Mnaofikiria kufanya kazi na Manara baada ya haya mjiulize mara mbili. Anachowafanyia Simba nanyi atawafanyia

Mnaofikiria kufanya kazi na Manara baada ya haya mjiulize mara mbili. Anachowafanyia Simba nanyi atawafanyia

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Waswahili wana usemi '"Jasiri haachi asili" hivyo wanachopitia Simba kwa sasa kupitia aliyekuwa anafanya kazi hapo ni fundisho tosha kuwa mkae nae kwa tahadhari kwani si Mtu wa staha.

Mtu aliye tayari mpoteze yote mliyofikia kwa kuwa tu maslahi yake yamevurugika ni Mtu Mbaya na Msaliti.

Manara sasa ameonesha rangi zake halisi, kwamba kwake maslahi yake ni muhimu kuliko ya kundi, hata kama aliwahi kuwaaminisha Wanakikundi Wenzake kuwa yeye ni Mwenzao wa kufa na kuzikana.

Kama Manara alituhumiwa na Wenzake kuwa 'anaropoka' siri za kambi kwa Wapinzani...kwa anayofanya sasa bado anataka tuamini kuwa alikuwa anasingiziwa?

Simaanishi kuwa Manara hakukosewa au hakupitia maudhi ya hapa na pale ndani ya Simba, lakini ni vipi Askari akiamua kutoka hadharani kuanza kuropoka kila yanayomkuta kwenye kambi yake?

Au Muajiriwa aanze kuropoka mapungufu ya Kampuni/Taasisi aliyokuwa anafanya nayo kazi kabla?...huenda kwa wakati huo kama Mshindani/Mpinzani utafurahia kusikia...lakini kama una akili lazima utabaki na maswali "je mimi nitakuwa salama kuwa karibu na Mtu kama huyu?"

Anachokifanya Manara ni dhahiri kuwa kwa sasa hajali tena nini kitatokea kwa Simba. Kama ana ugomvi na Moo hivi kuna haja gani kutamani kuwasumbua wote wanaoifuatilia na kupenda mafanikio ya Simba?

Mnapokuwa katikati ya kusheherekea matunda/mafanikio ya kazi Mtu pekee mnayemtarajia aje awavurugie sherehe yenu ni yule ambaye siku zote anapingana nanyi na hapendi mafanikio yenu, na si yule aliye/anayewaaminisha siku zote kuwa ni sehemu yenu .
 
!
20210805_091648.jpg
 
Ni suala la muda tu tutakuja kujua mengi ya wakina Bakhresa na na wakina GSM. Kwa jinsi alivyokuwa anajionyesha ana ukaribu wa kupitiliza na Mo halafu kaja kumvua nguo mbele ya waandishi wa habari kiasi kile basi wanaofuata kwenye mstari ni hao Bakhresa na GSM.
 
Haji anaweza kuwa kakosea kwenye baadhi ya kauli zake ila kilichomuuma zaidi ni kuambiwa kuwa anaihujumu team anayaoipenda.

Root cause ya hasira za Haji zilianza kwa kuambiwa kuwa anaihujumu team, kama ni maslahi mbona kayavumilia kwa miaka 6?
 
Mbumbumbu fc mshasahau kuwa mlipomtimua Kaduguda aliongea mbovu na kudai hela zake za maandazi na mihogo aliyokuwa anawanunulia wachezaji pia akidai cone zake za mazoezi,lakini leo hii yupo Simba kama kiongozi. Na Manara atarudi tuu.
 
Haji anaweza kuwa kakosea kwenye baadhi ya kauli zake ila kilichomuuma zaidi ni kuambiwa kuwa anaihujumu team anayaoipenda.

Root cause ya hasira za Haji zilianza kwa kuambiwa kuwa anaihujumu team, kama ni maslahi mbona kayavumilia kwa miaka 6?
Hakika,Haji kuitwa msaliti hii ndo imemvuruga kichwa mpaka akaachia voice not kwa bimdada CEO.
 
Haji anaweza kuwa kakosea kwenye baadhi ya kauli zake ila kilichomuuma zaidi ni kuambiwa kuwa anaihujumu team anayaoipenda.

