Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ditopile Mzuzuri akamatwa kwa mauaji ya Dereva wa Daladala

Kwenu mlioko Bongo hebu tupasheni hii habari nasikia Ditopile kaachiwa kwa dhamana na anatinga nje ya Keko hivi sasa.
 
tena out on bail !! mie sikushangaa tokea siku ile ile waliposema bastola ya ditto imepotea, i knew this case was going 2 be twisted ! anyway, haki kwa hapa duniani ni ngumu, and freedom is never free !! so lets take it like the way it is !!!!!!!!!!!!!!!
 
Maisha yangu yote nilijua kuwa kosa la mauaji yawe ya kukusudia au la halina dhamana...sasa wale ndugu zetu ambao wanasota kwa miaka 12 au zaidi kabla ya kuachiwa kwa kukosa ushahidi inakuwaje?
 
Ditto bado hajatoka. Labda hiyo kesho kama atapewa dhamana.

Mafuchila, uzuri wa sheria ni kuwa zina-set precedence. Kama Ditto ataachiwa kwa dhamana, basi ni rahisi kwa lawyer mwingine mjanja katika kesi nyingine yenye mazingira kama ya Ditto kutumia kesi ya Ditto kama precedence kuwa Mahakama Kuu iliwahi kuamua hivi na hivi. Ni vigumu kwa Mahakama Kuu kujikanyaga mara mbili.
 
Maisha yangu yote nilijua kuwa kosa la mauaji yawe ya kukusudia au la halina dhamana...sasa wale ndugu zetu ambao wanasota kwa miaka 12 au zaidi kabla ya kuachiwa kwa kukosa ushahidi inakuwaje?

Hii ndiyo Tanzania yetu na utawala wa sheria na sheria hufuata mkondo kwa vidagaa tu na si kwasangara!Tusubiri tusikie kama ni kweli kabla hatuja hitimisha!Hapa ndipo palipofanya kuwepo na utitiri wa wanasheria maarufu ili kujustify Dhamana hiyo na hatimaye kuishia kiujanjaujanja na kesi kufikishwa Mahakama kuu kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu,Hapa ndiyo namkumbuka Nyerere(RIP) pamoja na mapungufu yake kama mwanadaamu sidhani kama jamaa angetoka hata kwa dhamana kwa hilo.Unajua nini kitatokea baada ya kutoka kwa dhamana ni kwenda kujitia Anajuta kwa Mzee Mbonde na kutoa pole ili ionekane anajutia hilo kosa na hakufanya kweli kwa kukusudia.Then will be a point of argument in the court room....................Guess what?stay tuned!
 
jamani tuwekeni sawa basi,nini huamuzi wa mahakama,au ndio wanapima joto lake kwanza ?
 
Kortini zali tupu...Kisa Dito

2007-03-08 16:36:45
Na Mwandishi Wetu, Mahakama Kuu


Kama ilivyokuwa kule kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo tena ile kesi inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile Mzururi, imezua zali lingine katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Waliokuwepo mahakamani hapo wanadai zali lenyewe limetokana na kitendo cha mtuhumiwa huyo kupitishwa kwenye mlango ambao si maalum kwa washitakiwa.

Habari kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania zinadai kuwa Dito alipitishwa mlango wa majaji, kitu ambacho si cha kawaida hata kidogo.

`Majaji hawakupenda hali hiyo hata kidogo?ilibidi msajili wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam ahoji sababu za kufanya hivyo,` mmoja wa maofisa wa mahakama hiyo amemuambia mwandishi wa habari hizi aliyekuwa kortini hapo.

Dito ametinga Mahakama Kuu saa 2:54 asubuhi akiwa chini ya ulinzi mkali.

Eneo la mahakama lilikuwa na watu wengi huku baadhi ya ndugu zake wakionekana kuzama kwenye fikra nzito.

Kesi hiyo iliyo mbele ya Jaji Augusto Mwaringa ilikuwa ianze kusikiliza maombi ya dhamana ya mshitakiwa huyo jana, lakini ikakwama baada Ditopile kucheleweshwa kuletwa kortini.
Jaji aliahirisha kesi hiyo hadi leo saa tano asubuhi.

Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, Dito alikuwa bado `selo` ya mahakamani hapo akisubiri muda wa kuitwa kwa kesi yake.

Februari 15 mwaka huu wakati kesi hiyo ikiwa katika mahakama ya Kisutu, mawakili wa upande wa utetezi wa Dito na ule wa mashtaka, walisuguana vikali kisheria kuhusiana na ombi la upande wa mshtakiwa waliotaka Dito apewe dhamana.

Siku hiyo, jopo la mawakili watano wanaomtetea Dito, likioongozwa na Nimrod Mkono, liliiomba mahakama hiyo ya Kisutu impatie dhamana mteja wao kwa madai kuwa kisheria, kesi ya kudaiwa kuua bila ya kukusudia haimzuii mtuhumiwa kupata haki ya kuachiwa kwa dhamana.

