nenda kwa cdf general john jacob mkunda anazo zote hadi picha na taasisi zao sawa?Evidence
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
nenda kwa cdf general john jacob mkunda anazo zote hadi picha na taasisi zao sawa?Evidence
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki kwenye Mkutano wa Saba wa CDF na Makamanda unaofanyika 302 KV Brigade Mess, Mwenge jijini Dar es Salaam leo tarehe 22 Januari, 2024
CDF: VIJANA WETU WA MIAKA 15 HADI 35 WANALENGWA NA WANA MTANDAO WA UGAIDI
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (CDF), Jenerali Jacob John Mkunda amesema hali ya ulinzi na usalama ni shwari licha ya uwepo wa matukio ya kigaidi na itikadi kali na kuwa kuna vijana wanaochukuliwa na kwenda kujiunga kwenye makundi ya Kigaidi Nchini DR Congo, Msumbiji na Somalia.
Amesema hayo mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan ambaye anashiriki kwenye Mkutano wa Saba wa CDF na Makamanda unaofanyika 302 KV Brigade Mess, Mwenge Jijini Dar es Salaam, leo Januari 22, 2024.
CDF: BAADHI YA WAKIMBIZI WAMEPEWA TEUZI SERIKALINI KATIKA NAFASI ZENYE MAAMUZI
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (CDF), Jenerali Jacob John Mkunda amesema kuanzia Januari Mosi, 2023 hadi Desemba 31, 2023 jumla ya Waomba Hifadhi 138,149 walipokelewa Nchini Tanzania.
Ameongeza kuwa imebainika baadhi ya Waomba Hifadhi au Wakimbizi au familia zao wameteuliwa Serikalini katika nafasi zenye maamuzi.
Amesema hayo katika Mkutano wa Saba wa CDF na Makamanda unaofanyika 302 KV Brigade Mess, Mwenge Jijini Dar es Salaam, leo Januari 22, 2024.
RAIS SAMIA: JESHI LIWE TAYARI KUKABILIANA NA CHOCHOTE KITAKACHOJITOKEZA
Rais Samia Suluhu amesema "Ombi langu kwenu (JWTZ) ni kwamba Mwaka huu (2024) na Mwakani (2025) tunatarajia kuwa na chaguzi na hapa ndipo usalama mkubwa ndani ya nchi unapotakiwa kuangaliwa kwa ukaribu zaidi, niwaombe sana Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwenye Kamandi zenu tofauti kujipanga kwa ajili hii.”
Amesema hayo katika Mkutano wa Saba wa Mkuu wa Majeshi-CDF na Makamanda wa Mwaka 2023 Jijini Dar es Salaam, leo Januari 22, 2024.
Ameongeza “Ni chaguzi zinazoshirikisha vyama vingi vyenye nia tofauti, hatuoni kwamba kila kitu kitaenda kama kilivyopangwa, ni vyema tukakaa tayari kukabiliana na chochote kile kitakachojitokeza."
nenda kwa cdf general john jacob mkunda anazo zote hadi picha na taasisi zao sawa?
Hussein Bashe hana uwezo huo. Yeye atakuwa anatumiwa tu na nchi yake ya Somalia kuipeleleza Tanzania kwa maslahi ya taifa lake.Hiv kwamfano hapo msomali akafanya yake tokea mbali ikawa juu chin chini juu itakuaje?????
Kwani alimteua yeye? Hakumfanyia vetting ya kutosha?Kwani unadhani hajui, anajua Sema makusudi tu.
Naibu ni mTanzania?
acha kunipotezea muda kwani utakuwa umevimbiwa upumbavu sawa?Wewe ndio umeanzisha uzi. You were supposed to put evidence , when you tell people to search for evidence , it becomes an accusation
Mamlaka ya Intel inafanya kazi vizuri
Hata huko jeshini wapo na ni kazi ya Tanzania Intel
Si wampige repatriation tu arudi kwao Burundi badala ya kuanza kumfanyia visa mzee wa watu? Mzee kwanza tangu aumwe korona hajapona vizuri wanaanza kumchokonoa!Mipango juu ya mpango
Uingereza, Ufaransa na Uholanzi.kwa taarifa za uhakika nilizinazo kuna nchi tatu ambapo mbili ni kubwa na nyingine ndogo ila ina watu makatili mno ndizo zimepandikiza watu wake katika taasisi muhimu na nyeti za tanzania
Wapo akina BashungwaSi wampige repatriation tu arudi kwao Burundi badala ya kuanza kumfanyia visa mzee wa watu? Mzee kwanza tangu aumwe korona hajapona vizuri wanaanza kumchokonoa!
Safari yoyote unapoelekea usipopajua ni mbali kwenda tu sababu muda mwingine utautumia kuulizia uelekeo au kuutafuta uelekeo Ila kurudi sio mbaliAmeongeza “Ni chaguzi zinazoshirikisha vyama vingi vyenye nia tofauti, hatuoni kwamba kila kitu kitaenda kama kilivyopangwa, ni vyema tukakaa tayari kukabiliana na chochote kile kitakachojitokeza."
Na mimi naona hivyoCDF ameongea mambo mazito mno kuhusu wakimbizi na walowezi wengine kujipenyeza serikalini kwenye nafasi nyeti, ni maajabu amiri jeshi mkuu kwenye hotuba yake ameonesha kuwa yeye anawaza uchaguzi tu na namna ya kulitumia jeshi kuvuka.
Inawezekana wamemwambia sana huko sirini lakini hana muda na hilo, wameamua kuweka mambo hadharani wananchi tujue, wakijua labda SSH atapata msukumo wa kulivali njuga.
