Mke wangu kaniambia nimwandikie kurasa ishirini za sababu kwanini mpaka sasa nimeshindwa kununua gari

Mke wangu kaniambia nimwandikie kurasa ishirini za sababu kwanini mpaka sasa nimeshindwa kununua gari

Ko amesema amakalili vituo vya daladala kama konda sindio
 
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Mtafaruku ni Mkubwa. Huu mwaka naona unaisha vibaya Mno. Kama sitakuwa macho nyumba yangu inaweza kuvunjika.

Sorry nianze kwa Salamu maana Leo mtanifaa Sana kwa ushauri Bora.

Assalam alyekum kwa Waislam,
Tumsifu Yesu Kristo kwa Waislam.
Wapagani, salama!!

Nimeoa Miaka tisa iliyopita. Nimejaliwa watoto wawili sasa.
Juzi familia yangu ilipata mualiko kwenda kwenye sherehe ya harusi ambayo ukumbi ulikuwa kwenye Moja ya visiwa vilivyoko bahari ya Hindi karibu na Jiji la Dar.

Basi huko mambo yalienda vizuri kwa upande wangu lakini nilishangaa kuona mke wangu Akiwa Hana furaha.
Sikumzingatia Sana ili asijeiharibu furaha yangu nikiwa nimepanga kumuuliza tukiwa tumerudi nyumbani.

Kufika nyumba, mwanamke amevuta mdomo kama kang'atwa na Nyigu. Kulikoni Mke wangu. Ndipo akaanza kushusha risala ndefu yenye shutuma, lawama na kejeli.

Nilinangwa!

Nilikaangwa!

Oooh! Miaka yote tisa tunapanda Daladala Mpaka tumekariri vituo kama Makonda wa Daladala.

Miaka tisa yote nimevumilia.

Watoto wadogo kina Chief Godlove wamezuka huko wanakupiga bao kama mjingamjinga.

Nikasema kimoyomoyo. toba! Nimekuwa mjinga tena.

Hivi gari la Milioni Saba tuu hata kama ni used umekosa?
Hata kama ni mkwechemkweche gari ni gari.

Alafu unajiita Taikon, taikon gani.
Nitakupeleka kwa Kina Mwamposa wakupe Upako wa Gari.
Nikasema mmmh! Yamefikia huko.

Akaendelea;
Mimi kukupenda usichukulie kama udhaifu wa KUFIKIRI sipendi maisha mazuri. Nataka maisha mazuri Mimi. Nimechoka Baby T kukimbizana na Daladala.

Mambo ya kunukishana mijasho na kubambiwa sitaki.

"Eeeh! Aaa mke wangu Maneno gani tena hayo" nikasema.

Wewe unafikiri mbanano ule wa Daladala nitaachwa kubambiwa na kunukishwa mijasho?
Nikasema, aaaah!

Akaendelea;
Wewe si bingwa wa kuandika mamakala mrefu huko Mitandaoni ambayo hayakuingizii chochote. Alafu unanikeraga Sana.

Sasa niandikie kurasa ishirini za sababu zilizokufanya ushindwe Kununua gari tangu unioe huu mwaka wa Tisa.
Ziwe sababu zilizoshiba.

Akaenda bafuni akiniacha nimetekewa. Alaaah!

Sasa Mimi nitaandika nini jamani!
Yaani hapa kichwa kimefura sijui niandike nini.
Pointi haziji.

Naombeni ushauri. Wenye matusi Leo sitayajibu. Siwezi jibu matusi wakati ndoa yangu IPO taabani .

Leo sipumziki.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Andika tu sababu moja

"Sababu nna mwanamke mwenye nuksi/gundu kwani wanawake wenye nyota husaidia ktk kusafisha njia ya mafanikio, akikujibu nko palee

Ujue wanaume tunapambana sana kuhakikisha familia haiteteleki, sometimes magari tunayaweka pembeni ili kupisha mambo ya msingi zaid, kwani gari si assets bali liability, gari hutoa pesa mfukoni wakati asset inapaswa kuleta pesa mfukoni

Kama ataendeleza kelele piga makofi aende kwao akalete sample ya gari ambalo babaake alinunua
 
Andika tu sababu moja

"Sababu nna mwanamke mwenye nuksi/gundu kwani wanawake wenye nyota husaidia ktk kusafisha njia ya mafanikio, akikujibu nko palee

Ujue wanaume tunapambana sana kuhakikisha familia haiteteleki, sometimes magari tunayaweka pembeni ili kupisha mambo ya msingi zaid, kwani gari si assets bali liability, gari hutoa pesa mfukoni wakati asset inapaswa kuleta pesa mfukoni

Kama ataendeleza kelele piga makofi aende kwao akalete sample ya gari ambalo babaake alinunua

😀😀

Mkuu hii ni Njia ya HEKIMA kweli. Mimi nataka mambo yakae Sawa sio kuchochea huu mgogoro
 
Inawezekana shida ni yeye,nyota yake haiko vizuri ndio maana unashindwa kumiliki gari.Mkiwa kwenye ndoa nyota zenu ziking'aa kila kitu kinafunguka....
 
Kijana nani mwanaume humo kwenye hiyo nyumba mnayoishi.

Huyo mwamamke anakupima uthabiti na uwezo wako wa kummudu.Hii inaashiria umeanza kuwa msoft soft na mkeo ameanza kuota pembe.

Leo anataka gari kesho atakuja na takwa la kutaka kulala gorofani atakwambia amekuvumilia miaka 9 yote mnalala kwenye kakibanda chenu anataka gorofa kama la dj Ali B au Mwijaku.

Rudi kwenye uanaume acha kuwa soft soft kuna siku atakwambia anataka mwanaume mwenye kitambi😄😄😄 wanawake sio wa kuwasikiliza kama usingeweza kumsikiliza mtoto wa miaka 5 akitoa demand zake zisizo na mashiko vivyo hivyo hupaswi kumzingatia huyo mwanamke.

Yamkini unashida sana nyumbani ameanza kukuona kama shoga yake. Potea hapo nyumbani don't be available kirahisi rahisi.

Nauhakika huyo binti kwao babake hana hata stalet, akizingua mlambe makofi afunge virago aende kwao akaendeshwe na dereva wa babake, pumbavu kabisa.

Mwisho kabisa nimeona jina hapo la yule SCAMMER wa Kawe, hiyo ni red flag 🚩🚩🚩,huko Kawe wanaenda mazombie piga MARUFUKU mara moja!!!


#KATAA NDOA 3-0 WENYE NDOA BILA MKWANJA😄😄😄

Kijana kama hujajipata kataa ndoa, hakuna mwanamke mwenye huruma na wewe, ndoa ni biashara yenye faida kiduchu kwa mwanaume.

#kataa ndoa, ndoa ni utapeli.Afya ya akili ni muhimu kwa maisha yako!!!
 
Kwanza ni kweli huna gari au ni makala ya kusadikika?
 
Huyo mwanamke alitakiwa kwanza ampe baba yake, kaka zake, baba zake wadogo na wakubwa na wajomba zake hilo zoezi la kuandika kurasa 20 kwa nini mpaka sasa wameshindwa kununua magari

Mwanamke masikini amlaumu sana baba yake mzazi kwa kushindwa kumtengenezea maisha mpaka anakuja kusumbua vijana ambao bado wanapambana.

Angekuwa anajiweza angenunua gari lake kwa matumizi yake. Kuoa wanawake waliotokea familia masikini ni changamoto sana

Kwa saikolojia ya wanawake huyo mke wa mtibeli atakuwa ameshaanza kutoa mzigo kwa wenye magari
 
Back
Top Bottom