Mke wangu hataki niendeshe gari alilonunua. Nakereka sana

Mke wangu hataki niendeshe gari alilonunua. Nakereka sana

Kosa number moja: ulikosea sana kujitenga na gari tangu hatua za mwanzoni kabisa, kwakuwa Mzee wa boda yeye kakushusha thamani yako
Ushauri wangu : gangamala ununue gari lingine hilo ndio liwe lako
Mimi ni mwanaume wa kawaida, nimejaaliwa kipato cha wastani tu kinachotokana na juhudi za kujihusisha na hiki na kile kwa kupitia kujiajiri.

Mke wangu pia ni mchakarikaji na anaitumikia biashara ya vyombo vya ndani na mapambo ya ndani ambayo kwa pamoja tuliifungua na inafanya vzr sana.

Tumejaaliwa kuwa na gari moja Suzuki modeli mpya ambayo kiukweli aliinunua yeye mwaka Jana January. Kwasasa mimi ni fundi wa mashine za aina mbalimbali ikiwemo majenereta, magreda, kreni n.k. Na kwa kuwa mishe zangu za kiufundi hazihusishi sana matumizi ya gari ya kutembelea kwahyo huwa naitumia mara chache sana.

Baada ya kumfundisha mkewangu kuendesha akawa nayo kuanzia hapo. Mie Nina pikipiki ambayo hunipeleka huku na kule na kunifanikishia mishughukiko yangu yote bila tashwishi . Ninapohitaji gari kwa ajili ya matumizi ya hapa na pale au ninapoonyesha dalili ya kwamba nitatumia gari siku hiyo, papo hapo mke wangu huanza kujiskia karaha na ataanza kuongea maneno ambayo yanatoa ishara kwamba hataki ntumie gari.

Ukweli sipendezwi na hali hiyo maana inaudhi sana. Kwakuwa nimeshamjulia huwa nampuuza afu nachukua gari naenda kwenye kusudi nililolenga lkn furaha yake hutoweka kwa siku hiyo na hukereka kiukweli. Ingawa mie ndo niliyemfundisha kuendesha lkn pia haniamini napoendesha gari na hapendi nimuendeshe na kila wakati anasikika akinikosoa ninapoendesha, yani huwa dereva namba moja wakati aliyeshika usukani ni mimi.

Na kwa vile ameshajua pia nampuuza katika hilo, mara nyingi mke wangu huamua kukaa siti ya nyuma kwa vile haamini udereva wangu na huona kama nitamsababishia ajali akikaa mbele.

Kwa ufupi hapendezwi ninvyoendesha gari na hili jambo linanikera sana.

NAOMBENI USHAURI WENU WA KUNIJENGA KTK HILI.

Sent using Jamii Forums mobile app

Jr[emoji769]
 
Mkuu wangu, kila hatua alinihusisha na ninataka nikuhakikishie kwamba pesa za manunuzi zilitokana na biashara na hiyo biashara ni yetu. Naiita ni yetu kwa mantiki mimi ndiye mtoa mtaji kwa 100% na nikamkabidhi kama ajira yake lkn kitega uchumi cha familia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu unakosea Sana, yani umpe mke biashara aendeshe halafu usifuatilie mapato?
Wewe ndiye unapaswa uamue matumizi ya mapato sio yeye kujiamulia.
Leo amenunua gari kwa jina lake kesho atajenga nyumba kwa jina lake kitakachofuata hapo ndipo Utajua mke sio ndugu.
 
Yaani umewaza kama mimi!!
Pole mkuu..hilo gari sio lake..yeye ni kivuli tu cha alionalo,atakua kuna mtu aliweka fungu lake kubwa ili amfanikishie anunue hilo gari ndo maana anaona jau ukiwa unataka kuliendesha usijepishana na mwenye nalo..yeye kukaa nyuma anahifia mkionwa pamoja..maana ukionwa wewe pekeako anaweza sema wewe ni mfanyakazi wao alikutuma..

Kama si hivyo nnavyofikiria tofauti na hapo huyo mwanamke ana roho ya uchoyo sana..


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Achana na Gari yake, ww fanya safar zako bila gari yake ila hakikisha ukirudi sifia Demu aliekupa lift kuwa ana roho ya huruma na ubinadam sana.

