Mnajisikiaje kuona msiyempenda ndiye anashangiliwa na wapiga kura?

Mnajisikiaje kuona msiyempenda ndiye anashangiliwa na wapiga kura?

A. Mazuri ya JPM. 1. Uhodari na uthubutu. 2. Nidhamu serikalini hadi chama (walitiishwa) kwa nguvu ya hatari. 3. Kujipambanua kuwa mtetezi wa wanyonge (akiliona bango lako au sauti ya kilio chako ikisikiwa, basi utaskia "mwacheni aje" ). 4. Kudhibiti utoroshwaji madini kwa jitihada za kujenga ukuta wa milerani nk. 5. Majangili (wauaji) wa tembo walipoteana. 6. Kujenga hospital za wilaya. Barabara, madaraja, reli, kufufua reli ya kaskazini. Jamani na mengine mengi sana sana. B. MABAYA YALIYOJITOKEZA KTK UTAWALA WA JPM: 1. Wasiojulikana. Hawa jamaa walikuwa hatari. 2. Demokrasia ilifariki na kuzikwa. (hakukuwa na uchaguzi, bali maigizo ya uchaguzi). Wagombea wa upinzani walienguliwa kibabe kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa hadi uchaguzi mkuu. Huku lete fyoko uone. 3. Kushtakiwa na kutupwa gerezani kwa kundi flani. Jamani kweli mazuri ya JPM ni mengi kuliko MABAYA. Tuendelee kumkumbuka kwa MEMA kama alivyosema yeye. LAKINI, kama wapo walioumizwa naye na wanamkumbuka kwa mabaya, basi ni haki yao pia.
 
Sawa amekwenda, lakini ana nguvu mara mia zaidi ya walio hai. Hapo unasemaje?
Nguvu ipi Sasa? Yaani 2025 ni Samia vs Lissu na wote hapo hawampendi JPM Sasa nguvu ipi hiyo unaongelea?
 
Aliyemdanganya SASHA kwamba kutambua juhudi za JPM kunamshushia umaarufu alimdanganya sana, kifupi anampoteza na kumfanya aonekana kituko
Hivi SASHA ndo nani mkubwa?
 
Hii habari naona imekuwa posted mara ya 8 sasa hapa JF
Jamani huyo mtu kama hamuwezi kumtumia Gwajima amfufue ndio basi tena, hata ashangiliwe namna gani haisaidii
Ungekuwa na akili ungejali thamani yetu sisi tunae amini katika uzalendo wake ambae tuko hai cc ndo tuna maamuzi ya asali zenu ila kwa sababu ya kiburi endeleeni kumdharau
 
Ungekuwa na akili ungejali thamani yetu sisi tunae amini katika uzalendo wake ambae tuko hai cc ndo tuna maamuzi ya asali zenu ila kwa sababu ya kiburi endeleeni kumdharau
Nyie ni misukule wake mliokuwa mnaaminj uongo wake
 
Yani hata leo huko ccm wangepambanisha kivuli cha Jpm na mtu kama Hangaya au Kikwete bado Jpm angeshinda tu.yule mzee alikubalika bwana
 
Kazi ya Mungu haina makosa na wala hairekebishwi na binaadamu yeyote
 
Kisha baada ya kushinda anaenda kuongoza kuzimu?
 
Mtu amekufa miaka miwili imepita ila anawashinda waliohai, teh teh teh teh.
Pamoja na maisha magumu wananchi waliokuwa nayo, walitaka waziri wa nishati au Mku wa TANESCO amutaje kwa jina "JPM" kwamba ndie alieamua kumuenzi kwa vitendo Mw.Nyerere angalau kuanza ujenzi wa Bwawa la Umeme.
Na zawadi pia zikagawiwa sawa kwa viogozi wote tangu awamu ya kwanza mpaka ya 6.
 
Back
Top Bottom