Mnawachukuliaje watu wa GNLD na Forever Living Products?

Mnawachukuliaje watu wa GNLD na Forever Living Products?

wale wa zaman zamani walikua na trainings za maana kuhusu networking marketing, afya na mambo mengine ya maana ..nakumbuka mama yangu mdogo alikua anaenda south africa mara kwa mara kwa michongo ya gnld nafikiri alikua Ruby cjui na kitu gani nilikua mdogo ila nakumbuk kulikua na shelfu limejaa folders na kanda za GNLD miaka ya 2000 kurud nyuma ...sijui waliishia wapi ingawa nakumbuka walikua na dawa moja ya kuondoa alama mf ukijikata ukipaka unapona wala alama haibaki na dawa za pumu ambazo binafsi zilinisaidia sana..ile ya madoa nilikua nikipigna nikiwekwa ngeu napaka naamka asubuh niko safi ..then ikaja hii forever living nafikiri walikua na ubi na CC Africa mama yangu mzazi aliunganishwa na mke wa Canon mmoja kutoka uingereza alipata mafunzo mengi ya misosi na ARV na mambo mengine ya ukimwi ukimwi akawa anaenda Nairobi naweza kusema hiyo ilikua ni first version ..sasa ikaja hii nyingine ya kisasa asee naona sound sana ambayo wengi ni wamatumbi wanazingua sana.
Naona huyo mama yako alikuwa yupo level za juu hawa wa chini naona wanakuwa machinga wa hayo makampuni na hawafaidiki naona kazi yao ni kualika watu tu
 
Biashara yoyote ya halali naweza kufanya lakini hii ya kualikana haijawahi kunivutia hata siku moja[emoji116] [emoji116] [emoji116]
1b8262962debb269e57e8361b4f77f24.jpg
1b34a6c0c5aa41e17d210546fb47f865.jpg
 
Hao jamaa hawafai
Binafsi walinirubuni nikapoteza laki 3 yangu naikumbuka sana hata hiyo supergrow ilinibidi nipigie miti yangu nyingine nikaigawa bure!
 
Two things in common
1.) Ina promise pesa bila kuzalisha mali/ huduma.
2.) Ili mtu apate ni lazima mwingine apoteze kiwango sawia?
Yah! Binafsi mimi pia ni muumini wa pesa zinazopatikana kwa uzalishaji mali na sijahiwa kuwabali hawa jamaa
Ila nilikuwa nasema forex na AIM global,forever living,qnet n.k wanatofauti kubwa sana ya kimfumo forex hakuna kuinvite yani kama unakufa unakufa mwenyewe tu ila hao wengine lazma uinvite watu walipe hela na wewe upate kamisheni yako
 
Kitu kingine bidhaa zao ni ghal sana kuweza kuziuza. Dawa ya meno ina 17000 nan utamuuzia kama hutabak kutumia wewe tu
 
Kitu kingine bidhaa zao ni ghal sana kuweza kuziuza. Dawa ya meno ina 17000 nan utamuuzia kama hutabak kutumia wewe tu
 
Hakuna uyofauti wa Aina yeyote ile,ni biashara za Aina moja hizi.nazijua sana na nimeshashiriki sana kwenye misemina yao
kwahiyo kutokana na semina ulizoenda unataka kusema forex na hao nertwork marketing kama AIM,GNDL na forever living wanafanana
 
Naona huyo mama yako alikuwa yupo level za juu hawa wa chini naona wanakuwa machinga wa hayo makampuni na hawafaidiki naona kazi yao ni kualika watu tu
nadhani pia haya makampuni yamejibadilisha now ni kma huduma za kawaida na wale wa asili hawapo
 
Naona kuna watu wengi humu wanaongea wasichokijua Ngoja nijaribu kujibu baadhi ya comments nilizoziona humu kwa kadri ya uelewa wangu.

