Elections 2010 Mkutano Wa Hadhara Wa Wana-JF [Online]

Elections 2010 Mkutano Wa Hadhara Wa Wana-JF [Online]

Health Insurance ndio priority kwangu.
Maisha ya watanzania ni magumu. Hela za kulipia hospitali kila tunapougua hatuna. Serikali iboreshe sector ya afya na kuanzisha bima ya afya. Hata kama itaendelea kutoa huduma duni, lakini tuwe na uhakika wa kutibiwa. Hichi ni kitu cha msingi sana kama serikali inania ya dhati kuwakomboa wananchi wake.

Kuongeza wigo wa mapato na kudhibiti matumizi.
Nimefurahi kuanzishwa kwa zile cash register ambazo wauzaji hawawezi kukwepa kodi. Ubunifu wa aina hiyo ndo unahitajika continuously pale TRA. sio kila siku kuongeza kodi kwenye soda, bia na sigara.

Tatizo la serikali ni kwenye matumizi. Vitu vinavyofanyika serikalini havina value for money.
Kama mimi ndo ningekuwa Rais; ningeongeza mishahara ya wafanyakazi wote serikali
kima cha chini 1mil, watakaoa kuwa kwenye managerial levels, kima cha chini 2mil depending na sector.


Kwanini niongeze mishahara kiasi hicho?
  • Kupanua wigo wa kodi
  • Kuyaongezea uwezo mashirika kama NSSF, PSPF, PPF yaweze kufanya kazi za maendeleo zaidi kwasababu yana usimamizi mzuri. Hii itatokana na michango ya wanachama. Tunajua ni jinsi haya mashirika yanavyotumika kuleta maendeleo kila sehemu ya dunia.
  • Kuboresha maisha watanzania
  • Kupunguza uombaji wa rushwa kwa wafanyakazi wa serikalini
  • Ku-attract talented individuals wajitokeze kuifanyia kazi nchi yao
Huu mshahara utakuja na machungu yake
  • Kufuta allowances zote za vikao, ili watu wakae ofisini kufanya kazi
  • Kununua magari yasiyozidi CC 2500 kwa watumishi wote wa serikali wanapohitaji kuwa na magari ya serikali
  • Kufuta marupurupu ya safari za nje - ambapo mfanyakazi yeyote wa serikalini mpaka kufikia level flani, akisafiri nje ya nchi, tulipa gharama zake based on actual cost. Akiwa anafanya retirement aambatinishe na vithibitsho ya fedha aliyotumia inayobaki anarudisha hazina. Hiyo itapunguza sana demand ya USD. Safari za ndani zitaendelea kuwa na allowances kwasababu zinatija
Elimu ya bure mpaka kidato cha nne

Tunahitaji mabadiliko makubwa sana katika sector ya elimu. Walimu ndo wanatakiwa wawe watu wanaolipwa vizuri kuliko wafanyakazi wa maofisini. Ila hayo malipo mazuri yaanze baada ya mabadiliko yafuatayo
  • Walimu wachaguliwe kutoka wanafunzi waliofauru vizuri na sio failures: Huwezi kumchukua mwanafunzi aliye fail F4 akapata course ya miezi 3 aje kufundisha ukitegemea utapata taifa lenye watu wasomi na wenye uwezo mkubwa wa kufikiri. Tunaiua nchi yetu bila wenyewe kujua
  • Upimaji wa ubora waalimu uwe unafanyika, na ndio kiwe kigezo cha malipo. Sio shule kila siku inakuwa imejaza Div 4 halafu mwalimua wa hiyo shule awe analipwa sawa na anafaulisha vizuri.
Ubora wa elimu ni kitu tunachokiangalia juu juu sana, ila miaka kumi mbele hili litakuwa tatizo kubwa sana kwa taifa letu.

