Uchaguzi 2020 Mnyika: Sakata la Wabunge wa Viti Maalum limehusisha mfumo wa Serikali kufifisha ajenda ya 'Uchaguzi haramu'. Ahoji Nusrat kuteuliwa akiwa gerezani

Uchaguzi 2020 Mnyika: Sakata la Wabunge wa Viti Maalum limehusisha mfumo wa Serikali kufifisha ajenda ya 'Uchaguzi haramu'. Ahoji Nusrat kuteuliwa akiwa gerezani

Chama sio biashara binafsi. Huwezi kufukuza watu kwenye chama kwa kigezo cha hisia tu.

Chadema haina hoja ya kupinga matokeo ya uchaguzi na kuzuia wabunge kufanya kazi yao.

Kisheria huwezi kumfukuza mtu kwenye Chama kama anatimiza wajibu wake wa kikatiba.

Wakifanya hivyo, basi litaamuliwa mahakamani. Mahakama huangalia maslahi mapana ya taifa.
Kukosa maadili kwenye siasa haliwezi kuwa maslahi mapana ya Taifa!
 
Katibu Mkuu wa CHADEMA anazungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mchakato wa wabunge wa Viti Maalum ambao wameapisha siku ya jana tarehe Novemba 24, 2020.

Tumewaita kuwaeleza kwamba CHADEMA hakijateua wabunge wa viti maalum wala hakijawasilisha orodha yoyote Tume ya Uchaguzi ya uteuzi wa wabunge wa viti maalum

Mimi kama Katibu Mkuu wa Chama sikuwahi kujaza fomu yoyote, kumthibitisha mtu yeyote mahali popote, kilichofanyika ni biashara haramu ya kugushi iliyohusisha mfumo wa kiserikali.

Mawasiliano yangu ya mwisho na Tume ya Uchaguzi zilikuwa ni barua 2, Nov 9 , niliiandika baada ya Mkurugenzi wa NEC kunukuliwa na vyombo vya habari kwamba CHADEMA imewasilisha orodha ya wabunge wa viti maalum na yeye amekwishaipeleka bungen

Kwa katiba ya CHADEMA mamlaka ya uteuzi wa wabunge yako kwa kamati kuu ya chama, na kamati kuu ya chama haijawahi kufanya kikao cha uteuzi wa majina ya wabunge wa viti maalum na mimi Katibu Mkuu sijawahi kuwasilisha orodha yoyote

Katibu Mkuu, John Mnyika amewataka wabunge wote walioapishwa kuwa wabunge wa Viti Maalum kufika kwenye ofisi za Makao Makuu ya Chama siku ya Novemba 27, saa mbili asubuhi bila kukosa kwa ajili ya utaratibu mwingine.

Mwanachama wetu aliyekuwa na kesi ya jinai ya kubambikiwa kwa muda mrefu Nusrat Hanje alitolewa gerezani tarehe 23 Novemba na mfumo ili watimize adhma yao.

Katibu Mkuu amesema kwamba wabunge wote walioapishwa Novemba 24 wamewekwa na mfumo na hawana baraka za chama cha Demokrasia na Maendeleo.

Kauli iliyotolewa jana na kumhusisha Mwenyekiti, Freeman Mbowe haina ukweli. Mbowe ataongoza kamati kuu na itawasikiliza wahusika. Kati ya walioapishwa kuna wajumbe wa kamati kuu wanafahamu uteuzi haukufanyika na wanajua wameshiriki biashara haramu

==========

JOHN MREMA: Mbele yetu katibu mkuu wa chama, John John Mnyika akiwa na mkurugenzi wa Itikadi, Uenezi na mahusiano ya mambo ya nje na msemaji mkuu kwa siku ya leo atakuwa katibu mkuu wa chama.

JOHN MNYIKA: Tarehe 28 Oktoba kulifanyika uchafuzi ulioitwa uchaguzi mkuu ambapo mtakumbuka kati ya mambo yaliyofanyika ni hujuma za wazi za mfumo wa kiserikali ukihusisha tume ya Taifa ya uchaguzi kupika matokeo ya uchaguzi.

Chama cha demokrasia na maendeleo hakijateua wabunge wa viti maalum au wagombe ubunge viti maalum wala hakijawasilisha orodha yoyote tume ya Taifa ya uchaguzi ya uteuzi wa wabunge wa viti maalum.

Kwa katiba ya CHADEMA, mamlaka ya uteuzi wa wabunge yapo kwa kamati kuu ya chama. Kamati kuu ya chama haijawahi kufanya kikao cha kuteua majina ya wabunge wa viti maalum wakati wowote.

Pili katibu mkuu wa chama ambae ndie mwenye mamlaka ya kimawasiliano ya kuwasiliana na tume ya Taifa ya uchaguzi, katibu mkuu wa chama sijawahi kuwasilisha orodha yoyote tume ya Taifa ya uchaguzi ya wanaoitwa waliopendekezwa wabunge wa viti maalum.

