Mnapofanya Maendeleo msisahau kushirikisha ndugu zenu hata Kama mna ugomvi

Mnapofanya Maendeleo msisahau kushirikisha ndugu zenu hata Kama mna ugomvi

Je yeye Mke wako, miradi yake wewe inaifahamu?
Hiyo ni yake. Akitaka niifahamu atanijulisha. Mimi niko very focused na mambo ya familia yangu.

Sijui hata makeup zake kwa majina. Yeye ni minor kwangu, kwa nini nimchunguze na kumfuatilia?

Kila siku natakiwa niwe Bora kuliko nilivyokuwa Jana. Daima nashindana na Jana yangu, ndio adui yangu mkubwa
 
Wanandoa wamekuwa wabinafsi sana siku hizi, kila mmoja anajifanyia maendeleo yake bila kumshirikisha mwenzake. Wake hujenga kwao kwa siri, waume hujenga nyumba kwa siri mke hajui wala ndugu hawajui
 
Wanandoa wamekuwa wabinafsi sana siku hizi, kila mmoja anajifanyia maendeleo yake bila kumshirikisha mwenzake. Wake hujenga kwao kwa siri, waume hujenga nyumba kwa siri mke hajui wala ndugu hawajui
 
We chukua tu hiyo nyumba maana kwa wabongo sisi unakuta hata hizo pesa alijengea ni za wizi kama vile rushwa au utapeli.

Ni sawa tu hizo mali wakatumia usiowajua ukifariki kuliko kufaidisha ndugu mkuda, mnoko na asiyependa maendeleo yako...

Wanandoa wamekuwa wabinafsi sana siku hizi, kila mmoja anajifanyia maendeleo yake bila kumshirikisha mwenzake. Wake hujenga kwao kwa siri, waume hujenga nyumba kwa siri mke hajui wala ndugu hawajui
Kabisa mkuu
 
Nina Jirani ( sasa ni marehemu) alikuwa na Mgogoro na mke wake, kuhusu Mgogoro wao hatukujua mpaka jirani alipofariki.

Sasa hii story ni mrefu ila Kwa unduly Jirani alijenga nyumba ya biashara ( guest house, na frame za maduka) maeneo ya Kigamboni bila mke wala watoto kufahamu, na alipojenga pembeni kilibaki kiwanja Kikubwa tu, na aliyejua Alikuwa ni rafiki yake mmoja tu.

Baada ya msiba, rafiki wa maehemu alijishauri sana kuhusu kumwambia mke juu ya Mali hii ambayo alikuwa na uhakika mjane hajui.

Anyway long story short Yule bwana aliuza kiwanja cha pembeni ila ila nyumba alikabidhi Kwa mjane.

Baada ya mjane kugusiwa kuwa marehemu alikuwa anamiliki vyote Yule bwana ( rafiki wa marehemu) aliruka na kudai Yeye na marehemu walimu ya pamoja.

Wadau tujitahidi hata kuacha wosia kama unahisi ndugu hawaaminiki
 
Nina Jirani ( sasa ni marehemu) alikuwa na Mgogoro na mke wake, kuhusu Mgogoro wao hatukujua mpaka jirani alipofariki.

Sasa hii story ni mrefu ila Kwa unduly Jirani alijenga nyumba ya biashara ( guest house, na frame za maduka) maeneo ya Kigamboni bila mke wala watoto kufahamu, na alipojenga pembeni kilibaki kiwanja Kikubwa tu, na aliyejua Alikuwa ni rafiki yake mmoja tu.

Baada ya msiba, rafiki wa maehemu alijishauri sana kuhusu kumwambia mke juu ya Mali hii ambayo alikuwa na uhakika mjane hajui.

Anyway long story short Yule bwana aliuza kiwanja cha pembeni ila ila nyumba alikabidhi Kwa mjane.

Baada ya mjane kugusiwa kuwa marehemu alikuwa anamiliki vyote Yule bwana ( rafiki wa marehemu) aliruka na kudai Yeye na marehemu walimu ya pamoja.

Wadau tujitahidi hata kuacha wosia kama unahisi ndugu hawaaminiki
Kabisa kaka
 
Hapana mkuu. Kaondoka mafundi wakiwa wanamdai na nikatoa Hela zangu zaidi ya 5m nikajua akija atarudisha. Mpaka Leo. Lazma angetoa taarifa.

