The Palm Beach
JF-Expert Member
- Dec 30, 2015
- 1,967
- 4,267
Mkuu wa nchi ambae ndio ndio custodian wa mali za taifa la watanzania kudai kuwa hawezi kufokea mtumishi wa umma ni kushangaza umma wa watanzania.
Kwamba watumishi wa umma wakiharibu atawabembeleza?
Nimekaa na wazee wengi waliofanya kazi na hayati Julius Nyerere wanasema wazi kuwa Mwalimu alikuwa mkali sana.
Ilitokea akikuita kwake Msasani au Ikulu ilikuwa lazima upate wasiwasi na woga mkuu.
Wengine aliwaita kuwapongeza lakini hawakuamini walichoitiwa wapo pia aliowafokea hadaharani au hata kifichoni.
Kwamba mkuu wa nchi unafanya kazi kwa kuonea aibu wateule wako? Kwamba utakuwa unawabembeleza?
Mbona hii sio sawa? Mkuu wa kaya lazima uwe mkali ili nidhamu ipatikane kuanzia juu mpaka chini.
Hatusemi ufokee watu kama watoto wako. Bali uwe na maamuzi na maelekezo yenye kuonyesha kuwa kuna kiongozi mwenye mamlaka aisiyetaka mzaha na anataka watu wafanye kazi.
Mfano, tulitegemea umkaripie January Makamba maana mradi wa JNHP unaweweseka kama vile hauna manufaa kwa wanaCcM wenzake.
"UKALI" tu usiozingatia misingi ya utu, heshima, busara, hekima na sheria, ni UPUMBAVU na UJINGA na ni dalili za wazi sana za UTAWALA WA UDIKTETA..
Kwani binadamu gani aliyekamilika na asiyekosea? Hayupo!
Hata huyu mtu mwenye cheo cha kidunia cha "URAIS" naye ni binadamu na anakosea...!
Turudi kwa utawala wa Mwl. Julius K. Nyerere
Mwl. Julius K. Nyerere alikuwa mkali kweli. Lakini ukali wake haukuwa kama wa yule Mwendazake Magufuli.
Hili umethibitisha mwenyewe kuwa alikuwa akiwaita na kukemeana wenyewe kwa wenyewe huko ndani siyo hadharani mbele ya wanaoongozwa ktk namna ya kutweza utu na heshima ya mtu.
Nakupa changamoto moja na kisha tuambie hapa.
Katika utawala wa karibu miaka 25 ya Urais wa J. K. Nyerere, ni wapi aliwahi kumtukana waziri wake hadharani kwenye mkutano wa hadhara? Ni wapi amewahi kufukuza kazi mtumishi wa umma hadharani bila kufuata utaratibu wa kisheria?
All in all hujamwelewa Mama Samia na kauli yake hiyo. Hana maana ya hiyo unayoidhania wewe..!!