1.Nimeona watu wanapoteza hela

Hii ni biashara kama nyingine Ni kweli kuna watu wanapoteza hela hata mimi nimeona watu wanapoteza pesa kwenye biashara ya duka, daladala, taxi n.k nimeshuhudia baa kubwa na nzuri Kinondoni na hata sinza lakini hazina wateja.

2.Ni utapeli

Kwa kampuni halali iliyosajiliwa huwa hamna utapeli. Jambo la muhimu unapofanya biashara yoyote mtandaoni chunguza kama hiyo kampuni iko regulated yaani kuwe kuna taasisi zinaisimamia. Iwe unafanya biashara ya forex, unanunua mzigo online, iwe betting n.k. kwa mfano Alliance ana Leseni ya Tanzania na nchi mbalimbali ambazo anafanya biashara, pia yuko regulated na MLMIA, Phillipines chamber of commerce, DSAP, SGS, FDA HSA na kadhalika. Epuka kampuni ambayo haiko regulated.

3.Wanajifanya wana hela

Ni kweli wako ambao wanaona ili wakushawishi kuwa hii biashara inalipa basi waigize kuwa wao wenyewe ni mambo safi. Huku ni kutojiamini sio lazima mimi niwe tajiri ndipo na wewe uamini kuwa utafaidika naweza kukuonyesha njia (na hasa pale ambapo na mimi ndio naanza) wewe ukafanikiwa na mimi nikakwama. Naweza kuwa na kitambi lakini nikakufundisha kutengeneza six packs.

3.Ni biashara ngumu

Well kama zilivyo biashara nyingine lazima uweke juhudi. Kama una mawazo kwamba hii ni pesa ya bure bure huwezi kufanikiwa na bahati mbaya baadhi ya waelimishaji wanapotosha kwa kukuambia ni rahisi tu wewe tafuta watu wawili hao wawili walete wawili na hao pia wataleta wawili basi mtandao wako utakuwa mkubwa. Nikuambie ukweli hao mamilionea wana mtandao mkubwa sana wanatumia websites, facebook insta na kila mitandao kutangaza biashara. Wanafanya semina mkoa kwa mkoa na nchi kwa nchi ili kutangaza biashara. Mimi nafamihana kwa ukaribu na mmoja kati ya members waliofanikiwa Alliance yeye akaunti yake ana watu hadi Rwanda Kenya Uganda n.k ukiwa na wanafunzi mkoani ukaandaa semina anafunga safari anakuja kuwafundisha.

4.Wananufaika waanzailishi

Hiyo naamini ina ukweli kiasi ukiwa juu una nafasi zaidi ya kukuta wanaojiunga chini wanakuwa wanakunufaisha, hata hivyo bado swala la juhudi binafsi linahusika yaani sio tu ujiunge halafu uwe dormant halafu utegemee matunda. Hii ndio imenifanya hata mimi nichague Alliance japo nilikuwa nawajua Forever GNLD Trevo n.k Alliance kwa bongo bado ni ya motomoto.

Mwisho Kwenye maisha usiangalie waliofeli angalia waliofaulu. Aliyefail hawezi kuwa role modal wako na iko wazi siku zote kuwa wanaofeli ni wengi kuliko wanaofaulu. Masikini ni wengi kuliko matajiri, wanaothubutu ni wachache kuliko wanaoogopa na kupiga porojo. Be yourself!
basi prepare huko uliko ....
 
nadhani pia haya makampuni yamejibadilisha now ni kma huduma za kawaida na wale wa asili hawapo
labda lakini mimi naona mfumo wao ndo tatizo yaani wao wanataka uwaingize watu kadhaa ndo upige pesa
sasa hii inapelekea watu kuwa waongo ili wapate watu wa kuwaingiza na kujaribu kurudisha pesa zao na hao watu wakijoin na kushindwa kuinvite watu wengine wanaishia kupoteza pesa na utapeli ndo unapoanzia hapo maana utakuwa na product zao labda za laki sita ambazo huwezi kuuza unaishia kuzitumia mwenyewe tu
 
Back
Top Bottom