Mnaotumia bidhaa za Apple® Mnapigwa sana. Sijui hata mnavyotoa hela mnafikiriaga nini?

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
Kampuni la Kimarekani Apple, maarufu kwa kuuza bidhaa za electronics na accessories zake, wanauza ivyo vitu bei ghali sana.

Inawezekana ikawa ni value for money, ila kuna baadhi ya vitu ni wazi wanawaibia "loyal customers" wake, sema ndio ivyo hawaoni au wanajizima data.

Tuachane na iPhone zao kua Million 3 kwenda juu, au Laptop zao za kishua. Ebu Kwa mfano checki izi products:

Mac Pro wheels $700 (Tsh Mil 1.8)

Hii sio computer, ni magurudumu manne ya kuweka kwenye CPU sijui tuiite ya Mac Pro. Hujakosea kusoma.

Haya matairi ilibidi wayagawe bure unavyonunua iyo bidhaa yao.

Mac Pro stand $1000 (Tsh Mil 2.6)

Naam. Mil 2.6 tunanunua stendi ya kuiwekea Monitor yetu ya Mac.
Hii pia ilitakiwa upewe bure. Kwann walitengeneza computer isio na stendi?

Mikanda ya saa $100 (Tsh Laki 2.6)

Achana na bei ya saa, mkanda tu huu unauzwa laki 2 na nusu na zaidi.


Airpods Max $550 (Tsh Mil 1.4)
Utakua ushakutana na mabishoo wamevaa copy ya aya madude.

Aisee original yake ndio ivo, Mil 1.4 cash.

Apple Pencil $130 (Tsh 340,000/=)
Hii wenzio Samsung ukinunua Tab wanakupa bure sijui kwann wao wanauza.


Mac Pro $7000 (Tsh Mil 18)
Ukiliona kwenye picha kama kidude cha kusugulia nyanya au karoti. Ila ndio ivyo tena, bei ya gari.



Waya type C $30 (Tsh 77,000/=)
Waya tu, wa mita 2 unauzwa hivi. Bila kichwa. Bila protector. Bila kava. Waya.


Cover la Simu la Silicon $50 (Tsh 130,000/=)
Haya makava tunayaona kwa elfu 5 yanauzwa Kariakoo. Wao wanauza bei ya simu.



Mac Pro Display $1500 na Stendi yake inafika hadi $2000 (Tsh Mil 3.9 hadi Mil 5.1)

Hii ni display ya kile kidude cha kusugulia nyanya. Display tu.



Airpods Pro $250 (Tsh 650,000)
Sijawahi tumia kwahiyo sijui mziki wake ila kutoa Laki 6 kisa utu tudude hapana.


Polishing Cloth $20 (Tsh 52,000)
Kitambaa cha kusafishia kioo cha simu au laptop au ipad kinauzwa bei ivo.


Apple Mouse $100 (Tsh 250,000)
Hii ni mouse kama unayoijua sema ya kuchaji.Hafu port ya kuchajia ipo chini kwahiyo ikiisha chaji hauwezi kutumia. Kha.

Mi labda sina hela, ila kununua bidhaa ya Apple naona kabisa napigwa. Ata iPhone najua ina nguvu ina balaa ila kama wanakuibia kwenye bidhaa zingine kwann wasikuibie kwenye iPhone.

Nimejiandaa kuambiwa nitafute hela.
 
Hongera sana kwa uchambuzi wako mzuri..
 
Ukimuuliza kwanini unanunua iPhone ya mamilioni wkt Hali yako Ni dhoofu bin Khali utamsikia oooh iPhone Ina security Kali Sana,vitu vyangu viko salama Sana.

Yaani we jamaa wa huko ikungi Nani ana shida ya kuku-hack wkt vitu vyenyewe ulivyojaza kwny simu yako Ni porno tu za xvideos,xhamster.
 
Vitu vyao ni bora sana hata hivyo hela yetu ukiibadili kwenye hela yao ndio unakutana na hayo Mamilioni ila wao wanauza bei za kawaida kwa Wateja wao...hao jamaa bidhaa zao zipo sawa sana ni vile hela hatuna tupo busy kuwaponda...istore ya East Gate Mall..
 

Attachments

  • 20240517_132309.jpg
    1.6 MB · Views: 6
  • 20240517_132321.jpg
    2 MB · Views: 12
  • 20240517_132025.jpg
    1.6 MB · Views: 7
  • 20240517_132333.jpg
    1.7 MB · Views: 7
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…