Mkutano maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa na wadau wa Demokrasia tarehe 04 Januari 2024

Naamini kabla ya wabunge kwenda kujadiliana. Naamini Waziri atayachukua na kuyafanyia kazi.
 
Jenista Muhagama anaongea sasa.....
 
Wajumbe wa Baraza waliniita jana kuwa mimi ni Mama Ufunguo.
Kuna mwakilishi wa Diaspora yupo hapa naomba asimame. Tunaomba mchango wenu mnaweza kuuwasilisha hata kwa maandishi.

Naomba Mkuu wa Mkoa Atusalimie. Maana mkutano huu umewanufaisha wana Dar es salaam.
 
Mkuu wa Mkoa:
Wakati najiunga nachuo kikuu cha Dar niliamua Nisome Political Science and Languages. Kwa sababu niliona mabishano ya wabunge wakibishana. Nakabla ya kujiunga nilihamasishwa na Gollan.

Kama watu wanaweza kubishana na kuwa common understanding niliona kitu kinachowafanya wafanye hivyo ni Lugha nikaona nisome Lugha.

Jambo hili mlilolifanya mmefanya kubwa sana.
Mh. Rais ametumia power na kuwaweka hapa ili mpate common Understanding
 
Wamesombwa , wapige picha, leo leo usiku MABEBERU wanatumiwa ili wachie MIKOPO ya muda mrefu.
 
Jenista Muhagama Anaendelea..
Maelezo yangu mafupi sana.
Anaeleza kuwa Serikali imekuja hapa kusikiliza kama alivyotuagiza Mh. Rais kuwa na masikio marefu.
 
Lengo la mkutano huu maalum. Limeelezwa vizuri sana na Jaji Mtungi. Ilikuwa ni kukusanya watu wengi iwezekanavyo ili watoe mapendekezo yao.
Tumekuwepo hapa kama waalikwa. Lakini wenye mkutano huu ni Baraza la vyama vya Siasa.
Tutaendelea kuwaunga mkono kama serikali.

Chimbuko la miswada hii ni zile R4 za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Majadiliano yaliyofanyika hapa jana na leo yanayo akisi maono ya 4R za Rais. Inatakiwa sasa zifundishwe kwa watanzania wote.
Jambo hili limejitokeza sana katika siku hizi mbili. Ni muhimu kuongeza nguvu ili watanzania wote waweze kuzielewa
 
Falsafa hii ya 4R imeleta uchochezi wa mabadiliko. Utekelezaji wa maoni ya kikosi kazi, tutakuwa tunatoa hatua iliyofanyika kila tutakapokuwa tunakutana na baraza.

Tunakuahidi mgeni rasimi kuwa tutakuwa wasikivu katika maoni yanayotolewa na watanzania.
 
Mgeni Rasmi anakaribishwa sasa....
 
Mgeni Rasmi;
Naanza kwa kumshukuru Mungu kutuwezesha kukutana na kujadili mambo haya. Nawatakia Heri ya mwaka mpya.
Nakupongeza mwenyekiti wa mkutano huu.
Nalipongeza Baraza la vyama vya siasa.

Niseme hakuna kazi rahisi kama kufunga mkutano.
 
NInamshukuru Mh. Rais Samia kwa kuimarisha Demokrasia.
Nimejulishwa kuwa mkutano huu umekuwa wenye tija. Nadhani kabisa wadau wameweza kutoa maoni yao mbalimbali
Na yale yatakayosemwa hapa Serikali hana majibu.
Spika wa bunge amealika wadau mbalimbali kwenda pale Dodoma kwenda kutoa maoni yetu
 
Naomba niwashukuru wote waliotoa maoni yao.
Nimeelezwa kuwa mmejadiliana kwa uungwana. Hata aliyejadili nje ya mada amevumiliwa. Tunaudhaifu mkubwa katika zama hizi badala ya kujadili mada tunajadili watu. Na mwisho tunakuwa hatuna suluhu.
Lakini mkutano huu haukuwa wa namna hiyo. Kwamba wa chama fulani anamawazo mazuri ya mtu mwingine.

Imani yangu kwa yale mliyojadiliana itakuwa maridhiano
 
Mgeni rasmi ni nani?
 
Sheria zipo kwaajili yetu siyo sisi kwaajili ya sheria. Kama kuna changamoto katika sheria Rais anasisitiza tukae tuweze kuzungumza.

Bungeni kuna kamati watasikiliza maoni yenu.
Nimalize kwa kuwapongeza sana sana.
Mmechukuwa Space yote katika nchi hii.
Ngoja nimalize sasa maana kunahatari sana kuzungumza na watu wanaojua kuzungumza.

Ili uweze kuwapata watu. Nenda kwenye timu ya watu ambayo ina watu. Wafuate hao wanaoaminika uzungumze nao. Utapata platform ya kuzungumza na kusikilizwa
 
Sema kazi yenu ni kuongeza idadi ya Wanawake kwenye ngazi za juu ili mtawale nchi vizuri kama ilivyo Rwanda na Uganda.
 
Bwana Hashim endelea ili tupate mwafaka sahihi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…