Wakati mwingine mwambie kuna rafiki ako wa kike atakuazima gar yake ili yeye asikose kitoka na gari yake
Hahaha unataka mkewe avimbe na kupasuka kwa kihoro cha wivu?
Hivi hapo atakuwa anajenga au anazidisha ufa?
 
Wanawake wana mambo mengi,, ukute hapo alishajitapa kwa marafiki zake kuwa hilo gari wewe huligusi kwani shughuli zako zinakamilishwa na hiyo bodaboda yako.

Sa siku ukiligusa ni kama vile mashostito wake humsuta kimoyomoyo.
Mshauri apunguze misifa isiyo na maana kwa mashost wake(nafikiri tu kama ndo chanzo)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimejikuta nawachukia sana watu wanaotoa siri za wapenzi wao hadharani, hivi unadhani nani anajali? inatusaidia nini>? Jifunze kumheshimu mke au mume wako, social media kamwe haiwezi kukusaidia matatizo yako zaidi utaishia kupata majanga zaidi
Kwani huyu jamaa unamfahamu yeye na mkewe?Au unaongelea wale unaowafahamu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana..
Achana na hiyo gari, vaa uso wa mbuzi deal na mambo yako!
 
Mkuu wangu, kila hatua alinihusisha na ninataka nikuhakikishie kwamba pesa za manunuzi zilitokana na biashara na hiyo biashara ni yetu. Naiita ni yetu kwa mantiki mimi ndiye mtoa mtaji kwa 100% na nikamkabidhi kama ajira yake lkn kitega uchumi cha familia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi nilichoona

Mke si kwamba hapendi utumie gari ila hapendi uendeshaji wako, yawezekana u rough rider...unaendesha hovyohovyo kiasi kwamba mke ana hofu na gari kuharibika na kupata ajali. Au ushagongwagongwa huko.

Cha kufanya kila unapolihitaji kama inawezekana mwombe akuendeshe na hata mnapotoka wote mwachie aendeshe kwani yakugharimu nini?

Au badilisha uendeshaji wako. Endesha kwa ustaarabu, acha kushindana na kulumbana na madereva barabarani, wapishe wapite.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna jingine umetuficha, wanawake tu napenda sifa, yaani mwanaume akikuendesha mkashuka sehemu raha sana, mkeo ana shida gani ulotuficha?

Ishiiiiii kwani yeye nani? Mwachie gari lake tumia pikipiki yako, hata kama mnaenda sehemu mwambie atangulie

Usihusike sijui mafuta,sijui service, jifanye hulioni gari lake. Uje utupe mrejesho.
 
Nimejikuta nawachukia sana watu wanaotoa siri za wapenzi wao hadharani, hivi unadhani nani anajali? inatusaidia nini>? Jifunze kumheshimu mke au mume wako, social media kamwe haiwezi kukusaidia matatizo yako zaidi utaishia kupata majanga zaidi
Wewe unawafahamu mleta uzi na mke we?
Kwa taarifa yako ni mara 100 uombe ushauri hapa kuliko kuomba hukoo kitaa maana inakuwa unajichoresha. Kuna vitu inakuwa ngumu kuomba ushauri huko kitaa lakini huku ni possible.

God save us
 
Mkuu unakosea Sana, yani umpe mke biashara aendeshe halafu usifuatilie mapato?
Wewe ndiye unapaswa uamue matumizi ya mapato sio yeye kujiamulia.
Leo amenunua gari kwa jina lake kesho atajenga nyumba kwa jina lake kitakachofuata hapo ndipo Utajua mke sio ndugu.
Huyu mwamba amechemka sana.
 
Kama wewe ndiye ulitoa mtaji kwa 100% na una uhakika hilo gari lilinunuliwa kwa pesa za biashara hiyo kwa nini uliite gari lake? Yawezekana ndoa yenu ipo ktk mfumo jike au kuna kitu unatuficha. Hilo gari litakuvunjia ndoa pambana umueleke mkeo ajue namna anavyokukosea na unavyojisikia. Ikishindikana pambana gari liuzwe aidha mbaki bila gari au linunuliwe lingine ambalo litakuwa la baba anayemwachia gari mkewe

Ila nahisi unatudanganya kwenye hii stori yako. Hivi kweli wewe ndiye uliyemfundisha kuendesha gari hadi akajua halafu sahzi hakuamini ukimuendesha hadi anakaa siti ya nyuma!? Ha ha ha ha hii chaiiiiii!!!!
 
