Pwani ya wapi mbona Zanzibar hawajui kupika mboga.
Vijana wa vijiji hawana vitambi kwasababu ya aina ya vyakula wanavyo kula.Huwa wanaishi maisha marefu yenye nguvu kweli nafikiri sababu ya food style, pia huwezi kuta wananenepeana, unakuta kizee cha kipare kiko 75 ila kina nguvu kweli na shamba kinaenda.
Hivi vyakula vinavyofurahisha kinywa nadhani si rafiki kwa mwili maana vijana wa mjini kuna vitambi fulani huotaga mtu anaonekana mzembe kweli. Waangalie kwenye majukwaa ya mipira utawaona.
Hiyo huku nilipo,nikienda kwa jirani wananiambia kabisa karibu chai lkn haina viungo kama ulivyozoea,Kwanza wanawake wa kiislamu asilimia kubwa ni wapishi wazuri hata awe kijijini, lakini pia watu wanaoishi mwambao mwa bahari au ziwa bila kujali itikadi yao hawa wanafahamu mapishi sana, aibu utaipata bara labda kwa watu wachache tu niliwahi kunywa chai kibondo wamechemsha maji tu, wakaweka majani na sukari imeisha hiyo wakati nishazoea chai ina mdalasini, hiriki na tangawizi kwa mbali au wali unakua na harufu safi sana inabidi wanawake wajifunze mapishi ya aina tofautitofauti
Vyakula hamna[emoji16], na kijijini nako ukame.Mjini pia kuna hali tete
Boss, Embu niambie, kwenye hii miji uliyotaja mjini ni wapi na km ngapi? Maana hii ni nchi yetu sote na tunaijua kutokana na shughuli zetu tunazifanyia humu.Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Morogoro, Mbeya na Dodoma zina sehemu kubwa ya maeneo ambayo ni mjini.
Kabisa mkuuVijana wa vijiji hawana vitambi kwasababu ya aina ya vyakula wanavyo kula.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Inategemea
Huyo aliyeenda huko na kuibuka na uzi huu unadhani anajua kupika? Kama anajua kwanini asiwapikie? Diko diko hata la dagaa lipo.Hawana option kuna njaa,nao wanatamani kula madikodiko,pili hawajui kupika
Naam ulimi unafurahia lakini mwili unakulaumu unasema huyu jamaa huku kuunga unga kwa nini...., Wakati michemsho au sometimes kwa mboga partial cooked inatosha kupata nutrients.... Ngoja tumkomoe kwa vijimagonjwaNilienda usukumani. Picha linaanza wamechinja mbuzi hawaweki vitunguu swaumu kukata shimbi wala ndimi nkawaambia naombeni nipike mchuzi walibloo wenyewe wakashangaa eti htujui km kitunguu swaumu kinakata shombo, Wana karanga ila kande hawaweki karanga nikawawekea siku hyoo weee walikula balaa, kupika mi ndo nilikabidhiwa jiko,asubuhi chapati za mafutazsiku moja nkapika tambi kulikua na mgonjwa bwana wee waliinjoi mgonjwa alikula mpk akatamani tena.
Inshort mapishi Yako pwani bwanaaa tunajua hasaaa,nilikua napika wali Nazi plus ndondo wanakula hawabakishi hapo mi kwetu ndo sijui kupika sasa, nikawa nasema kimoyo wangekua wanakula vya wadogo zangu Hawa [emoji1][emoji1][emoji1]wangepagawa ila mlenda, mtindi na ugali vilinishinda aseehh.
Nimekanyaga mikoa yote ya nchi hii.
Ukiona chakula kitamu Sana huko bara basi fuatilia Routes zote za mpishi WA chakula hicho lazima awe amewahi kufika Pwani au amewahi kuishi na watu walioishi Pwani
Uko sahihi,kuna mkoa nilikula ile chapati yenye kurasa nikauliza mpishi nikaonyeshwa kijana toka zanzibarNimekanyaga mikoa yote ya nchi hii.
Ukiona chakula kitamu Sana huko bara basi fuatilia Routes zote za mpishi WA chakula hicho lazima awe amewahi kufika Pwani au amewahi kuishi na watu walioishi Pwani
Sahihi kabisa,dagaa ni mboga moja safi sana ila watu wa bara hawaijuliiWanaokupikia hawajui
Utaotaje kitambi huku umeshinda shambani unalima hekari nzima peke yako,ukirudi unakutana na michembeVijana wa vijiji hawana vitambi kwasababu ya aina ya vyakula wanavyo kula.
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji119]Ni kudra za mwenyezi Mungu tu kuwa bado mnaishi. Niko kijiji fulani sitataja mkoa. Niko na wenyeji wangu.
Asubuhi uji hauna sukari, mchana tumekula michembe. Usiku udaga na dagaa kama saba hivi kwenye bakuli.
Maisha haya magumu sana kijijini. Tuwaombee
Ni Dsm pekee ambayo unaweza enda km 30 kila upande na bado pamechangamkaBoss, Embu niambie, kwenye hii miji uliyotaja mjini ni wapi na km ngapi? Maana hii ni nchi yetu sote na tunaijua kutokana na shughuli zetu tunazifanyia humu.
Arusha ina km kama 37 elfu ikiwa na maeneo haya
Arusha district
Arusha city council
Karatu
Ngorongoro
Longindo
Monduli
Mwanza kama km elf 25 ikiwa na maeneo haya
Ilemela
Magu
Kwimba
Misungwi
Nyamagana
Sengerema
Ukerewe
Dodoma km elf 41 kama sio 42
Maeneo
Dodoma
Bahi
Chamwino
Kongwa
Mpwapa
Chemba
Kondoa
Tembea uoneDar es Salaam, Mwanza, Arusha, Morogoro, Mbeya na Dodoma zina sehemu kubwa ya maeneo ambayo ni mjini.
Ukivuka igoma tu unautafuta kisesa,hivi kisesa ni mwanza au simiyuNi Dsm pekee ambayo unaweza enda km 30 kila upande na bado pamechangamka
Majiji mengine yote ukivuka km 10 tu kila upande hakuna kitu.
Mwanza ukivuka Igoma tu hakuna kitu