Kwa ufupi mambo makuu matatu ambayo ntapenda Kiongozi atakae ingia madarakani ayasimamie ni
Healthy Insurance
Ukusanyaji na usimamizi madhubuti wa matumizi ya serikali
ELimu ya bure ambayo ni bora kwa watanzania wote kuanzia shule za awali mpaka kidato cha 4
 
Aisee . . . Nimerudi sasa . . . Wakati tunapitia hoja zilizotolewa naomba wafuatao waje jukwaani kutoa maoni yao:
Msanii
Jile79
Njaa
Dark City
Eeka Mangi
Butterfly
jethro
Mburahati
safina
Xuma
Ambassador
Mr. Zero
Chesty
ThinkPad
Mujuni2
mlachake
Ahsante Mwenyekiti kwa rukhsa yako.
Ninapendekeza kwa serikali mpya kwamba, viongozi wa serikali hasa mawaziri watakapotoa taarifa zisizo za kweli iwe BUNGENI au popote pale wawajibishwe kwa manufaa ya UMMA.
Pili, ieleweke kwamba waziri au mwanasiasa yeyote anayeingia kutumikia umma kwa cheo chochote avuliwe madaraka yake kwenye Chama (chochote kile) ili kuwepo na uwajibikaji na kujituma kwa uadilifu.
Tatu, serikali mpya ifilisi mali za wooote waliokwiba mali za umma.
Nne, serikali iboreshe elimu kwa kuwaongezea mshahara walimu na wanaohitimu na kupata daraja la juu ndio wapelekwe ama waruhusiwe kujiunga na vyuo vya ualimu.
Tano. Maabara za kisayansi ziimarishwe kuchechemiza wabunifu na madediketa wa sayansi kuzitumia kwa manufaa ya taifa
 
Mwenyekiti.
ninatoka nje kidogo kunusa ugoro maana zogo la humu ndani, hatusikilizani.
ntarudi punde
 
M/Kiti,

Samahani nimechelewa kwenye mkutano maana kama unavyojua hii nchi yetu usipokuwa dar tum jua uko kwenye unreliable territory ktk intaneti na mambo kama hayo. Nimefika tu na kukuta agizo la mkutano inakwahi huku!

Mkuu mimi priority napendekeza kuwa kama ifuatavyo;

1) Elimu- Mfumo wa elimu ubadilishwe, ubuniwe mfumo utakao endana na hali yetu, na changamoto za soko la ajira duniani. Bado tuna mfumo wa elimu unaopelekea utegemezi wa ajira, ilhali serikali haijawahi na haina mpango wa kubuni ajira kwa wahitimu wetu. Muundo mpya uendane na matayarisho bora ya walimu, mashule, vifaa vya kufundishia. Pia mfumo wa kukopesha elimu ya juu urekebishwe kuwa wa wazi zaidi na wa ki-halisia zaidi.

2) Kilimo- Kwa kuwa toka uhuru kilimo kilikuwa na kimeendela kuwa eneo pekee lenye kuajiri watu wetu kwa zaidi ya 80%, serkali ijayo, kwa makuudi kabisa ifanya mapinduzi ya kilimo ya kweli ili kuboresha kilimo. Hii iendane sambamba na miundo mbinu sehemu za kulima ili kuyapa mazao value badda ya kuvunwa, kuwepo uhuru na uwazi katika soko la mazao, bei za mazao ziwe za uhalisia zaidi. Kwa makusudi kabisa serikali itengeneze mazingira na kuhakikisha mazao yetu yanakuwa processed hapahapa nchini lwa ubora unaokubalika na kuuzwa ndani ili kuondokana na hali ya kuagiza packed food toka nje. Inshallah naamini hili likienda vizuri tutauza nje baada ya kujitosheleza. Haya yafanye kiuhalisia zaidi kuliko KILIMO KWANZA ambayo imekaa kisiasa zaidi.

3) Katiba mpya iandikwe ndani ya mwaka mmoja ili kuleta mfumo mzuri wa kujitawala

Naomba kuwalisha ndugu mwenyekiti.


Nyunyu karibu sana. Toka jana nilituma watu wakutafute nikaambiwa umekwenda kule nanihii . . . kunanihiii . . . shughuli muhimu.

Siku nyingine ukisikia kikao muhimu kama hiki jitahidi kuwahi. Na siku hizi kuna Boda Boda so, kuwahi siyo issue ya foleni tena.

Turudi kwenye hoja sasa:

Hili na katiba liko sawa na limekaa vema. Tusaidiane kumtafuta dr. Mvungi atuletee draft tuanze kuipitia hapa.

