Mkopo alioutoa Madaraka Nyerere wamuhamisha mtu nchi

Hizi siasa zetu hizi 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂
 
Ukoo una watu wana vituko sana
 
Binadamu hamna jema, Hii famiia wangekwa wanamiliki Mabenki Nchi hii (angetaka asingesindwa) pia msingekosa la kusema na kuwatukana kila kukicha.

Hivi hao Mafisadi kwani wao hawana jukumu la kuona wanachofanya sio sawa mpaka wangeambiwa na Mwalimu?.

Ok basi Mwalimu yeye alicheza part yake iliyokuwa ndani ya uwezo wake, wewe ume/unafanya nini kuweka mambo sawa?.
 
Hao hamna kitu mzee mwenyewe alishaona hata akiwaachia mabenki hakuna watakachofanya zaidi ya ulevi tu Hadi wajukuu ni hewa tupu wanaishiaga kuvurumishiana ngumi pale msasani walinzi ndio wanawatenganisha wasipigane.

Hakuna kitu hao yaani hata baba yao alijua hamna kitu, we unadhani watawala waliofuata wameshindwa kuwapa vyeo? Yaani mtoto wa Mwinyi awe Rais wa Nyerere asiwe? Kwamba hata kama baba yao hakuwapa maisha Ina maana wao hawatamani hata mmoja awe Waziri au hata Makamu wa Rais?

Watoto wa Kawawa wapo kwenye system hao wa Nyerere wanazubaa tu hata kwenye kura za wajumbe hawakubaliki Yani infact hao ni hewa tupu hawabebeki na ndio maana tunawalisha tu na vimisaada vya hapa na pale kuhakikisha hawapati vichaa.

Tena afadhali hata huyu Madaraka kidogo ana akili kushinda hata yule RC chapombe. Hawa watu hawabebeki taia limejaribu sana kuwabeba Ila ndio wameishia na njia zao jiulize watoto wa viongozi wote wanapewaga michongo mirefu Hawa wenzetu mbona kimya? Basi hata wapige mabiashara kwa kutumia connection za jina la baba yao wangekuwa hata na biashara ubia mkubwa sana pale TBL Ila wao ni kukimbilia Ulaya kusoma visivyoeleweka na kurudi kulewa tu.
 
Duh.
 
Mkuu Bujibuji Simba Nyanaume , naomba umtendee haki Madaraka, usimuaibishe ikaeonekana sasa na yeye akili zake zimeanza kuwa kama za kaka yake Andrew!. Kama kaka yao mkubwa Magige ni issue excuse ikawa ni alikuwa jeshini kikosi cha mizinga na alipigana Vita vya Kagera, hivyo zile kelele za mizinga ndio sababu. Mako, tulikuwa tunakesha nae night clubs hadi majongoo, ni kukata maji na naniliu. Mtoto mtulivu wa Mwalimu ni Madaraka, Anna na Pauleta, sasa kitendo cha kuileta hii humu, unamaanisha na Madaraka nae... Oh please not!.
P
 
Walipe hela ya watu mzee. Hao watu wameendekeza kubebwabebwa tu.
 
Tuliokua na kumfahamu vyema Mwalimu, angekuita malaya!
 
Walipe hela ya watu mzee. Hao watu wameendekeza kubebwabebwa tu.
Yes siku zote, dawa ya deni ni kulipa, kwa vile Madaraka Nyerere ni mtoto wa Mwalimu Nyerere, na Mwalimu alichukia rushwa, hivyo it is expected Madaraka hawezi kutoa rushwa yoyote.

Kilichotokea ambacho Madaraka hakukisema, ni baada ya kujaza fomu kuomba ubunge, mmoja wa wajumbe akamfuata na kumweleza ukweli wa mambo kuwa bila kunyoosha mkono, kutoa kidogo dogo, huwezi kupita, hivyo Madaraka akauliza kama kiasi gani kwa mjumbe, jamaa akamjibu 50,000. Madaraka akakubali na kumpa 50,000 ili ateuliwe, ila akamwambia, usipoteuliwa nitakurudishia.

Kitu ambacho Madaraka hakujua, ni hiyo 50,000 ni kwa kila mjumbe!. Yeye katoa kwa mtu mmoja tuu!. Matokeo yake ni moja ya zile kura mbili ndio 50,000 yake!. Hiki ni kiendacho kwa mganga!.
Madaraka hakutakiwa hata kulisemea hili!.

