Mkuu wa nchi lazima awe mkali na aogopwe. Asipoogopwa kila kitu kitakwenda mrama. Hata hayati Julius Nyerere aliogopwa na alikuwa mkali

Mkuu wa nchi lazima awe mkali na aogopwe. Asipoogopwa kila kitu kitakwenda mrama. Hata hayati Julius Nyerere aliogopwa na alikuwa mkali

Mkuu wa nchi ambae ndio ndio custodian wa mali za taifa la watanzania kudai kuwa hawezi kufokea mtumishi wa umma ni kushangaza umma wa watanzania.

Kwamba watumishi wa umma wakiharibu atawabembeleza?

Nimekaa na wazee wengi waliofanya kazi na hayati Julius Nyerere wanasema wazi kuwa Mwalimu alikuwa mkali sana.

Ilitokea akikuita kwake Msasani au Ikulu ilikuwa lazima upate wasiwasi na woga mkuu.

Wengine aliwaita kuwapongeza lakini hawakuamini walichoitiwa wapo pia aliowafokea hadaharani au hata kifichoni.

Kwamba mkuu wa nchi unafanya kazi kwa kuonea aibu wateule wako? Kwamba utakuwa unawabembeleza?

Mbona hii sio sawa? Mkuu wa kaya lazima uwe mkali ili nidhamu ipatikane kuanzia juu mpaka chini.

Hatusemi ufokee watu kama watoto wako. Bali uwe na maamuzi na maelekezo yenye kuonyesha kuwa kuna kiongozi mwenye mamlaka aisiyetaka mzaha na anataka watu wafanye kazi.

Mfano, tulitegemea umkaripie January Makamba maana mradi wa JNHP unaweweseka kama vile hauna manufaa kwa wanaCcM wenzake.

"UKALI" tu usiozingatia misingi ya utu, heshima, busara, hekima na sheria, ni UPUMBAVU na UJINGA na ni dalili za wazi sana za UTAWALA WA UDIKTETA..

Kwani binadamu gani aliyekamilika na asiyekosea? Hayupo!

Hata huyu mtu mwenye cheo cha kidunia cha "URAIS" naye ni binadamu na anakosea...!

Turudi kwa utawala wa Mwl. Julius K. Nyerere

Mwl. Julius K. Nyerere alikuwa mkali kweli. Lakini ukali wake haukuwa kama wa yule Mwendazake Magufuli.

Hili umethibitisha mwenyewe kuwa alikuwa akiwaita na kukemeana wenyewe kwa wenyewe huko ndani siyo hadharani mbele ya wanaoongozwa ktk namna ya kutweza utu na heshima ya mtu.

Nakupa changamoto moja na kisha tuambie hapa.

Katika utawala wa karibu miaka 25 ya Urais wa J. K. Nyerere, ni wapi aliwahi kumtukana waziri wake hadharani kwenye mkutano wa hadhara? Ni wapi amewahi kufukuza kazi mtumishi wa umma hadharani bila kufuata utaratibu wa kisheria?

All in all hujamwelewa Mama Samia na kauli yake hiyo. Hana maana ya hiyo unayoidhania wewe..!!
 
Waulize watu wazima walinunua mafuta ya kula na sukari shillingi ngapi mwaka 2014 nq 2015 na kisha wakaja kununua shillingi ngapi mwaka 2017 na kuendelea
Ndio Magufuli alikuwa Hana hayo yote ila hatukuwahi kuona umeme unakatika hovyo , inflation rate Leo Ni kubwa kuliko miaka mitano nyuma.

Jana nimeenda dukani nimekuta sabuni ya unga ya 1,000 inauzwa 1,200 na Soda ya 500 inauzwa 600.

Maji ya Uhai ya 500 yanauzwa 600. Kama huna Cha kujifunza hapa Basi.


Magufuli alikuwa na mapungufu Yake kama binadamu ila Kuna mazuri mengi alifanya.
 
Upo sahihi sana. mimi nampenda sana mama samia ktk utendaji wake ila la hili la nidhamu ya moyoni kwa watumishi wa umma mama aliangalie vizuri.

Kuchelewa kazini, kutokatoka hovyo kuzurula, kwenda kucheza kamali wakati wa kazi na vijiwe vya mpira vinashusha sana nidhamu ya kazi ktk secta zote.

Utakuta 80% ya watumishi wa umma wanastahili kufukuzwa kazi kila siku kwa utovu wa nidhamu.

utakuta wizara zote za serikali zina cheo kiitwacho ofisi supevisor maajabu yake ofisi supevisor hafuatilii watoro kazini, wacheza kamali, wafanyao ngono maofisini wala kuwabana wachelewaji.

