Mnoifahamu Katoro, tafadhali nijuzeni kuhusu Ukuaji, Maendeleo na Matarajio

Tatizo la huko ni ushamba mwingi na ushirikina kipindi cha nyuma kulikuwa na ujambazi ila kwasasa kumepoa Pako vizuri ni mji unaochipukia ila hakuna mipango miji kama Miji mingine ya Tanzania
Duh...
 
Na hii ndiyo changamoto viwanja viliuzwa Kwa fujo mpka Sasa hakuna eneo la kujenga hata shule hawakukumbuka kuacha open space yoyote ile
 
Katoro ni mji unaokuwa Kwa Kasi kutokana na mzunguko wa biashara kuwa mkubwa na pia maisha ya pale sio ghali kabisa ikilinganishwa na miji mingine inayokuwa Kama Kahama na ndio kitu kinachowavutia wafanyabiashara na wateja wengi. Shughuli kubwa ni biashara na madini. Kilichoongeza thamani ya mji ni uwepo wa wafanyabiashara wanaoagiza mzigo mkubwa kutoka China na nchi nyingine za bara la Asia pasipo kutegemea kuagiza kupitia Kwa wafanyabiashara waliopo Dar es salaam
 
Sio kweli, kuna zaidi ya hekari hamsini(50) za eneo la serikali
Hizi takwimu ni Kwa mujibu wa aliyekuwa afisa elimu mkoa Mr Anorld Msuya kabla hajaamishwa. Kwa pale mjini eneo limeshabana mpka pembezoni mwa mji
 
Hardware ni mradi mzuri sana bro
Mimi nipo hapa katoro!
Wachimbaji wa madini wanapopata dhahabu huwekeza sana katika ujenzi..

Hutojuta kuanzisha hiyo biashara.
Maeneo kama Ccm, buseresere, stamico!

Gharama za maisha zipo kawaida sana.
N.k

Itoshe kusema ni mji unaokua kutokana na wageni wanao hamia ni wengi zaidi.
Nimji unaojengwa nawafanyabiashara kuliko watumishi( watumishi sio wengi kivile)
Karibu katoro
Ahsante..Vp uwekezaji wa hardware, ni mzuri pia kwa pale
 
Aisee kumbe ni mji sio wa mchezo mchezo, nashukuru sana boss wangu...kwa maelekezo
 
Daaah..kumbe katoro ni ishu nyingine...
 
Mkuu kuna jamaa alitaka kuniuzia maeneo sehemu inaitwa Nyamigota, vipi kutoka hapo Nyamigota hadi Centre ya mji wa Katoro ni kama umbali gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…