Hili na Elimu nadhani ni Muhimu ila mpaka sasa hatujaliweka sawa. Kuna moja alisemaa elimu ya msingi iwe hadi kidato cha nne. Je baadaa yaa hapo itakuwa imemwandaa kijana wa Kitanzania kukabiliana na maisha?

wale waliobahatika kuhudhuria Silivan Summit mlimsikia Rais wa Mozambique akiongea kuwa yeye Mpango Mzima wa Elimu ni kujenga Vocational training Centres mapka level ya kata. ameshafanya hivyo kila wilaya sasa. Na akasema vijana wakimaliza wanaingia moja kwa moja katika soko la ajira ya kazi za mikono na uzalishaji.

Tuna shida kwani haapa vijiweni down town nawaona hadi university Graduates na wengine na Masters wakitafuta ajira. Wa diploma na advanced ndo usimseme, tayari nina CV 10 wakiomba niwatafutie ajira nami wala sijawapatia bado kwani hazipo.

Hebu tuelewane katika hili, tunataka nini hasa katika Elimu? Let us be brief and to the point.
 
Nyunyu, kuna suala la Kilimo nadhani umelielezea vema sana. lakini bado linataka ufafanuzi.

Hawa 80% wako vijijini. Na 50% wana mapato chini ya $ 1.00 kwa siku. wana watoto wanawasomesha, wanahitaji matibabu, malazi, nguo, chakula nk? Sasa serikali iaanzie wapi?

Iwape pesa au ruzuku? Iwape mashamba walime?

Iwaanzishie vijiji vya Ujasiliamali (siyo Ujamaa) vilivyojikita katika kilimo?

Au wafanye nini hasa?
 
EEE Ndugu munyaaaaaaakiti. Naomba unisamehe babaangu nimechelewa kidoooo kidoko tu msee. Huku kwetu tunatumia fibajaji. lakini hivi tunaambiwa ni fya mama wajawasito hifyo haviendi kwa haraka ndio manake nikachele nikachewa kwa kweli. Yewuuuwi nimesahau nilitaka kusema nini tena mseee! nikumbusheni basi waseee!

Aisee Mangi, umenichekesha sana. Unakuja town na Bajaji? Daladala haifiki kwenu au Bodaboda hakuna? Ndo maana umechelewa.

Sasa ukikumbuka unachotaka kusema uje hapa jukwaani.

Halafu lugha ya kejeli haturuhusu. Hivyo vibabaji kubeba mama wajawazito ndiyo nini sasa?
 
ASANTE M/kiti kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia Angenda Kuu 2010 ambazo chama Kitakachopata ridhaa ya
wananchi kisimamie kikamilifu.
Wakati napita hapa nilisikia swala la elimu likitajwa lakini sidhani kama limepewa msukumo wakutosha. Wizara ya Elimu ina matatizo makubwa ya kubadilisha mfumo wa Elimu ya Tanaznia. Kila siku tuko kwenye majaribio, Ni dhahiri kabisa kuna nchi ambazo zimepiga hatua ya haraka sanaKimaendeleo kwa kuwa na mfumo wa elimu unaoeleweka. Sisi kila siku ni
kubadilisha mifumo, mara futa mashindano ya michezo mashuleni siku mbili tena rudisheni michezo,Mara tena futa Shule za Ufundi Kesho yake tena rudisheni hizo shule Kila siku tunayumbishwa Sababu waziri kashauriwa sijui na haw*** yake,Samahani
M/kiti. Leo hii vijana elimu ya kazi za mikono imeachwa kabisa tunatengeneza Taifa la wakaa vijiweni tu maana hawathamini kazi za mikono. Ukifika vijijini sasa hivi kuna vikongwe tu ndiyo wako mashambani lakini vijana wenye nguvu wako Vijiweni. wanauza Soksi na chupi za kina mama,wengine eti wapiga debe tu hivi hiyo ni akili kweli kuruhusu ajila za kijinga namna hii halafu unasema kifua mbele ajira zimeongezwa, HII NI HALALI KWELI M/KITI, Naomba sana swala la Elimu lisifanyiwe mchezo
hapo tunanyonga Taifa kama Hatuelewi. Samahani M/kiti msg imeingia nipeleke uji wa mama mkwe amejifungua watoto wawili, Thanks
bye baadaye

Asante Kijana, ukishapeleka uji urudi.

Hoja yako imekuwa na nguvu ya kuleta tetemeko. Yaani kwa maana nyingine hoja yako ni timilifu katika suala la Elimu. Nadhani katibu liweke vema hasa kuzingatia ni vipi Elimu itasaidia kutoa ajira kwa vijana wanapomaliza masomo.
 
