Mliokulia kijijini poleni sana, mnakula vyakula duni sana

Mliokulia kijijini poleni sana, mnakula vyakula duni sana

Hakuna chakula cha ajabu hata kimoja hapo,tatizo ni kwamba wewe unataka vyakula vizuri kwa muonekano

1.Makande hayo ndio yana virutubisho kwa sababu hayo mahindi unayosema magumu hayajakobolewa yana kile kiini

2.Wali na samaki ambaye hajaungwa ni kwamba hapo hupati cholesterol inayotokana na mafuta ya kuungia

3.Maziwa mgando yana nutrients kibao

Nashagaa unataka makande ya mahindi yaliyokobolewa halafu yawekwe sukari,hivi utaacha kuugua kisukari na presha kweli

Jifunze kuhusu vyakula aisee,hayo maandazi unayoyasifia yamepikiwa ngano iliyokobolewa na yakawekwa sukari yakapitishwa kwenye mafuta ni sumu tu,faida yake mwilini ni ndogo mno
Ni mazoea ndo tatizo ...sijazoea kabisa vyakula vyao kwa kweli..
 
Kuna uhaba wa msosi na kutojua kupika.
Na kweli mikoa mingine msosi kwao ni janga kinoma, uko hata kama unajua kupika ni sawa na bure maana misosi hamna.
Kwamfano mkoa wa mbeya misosi ipo kibao ila wanyakyusa na mapishi ni mbingu na ardhi, wengi hawajui kupika.
Hata ukifika mbeya town ukila kwenye migahawa yao msosi wao sio mzuri kama migawa ya dsm japo vinavyopatika dsm na mbeya pia vinapatikana kwa wingi tu.

Nazi na vikolokolo vyote vipo ila ndo ivo watu wa mbeya kupika wengi hawajui.
 
Mpaka leo hii mimi sio mtu wa kuumwa umwa na shukrani zote ni kwa MUNGU kwanza kisha ni hivyo vyakula duni vya kijijini unavyosema.
Vile ndio vyakula sasa sio hivi processed foods vinaleta kansa tu kila kitu makemikali ya viwandani.

Japo kijijini nilikuwa naenda likizo tu kwa bibi ila naweza sema faida nyingi mno kiafya na hata vile nachukulia maisha kiujumla.
 
Mpaka leo hii mimi sio mtu wa kuumwa umwa na shukrani zote ni kwa MUNGU kwanza kisha ni hivyo vyakula duni vya kijijini unavyosema.
Vile ndio vyakula sasa sio hivi processed foods vinaleta kansa tu kila kitu makemikali ya viwandani.

Japo kijijini nilikuwa naenda likizo tu kwa bibi ila naweza sema faida nyingi mno kiafya na hata vile nachukulia maisha kiujumla.
Cha ajabu ukiwapikia misosi ya town wanafurahi kinoma
 
Kuna mkoa siutaji niliendavkikazi huko kwenye kata fulani nikaagiza wali nyama nilishindwa kula,nyama imeungwa kwa mafuta mengi sana,shombo tupu,na ni migahawa yote,niliishia kula wali maharage wiki nzima
Duhhh ...balaaa
 
Nilienda usukumani. Picha linaanza wamechinja mbuzi hawaweki vitunguu swaumu kukata shimbi wala ndimi nkawaambia naombeni nipike mchuzi walibloo wenyewe wakashangaa eti htujui km kitunguu swaumu kinakata shombo, Wana karanga ila kande hawaweki karanga nikawawekea siku hyoo weee walikula balaa, kupika mi ndo nilikabidhiwa jiko,asubuhi chapati za mafutazsiku moja nkapika tambi kulikua na mgonjwa bwana wee waliinjoi mgonjwa alikula mpk akatamani tena.

Inshort mapishi Yako pwani bwanaaa tunajua hasaaa,nilikua napika wali Nazi plus ndondo wanakula hawabakishi hapo mi kwetu ndo sijui kupika sasa, nikawa nasema kimoyo wangekua wanakula vya wadogo zangu Hawa [emoji1][emoji1][emoji1]wangepagawa ila mlenda, mtindi na ugali vilinishinda aseehh.
Chakula ndo tafsiri ya ustaarabu,bara hakuna wanachojua kuhusu chakula zaid ya kuchemsha na maana tunasema hakuna ustaarabu!
 