Hwa maO.S, utakuta siku zote ni father X-mass tuu na hupenda kununua stationary tuu!matokeo yake katika wizara zote za serikali huwezi kumtuka mfanyakazi aitwae workaholic(yaani yule aketie kitini na kujituma kazini mpaka anaambiwa nenda nyumbani kinguvu}

mimi binafsi namuomba sana mama awe mkali sana na avae ndita muda wote maana tupo katika kipindi cha heated economy la sivyo wajanja watamuangusha kisawasawa..
Namuunga mkono Samia hatakiwi kufanya ukiranja kwa kila mtumishi.
Laa sivyo basi nafasi za Uwaziri, Ukatibu Mkuu,Ukurugenzi/Ukamishna viondolewe.
Watumishi wote wawe level moja.
 
Sisi bado ni nchi maskini wewe kilaza, achana na zile propaganda na blah blah za sisi ni dona,.sisi ni matajiri
Jiandaeni kushuka na kuwa nchi maskini tena, muda si mrefu subiri IMF wafanya kikokotoo chao, mtatafuta pa kujificha
 
Jiandaeni kushuka na kuwa nchi maskini tena, muda si mrefu subiri IMF wafanya kikokotoo chao, mtatafuta pa kujificha
Ni lini Tanzania imewahi kuwa nchi tajili? Au na wewe ndio wale mazuzu waliaminishwa na yule mgonjwa wa akili kwamba Tanzania ni Dona kantre?
 
Mkuu wa nchi ambae ndio ndio custodian wa mali za taifa la watanzania kudai kuwa hawezi kufokea mtumishi wa umma ni kushangaza umma wa watanzania.

Kwamba watumishi wa umma wakiharibu atawabembeleza?

Nimekaa na wazee wengi waliofanya kazi na hayati Julius Nyerere wanasema wazi kuwa Mwalimu alikuwa mkali sana.

Ilitokea akikuita kwake Msasani au Ikulu ilikuwa lazima upate wasiwasi na woga mkuu.

Wengine aliwaita kuwapongeza lakini hawakuamini walichoitiwa wapo pia aliowafokea hadaharani au hata kifichoni.

Kwamba mkuu wa nchi unafanya kazi kwa kuonea aibu wateule wako? Kwamba utakuwa unawabembeleza?

Mbona hii sio sawa? Mkuu wa kaya lazima uwe mkali ili nidhamu ipatikane kuanzia juu mpaka chini.

Hatusemi ufokee watu kama watoto wako. Bali uwe na maamuzi na maelekezo yenye kuonyesha kuwa kuna kiongozi mwenye mamlaka aisiyetaka mzaha na anataka watu wafanye kazi.

Mfano, tulitegemea umkaripie January Makamba maana mradi wa JNHP unaweweseka kama vile hauna manufaa kwa wanaCcM wenzake.
Rais anajuwa kila kinachoendelea katika huo mradi wa umeme hiyo kampuni magu aliyoipa tenda bila ya ushindani haina uwezo wa kutosha mradi uko nyuma ya wakati na magufuli alikuwa halipi kwa wakati hayo ndiyo yaliyochelewesha mradi sasa unataka January afanye nini au rais amfukuze kwa sababu gani .Halafu haitakiwi rais aogopwe inatakiwa aheshimiwe na yeye awaheshimu wasaidizi wake ndio utaratibu mambo ya kufokeana ni ushamba ,samia anaendesha nchi kutokana na ethics za uongozi law sababu yeye mbobezi katika taaluma ya utawala wa umma si mwanajeshi wala mtafiti wa mabibo ya korosho kwa hivyo tumwachie mama afanye kazi chuki zako weka pembeni.
 
Matatizo ya watumishi uliyoyataja hapa yanaweza kumalizwa kwa kurekebisha mfumo wa ajira na ngazi za uwajibikaji sio kwa Rais kuzunguka maofisin na kufokea watumishi wa ngazi za chini na wasimamizi wao.

Bodi za hospitali, bodi za shule, bodi za vyombo kama TRA, polisi,TANROADS, TARURA, Halmashauri, ofisi za DMO, vinapaswa viwe na mamlka ya kufukuza watumishi wasiokidhi vigezo kwa haki na wepesi bila urasimu.
Upo sahihi sana. mimi nampenda sana mama samia ktk utendaji wake ila la hili la nidhamu ya moyoni kwa watumishi wa umma mama aliangalie vizuri.

Kuchelewa kazini, kutokatoka hovyo kuzurula, kwenda kucheza kamali wakati wa kazi na vijiwe vya mpira vinashusha sana nidhamu ya kazi ktk secta zote.