Mwenye kigoda!

Ajenda ya kwanza ni kubadilishwa kabisa kwa katiba!

Ili mawaziri wawe waaajiriwa na watu wote walio chini yao! Kuvunjwe huu utitiri wa miko na visingizio vya kusogeza huduma kwa wananchi.

Local goverments zipewe mamlaka zaidi juu ya uendeshaji wa maeneo yao husika nako huko watendaji wasiwe wanasiasa!

Madaraka ya Rais wa Jamhuriya Muuungano yapunguzwe kwa mujibu wa wakati tulionao sasa!

Ajenda ya Pili ni Elimu;
Isukwe upya muundo wake kwani uliopo sasa umepoteza ubora!

Ajenda ya Tatu ni Kilimo;

Yafanywe mapinduzi ya kweli yatakayomshirikisha zaidi mkulima mwenyewe na si haya ambayo viongozi wanapanga na kuwapelekea wananchi! Hii ikiwa ni pamoja na kusimamia zoezi zima la kurasmisha mali zao kwa uaminifu ili waweze kusaidiwa na misaada inayoelekezwa kwao.


Swadata! Umenena vema, nadhani haya yote tutayaingiza katika maazimio yetu.
 
1. Elimu
2. Afya
3. Miundo mbinu
Nawasilisha


Aisee baba yangu, unaweza ukayatolea ufafanuzi wa kina ili tutakapoipa serikali inayoingia madarakani iweze kuyafanyia kazi kwa ufanisi?

Tunasubiri hoja zako za ziada!
 
Aiseee..Foleni imenisababishiwa nichelewa mkutanoni, sijui nayo niweka katika Agenda la jungu hili. Kiukweli Katiba inatakiwa kufanyiwa kazi upya kabisa na pia umakini katika Separation of Power unahitajika sana kupewa kipaumbele na kupitia kwa umakini zaidi.

Katibu wa mkutano huu pamoja wahusika wote, ni vizuri feedback na majumuhisho ya mkutano huu yatolewa, nina uhakika italeta chachu kwa Taifa.

Kipepeo tuko pamoja na hili la katiba limekaa vema.

Bila ya shaka tutafanya majumuisho katika kutoa maazimio ya huu mkutano.

Ukiwa na hoja ya zaida haasa katika suala la kuondoa umasikini karibu sana.
 
Kipepeo tuko pamoja na hili la katiba limekaa vema.

Bila ya shaka tutafanya majumuisho katika kutoa maazimio ya huu mkutano.

Ukiwa na hoja ya zaida haasa katika suala la kuondoa umasikini karibu sana.
Mwenyekiti hebu tuwekee pannel yako ya wanamajumuisho maana unaposema kutakuwa na mjumuisho hapo unaniacha njia panda kwani sijajua nani ni nani ktk mjadala huu
 
Sijaalikwa
ila naomba kushiriki
Vipaumbele vyetu ni vingi ila msingi wa yote ni udhibiti wa matumizi yalioykithiri ya fedha za UMMA.
hatutaweza kulipa mishahara bora, kujenga miundombinu mizuri wala kuinua kiwango cha elimu iwapo serikali itaendelea kutumbua fedha za umma na rasilimali zetu.

Nitakuja tena...

Msanii karibu sana. Toka jana nilituma watu wakutafute hawakukuona. Vipi ulikuwa wapi na huu mkutano unajua umuhimu wake? Au uko kwenye kampeni?

Hoja yako ina nguvu sana. Kuna walioshauri juu ya "Uadilifu, Weledi na Utawala bora" Pia kuna wazo kuwa iundwe mahakama ya "wahujumu Uchumi na mafisadi" na atakayepatikana na makosa, anyongwe hadhaarani hadi afe. Hili tumeliundia kamati inayoongozwa na WoS.

Pia tumekubaliana kuwa Mawaziri ziwe ni kazi za ajira. Na kuna waliosema nafasi za Ubunge ziwe hazina mshahara bali posho tu.
 
Aisee Mangi, umenichekesha sana. Unakuja town na Bajaji? Daladala haifiki kwenu au Bodaboda hakuna? Ndo maana umechelewa.

