Mlioacha kazi za kuajiriwa na kujiajiri wenyewe nahitaji msaada wenu

Mlioacha kazi za kuajiriwa na kujiajiri wenyewe nahitaji msaada wenu

Kwa atakayepitia hapa nafikiri mjinga atamuona ni nani kulingana na comment zetu,sina hofu wala uoga kimaisha naishi maisha ya kawaida kabisa amabayo nasema Mwenyezi Mungu asante (Hivi wakati mwingine mnaposhindwa kukoment kistaarabu mnapungukiwa nini? Hili ni jukwaa tu sio hukukumu wala hatuwezi kumlazimisha aliyeoomba ushauri aamue kama sie tunavyotaka ),safari ya biashara ina kitu inaitwa break even period,ni kipindi ambacho biashara lazima ikutegemee kabla hujaitegemea,ok...sawa nakubaliana na wewe kazi aache kabla hajaanza kuisoma " return" ya biashara atakuwa na mkondo gani wa kuimarisha biashara hiyo?,kumbuka maisha ya kila siku yanahitaji pesa itoke ndani "and at the same time" hujaisoma poa return ya biashara, akikurupuka kuacha kazi atakumbuka.Kaka hata sisi pia ni waajiriwa lakini "at the same time" tunaujasilia mali na maisha yanasonga.
Narudia tena kazi asiaache mpake aweze kusoma return ya biashara imekaaje,kwani kazi ni jela hawezi kuwa muuajiriwa na mwisho awa siku mambo yakisimama wima kazi unaacha ?maisha ya biashara sio 1+1=2.
Kwanza Break Even haina maana biashara ikutegemee wewe kama ulivyoandika.BEP ni hali ya biashara kutozalisha faida wala hasara.
ABUBAKAR SHEKAU ameshakueleza kwamba ameshaona return ya kilimo biashara unataka aone return ipi ndio aache kazi wakati ameshaeleza kilimo kinalipa.
Hata ukiwa kwenye kazi haina maana kuwa upo salama,kuna matukio mengi ambayo yanaweza kutokea na kuharibu maisha yako yote kuliko hata kilimo biashara unachoofia.Mfano kufukuzwa kazi,kuumwa,kupatwa ajali,au majanga mabaya ya kusingiziwa ukafungwa.Hata mie ni Mfanyakazi wa serikali nimeona matukio mengi watu wanakumbana nayo hata mengine yameshawai kunikuta.
Acha kumtia uoga mwenzako la muhimu hakuna kazi ya kuajiriwa au kujiajiri isiyo na changamoto. ABUBAKAR yupo vizuri muache aache kazi ya kuajiriwa akafanye kazi ya kujiajiri kwa muda mwingi itamlipa.
 
Wewe SELEKWA ni muoga wa maisha kubali au ukatae. Hakuna tajiri ambaye ana mfumo kama huo wako.
 
Habar wanajamvi mimi ni Muajiriwa katika shirika Moja lisilo la kiserikali na kazi ninayo jishuhulisha nayo nje ya ajira yangu ni kilimo na pia nina malengo ya kufuga kuku wa aina zote yaani chotara, wa mayai na wanyama na malengo yangu ni kuacha kazi na kusimamia shuhuli zangu za kilimo na ufugaji. Sasa wadau ambao mliacha kazi za kuajiriwa na kujiajiri wenyewe mlipitia changamoto gani pindi Mlipoacha kazi.
MKUU NAHITAJI KUJUA ELIMU YAKO NI KIWANGO GAMI.ILI HATA NIKIKUSHAURI NIJUE NAKUSHAURI NANI NA NINI
 
Fanya kazi za kuajiriwa kama njia tu yakupata mtaji ili nawe uanzishe mradi wako. Hii ndio akili ya kisomi.
 
mkuu swali jingine una ekari ngapi unazo lima na zipo mkoa gani.na je unalima kilimo cha aina gani kumwagilia su cha mvua za msimu?
Nimeanza na ekari 4 za mahindi, ekari 3 za Michungwa na niko Mbioni kuanza kilimo cha cabbage niko Tanga
 
