Uchaguzi 2020 Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM: Dkt. Hussein Ally Mwinyi achaguliwa Kugombea Urais Zanzibar kupitia CCM. Membe afukuzwa rasmi

Uchaguzi 2020 Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM: Dkt. Hussein Ally Mwinyi achaguliwa Kugombea Urais Zanzibar kupitia CCM. Membe afukuzwa rasmi

Wazanzibari hata siwaelewi; yaani wana jeshi, mahakama, wimbo wa taifa lao, na bunge.

Lakini pamoja na mbwembwe zao zote hizo, Rais wao anachaguliwa Dodoma, Tanzania Bara, sijui wanakwama wapi?!.

Hii ni sawa na baba wa familia kuwa na nyumba yako, unaacha pesa ya matumizi kila siku, lakini chakula kinapikwa kwa jirani, na umeshazoea kwenda kula huko.

Walimtimua Jamshid kwa kukataa usultani lakini ccm unawarudishia USULTAN kwa kupitia kwa Mwinyi!
 
johnthebaptist,

Mnataka kumpa kiti Hussein mwinyi bora hata mgempa Jecha mnalisishana vyeo ili muibe Mali za watz.

Watu wengi kwa sababu wanazozijua Wao wanadhani Hussein Mwinyi ndiyo atapitishwa ila ninawaombeni tu mjiandae Kisaikolojia kwa Mabadiliko.
 
Leo Halmashauri Kuu ya CCM inapokea mapendekezo ya Kamati Kuu kuhusiana na waliopendekezwa kugombea Urais wa JMT na ule wa Zanzibar.

Kadhalika itapokelewa ripoti ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwa miaka 5 iliyopita na kupitishwa ilani ya miaka 5 ijayo.

Up dates;

Maendeleo hayana vyama
Mbona hakuna updates?
 
Kuna kijana amezuiwa kupewa maiti ya mkewe hapo Muhimbili National Hospital mpaka atakapolipa shilingi 1,470,800.

Wasamaria walimsaidia kuchimba kaburi ili amhifadhi marehemu mkewe lakini kutokana na kuwekewa ngumu na serikali ya wanyonge, wamelazimika kufukia kaburi kisha kumchangia fedha za nauli kijana huyo ili arejee kwao Mtwara...
Mbaya ni kuwa unaweza kukuta ana miliki kadi ya CCM yeye na ndugu zake wote watakao kaa kulia pamoja naye juu ya mkasa huo alio tendewa.

Ushenzi wa serikali hii unatokana na support ya wananchi hao hao wanao nyanyasika kila siku. Mateso waliyopata watu wa Mtwara na Lindi kuanzia wakati wa gas hadi korosho nilitegemea CCM kuwa na wafuasi wasio zidi elfu moja lakini sivyo! Hata wakati Magu kaenda kule wangemsusia lakini sivyo.
 
Mvua ni baraka kutoka kwa Mungu,na kiongozi huletwa na Mungu pia,kwa miaka mingi mvua haijawahi kuangusha tone hata moja la mvua lakini Leo katika nchi kame tunabakiwa kupata mvua za rasharasha.

Baraka tele kwa viongozi CCM, mvua imemuunga mkono Mh Rais Magufuli kwa kuleta mvua za rasharasha #dodoma ya kijani, CCM ya kijani#2020
 
Kuna kijana amezuiwa kupewa maiti ya mkewe hapo Muhimbili National Hospital mpaka atakapolipa shilingi 1,470,800.
Wasamaria walimsaidia kuchimba kaburi ili amhifadhi marehemu mkewe lakini kutokana na kuwekewa ngumu na serikali ya wanyonge, wamelazimika kufukia kaburi kisha kumchangia fedha za nauli kijana huyo ili arejee kwao Mtwara.
Hivi sasa huyo bwana yuko njiani akielekea makwao akiwa amebeba kichanga cha wiki tatu na maiti ya mkewe ikiendelea kushikiliwa hapo Muhimbili.

Huyu ni mmoja kati ya wapiga kura mnaowategemea. Kwa hakika hakuna chama cha kidhalimu duniani kinachoweza kuishinda CCM.

Kama umeguswa wasiliana na huyu mnyonge anayeteseka kwa kunyimwa mwili wa mpendwa wake kwa namba ya simu 0778 140 361
Mbaya ni kuwa unaweza kukuta ana miliki kadi ya CCM yeye na ndugu zake wote watakao kaa kulia pamoja naye juu ya mkasa huo alio tendewa.

Ushenzi wa serikali hii unatokana na support ya wananchi hao hao wanao nyanyasika kila siku. Mateso waliyopata watu wa Mtwara na Lindi kuanzia wakati wa gas hadi korosho nilitegemea CCM kuwa na wafuasi wasio zidi elfu moja lakini sivyo! Hata wakati Magu kaenda kule wangemsusia lakini sivyo.
 
Umekosa mvuto wakati wewe umevutika kuja kuchangia hapa!
Macho na masikio yote Dodoma wikiendi hii
Kwanza huo mkutano una faida gani kwangu mimi ninayehangaika kupata sh.20,000 ya ada ya mwanafunzi wangu wa hii shule ya kata isiyo hata na mwalimu?
 
Ainisha mambo matano tu abayo yamo kwenye ilani,lakini hayajatekelezwa
1.) Kukamilisha mchakato wa katiba mpya

2) Kuendeleza amani, umoja na mshikamano wa Watanzania

3) kuendelea kudumisha utawala wa sheria

4) Kukuza sekta za uchumi zinazokua kwa haraka kama utalii na madini

5) Kuimarisha sekta ya viwanda

6) Kuendeleza kilimo na kukifanya kuwa cha kisasa

7) Kukuza na kuongeza ajira kwa vijana

Hizi ni baadhi ya ahadi za CCM mwaka 2015, zilizokuwemo kwente ilani ya uchaguzi lakini CCM imeshindwa kabisa kyzitekeleza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijawahi kumwona mwana CCM yeyote anayejiamini kwenye uchaguzi bila kutegemea kubebwa na ama Tume au Vyombo vya dola.

Hata huo utitiri wa wagombea wa CCM ni kutokana na ile Kauli ya mwenyekiti wao kwamba atamshangaa mkurugenzi atakayemtangaza mpinzani kwamba kashinda.
 
Kabla hujamsikitikia, fanya uchunguzi, anasemaje juu ya uzuri wa CCM na sera yake ya kuwajali wanyonge.

Kuna watu mifumo ya utawala iliyopo inawatesa sana lakini unashindwa kuwaonea huruma kwa sababu hawajitambui. Kinachowatesa ndicho wanachokitukuza na kukishangilia.

Kuna uwendawazimu, nchini mwetu, mtu akiwa chama gulani anaamini wajibu wake ni kukisifia chama cha ke katika kila tendo hata kama ni la kinyama kiasi gani. Hali hiyo inawafanya watawala kutufanyia chochote wanachotaka wao bila ya kujali wanachokitaka wananchi. Huyo anayetaabika sasa hivi hatujui yupo kundi lipi.

Kumsaudia mtu ambaye hajitambui na wala hatoi mchamgo wowote ili kubadilisha migumo mibaya iliyopo ni kushiriki uovu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani mgombea wa nchi ya Zanzibar ni lazima nyie muamue??!!

Kwa nini?
 
Back
Top Bottom