Uchaguzi 2020 Mkutano wa Viongozi wa Dini wa kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli kuelekea Uchaguzi Mkuu!

Pepo mchafu toka
Pepo wa upumbavu na ujinga toka
Pepo unayeeneza ujinga na upumbavu toka.
Kwa kumbukumbu zangu, tangu Tanzania iasisiwe awamu hii ndio ya kwanza kutumia gharama kubwa kumsamisha Rais aliyeko madarakani.
Ndio maana ulaya na Marekani vijana hawana muda na mambo ya dini halafu huwa tunawaona wamepotoka, kumbe wako sahihi 💯💯

Kwa ujinga huu makanisa ni lazima yakose watu ndani ya miaka michache tu mbele.
 
Jaman hamna picha na list ya Waliohudhuria ?
Nime pledge 500,000 Kanisani kwa ajili ya ujenzi
Nataka ku withdraw pledge yangu
 
viongozi wa dini wa ukweli hawa hapa.... wanaongea vitu vinavyoeleweka.

viongozi wa dini hawasifu mtu - humsifu MUNGU pekee.

 
Waache kumchezea Mungu. Mungu siyo wa wana-CCM tu.
 
Viongozi wa dini sisi waumini tupo nyuma yenu.nyinyi mnaongozwa na roho wa Mungu,mema mnayofanya hakika ni miongozo iliyobarikiwa na Muumba mbingu na nchi.
Mungu awaongoze mzidishie upendo wenu kwa Rais wetu kipenzi JPM.
Mwaka huu tutaona mengi. Mara wasanii, mara viongozi wa dini. Wapiga ramli nao wataitwa kuunga juhudi?
 
Kwa hali hii hata viongozi wa dini wameshikishwa silaha kudhuru waumini wao ambao siyo wanachama wa CCM.
 
Mafarisayo hao. Wanafanya biashara
 
Wapuuzwe na nani sasa? Unadhani waumini watakusikiliza wewe ghost kuliko kiongozi wao? Bora muwashawishi wawaunge mkono kuliko hizo porojo.
Mimi mwenyewe ni muumini na nimewapuuza!Kama huyo paroko namsubiri kanisani,nitahoji upuuzi alioufanya!
 
Mnalala tu
Viongozi waliomba Mungu tukampa Rais "chuma"
Viongozi wa dini wamemuomba Mungu Corona ikakoromeka huko mbali nchi yetu ikabaki salama
Viongozi wa dini wanaziona juhudi za Rais wetu!
Kwa hiyo mnataka viongozi wa dini wawe upande wa
Vurugu
Maandamano
Fujo
Kupinga Kila kitu!
Mungu yupo upande wa amani na hasa kwa wamuitao, siyo Kama Yule mgombea wenu aliyekejeri Rais kumuomba Mungu Corona ipotee!
 
maagizo na vitisho, we uoni tangu askofu kakobe aaunge juhudi amekuwa mtanzania halisi ishu ya uaraia imekufa kifo cha mende
 
viongozi wa dini wapo Kenya kule huwezi kuta wanashirikiana na watu dhalimu ili wapate bahasha,usimama pamoja na walionewa,Viongozi wa dini congo walisimama kidete na wananchi hadi dikteta kabila akaachia madaraka baada ya kuvimbiwa na kulewa kodi za wakongomani na kupelekea kupitisha mkataba wa kutakiwa kukaa madarakani
 
Watafanya yote ila wakati wa mnara wa babeli kuanguka ukifika utaanguka tu.
 
Kila siku nawaambia dini ni upuuzi lakini hamsikii
 
njia sahihi ya kukubalika ni kuwanunua wananchi na sio kuwanunua wapinzani,wasnii,viongozi wa dini zote hizi bado zinabuma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…