Mnaotumia bidhaa za Apple® Mnapigwa sana. Sijui hata mnavyotoa hela mnafikiriaga nini?

Samsung kuna simu wanatumia mediatek, Nokia kuna simu wanatumia SPD, ulishasikia iPhone anatumia mediatek au SPD?

Apple alikuwa anatumia intel kwenye computer zake hivi sasa ana processor zake za M series, jamaa wapo vizuri...
Kwani MediaTek ni mbaya?
 
Hiyo AirPods Max kuna jamaa anayo copy, bas anavyosumbua wenzie.
Na kaletewa kutoka Australia, bas full tafraniii.
 
Cha ajabu vioo vyao wanamtegemea samsung ..?
 
Mchina aliniangusha aisee mimi mwenyewe nilikuwa na Redmi note 11 pro nilikuwa navimba mega pixel 108 AI Camera kumbe hamna kitu ila kuna vitu Redmi ipo poa sana
Sometimes uangalie hiyo Redmi ni Tsh ngapi na hiyo iPhone ni Tsh ngapi
In fact hata simu ya Xiaomi yenye Kamera kali kuliko zote (Xiaomi 14 Ultra) ina 50MP wakati midrange zake zina hadi 200MP. Kwa hiyo megapixel si kigezo cha ubora wa kamer
 
Wewe siyo mtumiaji wa bidhaa za Apple lakini unaandika makala ndefu sana na kujaza picha za bidhaa hizo zaapple kwa nini? Unataka kushwashishi wengine pia wasizitumuie kusudi muwe wengi? Kama humudu kutumia bidhaa za apple waachie wanaozimudu wewe tumia zile unazozimudu, maisha yanaendelea. Umeandika bdihaa za apple kama vile unatumia bidhaa nyingine zote sipokuwa za apple tu ilihali makampuni ya eletcronics leo yapo lukuki. Kama wewe hutumii Apple, kuna wengine hawatumii Samsung, kuna wasitotumia Tecno, kuna wasiotumia Huawei, Kuna wasiotumia BLu, kuna wasiotumia Google Pixle, Kuna wasiotumia Infix, Kuna wasiotumia Xiaomi, Kuna wasiotumia Motororola, Kuna wasiotumia Micromax, kuna wasitumia brand nyingi sana za electronics; je wewe unazitumia zote hizo isipokuwa apple tu?
 
ukiwa mwongo mwongo unapaswa kua na akili sasa wewe akili huna. tuishie hapo nisije kukuvua nguo.

nb. aya ya 1 naafikiana na wewe.
 
Mkuu naona labda sijui ni kwa makusudi au umeamua kufurahisha tu genge, vifaa vy Apple ni vifaa vyenye ubora sana, lakini pia kampuni nyingine nyingi zinatoa kompyuta/laptops ambazo bei zake ni sawa na hizi za Apple hapa Bongo tu kuna watu wanaunda PC za game na kuuza milioni 9 hiyo ni CPU tu bila monitor, sishangai kuona bei kubwa sababu pesa yetu ya madafu kwa sasa ipo chini sana kununua USD sasa ni 2690 , wa kulaumu ni serikali yakokwa kuifanya pesa ya madafu ishuke thamani, hata magari kuna benz, suzuki VX8 bei ha hata spare zake hazifanani mkuu. Nikuambie tu kama umetumia vifaa vya Apple basi ni sawa na mtu anayetumia VX8 au benzi umwambie aendeshe kirikuu mkuu. Kwa mtu ambaye maisha yake yanategemea data,graphics,game/videos rendering na takataka nyingine kuwa na vifaa vya apple ndio uwekezaji kwenye uzalishaji na si anasa,hiyo unayoita kikunia nyanya haina tofauti na PC wanazounda wabongo zipo hata za 10milion kulingana na uwezo wake. Ngoja na mimi nikuambie sijui umejiandaa? TAFUTA HELA, mengine yote utayaona rahisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…