Ndugu zangu, leo Katibu mkuu wa CHADEMA, Mh. Mnyika amejitokeza mbele ya waandishi was Habari na kusema wazi kwamba Chama hicho hakijawasilisha NEC orodha ya majina ya wabunge wa viti maalum kwa ajili ya kuapishwa! Kwamaana hiyo anatuambia orodha ile ni feki.
Lakini naomba tutumie akili zetu vizuri kuwaza na kuhoji. Wale walioenda kuapishwa sio watu wadogo, ni makada kindakindaki kuliko wengi wenu humu mnaokomenti, wanakijua chama kuliko ninyi, ni wajumbe wa vikao vikuu vya chama, kama kweli orodha hiyo ni feki inamaana wao ndio wameifoji? Siamini na haiingii akilini eti Mdee, Matiko na Bulaya na MAKAMANDA wale wengine wajiendee tu kuapishwa bila ruhusa! Na hapa nazungumzia ruhusa ya Mwenyekiti Mbowe! Naamini Mbowe amebariki wale wabunge wakaapishwe
Naamini amebariki kupeleka majina yale! Kweli kabisa Mdee na akina Matiko na Bulaya wajiamulie maamuzi haya makubwa namna hii? Hapana, Mwenyekiti ameamua kukinusuru chama kwa kuwaambia waende bungeni, liwalo na liwe! Chama kinahitaji kufanya siasa, na yeye anajua madhara ya kufanya siasa bila ya kuwa na wawakilishi bungeni! Chama kinahitaji ruzuku, ruzuku ni sawa na damu ndani ya mwili wa mwanadamu, bila damu kifuatacho ni kifo! Mbowe amekinusuru Chama kisife!
Mbowe amefikiria sana, hawa wapiga kelele kwenye Mitandao ni wanafiki, kura hawapigi, maandamano hawataki, kadi zao hawalipii ili kupata mapato ya chama! Wao kazi yao ni makelele tu! Wenzake wamemkimbia, eti wametishiwa maisha, wanasubiri Mbowe akijenge chama 2025 warudi waje wagombee, kwao wao chama kikipotea watahamia kwengine, Mbowe amepiga hesabu zake vizuri! Akipata ruzuku na wale wabunge 20 wakikatwa kila Mbunge mil 1.5 kwa mwezi, basi angalau hata hela ya kujaza mafuta gari ya Mwenyekiti kufanya siasa za chama zitapatikana!
Haya matamko ya Mnyika na Lisu ni Maigizo tu na Naamini Muda wao umewadia!0000