Watu wengi wenye utapiamlo wanapatikana vijijini zaidi. Vijijini mara nyingi huwa wanakula vile wanavyozalisha zaidi bila kuzingatia mlo bora.
Ni kudra za mwenyezi Mungu tu kuwa bado mnaishi. Niko kijiji fulani sitataja mkoa. Niko na wenyeji wangu.

Asubuhi uji hauna sukari, mchana tumekula michembe. Usiku udaga na dagaa kama saba hivi kwenye bakuli.

Maisha haya magumu sana kijijini. Tuwaombee
 
Vijijini ndio kuna kiwango kikubwa cha utapiamlo kuliko mjini. Mijini watu wengi wanakula mlo bora zaidi kuliko vijijini.
Huwa wanaishi maisha marefu yenye nguvu kweli nafikiri sababu ya food style, pia huwezi kuta wananenepeana, unakuta kizee cha kipare kiko 75 ila kina nguvu kweli na shamba kinaenda.

Hivi vyakula vinavyofurahisha kinywa nadhani si rafiki kwa mwili maana vijana wa mjini kuna vitambi fulani huotaga mtu anaonekana mzembe kweli. Waangalie kwenye majukwaa ya mipira utawaona.
 
Anahitaji elimu ya mlo bora.
Hakuna chakula cha ajabu hata kimoja hapo,tatizo ni kwamba wewe unataka vyakula vizuri kwa muonekano

1.Makande hayo ndio yana virutubisho kwa sababu hayo mahindi unayosema magumu hayajakobolewa yana kile kiini

2.Wali na samaki ambaye hajaungwa ni kwamba hapo hupati cholesterol inayotokana na mafuta ya kuungia

3.Maziwa mgando yana nutrients kibao

Nashagaa unataka makande ya mahindi yaliyokobolewa halafu yawekwe sukari,hivi utaacha kuugua kisukari na presha kweli

Jifunze kuhusu vyakula aisee,hayo maandazi unayoyasifia yamepikiwa ngano iliyokobolewa na yakawekwa sukari yakapitishwa kwenye mafuta ni sumu tu,faida yake mwilini ni ndogo mno
 
Ni kudra za mwenyezi Mungu tu kuwa bado mnaishi. Niko kijiji fulani sitataja mkoa. Niko na wenyeji wangu.

Asubuhi uji hauna sukari, mchana tumekula michembe. Usiku udaga na dagaa kama saba hivi kwenye bakuli.

Maisha haya magumu sana kijijini. Tuwaombee
Natural food hovyo..!!! Mjini kuna junk food za kutosha na ndo unazotambia
 
Ukame huu tango unalipata wapi, yaani kuna mikoa kama Morogoro, Mbeya na Kagera ina nafuu ila kuna mikoa ukame umewatandika wanakula wasife
Alaa, kumbe ni issue ya ukame na siyo kawaida tu ya kila siku?!!!!!!!
 
Tulienda kwa bibi aunt akapika wali na pilau wandava wakawa wanachukua pilau wanaweka juu ya wali kama mboga kudadeki kucheka nashindwa najikausha tu.
Kama hapakuwa na mboga walikuwa sahihi
 
Vijijini ndio kuna kiwango kikubwa cha utapiamlo kuliko mjini. Mijini watu wengi wanakula mlo bora zaidi kuliko vijijini.
Mijini wanategemea chakula kitoke vijijini wanunue.
Katika vijiji vyenye njaa ni kweli ulichosema. Ila vijiji vyenye neema ya mvua si kweli.
 
Nilishaonaga hiyo hali vijiji vingi nilivyowahi kufika lakini kilichonishangaza zaidi ni kwamba unakuta familia inakula ivo lakini baba ana ng'ombe zaidi ya 30 na mbuzi zaidi ya 50.

Unakuta ana uwezo wa kuuza ng'ombe wawili tu na kufungua biashara ambayo itaingiza kipato cha kuwahakikishia chakula kizuri kwa familia lakini kwao kuwaambia habari za kuuza ng"ombe hawakuelewi kabisa. Wanakwambia hawa ndo wanalinda familia. Umasikini upo akilini!!!!!!

Nilishuhudia mzee mmoja ameumwa mpaka akafariki lakini aligoma kabisa kuuza ngombe ili ipatikane hela akafanyiwe matibabu hospitali.
 
Mijini wanategemea chakula kitoke vijijini wanunue.
Katika vijiji vyenye njaa ni kweli ulichosema. Ila vijiji vyenye neema ya mvua si kweli.
Hata wakiwa navyo kupika ni shida
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Back
Top Bottom