there
taker + taker = hii inadumu sanasana wiki moja tu, hawa labda wabaki kufanya one night stand tu au friends with benefits.

Sasa wewe nahisi moja ni taker na mwingine giver, mlianza vizuri ila hiyo relationship sasa itaanza kwenda chini daily, msipotambua tatizo lenu mapema na kujaribu kulisolve mmeumia. Mimi ni giver ila kabla sijaingia kwenye relationship yoyote I tend to be very picky sitaki wanawake vimeo, sitaki walioshika dini sana (sina muda wa kushare mapenzi na yesu mimi, nataka awe wangu tu), sitaki pia ambaye ni kilaza, kama anaamini 5g inaleta corona huyo hatuwezi kukaa kua na smart discussion, napenda kukaa kuongelea sayansi, future technologies kama artificial intelligence, biashara, vitu exciting exciting sio boring stories za leo diamond kavaa chupi nyekundu wtf?
 
Mpaka Sasa najiuliza uyo mkee wako Kwa nn akae nyuma ya gari.*unaibiwa mkuu..
 
4) Inawezekana wewe siyo handsome wa kula naye bata ndo maana anaona choo kuendeshwa na wewe mzee wa spana za mashine muda wote unanuka greese na oil chafu.
Kwel umeongea...mkuu.unajua kuchambua ..vitu..😂😂😂
 
Kitu nachokiona ni kwamba huyo mwanamke amekua katika mazingira ambayo hawakua na gari nyumbani kwao...ushamba ni mzigo sana..kama vipi lichukue siku halafu lipigishe mzinga...biashara iiishe
 
Mkuu unakosea Sana, yani umpe mke biashara aendeshe halafu usifuatilie mapato?
Wewe ndiye unapaswa uamue matumizi ya mapato sio yeye kujiamulia.
Leo amenunua gari kwa jina lake kesho atajenga nyumba kwa jina lake kitakachofuata hapo ndipo Utajua mke sio ndugu.
Eti kuna wanao mshauri anunue lake dah.
Kila kitu chake lazima kiwe chini yangu tofauti na hapo namuachia mji kabla hayaja nikuta makubwa
 
Sasa umesema gari lake na kanunua yeye, kwahiyo acha akusimange na wee upate morare ya kununua gari lako. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mkuu samahani,
Hakuna uwezekano wowote ule kata kidogo kuwa wewe ni dereva mbaya? Unaendesha gari na kujipachika njiani kama vile upo kwenye bodaboda??
Pili samahani tena, uchangia hela za service za hilo gari???
Tatu samahani tena sana, ukikuta mafuta yapo nusu tenki, ukapiga route zako ukarudi home gauge bado itasoma kwenye nusu, zaidi au pungufu?????
 
Nimejikuta nawachukia sana watu wanaotoa siri za wapenzi wao hadharani, hivi unadhani nani anajali? inatusaidia nini>? Jifunze kumheshimu mke au mume wako, social media kamwe haiwezi kukusaidia matatizo yako zaidi utaishia kupata we manbo. WE KAAA NA MAMBO YAKO YAKUUE SISI TUNAWEKA MEZANI YANAJADILIWA MUBASHARA MUJARAB..... yaaaninkupacha mtoto ni siri..... au Kunywimwa unyumba ni siri haya basi kashapata ushauri na maisha yanaendelea
 
Pole kijana ila maisha ndo yalivyo.
Wewe ulimfundisha kuendesha gari hukuchangia kununua gari kwahiyo uwe mpole mpaka utakaponunua gari lako apo mtakuwa salama.
Kuhusu kumpuuza huwezi kujua anakwazika kiasi gani na hajari haina kinga ipo siku utachukua gari akiwa hataki utalibamiza na uo ndio utakuwa mwisho wa ndoa yenu.
Je wakati anajiandaa kununua ulishirikishwa hatua zote?
Je una uhakika pesa alonunulia gari zilitokana na biashara yenu?
Ukinijibu nitaendelea kukushauri.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaha hizo para za mwisho sasa !!!😂 😂
 
Kuna mengi huyajui! Siyo kwamba ukiendesha anaogopa kuwa utamsababishia ajali bali anaona aibu kuwa na wewe kwenye gari ndiyo maana anakaa nyuma. Kwa kifupi anaona wewe siyo type yake kwa sasa. Mengi huyajui ila ngoja niishie hapo!
Exactly 100% ... Anaona kuwa jamaa anamjazia nzi tu 😂
 
Back
Top Bottom