Katibu mkuu wa chama sio tu anatakiwa apeleke orodha bali anatakiwa apeleke fomu namba 8(d) kwa kila aliyekuwepo kwenye orodha ikiwa imesainiwa na katibu mkuu. Tume ya Taifa ya uchaguzi ilituletea fomu hizi hapa(Anazonyesha) ili tukishateua kama tungeteua, tupeleke orodha ya majina 113 kwa ujumla tukiwa tumejaza hizi fomu.

Mimi kama katibu mkuu, hakuna fomu yoyote ya mtu yoyote niliyowahi kuijaza popote kuthibitisha uteuzi wa yoyote.

Mchakato huo wote haukufatwa, kwa hiyo kwa tafsiri nyepesi, kilichofanyika ni biashara haramu ya kughushi ambayo imehusisha mfumo wa kiserikali, tume ya Taifa ya uchaguzi na kwakweli niseme vilevile imehusisha hao waliokwenda kuapa bila ridhaa ya chama na bila baraka za chama na bila kupishwa kwa mamlaka halali za chama.
Nawapongeza Sana , Sana CHADEMA kwa Tamko hili ! MUNGU awabariki Sana !
 
Hapo aibu kubwa ni kwa Halima Mdee, Very senior leader kushiriki ujinga huo kwa kweli si kwa leve yake inasikitisha sana.

Sidhani amefikia kiwango hicho ka kukosa hela hadi aisake kazi hiyo ya uwakilishi kwa nguvu bila hata kufuata utaratibu wa chama chake. Kwake watu walikuwa na imani kubwa mno hata kutabiri kumrithi Mwenyekiti Mbowe, kweli Mungu kawaonyesha rangi yake halisi mapemaa...

Yaani ipo hivi, CCM wamekula bakuli lote la nyama..... CDM wote wanapiga miayo njaa ni kali mateso na maumivu .....ohoooo kipande cha nyama kimoja kimerushwa kuwapima imani.. maskini eti huyu huyu Halima uvumilivu unamshinda anarukia kile kipande anakimega kidogo kisha anawagaia wenzake 19.... aisee inasikitisha na ni ngumu mno kuamini..

Pia yawezekana Bulaya akawa ndiye kirusi chenyewe kilichosambaza upendo...who knows!!
 
Mnyika kapwaya sana. Body language speaks. Inabidi tu amfuate Dr. Slaa.
 
Waswahili husema Usiangalie ulipoangukia bali angalia ulipojikwaa.

Tangu wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu jimbo la Kawe Halima Mdee alionekana kabisa kuwa anajiandaa kuwa mbunge wa viti maalumu na siyo jimbo.

Tukio la Halima Mdee silitofautishi sana na lile la Zitto Kabwe na Kitila Mkumbo.

Kimsingi Chadema kwa sasa ina kambi mbili Team Mbowe na Team Tundu Lisu na ubaya ni kuwa team Tundu Lisu wamejazana mitandaoni na siyo Ufipa street hivyo hawana madhara.

Maendeleo hayana vyama!
 
Chama sio biashara binafsi. Huwezi kufukuza watu kwenye chama kwa kigezo cha hisia tu.

Chadema haina hoja ya kupinga matokeo ya uchaguzi na kuzuia wabunge kufanya kazi yao.

Kisheria huwezi kumfukuza mtu kwenye Chama kama anatimiza wajibu wake wa kikatiba.

Wakifanya hivyo, basi litaamuliwa mahakamani. Mahakama huangalia maslahi mapana ya taifa.
Sheria ipi hiyo?

Amandla...
 
Utasubiri sana, ni mbinu bora kukabiliana na adui huwezi kupambana nae ungana nae.Kwa mbinu hii huenda JPM akatumia viti vyake 10 kupoza tena joto la siasa.Kisha wakiwa ndani ya system wataweza kuendelea kushawishi maboresho katiba na tume huru.
 
Chama sio biashara binafsi. Huwezi kufukuza watu kwenye chama kwa kigezo cha hisia tu.

Chadema haina hoja ya kupinga matokeo ya uchaguzi na kuzuia wabunge kufanya kazi yao.

Kisheria huwezi kumfukuza mtu kwenye Chama kama anatimiza wajibu wake wa kikatiba.

Wakifanya hivyo, basi litaamuliwa mahakamani. Mahakama huangalia maslahi mapana ya taifa.
Duuuh kuelewesha watz ndio ngumu hivi?
Swali: Hao walioapishwa, majina yao yamepelekwa na nani?? Sababu hata viti maalum wa mbogamboga wanautaratibu unaofatwa na chama kabla ya kupeleka majina, sio MTU anajipeleka bungeni halafu anaapishwa tuu!
Tuanzie hapa chifu
 
Back
Top Bottom