Mimi ni mwanaume wa kawaida, nimejaaliwa kipato cha wastani tu kinachotokana na juhudi za kujihusisha na hiki na kile kwa kupitia kujiajiri.

Mke wangu pia ni mchakarikaji na anaitumikia biashara ya vyombo vya ndani na mapambo ya ndani ambayo kwa pamoja tuliifungua na inafanya vzr sana.

Tumejaaliwa kuwa na gari moja Suzuki modeli mpya ambayo kiukweli aliinunua yeye mwaka Jana January. Kwasasa mimi ni fundi wa mashine za aina mbalimbali ikiwemo majenereta, magreda, kreni n.k. Na kwa kuwa mishe zangu za kiufundi hazihusishi sana matumizi ya gari ya kutembelea kwahyo huwa naitumia mara chache sana.

Baada ya kumfundisha mkewangu kuendesha akawa nayo kuanzia hapo. Mie Nina pikipiki ambayo hunipeleka huku na kule na kunifanikishia mishughukiko yangu yote bila tashwishi . Ninapohitaji gari kwa ajili ya matumizi ya hapa na pale au ninapoonyesha dalili ya kwamba nitatumia gari siku hiyo, papo hapo mke wangu huanza kujiskia karaha na ataanza kuongea maneno ambayo yanatoa ishara kwamba hataki ntumie gari.

Ukweli sipendezwi na hali hiyo maana inaudhi sana. Kwakuwa nimeshamjulia huwa nampuuza afu nachukua gari naenda kwenye kusudi nililolenga lkn furaha yake hutoweka kwa siku hiyo na hukereka kiukweli. Ingawa mie ndo niliyemfundisha kuendesha lkn pia haniamini napoendesha gari na hapendi nimuendeshe na kila wakati anasikika akinikosoa ninapoendesha, yani huwa dereva namba moja wakati aliyeshika usukani ni mimi.

Na kwa vile ameshajua pia nampuuza katika hilo, mara nyingi mke wangu huamua kukaa siti ya nyuma kwa vile haamini udereva wangu na huona kama nitamsababishia ajali akikaa mbele.

Kwa ufupi hapendezwi ninvyoendesha gari na hili jambo linanikera sana.

NAOMBENI USHAURI WENU WA KUNIJENGA KTK HILI.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo gari NI kifuta jasho baaada ya kutumikia kazi Fulani akiwa kama alivyozaliwa kuwa makini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una mdogo wako wa kike ambaye bado hajaolewa??? Maana umeandika material ambayo mke anapaswa kua nayo,nahisi hata mdogo wake atakua hivi hivi
Pole Sana Kaka. Pole Sana kwa mkeo kuwa KERO. Wanawake wenzangu tubadilike jamani. Mume wangu siku anataka kutumia gari.... Namuomba mapema kabisa anipeleke usafiri wa bajaji unapopatikana..... naendelea na ratiba zangu kama kawaida. Nikimaliza narudi nyumbani.... Raha mustarehe... Mapenzi Mubashara[emoji23][emoji28]. Mapenzi yana Raha Sana Wanawake wenzangu ... Haya Mambo madogo madogo haya tujifunze kuya-ignore. Tujifunze kujishusha kwenye baadhi ya mambo ambayo tunaweza kufanya na hayasumbui sana.... Kwani utapungukiwa nini .... Pia Tunapunguza mikwaruzano inayoweza kuepukika. Gari zipo tuu. Cha muhimu Penzi na Raha ya MUME.

Sent using, Mashikoro Mageni
 
Fanya kitu kimoja jizuie kabisa kuanzia leo kupanda gari ilo mkitaka kwenda maali tafuta gari kwa rafiki ili uokoe ndoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huko ni kuokoa ndoa gani wataishi hivyo mpaka lini? Amani kwake itakuwepo daima? Wauze hilo gari linunuliwe lingine liwe chini ya mume halafu awe anamwachia mkewe,siku akilihitaji anachukua na kutumia. Au wabaki bila gari mana muda si mrefu ataanza kuambiwa unajua pesa ya kununua hili gari ilivyopatikana?
 
Back
Top Bottom