Nategemea Mvua
mkuu usiache kazi kwanza.kama mashamba yapo tanga na unaishi tanga .cha msingi ni kutenga muda tu ndugu yangu kazi itakusaidia kuongeza ukubwa maeneo na poa kuendesha kilimo biashara kwa mfamo una michungwa panda miti kama peaches,figs,embe,hiliki ambazo zi zao adimu na yana faa kwa uoto wa tanga baada ya miaka 5 unaongea lugha nyingine
 
Habar wanajamvi mimi ni Muajiriwa katika shirika Moja lisilo la kiserikali na kazi ninayo jishuhulisha nayo nje ya ajira yangu ni kilimo na pia nina malengo ya kufuga kuku wa aina zote yaani chotara, wa mayai na wanyama na malengo yangu ni kuacha kazi na kusimamia shuhuli zangu za kilimo na ufugaji. Sasa wadau ambao mliacha kazi za kuajiriwa na kujiajiri wenyewe mlipitia changamoto gani pindi Mlipoacha kazi.
Abubakar shekau umeibukia huku, kundi lako siliskii tena vipi?
 
Kwanza Break Even haina maana biashara ikutegemee wewe kama ulivyoandika.BEP ni hali ya biashara kutozalisha faida wala hasara.
ABUBAKAR SHEKAU ameshakueleza kwamba ameshaona return ya kilimo biashara unataka aone return ipi ndio aache kazi wakati ameshaeleza kilimo kinalipa.
Hata ukiwa kwenye kazi haina maana kuwa upo salama,kuna matukio mengi ambayo yanaweza kutokea na kuharibu maisha yako yote kuliko hata kilimo biashara unachoofia.Mfano kufukuzwa kazi,kuumwa,kupatwa ajali,au majanga mabaya ya kusingiziwa ukafungwa.Hata mie ni Mfanyakazi wa serikali nimeona matukio mengi watu wanakumbana nayo hata mengine yameshawai kunikuta.
Acha kumtia uoga mwenzako la muhimu hakuna kazi ya kuajiriwa au kujiajiri isiyo na changamoto. ABUBAKAR yupo vizuri muache aache kazi ya kuajiriwa akafanye kazi ya kujiajiri kwa muda mwingi itamlipa.
my comment was compact...muamuzi ni yeye! BEP is when you are supporting the bussines before the bussines starts to support you,lenga kwenye kushauri mdau nafikiri itapendeza zaidi kuliko kunitafasiri mimi (Wewe pia toa ushauri sasa),kila mtu ana mtazamo wake na hili ni jema ,hope one day atapata maamuzi anayoona yanamfaa yote kwa yote ni kumsaidia afanikiwe tu,kama mtazamo wako ni mzuri ok ataufata ...worry not ..this is the forum
 
Wewe SELEKWA ni muoga wa maisha kubali au ukatae. Hakuna tajiri ambaye ana mfumo kama huo wako.
sikuelewi maana sasa inanibidi nicheke tu...haya bwana nitafasiri hivo ..sijajua mfumo (system) unayoiongelea ni ipi? all in all wapi nilitakiwa niseme kipi au kipi si sahihi kwa mtazamo wako?(tupo katika kupanuana maono ya kimaisha pia)Main point niliyokuwa nayo mimi ni kuisoma return ya biashara imekaa vipi,sasa suala la kufanya upembuzi na kujua changamoto ndicho we unachokiita mfumo? basi kazi !haya elekeza nguvu za kumshauri mwenzetu na mie pia nifundishe hiyo unayoiita mifumo nyie mliofanikiwa.
"Narudia tena kama ni mfanyakazi wa kuajiriwa fanya analysis kuona performance ya biashara yako uliyoiianzisha kabla ya kuacha kazi,najua kujiajiri kuna raha yake ila na kuajiriwa kwa kiasi fulani kunaweza kukunyima fursa lakini mshahara pia unaweza kukusaidia kupambana au kupunguza ukali wa changamoto za biashara unayoianzisha -ni mtazamo wangu."
 