Utakuta 80% ya watumishi wa umma wanastahili kufukuzwa kazi kila siku kwa utovu wa nidhamu.

utakuta wizara zote za serikali zina cheo kiitwacho ofisi supevisor maajabu yake ofisi supevisor hafuatilii watoro kazini, wacheza kamali, wafanyao ngono maofisini wala kuwabana wachelewaji.

Hwa maO.S, utakuta siku zote ni father X-mass tuu na hupenda kununua stationary tuu!matokeo yake katika wizara zote za serikali huwezi kumtuka mfanyakazi aitwae workaholic(yaani yule aketie kitini na kujituma kazini mpaka anaambiwa nenda nyumbani kinguvu}

mimi binafsi namuomba sana mama awe mkali sana na avae ndita muda wote maana tupo katika kipindi cha heated economy la sivyo wajanja watamuangusha kisawasawa..
 
Rais wa nchi sio kama mume wako au baba au mama kwenye familia. Nchi ni ya wananchi wote na inaendeshwa kwa mihimili mitatu, taasisi na mifumo kwa kuzingatia sheria na taratibu maalum.
Ndio maana hata familia imekushinda,unataka kila mtu ajiongoze yeye mwenyewe,nn maana ya kuwa kiongozi mkuu?
 
kwani sasa hivi hamuwi kwenye matatizo? siku yakikukuta utashukiwa individually.

Hata kipindi cha Magu walikuwepo nunda kama wewe, ndio maana leo tunawaona Makonda na Sabaya wakitiwa akili.

Wangekuwa wameisha watu wa hovyo basi jiwe asingekuwa anafukuza/simamisha watu kila leo.

Concern ya Rais ni smart sana,tusimamie taratibu kama wasomi na sio nguruwe mpaka aswagwe.

Tujenge taasisi imara za kusimamiana,rais atapita lakini taasisi smart zitabaki. Mf mzuri Hayati amesepa halafu mnabaki na nini?hayati angekuwa smart angeimarisha taasisi na sio kukaza kichwa tu kama vile utakuwepo milele
Ndio maana nasema ujinga ni mzigo,kwa hiyo taasisi itakuwepo bira mkuu wa taasisi?, kwani tuna viongozi?, kazi ya kiongozi ni kufanya nini?,kuimba mapambio ni kucheza kwaito?
 
Tabia na hulka za waafrika esp Watanzania kwa namna ya makuzi yetu kuanzia nyumbani hatuna kitu kinaitwa nidhamu ya moyoni tuna nidhamu ya uoga ambayo ndio imetusaidia kufika tulipo leo
Mkuu wa Nchi anaposema anataka nidhamu ya moyoni sio kwa Watanzania Hawa ambao makuzi yao yalitegemea
1. Baba na mama wanataka nini kutoka kwa mtoto Kama ni kusoma basi usome na siyo kucheza na huwezi kutoa maamuzi tofauti na yao
2. Shuleni tunafagia huku tukiwa tumesimamiwa na viranja wakiwa wameshika fimbo Kama walimu
Tumekuzwa makuzi ya kusimamiwa hivyo kuniambia nije kuwa na nidhamu ya moyoni nikiwa na miaka 30 itakuwa ni ngumu Sana kwa iyo nitakapo pata huo mwanya nitafanya kazi as usual tu siku ziende
Afrika ni tofauti na ulaya/America kwenye Mambo mengi Sana na siyo lazima Kila kitu kiende Kama wao ni lazima nasi tuwe na mfumo wetu ili mradi tumekubaliana kufika hata wao miaka hiyo wamepitia ndio maana walitumikisha ndugu zetu
 
Sheria zifuatwe na watu wafanye kazi zao ndio cha msingi na wasipofanya kazi wawajibishwe kwa kufuata sheria zilizopo,hayo mambo ya kuogopwa, ukali au kufokafoka havisaidii chochote na mara nyingi vinajenga nidhamu ya woga tuu na madhara yake ni kushuka kwa utendaji wa kazi na watu wanabaki kufanya kazi kwa kujipendekeza ili waonekane tuu
 
Usichanganye ukali na jazba. Mkali ni kuchukua hatua stahiki dhidi ya kosa halali au uzembe, na haya hufanyika pasi na kinyongo wala kusaka sifa za kijinga.

Jazba ni kuchukua hatua za kukomoa, na wakati mwingine ni kuchukua hatua kwa nia ya kukomoa ama kudhalilisha na kupandikiza vitisho na nidhamu ya woga.

Mfano mrahisi, Nyerere alikuwa mkali, lakini Magufuli alikuwa na jazba.
Sasa jaziba mwisho matokeo yake ni nini siyo ukali? we jamaa pimbi kweli

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Marekani na Ulaya, ambapo tunawaiga kwa demokrasia, hawabembelezani.