Na Hardware alikuwa ashaweka uaminifu hivyo alikuwa anachukua vifaa anakuja kulipa hata baada ya wiki moja, Mwenye Hardware mpaka anaondoka Kuna deni la 16m
Watu wana ishi!!
Yaani hardware tu za Mil.16 wakati hio M.16 huku uswazi ushajenga nyumba na kuhamia
 
Ndugu we
Wakuu Habari zenu.
Kuna jirani yangu huu mwaka wa 12 haonekani na namba yake ikawa haipatikani mpaka Sasa ukipiga amepewa mtu mwingine kabisa. Sijui nini kimemkuta ila Kwa asilimia kubwa atakuwa amefariki.

Kipindi nahamia kwangu, alikuwa hajaanza ujenzi na baada ya mda akaanza ujenzi wa Bangaloo lake, alikuwa na uwezo na alijenga jumba la kifahari haswa na mafundi aliotumia aliniomba nimuunganishe wale walionijengea.

Nyumba ikiwa hatua za mwisho hii ilikuwa October 2012 jamaa akapotea, simu ikawa hazipokelewi baada ya mda hapatikani kabisa, Hakuna mtu anaejua alikuwa anakaa wapi, site tulizoea kumuona akiwa mwenyewe.

Na viwanja vilikuwa Bado havijapimwa kipindi hicho, hata Ardhi hamna detail zake.

Nyumba yenye thamani ya zaidi ya Tsh 300m inapotea pasipo ndugu kujua.

Kuna mwingine ni mwanajeshi mstaafu alinunua bonge la pori Goba - Dsm kipindi Cha zamani, Hakushirikisha familia japokuwa alikuwa na mke na watoto wakubwa sana.

Alimuachia mamlaka yote ya uangalizi wa eneo balozi wa ule mtaa, Mwaka Juzi alianza kuuza lile eneo lake baada ya kulipima, Kipindi hicho alikuwa anaumwa Yuko Nairobi, mimi nilipelekwa na Dalali nikiwa natafuta kiwanja. Unapitia Kwa Balozi unaongea akiwa Nairobi anakupa Account unalipa mnaandikisha na Balozi Kwa niaba yake, Yule Mzee sijui Nini kilimkuta alikuwa anauza viwanja Kwa bei ya chini sana sqm moja Kwa Goba alikuwa anauza Tsh 45,000/=

Nilinunua baadhi ya viwanja pale, na Bado ananidai 30m

Mwaka huu tumepata taarifa kafa nashindwa kuitafuta familia yake kuwaambia kwamba baba yao anaidai maana wanaweza kuanziaha mgogoro, Japo mke wake yupo na watoto wake.

Tulinunua maeneo Yale wote tulishabadilishq umiliki

Alikuwa na bonge la eneo hekari 10 zinafika, mjumbe kafaidi huku mke na watoto hawajui Chochote.

Wakuu tunapofanya maendeleo tujitahidi familia zijue hata kama Kuna ugomvi kiasi gani, basi kama sio mkeo Tafuta ndugu mnaoelewana waoneshe, Hatujui kesho yetu, Kuna Vifo vya ghafla.

Huyu Kwa asilimia kubwa atakuwa kashakufa. Nyumba nimebaki naipalilia Mimi Kwa sababu ni Jirani yangu ili isiwe sehemu ya kutumza wadudu. Raia wanajua ni yangu
ndugu wengine wapuuzi sana bora ufe wasijue vipotelee tu uko
 
Nina kwangu mkuu na nisingependa penda iwe hivi. Nimejaribu kila njia kupata ndugu zake Bado nimegonga mwamba
Hata iwe vp haihalalishi kuitumia nyumba hiyo kwa vyovyote vile nenda serikalini kabidhi kisichokua chako huo ndio utaratibu. Bot kuna kitngo cha pesa chafu mfano umeokota bilioni na haikuwezekana kupata muhusika so I ahifadhiwa mfuko maalum lakin haimaanishi mtu ajitumbulie mtu yyte akipeleka tetesi kwenye mamlaka unaitwa mwizi au mvamizi
 
Back
Top Bottom