Baada ya ombi hilo la upande wa mshtakiwa kutolewa, Hakimu Michael Luguru alisema kwa maoni yake, Mahakama ya Kisutu bado haikuwa na uwezo wa kutoa dhamana na badala yake, suala hilo linaweza kuamuliwa na Mahakama Kuu ya Tanzania iliyo na uwezo wa kuisikiliza kesi hiyo.

Kesi hiyo ilianza kuunguruma katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu tangu Novemba 6 mwaka jana.

Katika kesi ya msingi, inadaiwa kuwa Novemba 4 mwaka uliopita, saa 1:00 usiku, katika makutano ya barabara za Bagamoyo na Kawe wilayani Kinondoni, mshtakiwa alimuua bila kukusudia dereva Hassan Mbonde.

SOURCE: Alasiri
 
Ditto ameachiwa leo kwa dhamana; tayari iko hewani kwenye news
 
Kakalende,
Nimeisikia Radio Tanzania kupitia RadioMaria. Pia VOA imemhoji wakili wake Tenga akithibitisha hilo.
 
Ditto ameachiwa leo kwa dhamana; tayari iko hewani kwenye news

Kwanza ataenda kuwaona wazee bagamoyo halafu atatinga kwa Mzee Mbonde!
kwelihaki ya kweli iko kwa mungu tu kwa wale wote wanaoamini hivyo! Ni kwa mara ya kwanza ktk historia ya Taifa letu mtu kuua for whatever reasons kuwa nje kwa dhamana!Tumefungua milango ya historia potofu.........................!
 
CCM ina mambo makubwa maana hata watetezi wa watu ikifikia kwa CCM huwa wanaahau na kuweka CCM mbele . Mkono ana heshima gani mbele ya jamii kwa kitendo cha kuona aliyeuawa ni mbwa tu ?Hivi kweli pesa inaweza na maana zaidi ya utu ama uhai wa mtu ?CCM nyie mnamtoa mtu ale nchi wakati kaua na mwenziwe kalala ardhini ?
 
mimi sishangai,maadam kisura amefungua ukurasa mpya,baada ya kusema watanzania ni hoi bin taabani katika elimu na haya ndio matunda yake.
 
Hao wanaodaiwa kuwa ndugu wa Ditto wanaopiga waandishi wa habari za picha na wanaachiwa na polisi ni ndugu kweli au vyombo vya dola na ndiyo maana polisi wanawaangalia tu??
 
Ndugu Ditto hajatolewa huru kama baadhi wanavyodai, shitaka lake lilibadilishwa na kuwa ni KUUA BILA KUKUSUDIA kulingana na ushahidi aliotoa na nature ya shitaka hilo ni kuwa anaweza kupata dhamana.

Ameshakaa ndani kwa miezi minne sasa na leo ameachiliwa kwa dhamana ya dola 20,000 na mahakama ilikataa ombi kuwa aachiwe eti kwa vile ni mtu maarufu, waliamua kwamba hiyo sio bond enough. Amesalimisha pasi yake ya kusafiria na kesi inaendelea.

Hizi speculations za nini?!!


Kama nilivyowahi kueleza hapo jana kuwa sheria kuchukua mkondo wake sio lazima underdog washinde ingawa najua huwa kuna sensation sana iwapo mtu wa hivyo akishinda.

Sasa bado kesi inaendelea leo BBC wamevurunda in my view wametoa text ya mtu akisema ''najua wewe Ditto ni mtu mzuri na utatoka tu'' kuna hatari ya contempt of court hapa....


Kesi inaendelea YETU MACHO!!
 
Ditto ameachiwa leo kwa dhamana; tayari iko hewani kwenye news

Ndugu Ditto hajatolewa huru kama baadhi wanavyodai, shitaka lake lilibadilishwa na kuwa ni KUUA BILA KUKUSUDIA kulingana na ushahidi aliotoa na nature ya shitaka hilo ni kuwa anaweza kupata dhamana.

Ameshakaa ndani kwa miezi minne sasa na leo ameachiliwa kwa dhamana ya dola 20,000 na mahakama ilikataa ombi kuwa aachiwe eti kwa vile ni mtu maarufu, waliamua kwamba hiyo sio bond enough. Amesalimisha pasi yake ya kusafiria na kesi inaendelea.

Hizi speculations za nini?!!


Kama nilivyowahi kueleza hapo jana kuwa sheria kuchukua mkondo wake sio lazima underdog washinde ingawa najua huwa kuna sensation sana iwapo mtu wa hivyo akishinda.

Sasa bado kesi inaendelea leo BBC wamevurunda in my view wametoa text ya mtu akisema ''najua wewe Ditto ni mtu mzuri na utatoka tu'' kuna hatari ya contempt of court hapa....


Kesi inaendelea YETU MACHO!!
Toka tupate uhuru hadi leo nipe mfano wa mtuhumiwa yeyote wa kesi ya mauaji amabaye kesi yake na jarida lake limewahi kupelekwa kwa mkurugenzi wa mashitaka kwa kipindi kifupi kama cha ditto?ni mtuhumiwa gani wa kosa kama la Ditto ambaye alishawahi kuomba dhamana na akapewa hata kwa masharti kama ya Ditto na akashindwa mwenyewe?
 
Back
Top Bottom