Trump alikuwa anafukuza watu karibu kila siku.

Hakuna kitu kinachoitwa nidhamu ya moyoni!
Ujinga wako ni kwamba hujui hata Rais wa Marekani ana mamlaka gani US.

Rais wa Marekani ana mamlaka ya moja kwa moja Jeshini, CIA, FBI ,Immigration, Posta, IRS, Mambo ya nje na sehemu nyingine chache sana. Huko ndiko uliona Trump mwenye kichwa kibovu akifukuza na kofokea watu hovyo.

Rais wa Marekani hana mamlaka na hawezi kufanya chochote zaidi ya kushawishi sera juu ya walimu, madaktari, manesi, polisi, maafisa kilimo, afya, pensheni, idara za maji, umeme na sehemu nyingine nyingi. Na hata sera ambazo hazipendwi kwenye hizo sekta zinaweza kupingwa mahakama za majimbo na mahakama kuu.
 
Mkuu wa nchi ambae ndio ndio custodian wa mali za taifa la watanzania kudai kuwa hawezi kufokea mtumishi wa umma ni kushangaza umma wa watanzania.

Kwamba watumishi wa umma wakiharibu atawabembeleza?

Nimekaa na wazee wengi waliofanya kazi na hayati Julius Nyerere wanasema wazi kuwa Mwalimu alikuwa mkali sana.

Ilitokea akikuita kwake Msasani au Ikulu ilikuwa lazima upate wasiwasi na woga mkuu.

Wengine aliwaita kuwapongeza lakini hawakuamini walichoitiwa wapo pia aliowafokea hadaharani au hata kifichoni.

Kwamba mkuu wa nchi unafanya kazi kwa kuonea aibu wateule wako? Kwamba utakuwa unawabembeleza?

Mbona hii sio sawa? Mkuu wa kaya lazima uwe mkali ili nidhamu ipatikane kuanzia juu mpaka chini.

Hatusemi ufokee watu kama watoto wako. Bali uwe na maamuzi na maelekezo yenye kuonyesha kuwa kuna kiongozi mwenye mamlaka aisiyetaka mzaha na anataka watu wafanye kazi.

Mfano, tulitegemea umkaripie January Makamba maana mradi wa JNHP unaweweseka kama vile hauna manufaa kwa wanaCcM wenzake.
Ni leadership style yake! Hakusema hatawachukulia hatua bali hatafoka. Hana aina ya uongozi wa kufoka. Atawalea watakaoshindwa atawachukulia hatua kali. Kwa hiyo Madam President is right ,Mzee Magufuli was right n Baba wa Taifa Mwalimu was right. Kwani leadership style inategemea pia personal attitude ya kiongozi. Tusome kidogo leadership and governance. # Tusikuze mambo .
🙏🙏🙏
 
Tengenezeni mifumo imara yakiutendaji itakayosimamia sekta zote.Tusidanganyane kua kuna nchi ambayo rais anasimamia kila kitu.Ukali wa rais hauwezi kua na maana kama nchi haitakua na mifumo thabiti yakumrahisishia rais na wananchi kazi.Tutoke kwenye zama zakumtegemea mtu.
 
Mkuu kwenye hii hospital ninayofanyia kazi siku hizi tunaingia ofisi 07:30 then tunakuwa na vikao vya Morning Report mpaka 09:00 hadi 09:30.

Hapo mtaenda kuhudumia wagonjwa hadi kwenye 10:30 halafu watu wanaenda canteen kunywa chai. Chai inanyweka huku stori zinapigwa hata mpaka 12:00 hivi au zaidi.

Mkirudi mnafanya kazi saa moja au moja na nusu mnarudi canteen kupata lunch ndio mpaka saa 15:30 watu wanarudi ku-sign out. Siku imeisha.

Hiyo ndio nidhamu ya moyoni ya hawa Watanzania hapa nilipo. Enzi za Magufuli tulinyooshwa na kazi zilifanyika kwa weledi knowing ukizingua imekula kwako.

RIP Magufuli.
Kwahiyo ilo nalo unataka hadi rais aje kuwaambiwa muwajibike.kwa jinsi mnavyofanya unadhani nani mjinga kati ya nyie wafanyakazi na huyo rais anayetaka kila mtu ajitambue nakujisimamia mahali pake pa kazi.inaonekana shule mlizosoma hazikuwasaidia ndo maana mnashindwa kujiongoza nakurekebishana hadi msubiri rais aje awaambie.Waafrika tusipende kua ng'ombe kila mara.
 
Back
Top Bottom