Mtajuana bwana. Sisi hayatuhusu tunawaza Umeme na Mfumuko wa bei.Mama atamuomba CDF ampe majina ya hao watu, bila shaka kama jeshi, hawawezi kusema hivi hivi, otherwise mkuu wa majeshi atapoteza credibility yake.
and, kwa nini ayaseme hadharani wakati kuna vikao vya Baraza la Taifa la Ulinzi na Usalama, na yeye kama Mkuu wa Majeshi ni mjumbe!? Pia Mkuu wa Majeshi kila siku kabla hajalala lazima ampe briefing Rais, na asubuhi lazima ampe hali ya usalama wa nchi, apart, ana direct access na Rais muda wowote ule!!!
Kingine CDF kuna gepu ameacha wazi angetaja na majina hata mawili matatu km mfano wa hao waliopenyezwa huko kwenye idara nyeti kwamba huyu hapa raia wa Somalia Ila kapachikwa TISS anafanya nini kule na kapewa mafaili yote nyeti yanayotuhusu kwanini?CDF ameongea mambo mazito mno kuhusu wakimbizi na walowezi wengine kujipenyeza serikalini kwenye nafasi nyeti, ni maajabu amiri jeshi mkuu kwenye hotuba yake ameonesha kuwa yeye anawaza uchaguzi tu na namna ya kulitumia jeshi kuvuka.
Inawezekana wamemwambia sana huko sirini lakini hana muda na hilo, wameamua kuweka mambo hadharani wananchi tujue, wakijua labda SSH atapata msukumo wa kulivali njuga.
Nadhani masuala ya immigration hayawazii sana anawaza masuala ya uchaguzi tu na mwamvuli wa Jeshi uwe juu yake umlinde ashinde uchaguzi hayo mengine ya uraia na majasusi kujipenyeza idara nyeti yanazungumzika tu Ila uchaguzi kwanza ndio wa muhimu inabidi CCM ashinde kwa Ulinzi na usalama wa Jeshi, ndio nilivyoelewaMama atamuomba CDF ampe majina ya hao watu, bila shaka kama jeshi, hawawezi kusema hivi hivi, otherwise mkuu wa majeshi atapoteza credibility yake.
and, kwa nini ayaseme hadharani wakati kuna vikao vya Baraza la Taifa la Ulinzi na Usalama, na yeye kama Mkuu wa Majeshi ni mjumbe!? Pia Mkuu wa Majeshi kila siku kabla hajalala lazima ampe briefing Rais, na asubuhi lazima ampe hali ya usalama wa nchi, apart, ana direct access na Rais muda wowote ule!!!
Hawa mnaowakataa kuwa hapa sio kwao ili hali walizaliwa hapa na babu zao wamezikwa hapa, mkiwafukuza mnataka waende wapi? Hawa wakiwa wengi ndio watakwenda misitumi na watawasumbua sana!Punguza mhemko. hajasema hawajulikani. Amesema wapo nchini kama waomba hifadhi na wakimbizi. bado utaratibu wa kupata uraia kamili haujafanyika au hata hawajaomba lakini wameingia katika ajira na wengine wamepenya hadi nafasi za maamuzi. Lakini pia mkimbizi au muomba hifadhi kupata uraia siyo haramu. Nchi hii ina wakimbizi wa tangu miaka ya 1970's, wananishi nchini na hawajapewa uraia rasmi. Kimsingi haowatu ni watanzania, hawawezi kuitwa wakimbizi maana wamezaa na wana wajukuu waliozaliwa ndani ya nchi.
Tuliona kwa JM Kikwete na akina Lt Gen Shimbo. Nadhani kuna 'copy and paste'.Tumekuwa tukifanya uchaguzi tangu enzi za Nyerere hadi sasa lakini jeshi halijawahi kuingilia kati. Inakuaje sasa Samia anataka kuliamuru Jeshi kuingilia uchaguzi? Nadhani anataka kupora uchaguzi kwa nguvu kwa kutumia nguvu ya jeshi. Labda atuambie nchi au magaidi wanaotaka kuvamia uchaguzi hadi aamue kutumia jeshi kwenye mambo ya uchaguzi badala ya polisi.
Hakuna shaka Polisi haiaminiwi na wenyewe lakini kuna hoja, kwa mtu aliyeeona Polisi amesimama masanduku ya kura feki yanaletwa anasema siyo kazi yake ni ya Tume, hapaswi kuaminiwa tena
Kufanya hivi pia ni ishara kuwa jeshi la polisi haliaminiwi tena kwenye masuala ya usimamiaji wa uchaguzi na pia katika mambo ya ulinzi na usalama wa raia pamoja na mali zao. Kwa maana hiyo basi ni bora akalivunje jeshi la polisi na kuimarisha jeshi la ulinzi zaidi. Polisi wanaonekana wapuuzi tu, hawana thamani wala msaada wowote kwenye masuala ya ulinzi. Hili ni tusi kubwa sana ambalo Samia amewatukana polisi kwa vitendo.
Hili ni jambo linalofanywa na Wanasiasa kwa faida za muda mfupi bila kujali madhara ya siku za baadaye.
Na pia kitendo cha kuamrisha jeshi lisimamie uchaguzi kitasababisha msuguano na uhasama kati ya polisi na wanajeshi. Au anataka kuwapiganisha kwa makusudi? Samia anapaswa achunge sana kauli zake kwani zina hatari ya kuwagawanya wanausalama kwa makusudi na kuwapa mwanya maadui wapenye nchini kwa urahisi. Kwa lugha nyingine ni kwamba kauli zake zinatia rehani maisha, usalama na mali za raia. Kuna shida mahali kwenye uongozi wa huyu mama; sio bure.