Sasa ukikumbuka unachotaka kusema uje hapa jukwaani.

Halafu lugha ya kejeli haturuhusu. Hivyo vibabaji kubeba mama wajawazito ndiyo nini sasa?

Bajaji ni ambulance za kisasa zaidi, Comfortable na zinafika kwa urahisi zaidi kijijini kuliko mjini. Zimetengenezwa kwa uimara zaidi. Na kubwa zaidi RAISI Wa Tanzania wa awamu ya 10 atakuwa mama yake alipelekwa dispensary pale kijijini na BAJAJI maana lazima awe na akili za ziada!
 
Tuvunje muungano..........wazanzibar warudi kwao tuendelee na mambo yetu kwani tunapoteza muda mwingi kujadili kitu hiki

Jile tumekupata . . . Hii itaingia katika Mjadala wa Muundo wa Muungano wetu na hatimaye kura za maoni.

Vipi kuhusu, masuala ya uchumi na kodi?
 
naona unatuchuria sisi wanaume we mwali we.
lakini naunga mkono hoja yako kwamba kabla ya ahadi tutazame zilizotolewa zimetimizwa zipi kwa kiwango kipi ndipo zije ahadi mpya. la sivyo ni uongo uongo tu

Nadhani Policy forum wanazo au nenda HAKIELIMU wanavijitabu vya ahadi za watawala na zipi zimetekelezwa.

Msanii safi sana . . . huwezi kupata soft copy uzibandike hapa? hatufanyi mchezo na agenda hizi. Tukimaliza tunachapisha na kukabidhi kwa serikali ijayo.

Naomba kuwakilisha.
 
Kaizer, kwanza umekuja hapa Jangwani umechelewa, halafu nakuona kama una Beer Can . . . Ni sawa? halafu unaongea wakati wengine wanaongea na hujapewa ruhusa . . . Jamani tuwe na uvumilivu wa kisiasa kwa kupeana muda . . .

Sawa. hata hivyo hoja yako ni ya msingi. Kwa hiyo kuna issues katika Muungano. Sasa ufumbuzi wake ni nini? Au tuitishe "Kura ya Maoni Juu ya Muundo Wa Muungano"?


Chaiman, ni kwlei nin can ya beer (LOL) maana siye kwetu ni kinywaji kama maji ,,,,,

Hili la muungani linanikera manake kila siku linaibuka kwa sura tofauti

nina uhakika tukiitisha referendum sasa hivi na watu wakipewa civic education, mwenyekiti watu watasema bora kila mtu ajue mji wake!

baada ya hayo, naomba kuwaaamkua umati uliofurika hapa jangwani!
 
Pamoja na kuwa mratibu wa mkutano huu hanipi nafasi. Naanza kuchangia agenda ya ELIMU. Ndugu wajumbe kwa mtizamo( kama sio mtazamo) Ningependekeza sera ya taifa ya elimu ya Tanzania kwa awmu ijayo iwe ya mfumo wa kuchangamana. Mfano Kijana anayezaliwa kiraracha akasomea shule ya msingi kiraracha, sekondari o na a kiraracha na labda pale chuoni marangu mtoni. Hutegemei mtu kama huyu ataweza kuhimili ushindani wa katika soko la Dunia ya sasa! Nikisema kuchangamana namaanisha kuwa Wasukuma waje shule za kiraracha na wale wa uchagani waende mbeya hali kadhalika. Tuwaandae vijana wa kitanzania kwa ajili ya ushindani na sio kuwaacha kama vifaranga wa kuku wa kienyeji. Nasema hivi kwa sababu naamini kuwa Watanzania wengi tu akili sana tena kuliko, sioni sababu ya kuajiri wakenya kwa kigezo cha kiingereza chao tu! Nilkuwa na wakenya fulani pale Nairobi kipindi fulani, Chuo kizima kuanzia mwaka wa kwanza hadi wa Tatu hakuna mtu alikuwa anaona WaTZ wamepita wapi. Tulikuwa tunawaacha mbali sana. Walikuwa wanafuatia kwa karibu kidogo ni Wasenegali na Wanigeria. Tatizo la kwetu lilikuwa presentation! Kusimama na kutoa mada was one of the biggest issue for the Tanzanians. Nimetumia 'Was' kwa sababu nji kipindi hicho! Elimu ya Tanzania ianjengwa kudhibiti Mtoto wa Tajiri na Msomi na inamwacha mtoto wa mkulima mbali. Tuangalie ni wangapi wenye uwezo wa kuwalipia watoto wao kwenye shule zenye kufaulisha, St Francis, Maria Goreti, Marian? Nk. Je nikweli kuwa hakuna wenye uwezo kuliko hao wanaosoma huko? Je ni mtoto wa mkulima gani atakayeweza kumlipia mtoto huko? Hata kama atafanikiwa kufaulu mitihani yao? Mto kati ya mtoto wa tajiri/msomi mwenye kipato na Mkulima umezidi kupanuka! Pamoja na sera ya taifa eti kiwango cha chini cha elimu iwe kidato cha sita! (kichekesho)! Mtoto anamaliza F4 ya kata hajui kuandika wala kusoma unataka aendelee hadi F6! Si kwamba hataki kujua ila Manpower hakuna. Waalimu Vodafasta unategemea nini? Unakuta mtoto wa mkubwa mkubwa mbumbu kabisa anapewa material na mtaalam anakwenda! Sisi akina sisi nani anajali! Nafikiri mfumo wa elimu Tanzania unahitaji ukarabati mkubwa.
kama muda unaruhusu mwenyekiti niendelee