Jimbo la Kawe kuna watu wametoa hadi 500,000 kwa kila mjumbe!. Wajumbe wako 400!.
Kuna mtu namfahamu, katoa TZS 10,000,000 kila kata, Kawe ina kata 10, kaambulia kura 1!. Alipouliza vipi, akaambia wewe unatoa kwenye kata, wenzio wanawawekea watu mifukoni!.
Yaani Madaraka ni mtu wa kuilizia hiyo 50,000 wakati ndio kiwango cha short time mitaa fulani!.
P
 
Anataka style ya Nyerere usawa huu aisee? Wao wameishi vizuri bana hatufanani nao hata kama ni watoto wa mchonga Ila huwezi kumfananisha na akina sisi aisee.

Mchonga alikosea sana kuiacha nchi ikiwa masikini ndio maana watu walideviate Ile siasa yake sababu ikionekana haijatusaidia kitu kwa miaka zaidi ya 30 .

Rushwa akageuka kuwa rafiki wa watu sio adui wa watu, naamini leo Nyerere angekuwepo na akagombea asingetoa rushwa asingepata kura hata moja Kama mwanae maana yeye ndio ametuleta huku kwenye Lindi la umasikini.

Unajua alipochukua nchi na tukiwa wachanga alijiingiza kwenye mambo mengi mno na mengi hayakuwa na msingi wowote alikuwa na haraka sana tofauti yake na Magufuli ni kwamba yeye alijaaliwa busara huyu mwingine alikuwa mwehu.

Nyerere laiti angestick kwenye siasa za kiafrika na kuhakikisha hajufungamani na wazungu Wala yellow kwa maana ya China and the likes of communists tungekuwa na style yetu ambayo nkrumah na Gaddafi waliitaka tatizo nae alikuwa anataka kuonekana ni alpha male kwenye duru za siasa za kimataifa.

Matokeo ya haya yote akatuacha tukiwa masikini mafundi nguo kazi kubwa ilikuwa kushona viraka badala ya kushona nguo, Fundi viatu ilikuwa kazi kubwa ni kushona viatu vilivyochanika na kuweka viraka ai patex kuvundisha viatu. Fundi baiskeli ilikuwa kazi ni kuziba pancha tu.

Huo no uchumi uliokuwa umekufa kabisa. Leo hii huwezi kuniambia nimchukue mtoto wa Nyerere nimpe uongozi anaweza kurudisha dogma za kipumbavu katika Karne hii. Watu wameshabadilika ndio wafahamu kwamba money talks baba yao ametusaidia kuongoza taifa and we thank him for that but we won't take a chance again.

Alidhani kuitwa Nyerere inamsaidia???? Watoe hela maana wamekula Kodi zetu sana. Na ulisema watu waliolikomboa taifa tuwataje hapa hao watoto wa Nyerere wanaweza kujikuta wao wameishi vizuri mno sisi wengine mababu zetu walipigania uhuru lakini hawakukumbukwa hata kwa shati au ndala. Ila tukaishi na tupo tu maisha yanasonga Ila wao wameishi vizuri sana na ulevi wakaupatia humo.
 

Wabongo mna shida sana, yani nyinyi munaona ili uwe na maisha mazuri uwe mwizi tu au?

Nyerere alikua President kwa miaka zaidi ya 20, siamini katika kipindi cha utawala wake kuna mtu ambaye alikua na mshahara na posho kubwa zaidi yake yeye kwenye hii nchi. Swali ni alijiengezaje katika kuboresha familia yake? hapo ndipo penye swali kuu.
 

Mkuu wewe ni huyo aliotoa laki 5 kwa kichwa au 10m kwa kata ?
 
Viongozi waliofuata baada ya Nyerere,wanaonyesha dunia na walimwengu kua alikosea kutowaandaa watoto wake,leo akina Rizione,mtoto wa Pinda,Mwinyi,Nape na wengine,wanakula maisha.Mzee kama anaangalia huko aliko,sijui atakua anajionaje?
Inauma sana watoto wamebaki kulewalewa na wengine kama wana msongo wa mawazo,huku mzee alikua mtu mkubwa,ni fedheha kwakweli.
 
Sanji
Sajini alimwaga pesa akuchukua jimbo kuwa ubunge. Leo ni naibu waziri wa mambo ya ndani. Nani atakemea rushwa huko jeshi la polisi?
 
Madaraka ni Public figure, kauli yake yoyote inahamasisha kumsikiliza. Kumuona kuwa dish limeyumba, huo utakuwa ni mtizamo wa msikilizaji mwenyewe.
All in all Madaraka alikuwa anachangamsha kijiwe
 
Huo ukoo vichwa vimepata moto sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…