usiache wewe tafuta mfanya kazi akusaidiage tuu

....Ili ufanikiwe kwenye biashara yako au shughuli yoyote yako mwenyewe ni lazima uisimamie mwenyewe vinginevyo ni kujidanganya tuu. Kama ambavyo watumishi walioajiriwa wanavyotafuta loop holes za kupiga hela, kuiba etc ndivyo hivyo hivyo kwa mtu utakayemuweka akusimamie wakati wewe hupo.
 
mhi, fata malengo yako mkuu hapa kila mtu atakushauri kulingana na level ya ujasiri wake

....Ni hivi hakuna kitu kizuri kama kusikia/kujua what others think about what you want to do. Yaani kama atapitia maoni ya kila mtu hapa akayaweka kwenye makundi 2 ( wanaotaka asiache kazi na sababu zao na wanaomuunga mkono aache kazi na sababu zao) he will be in a very good position to make a rational decision.
 
Inawezekana kaxi yako IPO karibu sana na biashara yako...c ukaribu wa km au mita...LA hasha ni ukaribu wa kutoka kazin na kuifuatilia muda wote na wakati wote....ukaribu ktk biznes unayofanya ni jmbo LA msingi...NI HILO TU

....Aisee hii imenikumbusha jamaa yangu mmoja alikuwa mwajiriwa wa serikali Morogoro, na akawa na muda wa kutosha sana kufuatilia shighuli zake za kilimo na mashamba. Alikuwa anavuna mpaka gunia 300 za mpunga na mahindi, na akawa yuko vuzuri tuu. Sasa akapata kazi NGO moja with good salary but nje ya Morogoro, na baada ya muda mfupi shughuli za kilimo ziliyumba sanaa, coz ile NGO ilimuweka so bussy jamaa mpaka basi na kwa kweli aliyumba sanaa kwa sababu mapato ya kilimo yalikuwa makubwa ukilinganisha na ule mshahara. Baada ya mkataba kwisha jamaa aliachana nao na kurudi tena serikalini kwenye kituo chake na kuendelea na kilimo chake.
 
Kama unataka kujiajiri,ni vizuri ukafanya resechi ya kutosha kabisa kwenye hiyo sector unayotaka kuingia.
Hiyo research haitoshi kumfanya aache kazi. Ajue business environment inabadilika kila siku. Cha msingi awe tayari kubadilika na anaweza kujikuta anafanya kitu tofauti na kilichomfanya aache kazi. Kwahiyo kama umeingia sekta binafsi hili jambo unalopaswa kulikubali.
 
....Ni hivi hakuna kitu kizuri kama kusikia/kujua what others think about what you want to do. Yaani kama atapitia maoni ya kila mtu hapa akayaweka kwenye makundi 2 ( wanaotaka asiache kazi na sababu zao na wanaomuunga mkono aache kazi na sababu zao) he will be in a very good position to make a rational decision.
Irokos uko sawa mkuu,kwamba kazi acha kwa sababu 1,2,3.....au kazi usiache kwa sababu 1,2,3,4....uko perfect.Ume saidia ku edit story.
 
Asanten kwa ushauri ila kwenye kilimo nishaona mafanikio yake ila changamoto ni muda kwani kuna kipindi natakiwa kusafiri kwenda kuangalia miradi yangu ya kilimo na huku kazini nahitajika hivyo nashindwa kujigawa hivyo inabidi nimtume mtu sasa hapo ndio garama inavyoongezeka kwani lazima kijana umgaramie kila kitu kisha umpe na posho
Kama unaona kilimo kinalipa na uzoefu unao tayari basi huu ni muda mwafaka wa kufanya maamuzi. Ukiwepo wewe utafanya kwa scale kubwa zaidi ya sasa.
 
Back
Top Bottom