Haaa haaa, umenifurahisha sana na dhana ya Elimu ya Kuchangamana. Nadhani hii ndiyo Mwalimu Nyerere aliitumia kuua Ukabila na Udini. Sasa sina uhakika huu mfumo wa sasa hivi kama unaangalia hili. Ukiongeza na hao waalimu unaowaita voda fasta basi ndo hivyo tena.

Labda nikuulize swali, tunahitaji Elimu ya namna gani hasa?
 
Asante Kijana, ukishapeleka uji urudi.

Hoja yako imekuwa na nguvu ya kuleta tetemeko. Yaani kwa maana nyingine hoja yako ni timilifu katika suala la Elimu. Nadhani katibu liweke vema hasa kuzingatia ni vipi Elimu itasaidia kutoa ajira kwa vijana wanapomaliza masomo.

Kama walivyosema wadau wengine, elimu ni kipaumbele cha vipaumbele vyote. Hata hivyo ni ngumu sana kuja na recipe ambayo ni muafaka sasa hivi. Niliwahi kusema huko nyuma kwamba ili hii nchi iende, inabidi kila kitu kipigwe chini na kuanza upya (to overhaul the main system and subsystems). Kwa upande wa main system, ndo hapo wadau wanaweka mkazo kwenye kuandika katiba mpya (nasisitiza tena na tena, kuandika katiba mpya). Kwenye sub-systems (sectors) kama elimu, ni muhimu kukaa chini bila kukurupuka na kuandaa education master plan (au road map) ambayo itakubaliwa na wadau mbali mbali. Kwa sasa ni vigumu kueleza ni mfumo gani wa elimu unafaa zaidi ingawa baadhi ya maoni ni mazuri sana.

Nawasilisha,.....DC
 
Health Insurance ndio priority kwangu.
Maisha ya watanzania ni magumu. Hela za kulipia hospitali kila tunapougua hatuna. Serikali iboreshe sector ya afya na kuanzisha bima ya afya. Hata kama itaendelea kutoa huduma duni, lakini tuwe na uhakika wa kutibiwa. Hichi ni kitu cha msingi sana kama serikali inania ya dhati kuwakomboa wananchi wake.

Kuongeza wigo wa mapato na kudhibiti matumizi.
Nimefurahi kuanzishwa kwa zile cash register ambazo wauzaji hawawezi kukwepa kodi. Ubunifu wa aina hiyo ndo unahitajika continuously pale TRA. sio kila siku kuongeza kodi kwenye soda, bia na sigara.

Tatizo la serikali ni kwenye matumizi. Vitu vinavyofanyika serikalini havina value for money.
Kama mimi ndo ningekuwa Rais; ningeongeza mishahara ya wafanyakazi wote serikali
kima cha chini 1mil, watakaoa kuwa kwenye managerial levels, kima cha chini 2mil depending na sector.