Root cause ya hasira za Haji zilianza kwa kuambiwa kuwa anaihujumu team, kama ni maslahi mbona kayavumilia kwa miaka 6?
Kwa jinsi alivyobwabwaja jana mbele ya waandishi wa habari na dunia yote ikasikia namana alivyoiacha Simba uchi kwanini tusiamini kuwa alikuwa anahujumu timu
 
Haji anaweza kuwa kakosea kwenye baadhi ya kauli zake ila kilichomuuma zaidi ni kuambiwa kuwa anaihujumu team anayaoipenda.

Root cause ya hasira za Haji zilianza kwa kuambiwa kuwa anaihujumu team, kama ni maslahi mbona kayavumilia kwa miaka 6?
Bado alikuwa na nafasi ya kutanguliza hekima na kuacha muda uongee.

Kuja hadharani hakumsafishi na tuhuma bali ni kuongeza tatizo kwani kila Mtu sasa atakaa naye chonjo...anaweza akapewa kazi na kampuni lakini hawatamuamini.
 
Na hapo kaongea kidogo tu, kuna sehemu alikua anawahi.

😀😀
Haji kuna maeneo kateleza kutokuchukua hatua mapema ilhali alikua keshaona viashiria vyote vya matatizo,ila nimemsikiliza kwa makini kabisa kwenye press yake kuna maeneo Mo na C.E.O wajirekebishe, la sivyo huko mbeleni ikitokea mgogoro mwingine wataoangisha na dot za Haji hapatokalika pale Msimbazi.
 
Kwa jinsi alivyobwabwaja jana mbele ya waandishi wa habari na dunia yote ikasikia namana alivyoiacha Simba uchi kwanini tusiamini kuwa alikuwa anahujumu timu
Haji kautangazia uma kuwa yeye si Mtu wa kushirikishwa mambo ya siri ya Mtu au Taasisi...kuna siku atayapeleka tu pasipohusika.
 
Haji kuna maeneo kateleza kutokuchukua hatua mapema ilhali alikua keshaona viashiria vyote vya matatizo,ila nimemsikiliza kwa makini kabisa kwenye press yake kuna maeneo Mo na C.E.O wajirekebishe, la sivyo huko mbeleni ikitokea mgogoro mwingine wataoangisha na dot za Haji hapatokalika pale Msimbazi.
Kabisa, hata mimi sipo hapa kumkingia Moo au Babra kifua.

Lakini bado naamini Haji alikuwa na nafasi ya kutanguliza busara na kuwasilisha yanayoendelea bila kulazimika kutaka kuitikisa Timu nzima ipoteze muelekeo, Timu ambayo yeye mwenyewe ni sehemu yake na anatamani iwe kwenye mafanikio muda wote.
 
Haji kajiharibia sana. Ni wazi ametumwa na Azam akaongee hivyo.

Awali alisema ataongea na waandishi kwa lengo la kuwashukuru wana Simba, badala yake ndio kaja kuharibu kabisa hata kumfikiria kumrudisha tena ni ngumu kwa kweli. Aliondoka Ezekiel Kamwaga mbona alikaa kimya na sasa amerudishwa.
 
Kajiharibia sana. Ni wazi ametumwa na Azam akaongee hivyo.

Awali alisema ataongea na waandishi kwa lengo la kuwashukuru wana Simba, badala yake ndio kaja kuharibu kabisa hata kumfikiria kumrudisha tena ni ngumu kwa kweli.
Atarudi tuu,mshasahau ya Kaduguda?
 
Haji kajiharibia sana. Ni wazi ametumwa na Azam akaongee hivyo.

Awali alisema ataongea na waandishi kwa lengo la kuwashukuru wana Simba, badala yake ndio kaja kuharibu kabisa hata kumfikiria kumrudisha tena ni ngumu kwa kweli. Aliondoka Ezekiel Kamwaga mbona alikaa kimya na sasa amerudishwa.
Hata kama sio kurudi kazini lakini kuna suala na mahusiano na kutunza heshima yako na ya Mwingine.

Kuna mahali unaweza ukawa na jambo lako Watu waka ku reccomend kwa uzuri.
 
Simba kwa hakika ni mbumbumbu, Kaduguda alichukua jezi, mipira, nyavu na vifaa vingine vya mazoezi baada ya Simba kushindwa kumrudishia fedha zake alizo wanunulia wachezaji chapati na vitumbua alafu vingozi wakamtimua chakushangaza Kaduguda karudi Simba na akawa mwenyekiti. Kwaiyo ata Haji atarudi na kuiongoza Simba kwakua umbumbumbuni hakuna fomula.
 
Back
Top Bottom