Kwanini niongeze mishahara kiasi hicho?
  • Kupanua wigo wa kodi
  • Kuyaongezea uwezo mashirika kama NSSF, PSPF, PPF yaweze kufanya kazi za maendeleo zaidi kwasababu yana usimamizi mzuri. Hii itatokana na michango ya wanachama. Tunajua ni jinsi haya mashirika yanavyotumika kuleta maendeleo kila sehemu ya dunia.
  • Kuboresha maisha watanzania
  • Kupunguza uombaji wa rushwa kwa wafanyakazi wa serikalini
  • Ku-attract talented individuals wajitokeze kuifanyia kazi nchi yao
Huu mshahara utakuja na machungu yake
  • Kufuta allowances zote za vikao, ili watu wakae ofisini kufanya kazi
  • Kununua magari yasiyozidi CC 2500 kwa watumishi wote wa serikali wanapohitaji kuwa na magari ya serikali
  • Kufuta marupurupu ya safari za nje - ambapo mfanyakazi yeyote wa serikalini mpaka kufikia level flani, akisafiri nje ya nchi, tulipa gharama zake based on actual cost. Akiwa anafanya retirement aambatinishe na vithibitsho ya fedha aliyotumia inayobaki anarudisha hazina. Hiyo itapunguza sana demand ya USD. Safari za ndani zitaendelea kuwa na allowances kwasababu zinatija
Elimu ya bure mpaka kidato cha nne

Tunahitaji mabadiliko makubwa sana katika sector ya elimu. Walimu ndo wanatakiwa wawe watu wanaolipwa vizuri kuliko wafanyakazi wa maofisini. Ila hayo malipo mazuri yaanze baada ya mabadiliko yafuatayo
  • Walimu wachaguliwe kutoka wanafunzi waliofauru vizuri na sio failures: Huwezi kumchukua mwanafunzi aliye fail F4 akapata course ya miezi 3 aje kufundisha ukitegemea utapata taifa lenye watu wasomi na wenye uwezo mkubwa wa kufikiri. Tunaiua nchi yetu bila wenyewe kujua
  • Upimaji wa ubora waalimu uwe unafanyika, na ndio kiwe kigezo cha malipo. Sio shule kila siku inakuwa imejaza Div 4 halafu mwalimua wa hiyo shule awe analipwa sawa na anafaulisha vizuri.
Ubora wa elimu ni kitu tunachokiangalia juu juu sana, ila miaka kumi mbele hili litakuwa tatizo kubwa sana kwa taifa letu.

Kwa ufupi mambo makuu matatu ambayo ntapenda Kiongozi atakae ingia madarakani ayasimamie ni
Healthy Insurance
Ukusanyaji na usimamizi madhubuti wa matumizi ya serikali
ELimu ya bure ambayo ni bora kwa watanzania wote kuanzia shule za awali mpaka kidato cha 4

Du! Kabengwe umenikuna baba'ke! Kula da deki. Mpango Mzima umekaa vizuri.

Nilikuwa nasoma hadi nacheka.

Hawa Waserikalini sijui kama wanasoma hapa . . . Inshallah ngoja tuweke kwenye majumuisho yetu.

Bravo sana! nakufagilia mkuu!
 
Ahsante Mwenyekiti kwa rukhsa yako.
Ninapendekeza kwa serikali mpya kwamba, viongozi wa serikali hasa mawaziri watakapotoa taarifa zisizo za kweli iwe BUNGENI au popote pale wawajibishwe kwa manufaa ya UMMA.
Pili, ieleweke kwamba waziri au mwanasiasa yeyote anayeingia kutumikia umma kwa cheo chochote avuliwe madaraka yake kwenye Chama (chochote kile) ili kuwepo na uwajibikaji na kujituma kwa uadilifu.
Tatu, serikali mpya ifilisi mali za wooote waliokwiba mali za umma.
Nne, serikali iboreshe elimu kwa kuwaongezea mshahara walimu na wanaohitimu na kupata daraja la juu ndio wapelekwe ama waruhusiwe kujiunga na vyuo vya ualimu.
Tano. Maabara za kisayansi ziimarishwe kuchechemiza wabunifu na madediketa wa sayansi kuzitumia kwa manufaa ya taifa

Msanii, kwanza karibu tena. Mkuu umetukuna sana kwa pointi zako. Zinatuweka vizuri kuongezea zilizopita hasa suala zima la katiba.

Hili la tano Msanii, unaweza kulitolea ufafanuzi wa kina?
 
Back
Top Bottom